Iringa: Kanisa Katoliki lawazuia waumini walioshiriki kongamano la Mwamposa kutopokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu mpaka watakapoungama

Mwamposa ni mtume hata waislamu wanamfata na wameikana dini yao ya majini
 
Waoh hawajazuia ww kwenda, Ila wametoa masharti Yao, mbona jamaa wameweka na facts kabsa.
Jaribuni kuwa waelewa. Wala hamna wanaotishwa, ni hivi ukienda huko Sisi tunaamin umepotea hakuna utajiri bila kazi,
Huo ndiyo ukweli, hakuna utajiri bila juhudi, jitihada na maarifa na bidii ya kufanya kazi!
Bulldoza anatembea kiroba na masandarusi ya kichina, kukusanya pesa, anauza maji, mafuta, kalamu, karatasi vyote vinasadikika kuwa na upako!
Yet, wagonjwa wapo bado wagonjwa, maskini bado maskini, jobless wanazurula kutafuta ajira, siku hizi maigizo yake. Yanalenga kubadili waislam kuwa wakristo!
 
Mwamposa anatoza sadaka nyingi si mchezo.
Hadi ana categorize watu wenye elfu 50 wataanza watamalizia wa elfu 5 kudadadeki
Ya mwisho inaitwa sadaka ya KUJIMALIZA! 😂 😂 😂
Wajinga wanatoa Hadi nauli za kurudia majumbani wanakosa!
 
Kanisa katolili ni kanisa lililojaa utajiri wa sala na novena

Waumin wakatoliki wanapokuwa na shida au wanapokuwa wanahitaji maombezi kuna njia huwa wanazitumia kufikisha taarifa kwa paroko au padre, kupitia jumuiya ndogo ndogo. Wagonjwa wanaponywa , wenye kuomba kazi wanapata wenye kuomba mke/mume wanapata ni vile tu watu walio nje ya ukatoliki huwa wanahisi kwamba Mungu yupo huko kwao tu ila kwa wakatoliko hayupo. Huwa mnajidaganya


Tunapokea shuhuda nyingi mno ambazo wakatoliki hutendewa kupitia EKARISTI TAKATIFU(mwili na damu ya Yesu Kristu) mlio nje ya ukatoliko hamuwezi kuelewa au kujua hicho kitu

Kama wakatoliki wangekuwa ni watu wa kupanda majukukwani kutoa ushuhuda nahisi hata muda usingetosha, vile tu hatunaga muda wa kuoanda majukwaani kutoa ushuhuda. Utaratibu wetu ni huu kama Mungu amekutendea basi unaalikwa kutoa sadaka yako ya shukrani au Misa ya shukrani kadri utakavyoguswa .

Shida kubwa tulioyonayo binadamu ni kuwa huwa tunapenda Mungu atende ile miujiza ya kwenye Biblia , yaani kichwa kinauma hapo hapo kipone tumbo la uvimbe linauma hapo hapo ukiombewa lipone, its okay lakin njia za Mungu za utendaji wake wa kazi ni nyingi, walokole wanampangia Mungu namna ya kufanya kazi. Kwamba wanataka atende hapo hapo na kama ingekuwa hivyo huyu Mungu asingeruhusu watu kusoma udactari ili unapoumwa kichwa au tumbo Mungu huyu akuponye kupitia kwa madactari.

Kwaio Ndugu zangu tusimpangie Mungu njia za kutenda kazi , ndo maana kanisa katoliki lipo wazi kabisa ,hata haya matatizo ya umaskini ambaya kwa kiasi kikubwa ndo yanawakimbiza watu kwenda kwa Mwamposa na kwa waganga wa kienyeji si kwamba hawayajui wanayajua ndo maana kila siku kanisa linajitahid linawahimiza kusoma linajitajid kusomesha watoto wenyw mazingira magumu, linajitahid kuelea watoto yatima linajitahidi kwa kila hali na mali kuwajali wagonjwa na wote waliokatika mazingira magumu,(kuwafariji) linaelewema maana mavuno ni mengi lakin watenda kazi ni wachache


Imani yako ndio itakayokuponya, kama unaamin katoliki si kanisa bora kwako hata uende wapi kama huna imani bado kwako utakuwa ni mtu wamasononeko tu.
 
