Ismael Jussa amesema kuwa Nyerere ndiye aliyemuua Abeid Karume, yana ukweli haya? Na kama siyo mbona bado anazunguka mitaani, akamatwe

Kwenye Siasa shutuma za maauji hata wewe ukiingia utapewa.

Kuendekeza wapumbavu ni upumbavu, sasa Kama Nyerere ndio nafanya hayo Sisi tufanyaje?
Wewe hukuisikiliza kesi kwenye tv ulikuwa hujazaliwa sikulaumu kamuulize Bibi yako
 
Ninachofahamu Karume aliuwawa na Captain Humud kwa sababu ya kulipa kisasi cha baba yake aliyeuwawa akiwajela tena aliapa mbele ya wanafunzi wenzake wakiwa Urusi akisoma kwamba akirudi Zanzibar lazima atalipa kisasi (Alkisas). Karume alijulishwa hilo lakini alipuuza akidhani kwamba akimpandisha cheo huyo kijana atasahau lakini ikawa hivyo tena
 
Jussa mmoja ni sawa na akili za wabunge 300 wa chama cha ccm walioko bungeni na kama inakuma jussa kusema hivo kamulize mjukuu kinda kindaki wa mwana mapinduzi fatma karume ukweli wote atakwambia na wazanzibar wote wanajua
Mbona unachekesha tunazungumzia mwendawazimu alafu wewe unataka tukamuulize kichaa?
 
Soma vizuri historia ya zanzibar waandishi wengi sana wameandika.
Soma kwa kutulia ndo utajua nani alimuua karume.
 
Mahaba ya waarabu yamekuzidia hadi huuoni ukweli..huwezi tenganisha biashara ya utumwa afrika mashariki na uhusika wa mwarabu.

Mwarabu kawadumaza watu wa pwani..kwa kuwapa elimu feki ya imani bila kuwapa elimu ya kidunia..kiufupi mwarabu alikuja kumnyonya mwafrika kiakili,kijamii na kiuchumi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Paskali wakati mwingine anakuwa anafanya makusudi, anajua kabisa kwamba hakuna...justification whatsoever unavyoshiriki kwenye uuzaji wa watumwa au ununuzi wa watumwa, ni offenders. Sasa utawakwepesha vipi hao waarabu na biashara ya utumwa, wao walikamata wakishirikiana na waafrika wachache, kimsingi biashara ya utumwa walioanzisha ni WAARABU NA WAINGEREZA.
 
Ndiyo mafundisho ya kanisani kwenu?
 
Mbona unachekesha tunazungumzia mwendawazimu alafu wewe unataka tukamuulize kichaa?
NIMEKUMBUKA BUNGE LA KATIBA

Na Ismail Jussa

Kwenye Bunge la Katiba mwaka 2014 nilitoa hoja kwamba kwenye Katiba Mpya ya Shirikisho la Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kiwepo kifungu kinachoruhusu nchi nyingine ya Kiafrika inayotaka kujiunga na Muungano huu na ambayo itatimiza masharti yatakayowekwa iweze kuruhusiwa. CCM wakakataa!

Sasa hapo ndiyo huja swali: Ikiwa miaka yote mmetuaminisha kwamba Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar ulisukumwa na dhana ya Umoja wa Afrika (Pan-Africanism) na ulikusudiwa kuwa mwanzo wa Muungano mkubwa zaidi wa Bara la Afrika, kwa nini tena CCM wanakataa Muungano mkubwa zaidi?

Katika Bunge la Katiba hilo hilo, CCM wakayashambulia na kuyaponda ponda maoni ya Watanzania walio wengi (61%) waliotaka Serikali Tatu huku waking'ang'ania muundo uliofeli wa Serikali Mbili uendelee. Tukawaambia tuko tayari tuendelee na Serikali Mbili lakini sasa Zanzibar na Tanganyika tubadilishane nafasi katika Serikali Mbili hizo.

Tukawaambia sasa Zanzibar iwe ndiyo Serikali ya Muungano na ishughulikie mambo yote ya Muungano (yakiwemo mapato yote yatokanayo na mambo ya Muungano kama ilivyo sasa) na pia ishughulikie mambo ya Zanzibar yasiyo mambo ya Muungano. Na kuwe na Serikali ya Tanganyika itakayokuwa kama ilivyo Serikali ya Zanzibar ya sasa ili ishughulikie mambo ya Tanganyika yasiyo mambo ya Muungano. Wakakataa!

Nimekumbuka tu!
 

jiulize wewe ulikujaje duniani wakati adamu na hawa waliumbwa ni watu weupe na wakaambiwa wakaitawale dunia
 
Mwarabu hajaanzisha biashara ya utumwa. Soma biblia au tukusaidie mistari?
 

Labda iwe hutaki kuyajua mkuu
 
Labda iwe hutaki kuyajua mkuu
No sio sitaki kujua bali binadamu hujua yale tuu anayojulishwa ama kwa kushuhudia, ama kwa kusimuliwa ama kwa kusoma. Niliyoyasoma ndio hayo, kama kuna mengine ya chini ya kapeti, ama tuhadithieni tuyasikie au yaandikeni tuyasome.
P
 

Bila ya shaka hiyo ndiyo vision muliolishwa na watawala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…