Israel anapata wapi hiki kiburi? Ameweka rekodi ya kuuwa wafanyakazi wengi zaidi wa UN na waandishi

Israel anapata wapi hiki kiburi? Ameweka rekodi ya kuuwa wafanyakazi wengi zaidi wa UN na waandishi

Mkuu hujanielewa....Na kwa nini nikupe link....It seems your Intellectually lazy.....Inawekekana hata hujui UNRWA nini......! Naona kuna kundi la Wavivu ambao hawapendi kufanya their only research.......Sina muda huo Mkuu....!
Hizo unazoongea ni propaganda
 
unaleta huruma hapa.Pambaneni.si mliwachokoza.mnawachokoza mkipigwa mnaleta huruma hapa..hamasi wakati wanashambulia walishambulia vijana tu? komaa
 
Jamani kuna maswali nauliza hapa jamvini kila mara, hakuna anayejibu lakini watu wanarudia maneno yale yale

1. Ugaidi ni kitu gani?
2. Nani anatoa hadhi ya Ugaidi na nani anaondoa hadhi hiyo.

Hebu tuanzie hapo
Mimi nachojua siku hizi kigezo kimoja cha kuitwa gaidi lazima ujihusishe na uislamu au uwe muislamu kinyume na hivyo utaitwa tu jina lengine hata ufanye nini.
 
unaleta huruma hapa.Pambaneni.si mliwachokoza.mnawachokoza mkipigwa mnaleta huruma hapa..hamasi wakati wanashambulia walishambulia vijana tu? komaa
Kwahiyo kinachoendelea sasa ni Israel kulipiza uchokozi au?
 
Tate Mkuu:

Mbona unaangalia upande mmoja Mkuu! Just balance your argument, Kwani Hamas sio katili? Walichofanya October 7 ilikuwa ni nini? na viongozi wanasema wazi wanasema watarudia October 7 wakipata nafasi tena tena.....

'We will repeat October 7 again and again' - Hamas official​


Hamas Official Ghazi Hamad: We Will Repeat the October 7 Attack Time and Again Until Israel Is Annihilated; We Are Victims - Everything We Do Is Justified #Hamas #Gaza #Palestinians pic.twitter.com/kXu3U0BtAP

— MEMRI (@MEMRIReports) November 1, 2023
Hata Hamas nao ni makatili tu. Ingawa huo ukatili wao kwa namna fulani umesababishwa na huo ukandamizaji wa miaka nenda, wanaofanyiwa na hao Mayahudi.
 
Watu wengi hawana habari za kutosha
Mwaka 2006 Israel na Hezbollah. Israel imeunda kamati ya kuchunguza na kukiri ili''shindwa Vita.
Kilichoangaliwa ni uwezo wao wa kijeshi na zana ukilinganisha na Wapinzania wao. Israel ikakiri ilishindwa

Vita inayoendelea, katika '' War room' yaani mipango inapopangwa Wamarekani wanaongoza.
Waziri wa Ulinzi alikiri nwapo lakini Israel ndiyo inatekeleza, akasema kuanzia Oct 7 baada ya tangazo la vita drone zipo Gaza.

Israel inapata silaha kutoka Marekani ambazo hazijauzwa mahali pengine na toleo la mwisho na la kisasa.
Ushauri wote wa Vita unatolewa na Marekani. Nchi za Magharibi kama UK na France nao ni Washirika.

Kitendo cha Israel kupiga majengo kililenga kutengeneza mazingira ya wao kuingia Gaza na kupunguza majeruhi.
Marekani iliwaeleza Israel kwamba katika vita zote za Iraq na Afganistan, Taifa hilo lilipoteza askari wengine kwa kinachoitwa ''urabn warfare''

Israel inafahamu kona zote za Gaza, ina silaha za kisasa iwe maderaya, ndege za kivita, meli na mizinga ya masafa.
Hamas wana makombora na paraglider ya kutengeneza wenyewe , hawana maderaya wal meli

Kuna majeruhi wengi na vifo vingi vya askar wa IDF lakini wanasitiri aibu.
Hili limemonyesha wazi kile kinachoitwa tishio la IDF na MOSAD si kweli. Hivi MOSAD Walishindwaje kugundua siri ya watu zaidi ya 1000.

