Israel na Hamas wakubali kusitisha mapigano eneo la Gaza

Israel na Hamas wakubali kusitisha mapigano eneo la Gaza

Ila yalioanza baada ya October 7 yamekuwa ya kinyama mno Karne hii.

Hamas hawawezi kukwepa lawama
Kwa mtizamo mwingine ni kama malengo ya Hamas yametimia japo kwa kumwaga damu sana.

Maana lengo la shambulizi la October 7 lilikuwa kupata mateka ambao watawatumia kama kete ya kukomboa wenzao walioshikiliwa na Israel. Na hiki ndo kimetokea sasa
 
Ila inaonekana Hamas wana ngome imara sana, sikutegemea kama mateka wa kiisrael bado wako hai wameshikiliwa mahali jeshi la Israel lilishindwa kufika
Halafu wameshikiliwa hapohapo Gaza, natamani sana kupata taarifa za kina kuhusiana na hilo maana Hamas wamenishangaza sana.

Israel wameigeuza Gaza juu chini lakini hadi wanafikia makubaliano hawajawahi kugundua walipo mateka, Hamas nimewavulia kofia.
 
Ila yalioanza baada ya October 7 yamekuwa ya kinyama mno Karne hii.

Hamas hawawezi kukwepa lawama
Hakuna mauaji mazuri na mabaya yote ni mauaji,kabla ya October 7 Israel ilikuwa inauwa wasitani wa wapalestina 800 kwa mwaka mamia wengine walikuwa wanabomolewa makazi yao na kunyanganywa ardhi yao ,mamia wengine wakiwemo watoto walikuwa wanapekwa jera

Hamas hawezi kuraumiwa kwa sababu tukio la October 7 lilikuwa ni muendelezo wa mgogoro na mgogoro hakuanzishwa na Hamas bali wao wali urithi tu.
Wewe na familia yako mngekuwa kwenye nafasi ambayo wapalestina wapo wala usinge jaribu kuandika hili ulilo liandika na ndio maana mpaka sasa pamoja na maafa yote bado hakuna mpalesitina yeyote aliye walaumu Hamas kwa wanacho kipitia.

Na bahati mbaya usidhani kuwa vita hii ndo ya mwisho kati ya Israel na makundi ya kipalesitina eti kwa sababu ya maafa yaliyo tokea kwenye vita hii ya sasa.

Ili mladi kiini cha mgogoro hakija tatuliwa basi vita italipuka tena huko mbele na wenda ikawa na maafa makubwa haya yakawa cha mtoto.
 
Kwa mtizamo mwingine ni kama malengo ya Hamas yametimia japo kwa kumwaga damu sana.

Maana lengo la shambulizi la October 7 lilikuwa kupata mateka ambao watawatumia kama kete ya kukomboa wenzao walioshikiliwa na Israel. Na hiki ndo kimetokea sasa
Nakiri, leo ndio nimeelewa umuhimu wa mateka wa kivita.

Bila hawa mateka ingekuwa vigumu Israel kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano.
 
Halafu wameshikiliwa hapohapo Gaza, natamani sana kupata taarifa za kina kuhusiana na hilo maana Hamas wamenishangaza sana.

Israel wameigeuza Gaza juu chini lakini hadi wanafikia makubaliano hawajawahi kugundua walipo mateka, Hamas nimewavulia kofia.
Yaan hilo ndo linalonishangaza zaidi, inaonekana Hamas walijipanga sana kabla ya kutekeleza shambulio lao kwa Israel October 7.

Halafu walivyo wasiri khs chimbo lao la mateka wa israel, nilitegemea kupitia ule mpango wao wa awali walipobadilishanaga mateka, nilijua IDF watajua mateka walikofishwa. Kumbe wapiii pamoja na technology yote hiyo ya mwisrael, duuh hawa jamaa noma
 
Nakiri, leo ndio nimeelewa umuhimu wa mateka wa kivita.

Bila hawa mateka ingekuwa vigumu Israel kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano.
Ooh pole sisy, shida wengi humu wanashabikiaga kimahaba zaidi pasipo kujua uhalisi wa mambo. Mbona ndo ulikuwaga mpango wao wa kutekeleza lile shambulio la October 7.
Walikuwa smart sana ktk kuuandaa na kuutekeleza. Sema hawakutegemea Israel ata-react kama alivyofanya. Wao walijua Israel kwavile inaonaga raia wake wanathamani sana kuliko wapalestina, basi itakuja moja kwa moja mezani kwa mazungumzo na siyo kuja kwa njia ya vita.
 