Taarifa imekaa kimbea mbea kidogo, yani haina hata nyama ni heading to.
 
Hili povu..mtabaki watatu kanisani wewe baba paroko na sisita.

Rc hakuna mwamko wa kiroho..kuna mafundisho ya kukariri vikongwe vya zamani vilivyokufa vya warumi..wanavyo viita vitakatifu na viwaombee.

#MaendeleoHayanaChama
 
KWANINI CHARISMATIC WALIJITENGA NA NYINYI MLIOPOA KIROHO.

HEBU TULIA. WENZIO TUMESOMA SEMINARY, TUNAIJUA RC NDANI NJE

UNAELEWA KIKUNDI CHA CHARISMATIC NDANI YA RC???
 
Hili povu..mtabaki watatu kanisani wewe baba paroko na sisita.

Rc hakuna mwamko wa kiroho..kuna mafundisho ya kukariri vikongwe vya zamani vilivyokufa vya warumi..wanavyo viita vitakatifu na viwaombee.

#MaendeleoHayanaChama
Point mkuu
 
Ya mwisho inaitwa sadaka ya KUJIMALIZA! [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Wajinga wanatoa Hadi nauli za kurudia majumbani wanakosa!
Na wewe acha unafiki..hao waumini walikuja kwako uwasaidie nauli ya kurudi makwao.?

Kama huna hoja kaa utulie.

#MaendeleoHayanaChama
 
Lkn hakuna nguvu ya Mungu,hatuoni nguvu ikidhihirishwa ili kuwafungua watu km neno la Mungu linavyosema!
38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.

41 Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.
 
Hili povu..mtabaki watatu kanisani wewe baba paroko na sisita.

Rc hakuna mwamko wa kiroho..kuna mafundisho ya kukariri vikongwe vya zamani vilivyokufa vya warumi..wanavyo viita vitakatifu na viwaombee.
Sawa mkuu. Umeshakanyaga mafuta lakini? Keki je?
 
Na wewe acha unafiki..hao waumini walikuja kwako uwasaidie nauli ya kurudi makwao.?

Kama huna hoja kaa utulie.

#MaendeleoHayanaChama
Ndiyo walikuja kwangu kuomba nauli na Kula na kulala baada ya kushinda juani!

Jukwaa huru, where we dare to speak openly, hulazimishwi kukubaliana NAMI!
 
Haya Mafuta ya Upako sijui hatima yake ni nini! Nimeshuhudia wagonjwa hasa wajawazito wakija hospital na haya Mafuta! Yaani imekuwa part ya matibabu kwa wagonjwa pamoja na mgonjwa kutumia dawa kabla ya Kuja hospital atakwambia pia ametumia Mafuta ya upako, sijui mechanism yake ya healing ila yana chukua nafasi ya local herbs kwa sasa.
 
KWANINI CHARISMATIC WALIJITENGA NA NYINYI MLIOPOA KIROHO.

HEBU TULIA. WENZIO TUMESOMA SEMINARY, TUNAIJUA RC NDANI NJE

UNAELEWA KIKUNDI CHA CHARISMATIC NDANI YA RC???
Kitendo cha ku reply kwa kuandika kwa herufi kubwa ukidhani kwamba ndo reply yako itaonekana inadhihirisha wewe ni mtu wa aina gani


Karismatiki katoliki, bado hawajatengwa na kanisa bado wanatumbulika ndani ya kanisani. Ingawa kuna baadhi ya parokia huwa wanasimamishwa kwa sababu mbalimbali

Kusoma kwako seminary hakukufanyi uujue ukatoliki, kuna wengi tu wamesoma seminary lakin wakiulizwa maswali hawajui chochote, kwaio usilete hoja yako hapa kwamba unaujua ukatoliki nje ndani kisa tu umesoma seminary..unafikiri utamtisha nani kwa hoja zako dhaifu hivi??



Rejea comment yangu ya juu pale jibu kulinga na comment yangu kule jjuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…