Tena limeonyesha udhaifu wa IDF bila Marekani na hilo limewapa jeuri Iran ndio maana wanatumia Houth na Hezbolla. Israel hawezi kusimama kidete na Iran ! Bila msaada wa Marekani Israel wanapigika vizuri sana


JokaKuu Pascal Mayalla

Mkuu Nguruvi3: Gaza inafanywa magofu....Hiyo Nguvu ya Iran iko wapi? Unasema Israel bila US haiwezi kusimama, Je Hamas bila msaada wa Iran inaweza kusimama....Nguruvi3 I always respect the way put your arguments kwenye mada nyingine, hili limekushinda!.
 
Andika utavyoandika lkn ukweli utabaki ukweli kwa sababu ni vita vya kuangamiza watoto wa waislamu. Ingalikua nchi yenye wakiristo wengi ukrain ungalisikia

Ukweli ni upi Mkuu? What is the Truth.....It may be subjective....Hamas iliua mbuzi Octeber 7? Sasa unaikataa hata Charter ya Hamas ambayo iko wazi.....? It seems you can not handle the truth! Inasikitisha sana jamaa yangu..

Labda rudia tena kuisoma ...Huu ndio UKWELI MTUPU......

The Hamas Covenant​


Article 15:

The day that enemies usurp part of Muslim land, Jihad becomes the individual duty of every Muslim. In face of the Jews' usurpation of Palestine, it is compulsory that the banner of Jihad be raised.

Huu ndio ukweli usiotaka kuusikia......!
 
Mkuu Nguruvi3: Gaza inafanywa magofu....Hiyo Nguvu ya Iran iko wapi? Unasema Israel bila US haiwezi kusimama, Je Hamas bila msaada wa Iran inaweza kusimama....Nguruvi3 I always respect the way put your arguments kwenye mada nyingine, hili limekushinda!.

Kuna nyakati kuna mijadila isiyofurahisha 'uncomfortable' , ni lazima.
Kwa wengine ukweli unatuongoza si mihemuko ya kipuuzi kama ya udini.

Tunafuatilia habari hizi kwa undani kutoka vyanzo tofauti hivyo perspective yangu na yako ni tofauti.
We can agree to disagree lakini hatuwezi kuwa na disputes katika facts.


Ni kweli mabomu yaliyopigwa Gaza yameiguza magofu. Hii wanaita 'indiscrimite bombing' wakitumia mabomu yanayoitwa 'dumb bomb' waliyopewa na Marekani. Upo Mkataba wa kimataifa wa kutoyatumia kwasababu hayana 'precision' lakini Israel inayatumia ''with impunity'' kama unanielewa.

Marekani inakingia kifua Israel kwa namna zote, UN kwa kura ya Veto, Intelejensia na silaha vitani .
Katika 'war room' mipango ni CIA na Pentagon kwa kushirikiana na IDF na MOSAD

Ikiwa Israel ina nguvu za kijeshi na kiintelejensia kama tunavyoaminishwa, Marekani inafanya nini katika War room?

Tofautisha kati ya Hamas na Hezbollah. Pili, Gaza ipo chini ya Israel hakuna kinachoingia au kutoka bila Israel kujua.

