Iran yarusha Makombora takriban 200 kuelekea Israel, Rais Biden aagiza Jeshi la Marekani kuyazuia

Kupitia Tv, live nimeona makombora mengi (zaidi ya 100) ya Iran kwenye anga la Tel Aviv, Israel na karibu yote yakionekana kuzuiwa angani kabla ya kutua, hii inatoa picha hii;
1. Iran ametangaza vita kamili dhidi ya Israel.
2. Iran amefanikiwa kupeleka makombora ya masafa marefu na kupenya moja kwa moja ndani kabisa ya Israel.
3. Mifumo ya Israel ya kutungua makombora angani iko imara.
4. Israel imepata sababu ya moja kwa moja kuishambulia Iran.
 
Iran kafanya kosa kubwa sana. Sasa karuhusu America ampige, ametafutwa muda mrefu sana. Hajuhi Natenyahu alikuwa USA juzi na hii mipango ya Natenyahu kuhutubia raia wa Iran imepangwa. Si kila mwanajeshi aliyevaa combat ya Israel ni Mu-israel, wengine ni kutoka US Army. Iran kaingia kizembe kwa kujitutumua.
 
Ayatolah anasema analipa kisasi cha Mkuu wa Magaidi ya Hamas Ismail Haniye.

Huyu Ayatolah utawala wake uondolewe ili Amani ipatikane.
 
Israel ni taifa pandikizi hapo mashariki ya kati ambalo limefanya unyama mwingi kwa muda mrefu...Halikuwekwa hapo kwa misingi ya amani bali kwa nguvu na ukandamizaji wa wapalestina...Kila siku zinavyoenda anajizolea maadui tu, hamas, houthi, hezbollah na sasa kaingia Iran...Hata kama ataweza kumshinda Iran, gharama yake itakuwa kubwa sana...ataamua mwenyewe...
 
Sawa analyst wa vita toka Tandale kwa mfuga mbwa
 
Mwisho wa aayatollah, ilikuwa lazima iwe hivyo.
Rais wa zamani wa Iran alionya MOSSAD wapo kila angle na kwenye kila mtandao ndani ya Iran
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…