Pre GE2025 Jaji Warioba: Tusipochukua hatua, uchaguzi mkuu utakuwa kama huu wa Serikali za Mitaa

Pre GE2025 Jaji Warioba: Tusipochukua hatua, uchaguzi mkuu utakuwa kama huu wa Serikali za Mitaa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huyu mzee katumwa kuongea haya, ili akina Mbowe warudi kwenye udanganyifu wa maridhiano.

Huyu mzee ana nafasi ya kuongea na wenye mamlaka ili kuwataka watende anayoyatamani na siyo kulalamika.
Hamna mtu ataridi kwenye mazumgumzo yasiyo na tija.

Mazungumzo ambayo wapinzania wanaweza kurudi mezani labda yawe na nguvu ya kisheria.
 
Ameiongelea ile Kauli...
"Kula kwa urefu wa Kamba"...
😳😳
Mzee kajikoki huyu
 
Huyu mzee katumwa kuongea haya, ili akina Mbowe warudi kwenye udanganyifu wa maridhiano.

Huyu mzee ana nafasi ya kuongea na wenye mamlaka ili kuwataka watende anayoyatamani na siyo kulalamika.
Labda umemfahamu leo mzee Warioba
 
Mzee ana hoja japokuwa atapuuzwa.
Wenye tamaa zao za madaraka wanam-zoom tu.
Ijapokuwa ukianza kusikia matamko ya wazee kama haya means there something is likely to happen au kuna watu wanapewa taarifa kuwa waache kutumika wasimamie weledi wa kazi zao
CCM sababu wamekosa mshipa wa aibu watasema mzee kaanza kukosa kumbukumbu - umri.
Ila kwa kweli JAJI kwa hoja zake zote kaliponya Taifa, Mzee yupo vizuri saana- ukiwa na wazee walau 50 tu wa namna hii katika nchi basi Serikali yako haiyumbi.
 
Msimamo wa kinafiki. Trust me anatumika.

Mbona alikuwa waziri mkuu na hakuibadili katiba hii mbovu? Kumbuka yeye ni mwanasheria, iweje atake mabadiliko akiwa nje ya ofisi?
Haujui mchango wake kwenye upatikanaji wa katiba mpya?
 
Nimeandika msg sasa hivi lakini imepotea. Inabidi niandike msg nyingine,kivingine.
Yaani Jaji Warioba ameongea kwa sababu wako kimya kuhusu swala.
Kwa hiyo anataka mjadala uendelee.
Ukimpinga,ndio anachotaka. Let us talk about this.
Lakini ukianza kutukama na kusema utamwita Makonda amshike shati( tena) that is disrespectful.
Hata hivyo mimi sikusikiliza Jaji Warioba amesema nini.
I am just vaguely aware kwamba analalamika kidogo kuhusu utendaji kazi wa TISS na Polisi katika Uchaguzi wa wiki iliyopita.
Polisi ni lazima watakuwa cautious.
Mtu katekwa,katekwa na nani.?
Labda katekwa na KMKM.
Kwa hiyo uchunguzi wa jambo lolote lazima uwe cautious.
 
Msimamo wa kinafiki. Trust me anatumika.

Mbona alikuwa waziri mkuu na hakuibadili katiba hii mbovu? Kumbuka yeye ni mwanasheria, iweje atake mabadiliko akiwa nje ya ofisi?
kama hajafanya hayo akiwa ofisini basi Hana haki ya kuyasemea hayo?
 
Mzee wetu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Jaji Joseph Sinde Warioba, Nampenda na kumkumbali sana sana,

Maelezo, maoni, tahadhari nk nk alizozitoa mzee wangu je Jukwaa alilotumia ni sahihi kiasi gani?

Je Mzee wangu kwani si member wa Baraza la usalama wa taifa?

Je kama ni member wa Baraza la usalama wa taifa wao kama wazee wastaafu waliolitumikia hili taifa kwa jasho damu na kwa nguvu zao zote na baadaye kutengeneza viongozi hata hawa wa sasa Wameshindwa je kukaa wao kwanza wastaafu wa hilo Baraza, kisha yale ambayo wanaona watawala hawako sawa wakutane ana kwa ana na Rais, Waziri mkuu, Mkurugenzi mkuu wa usalama wa taifa, CDF na IGP waambie ukweli na hali halisi anavyoona wao,
Je hii ya kutoka hadharani tena mstaafu mmoja tu rais na watu wake watafanyia kazi maneno ya mzee wetu?
Angesema haya katika baraza la usalama wa taifa wewe ungesikia maoni yake? Ametumia haki yake ya kikatiba kutoa ,aoni yake. Anayeyapuuza ni kati ya wale wanaojali njaa zao kuliko taifa. Ila mataifa mengi ya ki Africa yamejikuta yakiingia katika machafuko kwa kupuuzia sauti kama hizi. Watu wengine wanamanung`uniko kuhusu chaguzi zetu.
 
Angesema haya katika baraza la usalama wa taifa wewe ungesikia maoni yake? Ametumia haki yake ya kikatiba kutoa ,aoni yake. Anayeyapuuza ni kati ya wale wanaojali njaa zao kuliko taifa. Ila mataifa mengi ya ki Africa yamejikuta yakiingia katika machafuko kwa kupuuzia sauti kama hizi. Watu wengine wanamanung`uniko kuhusu chaguzi zetu.
Mzee wetu Joseph Butiku mwenyekiti wa kigonda cha Mwalimu Nyerere alipiga kelele sana kuhusu swala la Dp World kupewa Bandari yetu, na mimi nakafarijika kuona yupo upande wa wengi tuliokuwa haturidhii DPW kupewa,

je Samia alimsikiliza?
 
..ni mstaafu kwenye chama kinachoharibu uchaguzi na mjumbe kwenye vikao muhim ya chama chake, ni mstaafu wa serikali inayotumia vibaya vyombo ya dola na anashiriki vikao kuongelea mambo ya nchi..ajabu HAJAWAHI kuita aliowaita leo ili atoe angalizo na msimamo wake tabla mambo hayajaharibika, kwa hiyo anasubiri uchaguzi uvurugwe, watu wafe..ndio aongee aliyosema leo, je watu waliouawa watarudi? Uchaguzi ulioharibiwa utarudiwa? Km sio unafiki ni nini hiki anachofanya???
So hatakiwi kuongea? Ukute hana hata nafasi ya kupeleka mawazo Moja Kwa Moja sehemu huska ,

uchawa upo kwenye siasa Kwa maslahi binafsi sio rahisi kisikilizwa. Ametoa tahadhari juu ya kinachoendelea na amerejelea yaliyotokea Zanzibar.

Fair competition haikuwepo ni chuki tu inazidi kutengenezwa siku Hadi siku, na wengine wanafurahia Kwa sababu ni chama chao labda au Kwa sababu zao binafsi nyingine,

Si jambo la kufarahia hata kidogo. Mikakati pamoja na maelekezo ya kufanya dosari hizi inawezekana ilianza tokea wakati wa kuteua waandikishaji kisha kuteua wasimamizi wa uchaguzi.
Yakinyamaziwa haya mapema kunahatari zaidi huko mbeleni .
 
Msimamo wa kinafiki. Trust me anatumika.

Mbona alikuwa waziri mkuu na hakuibadili katiba hii mbovu? Kumbuka yeye ni mwanasheria, iweje atake mabadiliko akiwa nje ya ofisi?
Kila jambo Kwa wakati wake ndugu, kwani wewe huoni yanayoendelea?Hii kasumba ya kupuuzia watu wengine inatokea wapi?
 
Back
Top Bottom