Israel na Hamas wakubali kusitisha mapigano eneo la Gaza

Israel na Hamas wakubali kusitisha mapigano eneo la Gaza

Kwa kichapo walichokipata, naamini sasa watashika adabu zao.

Ni uzuzu kuanzisha zali ambalo mikikimikiki yake huwezi kuistahimili.
Unajua idadi ya askari israel waliouawa au kulemazwa,hadi kupelekea kuhitaji askari wengine (recruit) ,hata waliokua exempted jeshini wamelazimishwa kuingia, mjadala sasa duniani ni taifa huru la palestina,si oslo si korido za ikulu marekani, hukumsikia blinken juzi?!.. kwenye hili Hamas wameshinda,wameionesha dunia israel si proper army zaidi ya propaganda
 
Acha porojo,kuna kipindi israel waliamini mateka wapo misri na Lebanon,wakashangaa wanatokea Gaza,kuna mateka waliuawa na IDF wenyewe bila kujua,mara ngapi idf wamefukua makaburi Gaza kutafuta mateka chini ya makaburi!?
Sasa porojo ziko wapi katika niliyoyaandika?

Watu wengine bana. Hebu ziorodheshe hapa hizo porojo basi….
 
Unajua idadi ya askari israel waliouawa au kulemazwa,hadi kupelekea kuhitaji askari wengine (recruit) ,hata waliokua exempted jeshini wamelazimishwa kuingia, mjadala sasa duniani ni taifa huru la palestina,si oslo si korido za ikulu marekani, hukumsikia blinken juzi?!.. kwenye hili Hamas wameshinda,wameionesha dunia israel si proper army zaidi ya propaganda
Okay, sawa.

Hamas imeshinda na Israel imeshindwa na viongozi wote waandamizi wa Israel wameuliwa na Hamas.
 
Muda mchache uliopita taarifa kubwa kwenye vyombo vya habari vyote vya Kimataifa Aljazeera, CNN na nk ni juu ya Makubaliano ya Kusitisha Mapigano kati ya Israel na Hamas.

Kufikiwa kwa makubaliano haya kumefanya wakaazi wa Gaza kushangilia na kuandamana barabarani kwa furaha na vifijo.

Israel na Hamas wamefikia makubaliano ya kusitisha mapigano kwa lengo la kumaliza miezi 15 ya mzozo katika Ukanda wa Gaza. Makubaliano haya, yaliyosimamiwa na Qatar, Misri, na Marekani, yanafanyika kwa awamu tatu ndani ya wiki sita.
Awamu ya Kwanza: Hatua za Haraka
• Kusitisha Mapigano: Kusitisha mapigano kwa muda kutaanza Jumapili, Januari 19, 2025, na kusitisha vita vilivyokuwa vikiendelea.
• Kubadilishana Wafungwa na Mateka: Hamas itawaachilia mateka 33 wa Kiyahudi, wakiwemo wanawake, watoto, na wazee. Kwa upande mwingine, Israel itawaachilia mamia ya wafungwa wa Kipalestina.
• Msaada wa Kibinadamu: Makubaliano yanaruhusu msaada wa kibinadamu kupelekwa Gaza, ambapo malori 200 ya misaada yatapita kila siku.

Awamu ya Pili: Kuachiliwa Zaidi na Kuondolewa kwa Jeshi
• Kuachiliwa Zaidi kwa Mateka: Majadiliano yataendelea kwa ajili ya kuachiliwa mateka waliobaki, wakiwemo wanajeshi wa Kiume, kwa kubadilishana na wafungwa wa Kipalestina.
• Kuondolewa kwa Jeshi la Israel: Israel itaanza kuondoa majeshi yake kutoka maeneo yenye watu wengi Gaza, ili kuruhusu Wapalestina waliokimbia kurudi nyumbani.

Awamu ya Tatu: Ujenzi Mpya na Kusitisha Mapigano ya Kudumu
• Jitihada za Ujenzi Mpya: Mipango itatekelezwa kwa ajili ya ujenzi mpya wa Gaza, ikilenga kurejesha miundombinu na kusaidia raia walioathirika.
• Majadiliano ya Kusitisha Mapigano ya Kudumu: Mazungumzo yatalenga kuanzisha amani ya kudumu kwa kushughulikia masuala ya msingi ili kuzuia migogoro ya baadaye.

Makubaliano haya yamepokelewa kwa hisia tofauti. Waisraeli wengi wanaunga mkono makubaliano hayo kwa sababu yanatoa kipaumbele kwa kuachiliwa kwa mateka. Hata hivyo, baadhi ya wanasiasa wa mrengo wa kulia wa Israel wanapinga, wakihofia kuwa yanaweza kudhoofisha juhudi za kumaliza Hamas.