Mabomu ya Hamas ni 'local made' ndiyo maana haya 'precision'.
Influence ya Iran kwa Hamas ni kupitia Hezbollah, hakuna msaada wa moja kwa moja kama ilivyo Israel kwa USA

USA ina Fleet Carriers mbili katika Bahari ya Mediterranean pwani ya Israel.
Meli zinatoa msaada wa intelejensia na vifaa kwa Israel. Inatosha kusema ni '' Marekani Vs Hamas '' kupitia Israel

Kwasasa kuna vita kaskazini kati ya Hezbollah na Israel. Hezebollah wanatumia zana kutoka Iran na zina precision ya hali ya juu, Israel imekiri.

Kwamba wiki kadhaa wameweza kupiga vituo vya mawasiliano vya Israel kwa uhakika wakikwepa ' Iron dome' inayotumika kuzuia makombora ya Hamas ya Katush. Wameingiza drone na zimerudi kutoka Israel

Tishio la Hezbollah limelazimu Israel kuita askari 350,000 wa akiba. Fikiri kwamba hili ni Taifa linalosadikika kuwa na nguvu na vifaa . Hii ina maana hali si njema na wanahofia mzozo ukisambaa Iran ikaingia Israel ina wakati mgumu . Wataweza kusaidiwa na Marekani lakini wenyewe hawawezi kusimama kidete na Iran

Eneo la Israel ni sababu nyingine ya kuwafanya wawe Vulnerable. Sijui kama unajua eneo leneyewe linaukaribu wa Bagamoyo, Dar, Pwani . Hivyo Kombora moja linakuwa tishio.

Iran ilipiga kombora kwa kambi ya Marekani baada ya kumuua kiongozi wao Iraq. Unajua nini kilitokea, mamia ya askari wa Marekani walipata 'concussion' na madhara mengine. Kombora hilo lituua Tel Aviv ni madhara tupu.

Nadhani nimekusaidia kuona picha kwa ukubwa wake na si kwa jicho la ' kukaririshwa, headlines, dini '' n.k.
 
View attachment 2851446

Israel inaishambulia makazi ya watu, inaua watoto, wanawake, wagonjwa, waandishi wa habari, na hata wafanyakazi wa umoja wa mataifa
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa anasema kwamba tangu kuanzishwa kwa UN haijawahi kutokea wafanyakazi wake wengi kuuawa kwenye vita kama walivyouawa na Israel

Matamko na maazimio kibao ya umoja wa Mataifa yameitaka Israel kusitisha vita lakini imejibu kwa kiburi kuwa itaendelea na mauaji hayo hata Umoja wa Mataifa usema nini
Tatizo bwana zako Hamas wanajificha kwa raia
 
Mimi nachojua siku hizi kigezo kimoja cha kuitwa gaidi lazima ujihusishe na uislamu au uwe muislamu kinyume na hivyo utaitwa tu jina lengine hata ufanye nini.
Na hili ni tatizo kubwa sana katika jamii yetu

Matumizi ya neno Ugaidi yameongezeka lakini wanaoweza kueleza ni kitu gani, kinafanyikaje, nani anaidhinisha nani anatengua sifa ya Ugaidi, hakuna anayeweza kueleza. Hii ni kwasababu watu wamekaririshwa hawana muda wa kufikiri au kutafuta ukweli. Sasa ukiuliza Ugaidi ni kitu gani , wanakimbia na atakayeweza kujibu atakwambia Alshabab

Kuna watu wanaamini tatizo limeanza Oktoba 7 , hawana habari nini kilitokea September kurudi nyuma
Watu hao hawajui Msetla wa Israel wanafanya nini. Ni kwasababu akili zao zimefungwa katika upumbavu wa kwamba Israel ni 'Taifa teule' Ukiuliza uteule ni kitu gani hawana jibu. Hata dini wanasimuliwa lakini hawana ufahamu.

Nimepitia katika mijadla ya nchi nyingine kama Kenya, Nigeria na Zimbabwe naweza kusema bila aibu Tanzania tuna matatizo. Vijana wetu hawasomi, hawatafuti habari , hawataki kujifunza ni wavivu wa kufikri. Huko kweingine mijadala ni ya maana sana kiasi kwamba najiuliza hivi ni mitaala ya elimu au ni culture ya kujifunza.

