Inakuwaje mwanadamu ni mtawala asiye na nguvu juu ya hata viumbe viishivyo ndani ya utawala wake?

Tafikiri huzinigi wewe
 
ebu tueleze kuna watu tunaelewa sana unacho andika
 
Kama hawakuwa na njaa iweje baada ya Danieli kutolewa na kutupiwa wale wazee wengine ndani ya shimo hilo hilo wali-uawa kwa kuliwa vibaya sana na simba hao hao??
Brother hukuwepo icho kipindi nakusibitishia izo ni stori tu, embu leo tumtupe papa au mchungaji au awa wanajiita manabii uone kama hawaliwi!!! B yake tunaweza mtupa bibi mmoja wa sumbawanga na asiliwe😲😲 jitaidi kuamini vinavyowezekana ivyo ambavyo aviingii akilini wachana navyo avina maana
 
Nina shuhuda fulani, ni vile tu watu huwa wanahisi hao Simba ni hatari mbele za Mungu

Pia tusipende kuona vingi, kuna vitu Mungu anatuepusha navyo bila sisi kuona ni vya hatari na kutisha.
Live mkuu!
Lazima kuna mara nying sana Mungu ameingilia kati bila ss kujua, na kama asingeingilia basi tayar tungekuwa tumekufa.
 
Ninashuhuda ya maisha yangu binafsi,
Nikiwa mdogo wa miaka 7
Nilitekwa na watu katili nikiwa shule nikafungwa mikono na miguu, huku nimeshindiliwa mdomoni vipande vya magodoro na vitambaa vikuu kuu
Lengo lilikuwa kunipeleka nitolewe Kafara mirerani.

Kwa muujiza wa Mungu nilinusurika kimaajabu na kuanza kutambaa kuelekea Polini kwa siku kadhaa,
Ninatambaa kutumia makalio, Nikawanapishana na majoka makubwa manene mpaka leo nikiyakumbuka natetemeka, cha ajabu Sikuwa na hofu na yale majoka hata kidogo, zaidi nilikuwa na hofu na wale watu wasije kuniona wakaniua.
Hapo ndipo nikajua kuwa majoka huwa yanaweza kusimamia mkia na kupigana, huku wakiwa hawana kabisa time na mimi, wakati walikuwa wanauwezo wa kunimeza na wasinishibe[emoji15]

Wanyama wakali walikuwa wananipita wananitazama kana. kwamba wananishangaa wakiendelea na mambo yao mengine.

Mpaka nilipoishiwa nguvu kwa njaa na kiu ya maji nikapoteza fahamu nilipozinduka nikajikuta niko kwa Wamaasai wameshanifungua kamba na kunitoa Magodoro mdomoni.

Baada ya kunitibia majeraha makubwa nilokuwa nayo kwa muda mrefu, Ndipo walinieleza kwa kushangazwa kunikuta Kule mbugani Manyara nikiwa sijazuriwa na wanyama zaidi ya Ruba waliokuwa wamenijaa kwa kuwa sehemu nilipopotezea fahamu kwa muda ambao haujulikani kulikuwa na Dimbwi la tope afu kwa pembeni kuna Bonde la maji ambalo wanyama wengi uja kunywa.

Kwayo naamini kuwa Wakati ule sikuwa na dhambi Mungu aliwafunga vinywa, Macho na hata pua wale wanyama wote msituni wasinifanye ubaya, Maana ingekuwa sasa labda hata mfupa wangu wale Maasai wasinge uona machoni pa dunia hii.

Naamini maneno ya Vitabu vitakatifu vya Mungu vilivyoandikwa sisi ni watawala wa Vyoote[emoji735]
 
Hongera sana maana saivi usingeijua jf
 
, Mimi Kila nkutanapo mnyama mkali mfano mbwa wa mitaani aliekaa kichokozi,nyoka, au mnyama yeyote anaedhuru ni lazima nitamke maneno ya kuwa

#Mimi ni binadamu nmeumbwa kukutawala wewe mbwa/..... Usinidhuru Kwa vyovyote vile, nakuamrisha usinidhuru Kwa lolote..basi ndo kawaida yangu#

Nlisoma makala fulani basi nkawa nafanya hvyo Kwa Imani thabiti.
 
Ikawaje sema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…