Kwa upande mwingine, wakaazi wa Gaza wameonyesha matumaini kuwa makubaliano haya yataleta amani na fursa ya ujenzi mpya.

Kufikiwa makubaliano haya unategemea ahadi ya pande zote kufuata masharti na kushiriki kikamilifu katika mazungumzo ya awamu zinazofuata.
Tumewachoka, wangeachwa tu waendelee kuuana
 
HAMAS alitaka kuachia awa mateka tangu mwanzo lkn kibri cha Netanyahu kimefanya mateka kibao kufa IDF kibao kufa tena vijana wadogo baada ya majanga yoteeee!! ayo ndio Netanyahu anabaini HAMAS ni fupa gumu kwa IDF kulishinda sasa kakubali yaleyale aliokataa mwanzooo! YEMEN NDIO IMECHANGIA PAKUBWA HII AMAN.!!!!
Uwezo wa hamas,Hizbullah na ,Iran umeporomoka sn kuweza kuisumbua Israel. Pis anguko la Assad ni kutokana na athari za vita vya Gaza. Israel imeweza kudhoofisha maadui na kuwafanya wafikirie upya jinsi gani ya kupambana na mayahudi. Mwisho kabisa,Nada ya vita viongozi wengi wajuu wa hizbullah na Hamas Nasrallah,Haniya,Sinwar nk wamefyekwa. Wapalestina zaidi ya elf 40 wamekufa na malaki kujeruhiwa. Baada ya vita hamas lazima
 
Uwezo wa hamas,Hizbullah na ,Iran umeporomoka sn kuweza kuisumbua Israel. Pis anguko la Assad ni kutokana na athari za vita vya Gaza. Israel imeweza kudhoofisha maadui na kuwafanya wafikirie upya jinsi gani ya kupambana na mayahudi. Mwisho kabisa,Nada ya vita viongozi wengi wajuu wa hizbullah na Hamas Nasrallah,Haniya,Sinwar nk wamefyekwa. Wapalestina zaidi ya elf 40 wamekufa na malaki kujeruhiwa. Baada ya vita hamas lazima
Halafu unaambiwa eti Hamas wameshinda 🤣.

That kind of breathtaking stupidity is what led to their demise!

Hamas hawatorudia tena kuichokoza Israel kwa scale ya Oct. 7.
 
Hamas: Ceasefire Agreement is an Achievement for Our People and Resistance

Jan 15, 2025 The ceasefire agreement is an achievement for our people, our resistance, our nation, and the free people of the world. The ceasefire agreement is the result of the legendary resilience of our people and the heroic resistance in Gaza over more than 15 months. The agreement comes in response to our responsibility […]
Read on »
 
Israel IMESHINDWA
Hakuna makubaliano kati ya mshindi na mshingwa !!!!
Really? 🤣

IMG_7446.jpeg


IMG_7445.jpeg
 
Lengo lilikuwa kuiangamiza hamas je hamas imeangamia? Hezbollah wamesharudi kwenye mipaka ya kusini mwa Lebanon kama mwanza


Kiufupi Israeli hapo hajaambulia kitu na hamas inastahili ushindi coz imeizuia Israeli isifanye mageuzi ya kiutawala hapo ghaza
Mjomba chutama. Hiv unajua ukiachia yote Israel haitatoa jeshi ukanda wa filadefia mzee. Hiv unajua Israel imejiongezea eneo la kiulinz pale Golan height mkuu, hiv unajua Israel imejiongezea eneo katika na imeruhusu nyumba elfu 3 kujengwa upande Samaria na Judea mzee. Nakukumbusha tu. Kama vile hamas hawaish kwakuwa wanazaliwa kila siku, jews nao hawaish coz nao wanazaliwa kila siku. Binafs ninamshuluru Mungu hii vita issue maana kama kichapo Gaza imechapika na watu mateso wameyapata kweli kweli. Na usisahau wazir wa ulinz by then aliwaahid kuwa atakachokifanya hapo Gaza hawatakisahau miaka 50.
 
Kiukweli hua napenda kuingia nyuzi za hivi na kusoma jinsi waTz tunajaribu kuchambua kila kitu. Ingawa kati yetu hakuna mpiganisha vita, hakuna military strategist ni knowledge ya conspiracy theories, udini na movies za Jason Bourne ndiyo zinawapa watu uwezo wa uchambuzi.

Funny 😂
 
Kifo cha huyo mwanajeshi ndiyo ishara ya ushindi kwa Israel?
Ni mojawapo ya ishara!

Ishara nyingine ni Gaza. Kumebaki kifusi tu.

Ishara nyingine ni Syria na Assad.

Ishara nyingine ni Tel Aviv, Jerusalem, na Haifa zipo intact na watu wanaendelea na maisha yao vizuri tu.