Mijadal ya forum za nchi nyingine ipo objectively, huwezi kusikia watu wana insinuate upuuzi wa imani.
Watu wanajadili mambo kuanzia miaka 75 iliyopita. Huku kwetu Vijana wanajua tatizo limeanza Oktoba.

Tuna matatizo sana ndio maana vijana wetu ni incompetent katika EAC wakiomba serikali ilinde ajira.

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Tatizo bwana zako Hamas wanajificha kwa raia

Hii hoja ya Hamas kujificha katika makazi ni ya Israel ili kuhalalisha mauaji ya Raia wasio na hatia.

Nikweli kwamba Hamas wapo katika makazi. Unachopaswa kujiuliza ni kwamba eneo la Gaza lenye watu milioni 2 likitajwa kuwa 'densely populated' in the World ulitegemea Hamas wakae wapi?

Pili, hivi ulitegemea Hamas wasio na control na air , land or sea wajikusanye kama mashabiki wa Yanga uwanja wa Mkapa wakisubiri kulipuliwa.

Tatu, Zile Iron Dome za Israel zipo hadi kwenye makazi mbona husemi hilo ni tatizo? Kama kuna maeneo ya askari nitajie ni eneo gani ukienda utakuta askari wa Israel wamekusanyika kama washabili wa Yanga pale kwa Mkapa!

Kule Kibbutz kuna askari walitekwa na HamaS na wanashikiliwa hadi leo.
askari wa Israel walikuwa wanafanya nini katika eneo la Raia tunaloambiwa ni la mafunzo ya Kilimo?

Mbona tunaona askari wa Ukraine mijini katika makazi ya watu lakini hatusikii mkisema!

Tatu, Zile kambi za Majeshi yetu hapa Tanzania katika miji, je hazipo katika makazi ya Raia?

Ukisema Hamas wanajificja katika makazi hebu tueleze ulitegemea wawe eneo gani?

Narudia pale pale, lazima Watanzania tujifunze kitu kinaitwa '' Reasoning''

JokaKuu Pascal Mayalla
 
View attachment 2851446

Israel inaishambulia makazi ya watu, inaua watoto, wanawake, wagonjwa, waandishi wa habari, na hata wafanyakazi wa umoja wa mataifa
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa anasema kwamba tangu kuanzishwa kwa UN haijawahi kutokea wafanyakazi wake wengi kuuawa kwenye vita kama walivyouawa na Israel

Matamko na maazimio kibao ya umoja wa Mataifa yameitaka Israel kusitisha vita lakini imejibu kwa kiburi kuwa itaendelea na mauaji hayo hata Umoja wa Mataifa usema nini
Anakipata kwa Mmarekani na Muingereza na sasa ni NATO yote, kwani Waingereza na Wamarekani ndiyo walimtetea apewe ardhi Palestina na wameahidi kumlinda kwa lolote lile.
 
Kuna nyakati kuna mijadila isiyofurahisha 'uncomfortable' , ni lazima.
Kwa wengine ukweli unatuongoza si mihemuko ya kipuuzi kama ya udini.

Tunafuatilia habari hizi kwa undani kutoka vyanzo tofauti hivyo perspective yangu na yako ni tofauti.
We can agree to disagree lakini hatuwezi kuwa na disputes katika facts.


Ni kweli mabomu yaliyopigwa Gaza yameiguza magofu. Hii wanaita 'indiscrimite bombing' wakitumia mabomu yanayoitwa 'dumb bomb' waliyopewa na Marekani. Upo Mkataba wa kimataifa wa kutoyatumia kwasababu hayana 'precision' lakini Israel inayatumia ''with impunity'' kama unanielewa.