Ooh pole sisy, shida wengi humu wanashabikiaga kimahaba zaidi pasipo kujua uhalisi wa mambo. Mbona ndo ulikuwaga mpango wao wa kutekeleza lile shambulio la October 7.
Walikuwa smart sana ktk kuuandaa na kuutekeleza. Sema hawakutegemea Israel ata-react kama alivyofanya. Wao walijua Israel kwavile inaonaga raia wake wanathamani sana kuliko wapalestina, basi itakuja moja kwa moja mezani kwa mazungumzo na siyo kuja kwa njia ya vita.
Upo saaai mkuu lkn Hamas wa nawao wamebadilika wanakuwa na Mipango A na B kutegemea Israel atachagua upi sababu tumeona Israel ikipokea misaada ya kijesh kutoka washilika, Hamas ata chakula tu nishida kuingia GAZA lkn jamaa awajawai ishiwa silaha!!!!!!
 
Malengo ya Israel huko Gaza, pili Lebanon (Hezbollah), na tatu Syria yamefanikiwa kwa 100%. Yemen (Houthi) in good progres. Kubwa lao (Iran) limelemazwa kwa kiwango cha kutisha. So, with that in mind, Israel kubadili msimamo ni sahihi.

Lebanon imepata rais, uongozi wa Syria umebadilishwa, cream ya makundi ya kigaidi tishio kwa Israel (Hezbollah & Hamas) imefyekwa, Israel imejitwalia maeneo for military strategic reasons hayo ni mafanikio ya kupigiwa mfano katika medani za kijeshi. Majeshi duniani yakajifunze Israel!
Kama Hamas na hizbullah zimefyekwa,hayo makubaliano kule lebanon na Gaza israel kafanya na nani!?..akili zenu bana!!
 
Kwa mtizamo mwingine ni kama malengo ya Hamas yametimia japo kwa kumwaga damu sana.

Maana lengo la shambulizi la October 7 lilikuwa kupata mateka ambao watawatumia kama kete ya kukomboa wenzao walioshikiliwa na Israel. Na hiki ndo kimetokea sasa
Ila kwa Gharama na vifo kuliko wanaowakomboa
 
Kwa mtizamo mwingine ni kama malengo ya Hamas yametimia japo kwa kumwaga damu sana.

Maana lengo la shambulizi la October 7 lilikuwa kupata mateka ambao watawatumia kama kete ya kukomboa wenzao walioshikiliwa na Israel. Na hiki ndo kimetokea sasa
Wametoa sharti la kuachiwa wafungwa 250 wa kipalestina waliofungwa maisha israel,hao ni Hamas ileile,lakini kuna kikao cha dunia oslo kujadili taifa huru la palestina, wakati huohuo blinken kawazodoa waisrael wasidhani palestina wataacha mapambano kwa kuuawa njia pekee ya amani ya kweli ni palestina kuwa na taifa lao,kule Qatar wanaongelea taifa la palestina,hapa washindi Hamas na bwana sinawar atajengewa sanamu palestina
 
Ila inaonekana Hamas wana ngome imara sana, sikutegemea kama mateka wa kiisrael bado wako hai wameshikiliwa mahali jeshi la Israel lilishindwa kufika
Nah. Wala haiko hivyo.

Israel ilikuwa inajua mateka wako wapi.

Na IDF haikushindwa kwenda kuwaokoa.

Shida ilikuwa ni dynamics za mazingira.

Israel ilikuwa inajua walipo mateka. Na ilikuwa inajua wako hai.

Sasa kujua wako wapi hao mateka na kujua wako hai, haimaanishi ndo unaenda tu kichwa kichwa kama huna akili timamu.

Lengo la Israel lilikuwa ni kuwarudisha kwa wapendwa wao hao raia wake waliotekwa na Hamas ingali wakiwa hai.

Sasa watu mnajua mateka walipo. Na mnajua Hamas wanawatumia kama leverage katika majadiliano [negotiations].

Mnajua wako chini ya Hamas. Hamas ambao wako tayari kufa kwa kujitoa mhanga.

Mnayajua yote hayo. Ndo mtaenda kichwa kichwa bila kutumia akili?

Mkifanya hivyo, lengo lenu litashindwa.