Ishara nyingine ni Benjamin Netanyahu, Yoav Galant, Itamar Ben Gvir, Israel Katz, Ron Dermer, etc., bado wapo hai.

Ilhali, Ismaili Haniyah, Yahaya Sinwa, Hasani Nasrala, Fatah Sharrif, Nabil Kaouk, Fuad Shukr, Mohamed Deif, etc., wapo peponi wakivitomasa vibinti vibikira.
 
Baada ya vifo vingi vya Wapalestina na baada ya Sinwar na Haniyah kuuawa ndio makubaliano yamefikiwa.

Hamas imewaletea Wapalestina maafa.

Sinwar nasrallah Adiosamigo and 100 others
Sawa amini utakavyo ukweli Israel kadharaulika vibaya sana duniani kote, hajui vita anacho jua ni genocide kwa kutumia silaha za US na European.

Ikiwa unadhani Israel kashinda hi vita nenda katazame deni lake kabla ya vita, na sasa. Ikiwa unadhani Israel anaogopwa tena pale Middle East nenda kapime akili zako. Israel kaisha onekana ni dhaifu sana ule uwongo eti anga lake huwezi kupenya halipo tena kumbe ni nyumba ya baibui, pia US kachakazwa na Yemen pale Red Sea. Weka akilini kwako silaha hata uwe nazo vipi huwezi kuwashinda wanaume wa Hamas, Hezbullah na Ansarlah wa Yemen(Al Houth)
 
Ni mojawapo ya ishara!

Ishara nyingine ni Gaza. Kumebaki kifusi tu.

Ishara nyingine ni Syria na Assad.

Ishara nyingine ni Tel Aviv, Jerusalem, na Haifa zipo intact na watu wanaendelea na maisha yao vizuri tu.

Ishara nyingine ni Benjamin Netanyahu, Yoav Galant, Itamar Ben Gvir, Israel Katz, Ron Dermer, etc., bado wapo hai.

Ilhali, Ismaili Haniyah, Yahaya Sinwa, Hasani Nasrala, Fatah Sharrif, Nabil Kaouk, Fuad Shukr, Mohamed Deif, etc., wapo peponi wakivitomasa vibinti vibikira.
Israel haina mwanajeshi kafa?

Israel imeshambuliwa zaidi ya mara mbili pia swala la casualty ni debatable due to info.

Kwa vikundi kama Hamas kiongozi kufa siyo mwisho wa kundi kuendelea. Israel hajaanza leo kufanya target killing ya viongozi wa hivi vikundi.

At some point Hamas waliomba cease fire na walikua radhi kurudisha mateka. Netanyahu akagoma. Hamas wamefanya ambacho walikua radhi kufanya tangu mwanzo.

Israel inashinda ila kinamna fulani inakubali kusitisha mapigano?
 
Israel haina mwanajeshi kafa?

Israel imeshambuliwa zaidi ya mara mbili pia swala la casualty ni debatable due to info.

Kwa vikundi kama Hamas kiongozi kufa siyo mwisho wa kundi kuendelea. Israel hajaanza leo kufanya target killing ya viongozi wa hivi vikundi.

At some point Hamas waliomba cease fire na walikua radhi kurudisha mateka. Netanyahu akagoma. Hamas wamefanya ambacho walikua radhi kufanya tangu mwanzo.

Israel inashinda ila kinamna fulani inakubali kusitisha mapigano?
Upande wa Israel waliokufa ni wachache sana.

Hamas viongozi wa juu wote wamefyekwa fye fye fye.

Hizbollah wao wamelipuliwa puumbu.
 
Kwa mtizamo mwingine ni kama malengo ya Hamas yametimia japo kwa kumwaga damu sana.

Maana lengo la shambulizi la October 7 lilikuwa kupata mateka ambao watawatumia kama kete ya kukomboa wenzao walioshikiliwa na Israel. Na hiki ndo kimetokea sasa
sasa unataka kuokoa let's say mateka 400 at the same time unakwenda kupoteza watu 460000+ pamoja na viongozi wote waandamizi jumlisha miundo mbinu na kufanya Gaza kuwa kama fuvu sasa ina faida gani.Hii iwe fuzo kwa kizazi kijacho hapo Gaza kwamba ukiichokoza Israel kuna gharama zake watabeba.
 
sasa unataka kuokoa let's say mateka 400 at the same time unakwenda kupoteza watu 460000+ pamoja na viongozi wote waandamizi jumlisha miundo mbinu na kufanya Gaza kuwa kama fuvu sasa ina faida gani.Hii iwe fuzo kwa kizazi kijacho hapo Gaza kwamba ukiichokoza Israel kuna gharama zake watabeba.
Akili za Hamas na hawa wafuasi wao, hazina akili kabisa.
 
Back
Top Bottom