Jacqueline Mengi aendelea kudondokea pua rufaa, mahakama yaondoa maombi yake ya kutaka kuurudisha wosia

Jacqueline Mengi aendelea kudondokea pua rufaa, mahakama yaondoa maombi yake ya kutaka kuurudisha wosia

Kuna wanawake na majini, Ingawa mi ni mwanamke but I can't do that kwa visivyo halali yangu.. dada mbona mrembo tu.. angekomaa tu walau apate hata tumilioni milioni tu jamani na wale watoto.

Au ndo anataka awe first woman billionaire in Tanzania?!! Daaah
Huyo Golddiger wa kufa na kuzikana.
Mtoto mmoja wa kigogo anamjua vizuri,alitaka kuoa baada ya shughuli zoote imebaki siku 1 harusi Jack katoroka na mzungu mmoja tapeli tu la madini kwenda South,
Katumika sana huko badae ndo karudi bongo kawa mwimbaji
 
Huyo Golddiger wa kufa na kuzikana.
Mtoto mmoja wa kigogo anamjua vizuri,alitaka kuoa baada ya shughuli zoote imebaki siku 1 harusi Jack katoroka na mzungu mmoja tapeli tu la madini kwenda South,
Katumika sana huko badae ndo karudi bongo kawa mwimbaji
Kinje huyo nadhani enzi hizooo...mjanja mjanja sana Jacky Toka enzi hizooo

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Pole yake daah ...wagawane tu pasu pasu na mke mwenziwe kulingana na idadi ya watoto yaishe..

Wasije kuleta uadui baina ya watoto wakaja kuuana bure
 
Nae,anashindwaje kulea watoto wawili kwa kuuza nyanyachungu kwenye sinia?!....ndo tamaa za pesa zinavyoponza....unakosa kula ujana na kijana mwenzio unakimbilia zee coz of money.....utumwa,utumwaaa
Tena familia inasomesha watoto ist haina shida ,shida ilianza alivohamia Dubai Sasa akataka wasomeshwe kule Tena shule za kishua zile ndo hapo wakagoma then child support karibu millions of shillings


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Uyo jack ni boya nambari moja kitendo cha kuwa na mengi ni connection tosha kwake kipindi kile alitakiwa awe milionea mda huu siyo kugombea mali na watoto, angeanzisha miradi ya mahana ya pesa nyingi mzee angekuwa ana mpush tu mpaka mzee kufariki muda huu angekuwa milionea ..yeye alijua ataishi na mengi milele[emoji23][emoji23][emoji23]
Akili bro sio Kila mtu ana hyo akili,Hilo aliweza madam ritta wa BSS na yule Lilian,wengine wameshia magari TU
Jack Bado anataka uvip maana enzi mzee yupo alikua anahudumiwa kispecial mpk airport alikua anakaa vip lounge n.k Sasa hivi Kawa normal tu ndo maana anavurugwa mnoo!
So anajua akiwa billionaire atarudi tu kwenye Ile nafasi ya kibosi bosi

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huyu dada tamaa ya pesa itamfanya apoteze uhai. Amuulize yule mama aliyefariki juzi na wanae kwenye ajali ya gari.Infwakti Yule mama Immaculata Byemerwa kabla ya kuolewa na Engneer alikuwa na yuho mwanae Albert ambae ndo alikuwa dereva. Kaolewa kazaa Janet na Jolister.Na kumbuka kwamba alimkuta Josepahat ana watoto wakubwa .Sasa yule mama kapata ajali na kafariki na uzao wake wote. Kaacha watoto wa mzee wafaidi vizuri mali za baba na mama yao mzazi.
Jack acha tamaa.
[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]kumbeeee

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huyo Golddiger wa kufa na kuzikana.
Mtoto mmoja wa kigogo anamjua vizuri,alitaka kuoa baada ya shughuli zoote imebaki siku 1 harusi Jack katoroka na mzungu mmoja tapeli tu la madini kwenda South,
Katumika sana huko badae ndo karudi bongo kawa mwimbaji
Khaa *****
 

Jumamosi, Desemba 3 , 2022

Muhtasari:

Mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, Jacquiline Ntuyabaliwe na wanawe, wamekwama kutetea wosia ulioachwa na marehemu baada ya Mahakama ya Rufani kutupa shauri lake la kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu.