Mkivamia mahali walipo, mateka watauliwa. Na Hamas ama watajiua wenyewe au mtawaua nyinyi.

Sasa hapo mtakuwa mmefanikiwa nini katika lengo lenu la kuwarudisha mateka kwa familia zao wakiwa hai?

Kiteknolojia, na kwa msaada wa Marekani, Israel iko mbali sana.

Na Gaza ni eneo dogo.

Lakini wakati mwingine mazingira yanakuwa hayaruhusu baadhi ya operations kulingana na malengo mliyonayo.

Israel ina uwezo wa ku carpet bomb Gaza yote. Haishindwi hata kidogo kufanya hivyo.

Lakini, mtu yeyote mwenye akili hawezi kufanya hivyo huku akijua watu wake ambao bado wako hai, wapo pia kwenye hilo eneo na yeye lengo lake ni kuwapata wakiwa hai.

Israel iliyoweza kupenya katikati ya Tehran na kumuua kiongozi wa Hezbollah, haishindwi kuisafisha Gaza nzima ambayo ni eneo dogo sana.

 
Hawatakaa warudie huo upuuzi wa kushambulia...Sasa hiv wakajikite kurudisha miundo mbinu na wakae kwa kutulia..tofaut na hapo ni kichapo tu
 
Wananchi wa Gaza wamefurahi na kuandamana barabarani hii inaonesha wananchi wa kawaida hawataki vita
Of course!

Miscalculation na pia hardheadedness Hamas imewaponza raia wa Gaza.

In the grand scheme of things, [Hamas] hakuna walichofanikiwa.

Wapalestina zaidi ya 50,000 wameuliwa. Na si ajabu idadi halisi ni zaidi ya hapo.

Gaza imerudishwa zama za mawe.

Viongozi waandamizi wa Hamas karibu wote wameuliwa.

Wamefaidika na nini sasa hapo?

Upumbavu wa Hamas umewaponza raia wa kawaida wa Gaza.
 
Nah. Wala haiko hivyo.

Israel ilikuwa inajua mateka wako wapi.

Na IDF haikushindwa kwenda kuwaokoa.

Shida ilikuwa ni dynamics za mazingira.

Israel ilikuwa inajua walipo mateka. Na ilikuwa inajua wako hai.

Sasa kujua wako wapi hao mateka na kujua wako hai, haimaanishi ndo unaenda tu kichwa kichwa kama huna akili timamu.

Lengo la Israel lilikuwa ni kuwarudisha kwa wapendwa wao hao raia wake waliotekwa na Hamas ingali wakiwa hai.

Sasa watu mnajua mateka walipo. Na mnajua Hamas wanawatumia kama leverage katika majadiliano [negotiations].

Mnajua wako chini ya Hamas. Hamas ambao wako tayari kufa kwa kujitoa mhanga.

Mnayajua yote hayo. Ndo mtaenda kichwa kichwa bila kutumia akili?

Mkifanya hivyo, lengo lenu litashindwa.

Mkivamia mahali walipo, mateka watauliwa. Na Hamas ama watajiua wenyewe au mtawaua nyinyi.

Sasa hapo mtakuwa mmefanikiwa nini katika lengo lenu la kuwarudisha mateka kwa familia zao wakiwa hai?

Kiteknolojia, na kwa msaada wa Marekani, Israel iko mbali sana.

Na Gaza ni eneo dogo.

Lakini wakati mwingine mazingira yanakuwa hayaruhusu baadhi ya operations kulingana na malengo mliyonayo.

Israel ina uwezo wa ku carpet bomb Gaza yote. Haishindwi hata kidogo kufanya hivyo.

Lakini, mtu yeyote mwenye akili hawezi kufanya hivyo huku akijua watu wake ambao bado wako hai, wapo pia kwenye hilo eneo na yeye lengo lake ni kuwapata wakiwa hai.

Israel iliyoweza kupenya katikati ya Tehran na kumuua kiongozi wa Hezbollah, haishindwi kuisafisha Gaza nzima ambayo ni eneo dogo sana.

Acha porojo,kuna kipindi israel waliamini mateka wapo misri na Lebanon,wakashangaa wanatokea Gaza,kuna mateka waliuawa na IDF wenyewe bila kujua,mara ngapi idf wamefukua makaburi Gaza kutafuta mateka chini ya makaburi!?
 
Back
Top Bottom