Inasikitisha sana, kuna mtu ameomba kazi ya trainee akiwa na miaka 35

Inasikitisha sana, kuna mtu ameomba kazi ya trainee akiwa na miaka 35

Boss wangu alikua kanipa kazi niwapigie watu waje kwenye interview ya kazi ya Trainee iliyotangazwa hapa ofisini kwetu miezi kadhaa iliyopita.

Surprisingly katika kupitia cv zao, nimeona kuna mtu ana miaka 35 nae kaitwa. Nimejiuliza huyu mtu wenzake wa umri huo sasa hivi huenda wamefikia levels za umeneja au head of departments. Sasa huyu ndio kwanza anaomba Trainee.

Nimesikitishwa sana.
Kilichokusikitisha hasa ni nini? Wengine unakuta alikua sehemu kazini, ofisi ikapitia economic crises na ikafunga operation, usipende kuwajaji watu huwezi hata kuvaa viatu vyao hujui wamepitia mangapi
 
Mzeebaba ungetaja na kitengo unachofanyia kazi Mkuu ili tukuelewe vizuri.. Kama uyo Boss wako ni Baba ako endelea kushangaa ila kama na wew umeajiriwa hapo basi jua possibility ya wew kuja kumshangaza mwingine ni kubwa..just focus on your plate!
Safi sana umemwambia ukweli kuna watu wanachukulia maisha ya wenzao kama yao, hajui life aliyopitia mwenzake mpaka kufika hapo
 
Mkuu perry katika haya mambo ya kazi iko hivi,mfano mimi ni mwalimu na ka degree kangu ka ualimu,huko kwenye ualimu nina experience ya like 5 years,nikasema niongeze labda kamasters ka business administration, baada ya kupata hako ka masters kangu nikaona navutiwa sana na kazi za bank,nikaamua kuachana na ualimu wangu na kwenda bank,kule bank ntaanza kama fresher tu no matter nina umri gani.
Kwenye issue ya huyo jamaa labda alichelewa kupata kazi au aliugua muda mrefu akashindwa kumaliza shule kwa wakati.mimi nina rafiki yangu tulianza nae form 5 vizuri tu miaka mingi iliyopita ila sijui huko kwao wakawa wanamroga so akajikuta muda wa masomo anapata kama ukichaa hivi,ndugu zake wakahangaika nae kmtafutia tiba za asili matokeo yake alikuja kumaliza form 6 miaka 3 baada ya sisi, chuo napo kasoma kwa matatizo vibaya,kaja kumaliza Bachelor mwaka jana hapo udsm akiwa na karibia 37 years, sasa mtu kama huyu huwezi kumshangaa ila ni changamoto tu za maisha ndizo zimemchelewesha.
 
Wewe age is just a number..........Kuna watu tuna miaka 37 lakini ukituona kama tuna miaka 20.Then haya ni maisha jua kuwa kila mtu Mungu anambariki kwa namna yake na kwa muda wake.Mfano Daudi Mungu alimfanya mfalme wa Israel wakati akiwa tu kijana mdogo na Mungu huyohuyo alimpa Sarah mtoto wakati wa uzee wake.
 
Mkuu perry katika haya mambo ya kazi iko hivi,mfano mimi ni mwalimu na ka degree kangu ka ualimu,huko kwenye ualimu nina experience ya like 5 years,nikasema niongeze labda kamasters ka business administration, baada ya kupata hako ka masters kangu nikaona navutiwa sana na kazi za bank,nikaamua kuachana na ualimu wangu na kwenda bank,kule bank ntaanza kama fresher tu no matter nina umri gani.
Kwenye issue ya huyo jamaa labda alichelewa kupata kazi au aliugua muda mrefu akashindwa kumaliza shule kwa wakati.mimi nina rafiki yangu tulianza nae form 5 vizuri tu miaka mingi iliyopita ila sijui huko kwao wakawa wanamroga so akajikuta muda wa masomo anapata kama ukichaa hivi,ndugu zake wakahangaika nae kmtafutia tiba za asili matokeo yake alikuja kumaliza form 6 miaka 3 baada ya sisi, chuo napo kasoma kwa matatizo vibaya,kaja kumaliza Bachelor mwaka jana hapo udsm akiwa na karibia 37 years, sasa mtu kama huyu huwezi kumshangaa ila ni changamoto tu za maisha ndizo zimemchelewesha.
Dah umenikumbusha nakumbuka kwenye University niliyosoma kuna mtu nilimkuta na nilimuacha baada ya miaka kadhaa kupita nikasikia bado yupo chuo na issue ni kuwa amelogwa na watu wa kwao kuwa kamwe hatomaliza chuo kikuu apate degree yake so kila zikikaribia UE tu anaumwa kichaa yaani mpaka hospital ya chuo washamzoea. Nina ndugu yangu form 6 hakufanya vizuri so akaenda ualimu diploma, baada ya kumaliza ualimu akapata wafadhili fulani hivi wakimpromise kuwa watamsomesha degree ya 1 so akiwa anawasubiri akawa anafundisha, ka miaka miwili ikapita, akaona isiwe shida akaanzisha familia baada ya muda ndo akakumbuka kuwa bora aongeze elimu akasoma degree kumaliza akaaply hizo graduate trainee za bank fulani hivi akafanikiwa kupata kazi. So Perry kwa kuwa umeenda straight kwenye kupata elimu na ukapata kazi faster usishangae mtu kuomba graduate trainee akiwa na 35 years! Kingine aisee kulogana kwenye baadhi ya familia za kitanzania kupo sana nafahamu watu wengi tu walikuwa na uwezo sana shuleni but mwishowe shule wakaacha maana ni full kuugua maradhi yasiyoeleweka full kupandisha mapepo sasa wapo kadhaa huwa wanasurvive tu kibishi bishi mwishowe ndo unamkuta mtu yupo 30s plus ndo anagraduate na then anaanza tafuta kazi. Aisee ikiwa kwenye ukoo wenu au familia/jamii yenu hamna issue za ulozi shukuru Mungu sana. Halafu Perry mtu kuwa Meneja/Head of department aisee kuna vitu vingi hapo!! sio umri tu!! Ila hongera zako maana look like we mambo yako yanakuendea poa sana na soon utakuwa ni Meneja/Head of department mshukuru Mungu kwa hilo
 
