Uchaguzi 2020 Ipo mifano hai kuwa Lissu atashinda Urais 2020, CCM tusijipe matumaini nawaambieni

Uchaguzi 2020 Ipo mifano hai kuwa Lissu atashinda Urais 2020, CCM tusijipe matumaini nawaambieni

asante kwa uandishi mrefuuuuuuuuuuuuuuuu sana: maoni ya wananchi haya apa


izi ngonjera za jamii forum ziishe sasa mnaandika sana

Hawa siyo wananchi, ni wachumia tumbo wa uvccm wanaolipwa kutumika kwa propaganda
 
Atashinda njaa au?

Umaarufu au kuwa na wafuasi amfiki hata robo Edo ,uliza kilichotokea?

Hana mikakati,ana mvuto wa muda mfupi kutokana huruma ya majeraha aliyoyapata na baadhi ya watu kuwa na hamu nae kwasababu akuwepo nchini muda mrefu.

Mwisho alitakiwa apumzike siasa za kiharakati maana kiafya hayupo STABLE, je wafuasi wake lissu ataweza kumaliza mikoa,wilaya,kata ,kijiji na vitongoji kunadi sera? Huku tukijua anatembea kwa SPANA mkononi.
 
Lissu hawezi kushinda na kamwe hatakuwa rais wa Tanzania labda jua libadili uelekeo,kwa lipi lissu kaifanyia Tanzania na watanzania hadi wampe heshima ya kiongoza nchi yetu?

Lissu ni mtu hatari sana kwa mstakabari wa taifa letu kwani ni selfish person, ni mtu mwenye jazba,hana nidhamu,amejaaa chuki,na anatumika na nchi za magharibi ili kuvuruga mstakari na umoja wa taifa letu,huyu bwana hafai lazima apingwe kwa kila namna .


Harafu mtu anaposema lissu atakuwa rais no kujidanganya sana,ataongoza serikali ipi ikiwa chama chake hakina uhakika wa kupata japo wabunge watano,hii ni ndoto

Mwambie lissu kuwa amejidanganya na kama anamatumaini ya kuiongoza Tanzania basi kapotea sana,
Sikiliza nikuambie, unaandika kwa jazba na hofu kubwa iliyojaa chuki. Hiki kinaenda kutokea na kuweka historia. Hujui watanzania wana kipi kwenye nyoyo zao na usiwasemee kabisaa
 
Ni
Hakuna uchaguzi rahisi kwa CCM kama mwaka huu! Uchaguzi mgumu ulikuwa 95 ya kina mrema na 2015 ya Edo! TL wala hatishi kwa Magu
Ni kweli uchaguzi huu ni ngumu kupata kutokea,wananchi umaskini na maisha magumu umeongezea,wasio na ajira wameongezeka,wenye fedha wako magereza,watumishi Ni kilio Cha mtu moja moja,ukiteuliwa leo kesho hujui utaamkia wapi, ukabila, ukanda, wafungaji hawajui waelekee wapi, wajumbe kudai rushwa kwa hila na kupitishwa wagombea mamluki.
 
Wale vijakazi wa uvcmm mbona walishtukiwa mapema mpaka picha zao ziliwekwa mitandaoni nakuuliza tena wewe unaishi sayari gani mbona kama mgeni duniani.
Kamanda usipoteze muda kumjibu huyo anakutoa kwenye mada ,hakuna asiyejua wale waliofanya fujo ni vijana wa lumumba!!
 
Ndugu Mahanju,

Kwanza nikushukuru sana, nimesoma post yako ambayo ni very interesting, na ina facts nyingi.

Mimi ni a member na a big supporter wa CCM, na niko very very proud, lakini sio mshabiki wa kufunbia macho yasiyo pendeza au haki kudhulumiwa itendwapo na watu wangu na nikafurahia, apana nitakataa na kupinga uovu hata ndani ya nyumba yangu. Na always nitasherehekea lolote zuri linalofanywa na mtanzania au mwanadamu yoyote.

Katika point zako zote ninapinga hii hapo chini:

2. Kuna wabunge wa CHADEMA wenye kauli kali sana za kujiamini na zisizoogopa mtu kama vile Mbowe, John Mnyika, John Heche,Godbless Lema na Halima Mdee, tujiulize kama kweli watanzania hawapendi kauli kali kwanini wabunge hawa mpaka leo hawajawahi kushindwa kwenye majimbo yao?

Kama watanzania wanapenda kauli za ukali basi Lisu anaweza kutoboa na lazima tufahamu kua ukali wa Lissu na Dr Mafufuli ni tofauti kidogo, Lissu anazidi kidogo ukali na Ukali wake ni unaambatana na sequences zenye facts za kisheria na hivi ni mtaalam wa sheria.

Tukubali tuukatae ni lazima tuelewe kua uchaguzi huu wa mwaka huu siyo wa kawaida.