Marekani inakingia kifua Israel kwa namna zote, UN kwa kura ya Veto, Intelejensia na silaha vitani .
Katika 'war room' mipango ni CIA na Pentagon kwa kushirikiana na IDF na MOSAD

Ikiwa Israel ina nguvu za kijeshi na kiintelejensia kama tunavyoaminishwa, Marekani inafanya nini katika War room?

Tofautisha kati ya Hamas na Hezbollah. Pili, Gaza ipo chini ya Israel hakuna kinachoingia au kutoka bila Israel kujua.

Mabomu ya Hamas ni 'local made' ndiyo maana haya 'precision'.
Influence ya Iran kwa Hamas ni kupitia Hezbollah, hakuna msaada wa moja kwa moja kama ilivyo Israel kwa USA

USA ina Fleet Carriers mbili katika Bahari ya Mediterranean pwani ya Israel.
Meli zinatoa msaada wa intelejensia na vifaa kwa Israel. Inatosha kusema ni '' Marekani Vs Hamas '' kupitia Israel

Kwasasa kuna vita kaskazini kati ya Hezbollah na Israel. Hezebollah wanatumia zana kutoka Iran na zina precision ya hali ya juu, Israel imekiri.

Kwamba wiki kadhaa wameweza kupiga vituo vya mawasiliano vya Israel kwa uhakika wakikwepa ' Iron dome' inayotumika kuzuia makombora ya Hamas ya Katush. Wameingiza drone na zimerudi kutoka Israel

Tishio la Hezbollah limelazimu Israel kuita askari 350,000 wa akiba. Fikiri kwamba hili ni Taifa linalosadikika kuwa na nguvu na vifaa . Hii ina maana hali si njema na wanahofia mzozo ukisambaa Iran ikaingia Israel ina wakati mgumu . Wataweza kusaidiwa na Marekani lakini wenyewe hawawezi kusimama kidete na Iran

Eneo la Israel ni sababu nyingine ya kuwafanya wawe Vulnerable. Sijui kama unajua eneo leneyewe linaukaribu wa Bagamoyo, Dar, Pwani . Hivyo Kombora moja linakuwa tishio.

Iran ilipiga kombora kwa kambi ya Marekani baada ya kumuua kiongozi wao Iraq. Unajua nini kilitokea, mamia ya askari wa Marekani walipata 'concussion' na madhara mengine. Kombora hilo lituua Tel Aviv ni madhara tupu.

Nadhani nimekusaidia kuona picha kwa ukubwa wake na si kwa jicho la ' kukaririshwa, headlines, dini '' n.k.

Mkuu nimekuelewa, mimi ni mtu mmojawapo nisiyekaririshwa na vyombo vya habari, naweza kuwa na misimamo, lakini siifuati kama kipofu! Katika mgogoro huu nimekuwa na muda mzuri wa kuziangalia perspectives za pande mbili, nimerudia historia, niko nje ya nchi kwa sasa, hivyo na na accesses za vitabu, majarida zinazopatikana kirahisi.

Sikatai kuwa nina msimamo wangu, lakini lazima uwe umesimama katika facts, ingawa hata facts zinaweza kupata tafsiri tofauti! Nimeajadiliana na watu katika mgogoro huu ambao ni mazuzu kabisa nini kilitokea baada ya kuanguka Ottoman Empire na hata kurudi nyuma kabla ya hapo. Na hata wengi hawajui Partion Plan (Resolution 181) Iligawaje eneo hilo, na reactions za Waarabu na Wayahudi.

Na nimeshangazwa na mno na wengi wanaoandika humu hawajui juhudi za Kimataifa ambazo zimefanyika na kwa nini zilishindwa ( unaona sababu za kushindwa toka pande mbili)

Kwa hiyo mkuu siko katika kundi linaoishia kusikiliza tu , CNN, Aljezeera, hata Haaretz, Jerusalem Post nk au kuangalia clips za Tit Tok au Snap chat.

