Uchaguzi 2020 Ipo mifano hai kuwa Lissu atashinda Urais 2020, CCM tusijipe matumaini nawaambieni

Hakika
 
yani lisu aingie ktk ikulu mpya ya chamwino aliyeijenga magu... hichi kitu hakiingii akilini
 
Kamanda mr Ibu salute yako nakupa mkuu wangu
 
Magufuli ameathiri negatively maisha ya Watanzania wote kwa maamuzi yake ya chuki na kibaguzi.

Miaka 5 iliyopita Upinzani hawakuruhusiwa kufungua mdomo wakati wenyewe CCM waliendelea na kampeni. Kitu ambacho Magufuli alidhani anaua upinzani. Kinyume chake amejenga appetite kwa wa -Tanzania kusubiri wapinzani wateme nyongo.

Sioni Magufuli akipata hata 30% ya kura. Atapata kura za akina Makonda na ndugu zake wa Chatto anaowapa uteuzi kila siku.

Wa Tanzania wote au wenyewe au ndugu zao amewaathiri kimaisha kwa maamuzi haya:-
-Kuwaondoa wanafunzi wa UDOM
- Kufuta wafanyakazi wa vyeti feki
- Kuwatumbua wafanyakazi bila kufuata sheria
- Kutopandisha mshahara na madaraja
- Kutotoa ajira kwa wahitimu wa vyuo
- Kuvunja nyumba za Kimara na kuachia za Mwanza
- Kubagua maendeleo majimbo ya wapinzani kama Kilwa
- Kuzuia wanafunzi wenye mimba wasiendelee na masomo
- Kumtimua CAG makini
-Kuua wakosoaji kama BenSaa Nane na Azory Gwanda
- Kutumia vibaya fedha za Serikali kama ujenzi wa kiwanja cha Ndege Chato
- Kuwaweka rumande wafanyabiashara kwa makosa ya kubambikiza kama Rugemalira
-Kuwabambikiza makosa wakosoaji kama Kabendera
- Kutunga sheria kandamizi
-Kutawala kwa kidikteta
- Kufanya maamuzi bila kushirikisha Baraza la mawaziri

Hayo ni baadhi tu!!
 
Umejikita kwenye hoja likizo na nguvu na zimepitwa na muda. Uchaguzi una factors nyingi sana za kuangalia
 
Lissu hawezi kushinda na kamwe hatakuwa rais wa Tanzania labda jua libadili uelekeo,kwa lipi lissu kaifanyia Tanzania na watanzania hadi wampe heshima ya kiongoza nchi yetu?

Lissu ni mtu hatari sana kwa mstakabari wa taifa letu kwani ni selfish person, ni mtu mwenye jazba,hana nidhamu,amejaaa chuki,na anatumika na nchi za magharibi ili kuvuruga mstakari na umoja wa taifa letu,huyu bwana hafai lazima apingwe kwa kila namna .


Harafu mtu anaposema lissu atakuwa rais no kujidanganya sana,ataongoza serikali ipi ikiwa chama chake hakina uhakika wa kupata japo wabunge watano,hii ni ndoto

Mwambie lissu kuwa amejidanganya na kama anamatumaini ya kuiongoza Tanzania basi kapotea sana,
 
Hakuna uchaguzi rahisi kwa CCM kama mwaka huu! Uchaguzi mgumu ulikuwa 95 ya kina mrema na 2015 ya Edo! TL wala hatishi kwa Magu
Mrema alikuwa ni moto si mchezo, "rais wa walalahoi" watu walisukuma gari lake kwa mikono. Alikuwa na nguvu sana pamoja uhuru wa vyombo vya habari kuwa mdogo.
 
Shida chadema kuna wapiga mdomo wengi ila watendaji wachache.
 
CCM hawawezi kukubali kirahisi kuachia madaraka. Ingekua tume ipo wazi haiingiliwi nakubali 100% Lisu angeshinda. Lakini, kwa tume hii iliyowekwa mfukoni na CCM hakuna maajabu yanayoenda kutokea.
 
Akili zitawalejea tu mwaka, Lisu kakamata kila Kona, jamaa hakuwepo nchini miaka mitatu lakini maajabu ni kwamba umaarufu wake ni mkubwa kuliko hata yule anayezungumza mtaani kila wakati
 

Kutoka salama baada ya shambulio la risasi ni ishara kuwa Lissu sio wa kawaida. Ataisumbua Sana CCM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…