Dar es Salaam. Mjane wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi, Jacquiline Ntuyabaliwe na wanawe, wamekwama kutetea wosia ulioachwa na marehemu baada ya Mahakama ya Rufani kutupa shauri lake la kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu.

Jacquiline alifungua shauri mahakamani hapo la mapitio kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu, iliyokataa wosia uliodaiwa kuachwa na Mengi.
Shauri hilo la mirathi namba 39 ya mwaka 2019, lilifunguliwa na watu wanne, wakiwemo ndugu wa marehemu Mengi.

Mahakama hiyo katika uamuzi wake uliotolewa juzi na jopo la majaji watatu, Rehema Mkuye (kiongozi), Dk Paul Kihwelu na Panterine Kente lilitupa shauri hilo kutokana na kasoro mbili zilizoonekana kwenye kiapo cha Jacquiline na cha wakili wake, Audax Kahendaguza vilivyoambatanishwa katika maombi hayo.

Kasoro hizo ambazo mahakama imekubaliana nazo ni viapo kuwa na maelezo yasiyopaswa kuwemo kwa hoja zinazohitaji ushahidi, maoni, mapendekezo na hitimisho na nyingine ni kutokubainisha chanzo cha taarifa ziliozokuwemo kwenye viapo hivyo.

Mahakama hiyo ilifikia uamuzi huo kutokana na pingamizi la awali lililowekwa na wasimamizi wa mirathi hiyo walioteuliwa na Mahakama Kuu ambao ni Abdiel Reginald Mengi akishirikiana na mdogo wake marehemu Mengi, Benjamin Abrahamu Mengi, kupitia kwa mawakili wao, Michael Ngalo na Roman Masumbuko.

Katika uamuzi huo, mahakama imesema kiapo kinapokuwa na kasoro kama hizo, aya zenye kasoro huondolewa kwenye kiapo na kuendelea na aya nyingine zisizo na kasoro.
Hata hivyo, imesema aya zenye kasoro ndizo msingi wa shauri hilo na kwamba, baada ya kuziondoa zinazobaki haziwezi kusimama zenyewe.
“Kasoro hizo zinayafanya maombi haya kutoweza kusimama, hivyo tunayatupilia mbali. Kwa kuwa shauri linatokana na mirathi hatutoi amri yoyote kuhusu gharama,” imesema mahakama hiyo katika uamuzi huo.

Awali, watu wanne, Benson Benjamini Mengi, William Onesmo Mushi, Zoebu Hassuji na Sylvia Novatus Mushi walifungua shauri la msingi la mirathi Mahakama Kuu wakiomba kuteuliwa kuwa wasimamizi wa mirathi hiyo, kwa mujibu wa wosia ulioachwa na Mengi.
Hata hivyo, Abdiel na Benjamini waliweka pingamizi dhidi ya wosia huo unaompa Jacquiline na wanawe haki ya urithi wa mali za Mengi, wakipinga uhalali wake huku wakiwasilisha jumla ya sababu nne za kuupinga.
Mahakama Kuu baada ya kusikiliza hoja za pande zote ilikubaliana na hoja za pingamizi dhidi ya wosia huo na kuikataa kuwa ni batili.

Jaji Yose Mlyambina alikubaliana na sababu hizo za pingamizi huku akisema unawanyima urithi wanawe wengine (wakubwa, Abdiel na ndugu yake) bila kutoa sababu.

Pia Jaji Mlyambina katika hukumu yake hiyo ya Machi 18, 2021, aliukataa wosia huo akieleza kuwa ziliiingizwa mali za mke wake mkubwa na kwamba nakala yake alikuwa nayo mwenyewe Jacguiline Mengi ambaye alikuwa mnufaika.
Hivyo Jaji Mlyambina aliwateua Abdiel na Benjamini kuwa wasimamizi wa mirathi na akaelekeza mali za marehemu zigawiwe warithi wanaostahili kwa utaratibu wa kawaida kama wa mtu ambaye hakuacha wosia.

Mwananchi
Ana tamaa tu ila na yeye atapata mbona tena pakubwa tu na watoto wake pia,yaani anachofanya ni kuumiza tu wanawe jamani

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom