Uchaguzi 2020 Ipo mifano hai kuwa Lissu atashinda Urais 2020, CCM tusijipe matumaini nawaambieni

asante kwa uandishi mrefuuuuuuuuuuuuuuuu sana: maoni ya wananchi haya apa

izi ngonjera za jamii forum ziishe sasa mnaandika sana
Hawa siyo wananchi, ni wachumia tumbo wa uvccm wanaolipwa kutumika kwa propaganda
 
Atashinda njaa au?

Umaarufu au kuwa na wafuasi amfiki hata robo Edo ,uliza kilichotokea?

Hana mikakati,ana mvuto wa muda mfupi kutokana huruma ya majeraha aliyoyapata na baadhi ya watu kuwa na hamu nae kwasababu akuwepo nchini muda mrefu.

Mwisho alitakiwa apumzike siasa za kiharakati maana kiafya hayupo STABLE, je wafuasi wake lissu ataweza kumaliza mikoa,wilaya,kata ,kijiji na vitongoji kunadi sera? Huku tukijua anatembea kwa SPANA mkononi.
 
Sikiliza nikuambie, unaandika kwa jazba na hofu kubwa iliyojaa chuki. Hiki kinaenda kutokea na kuweka historia. Hujui watanzania wana kipi kwenye nyoyo zao na usiwasemee kabisaa
 
Ni
Hakuna uchaguzi rahisi kwa CCM kama mwaka huu! Uchaguzi mgumu ulikuwa 95 ya kina mrema na 2015 ya Edo! TL wala hatishi kwa Magu
Ni kweli uchaguzi huu ni ngumu kupata kutokea,wananchi umaskini na maisha magumu umeongezea,wasio na ajira wameongezeka,wenye fedha wako magereza,watumishi Ni kilio Cha mtu moja moja,ukiteuliwa leo kesho hujui utaamkia wapi, ukabila, ukanda, wafungaji hawajui waelekee wapi, wajumbe kudai rushwa kwa hila na kupitishwa wagombea mamluki.
 
Wale vijakazi wa uvcmm mbona walishtukiwa mapema mpaka picha zao ziliwekwa mitandaoni nakuuliza tena wewe unaishi sayari gani mbona kama mgeni duniani.
Kamanda usipoteze muda kumjibu huyo anakutoa kwenye mada ,hakuna asiyejua wale waliofanya fujo ni vijana wa lumumba!!
 
Ndugu Mahanju,

Kwanza nikushukuru sana, nimesoma post yako ambayo ni very interesting, na ina facts nyingi.

Mimi ni a member na a big supporter wa CCM, na niko very very proud, lakini sio mshabiki wa kufunbia macho yasiyo pendeza au haki kudhulumiwa itendwapo na watu wangu na nikafurahia, apana nitakataa na kupinga uovu hata ndani ya nyumba yangu. Na always nitasherehekea lolote zuri linalofanywa na mtanzania au mwanadamu yoyote.

Katika point zako zote ninapinga hii hapo chini:

2. Kuna wabunge wa CHADEMA wenye kauli kali sana za kujiamini na zisizoogopa mtu kama vile Mbowe, John Mnyika, John Heche,Godbless Lema na Halima Mdee, tujiulize kama kweli watanzania hawapendi kauli kali kwanini wabunge hawa mpaka leo hawajawahi kushindwa kwenye majimbo yao?

Kama watanzania wanapenda kauli za ukali basi Lisu anaweza kutoboa na lazima tufahamu kua ukali wa Lissu na Dr Mafufuli ni tofauti kidogo, Lissu anazidi kidogo ukali na Ukali wake ni unaambatana na sequences zenye facts za kisheria na hivi ni mtaalam wa sheria.

Tukubali tuukatae ni lazima tuelewe kua uchaguzi huu wa mwaka huu siyo wa kawaida.

Bw. Mahamju, Kauli kali sio sababu kuu au muhimu ya kumpandisha mtu au kumshusha, Ushindi wa wabunge wengi wa upinzani katika majimbo, unatokana na maono ya wananchi, upevukaji wa kisiasa na Zaidi ulikuwa ni uzembe wa chama cha CCM, kwani walijipa na kutegemea kwa vyovyote watashinda, Na chadema ya wakati huo, tusisahau kuwa mikakati ya ushindi wa hao wabunge uliowataja , ili wekwa na watu makini kama akina Zitto, Kitila na wengineo ambao leo hawapo chadema, na waliogozwa na DR.Slaa, Chadema walikuwa na very visionary team ambayo imesambaratishwa na umimi .