Bw. Mahamju, Kauli kali sio sababu kuu au muhimu ya kumpandisha mtu au kumshusha, Ushindi wa wabunge wengi wa upinzani katika majimbo, unatokana na maono ya wananchi, upevukaji wa kisiasa na Zaidi ulikuwa ni uzembe wa chama cha CCM, kwani walijipa na kutegemea kwa vyovyote watashinda, Na chadema ya wakati huo, tusisahau kuwa mikakati ya ushindi wa hao wabunge uliowataja , ili wekwa na watu makini kama akina Zitto, Kitila na wengineo ambao leo hawapo chadema, na waliogozwa na DR.Slaa, Chadema walikuwa na very visionary team ambayo imesambaratishwa na umimi .

Ndugu Mahanju, wachache wetu tumeishi njee ya nchi na wengine bado tuko huko, tusijaribu, kuleta siasa za nchi za ulaya hapa kwetu , hazitapokelewa vizuri na haziendani na mila zetu, watu wetu hawana uwezo wakimaisha (Financial support) na kuweza kufanya mgomo kwa siku mbili mfulilizo, they cannot be on the street Zaidi ya masaa mawili, na Zaidi ni kwa sababu hakuna kiongozi aliyekuwa tayari kujitolea, kama alivyokuwa Dr.Slaa, tusijidanganye, kila mmoja anachunga kivuli chake.

LISSU ni mzungumzaji mzuri, but haimfanyi mwanasiasa mzuri, siasa za fujo hazina mueleko wala hazitapokelewa,Upinzani wanijua solution, lakini hawana ubavu walifikia hilo kwa sababu ya UMIMI/ SELFISHNESS na uroho wa mali na madaraka.

Ni kweli yako Uchaguzi wa mwaka huu utakuwa na kelele na kashfa nyingi, Lakini tusije shangaa matokeo yasipokuja kuwa kama upinzani wanavyofikiria.
 
Hakuna uchaguzi rahisi kwa CCM kama mwaka huu! Uchaguzi mgumu ulikuwa 95 ya kina mrema na 2015 ya Edo! TL wala hatishi kwa Magu
Ccm itakaposhinda inaezekana mwaka huu ndo ukabaki kama reference ya hakuna uchaguzi mgumu kama wa 2020
 
Sikiliza nikuambie, unaandika kwa jazba na hofu kubwa iliyojaa chuki. Hiki kinaenda kutokea na kuweka historia. Hujui watanzania wana kipi kwenye nyoyo zao na usiwasemee kabisaa
Sasa wewe umejuaje? Unanizuia nisiwasemee huku wewe ukiwasemea,urais sio matako kwamba kila ntu lazima awe nayo,mwambieni lissu kamwe hawezi kuwa rais wa nchi hii,nakuambia hakika
 
yani lisu aingie ktk ikulu mpya ya chamwino aliyeijenga magu... hichi kitu hakiingii akilini
Ule ujenzi wa ikulu ni kama mtu anajua kwamba atakaa pale mielele mpaka kifo ila 2020 ataiona kwenye TV ikulu aliyoijenga.
 
yaani siyo Lissu tu hakuna namna mpinzani yoyote anaweza kushindana na Magufuli na safari hampati kiki yoyote ya kukamatwa na polisi, manaachwa mlopoke yote ili mwisho wa siku mtakavyopokea kipigo cha Mbwa mkose pa kutokea.
 
Kilikuwa na huo uzoefu walipokuwepo watu ambao ni vichwa kama akina kinana, Nape na Januari lakini hii timu ya sasa hakuna jipya siasa za mazoea zimepitwa na wakati.
Wamehamia chadema???
 
Magufuli ameathiri negatively maisha ya Watanzania wote kwa maamuzi yake ya chuki na kibaguzi.

Miaka 5 iliyopita Upinzani hawakuruhusiwa kufungua mdomo wakati wenyewe CCM waliendelea na kampeni. Kitu ambacho Magufuli alidhani anaua upinzani. Kinyume chake amejenga appetite kwa wa -Tanzania kusubiri wapinzani wateme nyongo.

Sioni Magufuli akipata hata 30% ya kura. Atapata kura za akina Makonda na ndugu zake wa Chatto anaowapa uteuzi kila siku.

Wa Tanzania wote au wenyewe au ndugu zao amewaathiri kimaisha kwa maamuzi haya:-
-Kuwaondoa wanafunzi wa UDOM
- Kutafuta wafanyakazi wa vyeti feki
- Kuwatumbua wafanyakazi bila kufuata sheria
- Kutopandisha mshahara na madaraka
- Kutotoa ajira kwa wahitimu wa vyuo
- Kuvunja nyumba za Kimara na kuachia za Mwanza
- Kubagua maendeleo majimbo ya wapinzani kama Kilwa
- Kuzuia wanafunzi wenye mimba wasiendelee na masomo
- Kumtimua CAG makini
-Kuua wakosoaji kama BenSaa Nane na Azory Gwanda
- Kutumia vibaya fedha za Serikali kama ujenzi wa kiwanja cha Ndege Chato
- Kuwaweka rumande wafanyabiashara kwa makosa ya kubambikiza kama Rugemakira
-Kuwabambikiza makosa wakosoaji kama Kabendera
- Kutunga sheria Maandalizi
-Kutawala kwa kidikteta
- Kufanya maamuzi bila kushirikisha Baraza la mawaziri

Hayo ni baadhi tu!!

Yericko Nyerere tufikishie hayo mambo kwa Lissu

-Awamu ya 5 imevuruga uhusiano wa kidiplomasia tumetengwa na nchi nyingi sana ,wafanyabiashara wamekimbia ,soko la biadhaa zetu nje limeshuka.

-Kifo cha Ben Saanane hakika aliyehusika hatokaa kwa amani na atapata taabu sana katika maisha yake hata kama kwa sasa anaishi maisha ya nje ya kifahari.
 
Tena Lissu ndo mwepesi kuliko wagombea wote waliowai kugombea Chadema.
 
Hakika nielimu iliyo njema kabisa, nikweli Sasa Basi uongo mwisho October 2020.
 
Fanya tafakuli ya kina juu ya ushind wa kibeberu cha waraabu kule zanzibar dhid ya shein uwanja wetu refa wet mashabiki wetu nyinyi ni amateur tu kwenye siasa hiz mywheather vs dula mbabe
Tukutane October 2020.
 
Wasalaam wajumbe wa jukwaa hili!

Naomba kudeclear kabisa kua mimi ni Mwanaccm toka 1997, nachozingumzwa hapa naomba nisipelekwe ufipani.

Ninachoshangaa na wanaccm wenzangu kujawa hopes kua tunaweza kushinda uchaguzi huu kwa urahisi hivyo, naomba ni waambieni kwa ushahidi huu kua Lissu ni kisiki kizito mara 10 ya Dr Slaa wa 2010 au LOWASSA wa 2015.

KWANINI LISSU ANAWEZA KUSHINDA?
Nikikumbuka na ya kuyafikiria haya ninashauri kabisa CCM tusibweteke na kujisahau.

1.Mwaka 2010 Tundu Lissu aliwahi kushinda ubunge katikati ya ngome ya CCM mkoa wa Singida na kujinyakulia Jimbo la Singida mashariki huku akiwa na madiwani 3 tu kati ya 17. Awamu iliyofuata 2015 alishinda tena na kuchukua kata 16 za madiwani akipoteza 1 tu.

2. Kuna wabunge wa CHADEMA wenye kauli kali sana za kujiamini na zisizoogopa mtu kama vile Mbowe, John Mnyika, John Heche,Godbless Lema na Halima Mdee, tujiulize kama kweli watanzania hawapendi kauli kali kwanini wabunge hawa mpaka leo hawajawahi kushindwa kwenye majimbo yao?

Kama watanzania wanapenda kauli za ukali basi Lisu anaweza kutoboa na lazima tufahamu kua ukali wa Lissu na Dr Mafufuli ni tofauti kidogo, Lissu anazidi kidogo ukali na Ukali wake ni unaambatana na sequences zenye facts za kisheria na hivi ni mtaalam wa sheria.

3. Kwanini hatuelewi kuwa Lissu ni mwanasheria mbozi, huu ushindi wa mezani wa kupita bila kupingwa tunajua atawashauri na kuwasomesha nini wagombea wa ubunge na udiwani?
Badala ya sisi kuweka mapingamizi basi tutakuta wao wametujazia mapingamizi.

Mkitaka kulijua hili muulizeni kuja jamaa moja anaitwa Wilson Nkhambaku mwaka 2010 alipohama CCM na kujiunga CHADEMA jimbo la Singida Magharibi baada ya kuonewa kwenye kura za maoni ccm, tulikimbilia kumwekea pingamizi lakini alichokifanya Lissu tunakijua mpaka huyo jamaa kupewa nafasi ya kugombea?

4.Niwaambieni kua Tundu Lissu ni zaidi ya jeuri kwenye mikakati ya uchaguzi, huyu ndiye aliyewashauri CHADEMA wenzake kua muda umeenda waachane na kulia na tume huru ya uchaguzi, aliwaambia "Tutashinda kwa tume hii hii pamoja na mapungufu yake".

Je, kuna nini hapo?

5.Jimbo la Singida Mashariki ni moja ya majimbo mengi Tanzania ambalo madiwani wake wote ni CHADEMA, Pamoja na jimbo kuchukuliwa Lissu akiwa ICU na kupewa Jamaa yetu moja wa CCM aitwaye Miraji Mtaturu lakini hakuna diwani hata mmoja aliyeunga mkono juhudi, tunajua Lissu aliwaambia nini?

Tukubali tuukatae ni lazima tuelewe kua uchaguzi huu wa mwaka huu siyo wa kawaida.
Na kasema akishindwa ataingiza wananchi mtaani.ina maana hata akishindwa kwa haki bado itafanya vurugu
 
Back
Top Bottom