Hivyo jamaa yangu mimi sisikumwi na jabza, mgogoro huu umeafanya niagize vitabu vingi ilikujenga msimamo wangu binafsi wa mgogoro huu, Sasa hivi nilikuwa napitia "Side by Side- Parallel Histories of Israel and Palestine

Side by Side: Parallel Histories of Israel-Palestine Paperback – March 6, 2012​

by Sami Adwan (Editor), Dan B

Kwa kifupi baadhi ya Watanzania ni intellectually lazy, ni ushabiki bila kujua ni kwa nini, na facts ni zipi!.....

Hivyo mkuu mimi siko kwenye kundi la kuswaga tu na kuimbishwa na CCN ali Aljezeera.......nina misimamo ambayo naweza kuitetea, wengi kwenye maada hii ni ushabiki tu!
 
View attachment 2851446

Israel inaishambulia makazi ya watu, inaua watoto, wanawake, wagonjwa, waandishi wa habari, na hata wafanyakazi wa umoja wa mataifa
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa anasema kwamba tangu kuanzishwa kwa UN haijawahi kutokea wafanyakazi wake wengi kuuawa kwenye vita kama walivyouawa na Israel

Matamko na maazimio kibao ya umoja wa Mataifa yameitaka Israel kusitisha vita lakini imejibu kwa kiburi kuwa itaendelea na mauaji hayo hata Umoja wa Mataifa usema nini
Kwani hamasi wameshauawawa wangapi mpaka muda huu. Ukipata jibu hilo utaona wacha kichapo kiendelee
 
Kuna nyakati kuna mijadila isiyofurahisha 'uncomfortable' , ni lazima.
Kwa wengine ukweli unatuongoza si mihemuko ya kipuuzi kama ya udini.

Tunafuatilia habari hizi kwa undani kutoka vyanzo tofauti hivyo perspective yangu na yako ni tofauti.
We can agree to disagree lakini hatuwezi kuwa na disputes katika facts.


Ni kweli mabomu yaliyopigwa Gaza yameiguza magofu. Hii wanaita 'indiscrimite bombing' wakitumia mabomu yanayoitwa 'dumb bomb' waliyopewa na Marekani. Upo Mkataba wa kimataifa wa kutoyatumia kwasababu hayana 'precision' lakini Israel inayatumia ''with impunity'' kama unanielewa.

Marekani inakingia kifua Israel kwa namna zote, UN kwa kura ya Veto, Intelejensia na silaha vitani .
Katika 'war room' mipango ni CIA na Pentagon kwa kushirikiana na IDF na MOSAD

Ikiwa Israel ina nguvu za kijeshi na kiintelejensia kama tunavyoaminishwa, Marekani inafanya nini katika War room?

Tofautisha kati ya Hamas na Hezbollah. Pili, Gaza ipo chini ya Israel hakuna kinachoingia au kutoka bila Israel kujua.

Mabomu ya Hamas ni 'local made' ndiyo maana haya 'precision'.
Influence ya Iran kwa Hamas ni kupitia Hezbollah, hakuna msaada wa moja kwa moja kama ilivyo Israel kwa USA

USA ina Fleet Carriers mbili katika Bahari ya Mediterranean pwani ya Israel.
Meli zinatoa msaada wa intelejensia na vifaa kwa Israel. Inatosha kusema ni '' Marekani Vs Hamas '' kupitia Israel

Kwasasa kuna vita kaskazini kati ya Hezbollah na Israel. Hezebollah wanatumia zana kutoka Iran na zina precision ya hali ya juu, Israel imekiri.

Kwamba wiki kadhaa wameweza kupiga vituo vya mawasiliano vya Israel kwa uhakika wakikwepa ' Iron dome' inayotumika kuzuia makombora ya Hamas ya Katush. Wameingiza drone na zimerudi kutoka Israel

Tishio la Hezbollah limelazimu Israel kuita askari 350,000 wa akiba. Fikiri kwamba hili ni Taifa linalosadikika kuwa na nguvu na vifaa . Hii ina maana hali si njema na wanahofia mzozo ukisambaa Iran ikaingia Israel ina wakati mgumu . Wataweza kusaidiwa na Marekani lakini wenyewe hawawezi kusimama kidete na Iran

Eneo la Israel ni sababu nyingine ya kuwafanya wawe Vulnerable. Sijui kama unajua eneo leneyewe linaukaribu wa Bagamoyo, Dar, Pwani . Hivyo Kombora moja linakuwa tishio.

Iran ilipiga kombora kwa kambi ya Marekani baada ya kumuua kiongozi wao Iraq. Unajua nini kilitokea, mamia ya askari wa Marekani walipata 'concussion' na madhara mengine. Kombora hilo lituua Tel Aviv ni madhara tupu.

Nadhani nimekusaidia kuona picha kwa ukubwa wake na si kwa jicho la ' kukaririshwa, headlines, dini '' n.k.

Mkuu Nguruvi

Nimepunguza kuchangia sana katika katika mada hii, hasa kwa sababu watu wengi sana humu ndani ni mihemuko tu ya kidini ( pande zote) Kwa wengine Israel ni taifa la Mungu na kwa wengine hii ni vita vya kukandamiza Waislamu, na sikatai kabisa, kuna religious attachment kubwa mno usio weza kuikataa ambayo iko pande zote.

Umezungumzia pia kuhusu facts....Kuwa hazipingiki....


"'Tunafuatilia habari hizi kwa undani kutoka vyanzo tofauti hivyo perspective yangu na yako ni tofauti.
We can agree to disagree lakini hatuwezi kuwa na disputes katika facts"

Nachotaka kusema hata katika facts tunaweza kutofautiana! Facts zinaweza kabisa kupata tafsiri tofauti! Watu wawili wanaweza kuwa barabarani pande tofauti na kuiona ajali ilitokea, ukiwauliza watakubal;i ajali imetokea, lakini maelezo yao yanaweza kuwa tofauti kabisa! Kwa namna walivyoiona ajali hiyo! Ndivyo ilivyo katika historia ya Middle East....

Hivyo ndugu yangu tunaweza kuwa na disputes katika facts! Wanazuoni nguli wa pande zote, Wayahudi na Waarabu wanazielezea facts muhimu katika sakata la Waarabu na Wapelestina kwa jinsi tofauti kabisa.....Ungepata nafasi soma vitabu hivi:

requently bought together​


Righteous Victims: A History of the Zionist-Arab Conflict, 1881-2001

This item: Righteous Victims: A History of the Zionist-Arab Conflict, 1881-2001


+
Hundred Years' War on Palestine
Hundred Years' War on Palestine


+
The Iron Wall: Israel and the Arab World
The Iron Wall: Israel and the Arab World


Ukimsoma Benny Morris (Myahaudi) na mwanazuoni wa Kipalestina, Rashid Khalidi wanazungumzia facts za kihistoria katika mgogoro huu, lakini tafsri zao ni tofauti kabisa.....Kwa mfano Partition Plan ya UN 1947 lila upande unaeelezea kwa mtazamo tofauti kabisa! Kitu ni kile kile (facts) lakini tafsri ni tofauti!

Nachotaka kusema mkuu, mgogoro huu si rahisi kama wengi wanavyoshabikia hamu, wengi mno hawajui chochote! Na kwa upande wa Tanzania, sidhani historia hii hata inafundiswa popote pale, labda kwa wale waliochukua mchepuo huo wa somo la historia chuo kikuu, wengi ni hadithi wanazosimuliwa Kanisani na Misikiti tu! Hawawezi kabisa kusimamisha hoja zao za hata kwa facts za Kihistoria.
 
Viburi vya watu vipo nyuma ya keyboard ila tusiombee vita hata siku Moja.
 
Back
Top Bottom