Ndugu Mahanju, wachache wetu tumeishi njee ya nchi na wengine bado tuko huko, tusijaribu, kuleta siasa za nchi za ulaya hapa kwetu , hazitapokelewa vizuri na haziendani na mila zetu, watu wetu hawana uwezo wakimaisha (Financial support) na kuweza kufanya mgomo kwa siku mbili mfulilizo, they cannot be on the street Zaidi ya masaa mawili, na Zaidi ni kwa sababu hakuna kiongozi aliyekuwa tayari kujitolea, kama alivyokuwa Dr.Slaa, tusijidanganye, kila mmoja anachunga kivuli chake.

LISSU ni mzungumzaji mzuri, but haimfanyi mwanasiasa mzuri, siasa za fujo hazina mueleko wala hazitapokelewa,Upinzani wanijua solution, lakini hawana ubavu walifikia hilo kwa sababu ya UMIMI/ SELFISHNESS na uroho wa mali na madaraka.

Ni kweli yako Uchaguzi wa mwaka huu utakuwa na kelele na kashfa nyingi, Lakini tusije shangaa matokeo yasipokuja kuwa kama upinzani wanavyofikiria.
 
Hakuna uchaguzi rahisi kwa CCM kama mwaka huu! Uchaguzi mgumu ulikuwa 95 ya kina mrema na 2015 ya Edo! TL wala hatishi kwa Magu
Ccm itakaposhinda inaezekana mwaka huu ndo ukabaki kama reference ya hakuna uchaguzi mgumu kama wa 2020
 
Sikiliza nikuambie, unaandika kwa jazba na hofu kubwa iliyojaa chuki. Hiki kinaenda kutokea na kuweka historia. Hujui watanzania wana kipi kwenye nyoyo zao na usiwasemee kabisaa
Sasa wewe umejuaje? Unanizuia nisiwasemee huku wewe ukiwasemea,urais sio matako kwamba kila ntu lazima awe nayo,mwambieni lissu kamwe hawezi kuwa rais wa nchi hii,nakuambia hakika
 
yani lisu aingie ktk ikulu mpya ya chamwino aliyeijenga magu... hichi kitu hakiingii akilini
Ule ujenzi wa ikulu ni kama mtu anajua kwamba atakaa pale mielele mpaka kifo ila 2020 ataiona kwenye TV ikulu aliyoijenga.
 
yaani siyo Lissu tu hakuna namna mpinzani yoyote anaweza kushindana na Magufuli na safari hampati kiki yoyote ya kukamatwa na polisi, manaachwa mlopoke yote ili mwisho wa siku mtakavyopokea kipigo cha Mbwa mkose pa kutokea.
 
Kilikuwa na huo uzoefu walipokuwepo watu ambao ni vichwa kama akina kinana, Nape na Januari lakini hii timu ya sasa hakuna jipya siasa za mazoea zimepitwa na wakati.
Wamehamia chadema???
 

Yericko Nyerere tufikishie hayo mambo kwa Lissu

-Awamu ya 5 imevuruga uhusiano wa kidiplomasia tumetengwa na nchi nyingi sana ,wafanyabiashara wamekimbia ,soko la biadhaa zetu nje limeshuka.

-Kifo cha Ben Saanane hakika aliyehusika hatokaa kwa amani na atapata taabu sana katika maisha yake hata kama kwa sasa anaishi maisha ya nje ya kifahari.
 
Tena Lissu ndo mwepesi kuliko wagombea wote waliowai kugombea Chadema.
 
Hakika nielimu iliyo njema kabisa, nikweli Sasa Basi uongo mwisho October 2020.
 
Fanya tafakuli ya kina juu ya ushind wa kibeberu cha waraabu kule zanzibar dhid ya shein uwanja wetu refa wet mashabiki wetu nyinyi ni amateur tu kwenye siasa hiz mywheather vs dula mbabe
Tukutane October 2020.
 
Na kasema akishindwa ataingiza wananchi mtaani.ina maana hata akishindwa kwa haki bado itafanya vurugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…