Well noted hakuna mwenye guarantee ya maisho.mwanaume usimcheke mwenzio kwenye harakat za kusaka ugali
Mzeebaba ungetaja na kitengo unachofanyia kazi Mkuu ili tukuelewe vizuri.. Kama uyo Boss wako ni Baba ako endelea kushangaa ila kama na wew umeajiriwa hapo basi jua possibility ya wew kuja kumshangaza mwingine ni kubwa..just focus on your plate!
 
Aisee!

Nakumbuka miaka hiyo ulipo kuwa pale jalalani (udsm) ukisoma electrial engineering wakala kichwa ukaja kuibukia kwenye economics!

Then ukasota sana kwenye ajira ..ukaenda TRA wakakula kichwa mwishoe ukaja ibukia kwenye ajira za serikali huko kigoma huko!

Leo umekuja unashangaa mtu kuomba ajira akiwa na miaka 35! Kweli dunia inakimbia kwa kasi!
Perry na mwenzake mpiga msuri [emoji23]

Walikuwa wanajifanya wajuaji Sana humu jukwaani [emoji23]

Yuko ajira ya halimashauri anakula 400K sasa hivi bila posho yeyote [emoji23]

Sent from my vivo 1938 using JamiiForums mobile app
 
Boss wangu alikua kanipa kazi niwapigie watu waje kwenye interview ya kazi ya Trainee iliyotangazwa hapa ofisini kwetu miezi kadhaa iliyopita.

Surprisingly katika kupitia cv zao, nimeona kuna mtu ana miaka 35 nae kaitwa. Nimejiuliza huyu mtu wenzake wa umri huo sasa hivi huenda wamefikia levels za umeneja au head of departments. Sasa huyu ndio kwanza anaomba Trainee.

Nimesikitishwa sana.

Usikalili mkuu kuna watu wapo kwenye special mission
 
Kwenye maisha hakuna kuchelewa wala kuwahi, Kuna muda ukifika wewe unayeona umetangulia na wewe unayeona umechelewa, wote mnakuwa mpo sawa tu. Infact, wakati mwingine naweza nikachelewa lakini baada ya muda nikakuzidi mbali sana uliyetangulia. Kutangulia si kufika
 
Dah umenikumbusha nakumbuka kwenye University niliyosoma kuna mtu nilimkuta na nilimuacha baada ya miaka kadhaa kupita nikasikia bado yupo chuo na issue ni kuwa amelogwa na watu wa kwao kuwa kamwe hatomaliza chuo kikuu apate degree yake so kila zikikaribia UE tu anaumwa kichaa yaani mpaka hospital ya chuo washamzoea. Nina ndugu yangu form 6 hakufanya vizuri so akaenda ualimu diploma, baada ya kumaliza ualimu akapata wafadhili fulani hivi wakimpromise kuwa watamsomesha degree ya 1 so akiwa anawasubiri akawa anafundisha, ka miaka miwili ikapita, akaona isiwe shida akaanzisha familia baada ya muda ndo akakumbuka kuwa bora aongeze elimu akasoma degree kumaliza akaaply hizo graduate trainee za bank fulani hivi akafanikiwa kupata kazi. So Perry kwa kuwa umeenda straight kwenye kupata elimu na ukapata kazi faster usishangae mtu kuomba graduate trainee akiwa na 35 years! Kingine aisee kulogana kwenye baadhi ya familia za kitanzania kupo sana nafahamu watu wengi tu walikuwa na uwezo sana shuleni but mwishowe shule wakaacha maana ni full kuugua maradhi yasiyoeleweka full kupandisha mapepo sasa wapo kadhaa huwa wanasurvive tu kibishi bishi mwishowe ndo unamkuta mtu yupo 30s plus ndo anagraduate na then anaanza tafuta kazi. Aisee ikiwa kwenye ukoo wenu au familia/jamii yenu hamna issue za ulozi shukuru Mungu sana. Halafu Perry mtu kuwa Meneja/Head of department aisee kuna vitu vingi hapo!! sio umri tu!! Ila hongera zako maana look like we mambo yako yanakuendea poa sana na soon utakuwa ni Meneja/Head of department mshukuru Mungu kwa hilo
Good thing jamaa amepata hiyo nafasi
Leo ndio ameanza rasmi.
So mjadala ufungwe.
 
Sasa hapo kinachoshangaza nini [emoji2369][emoji2369]
 
Kuna jamaa miaka 35 anafanya private candidate ili aingie chuo

Tema mate chini wewe dogo
 
Kuna jamaa miaka 35 anafanya private candidate ili aingie chuo

Tema mate chini wewe dogo
Dah.maisha haya,kuna jamaa yangu hapa mwenyewe amezaliwa 1987,ndio anaingia chuo mwaka huu kuanza diploma.
 
Ndugu mleta mada hii inatokana na safari yako ya maisha ilikuwa na changamoto kiasi gani
 
Back
Top Bottom