Jakaya Kikwete: Hayati Rais Mwinyi ndiye aliyenifikisha hapa nilipo leo

Jakaya Kikwete: Hayati Rais Mwinyi ndiye aliyenifikisha hapa nilipo leo

Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika kuhani msiba wa Hayati Ali Hassan Mwinyi huko Mikocheni Dar es Salaam ameonekana akiwa na huzuni kubwa sana na masikitiko makubwa akiwa anaongea na vyombo vya habari

Jakaya Kikwete amekiri kuwa yeye hakuwa lolote bali alikuwa katibu wa kawaida wa CCM wilaya ya Masasi huko Mtwara mara baada ya kutoka jeshini miaka hiyo ya 1980's

Kwa mujibu wa Jakaya Kikwete: Rais Mwinyi kwa maono yake ndiye aliyeamua kumtoa huko kijijini Masasi na kumpa ubunge wa viti maalum na baadae kumteua kuwa Naibu Waziri

Jakaya kikwete amesisitiza kwa yeye ni msiba mzito sana kwani amepoteza mtu muhimu kwenye maisha yake aliyamfikisha mpaka hapa alipo kwa sasa

Baada ya maneno hayo ya kukiri kutolewa kijijini Masasi na kuingizwa kwenye mfumo na hayati Rais Mwinyi, Jakaya Kikwete hakutaka kuulizwa maswali mengine toka kwa waandishi wa habari kutokana na majonzi aliyokuwa nayo
Huo ndio ukweli, ila dini yake ilimsaidia. Alimteua kuwa mbunge, akampatia uwaziri wa Nishati, Maji na Madini 1994. JK alivyo na tamaa akagombea urais 1995.
 
Ni kawaida ya mtu mnafiki na mwenye ghilba daima kupenda kuonekana ni mwema zaidi na anapendwa zaidi.

Ila kwa Kikwete hampati mtu tena. Ulimwengu wote unamjua kwa unafiki wake.
Mnafiki ni wewe
 
Hapo kwenye kuwa bright nakataa kwani 99% ya aliosoma nao hasa Chuo Kikuu wanasema alikuwa Mchovu kama akina Fred Michael na Papa Job wa Simba SC.
Kwa akili za kishuleshule huo ndo mtazamo wako. Yaani kuwa bright ni kufaulu masomo ya darasani.
Kwa hiyo kwako wewe matajiri ambao walifeli darasani kwako hao sio bright.
 
Huo ndio ukweli, ila dini yake ilimsaidia. Alimteua kuwa mbunge, akampatia uwaziri wa Nishati, Maji na Madini 1994. JK alivyo na tamaa akagombea urais 1995.
Binadamu, haswa wanaume, tumeumbwa kutafuta zaidi na kushindana zaidi......usiwe bwege wewe. Au mwenzetu umeleft nn mpaka unaongea maneno 'laini laini' kiasi hicho?!!!!

Aliowachagua Nyerere, Mkapa na Magufuli walibebwa na 'uwezo' wao.
Aliowachagua Mwinyi, Kikwete na Samia walibebwa na 'dini' yao. Haya, mbarikiwe binadamu nyie. Siye tunawaombea kheri tu.
 
Rc Ukiwaona Mwinshehe Ditopile Mzuzuri ndiye aliyemtengenezea cross pass kwa kumtambulisha kwa Rais Hayati Mwinyi !
Kwahiyo Swahiba wake ndiye hasa aliyeanzisha ile move iliyompandisha mhe Kikwete !
Na huyo sio mwingine bali ni Ukiwaona Mwinshehe Ditopile Mzuzuri !!
Ukweli utatuacha Huru 🙏🙏 !
Umemaliza kila kitu na uzi ufungwe,
 
Amiri Jeshi Mkuu mstaafu na Rais mstaafu wa JMT cheo ambacho kati ya watanzania milioni 60 tuliopo na zaidi ya milioni 100 waliopita ni watu 6 tu ndo walobahatika kukipata
Nchi hii hakuna cheo kama hicho serikalini, kipo chini ya wizara gani hiko cheo?
 
Hamna haja ya kutukanana. JK amefanya kazi Masasi ambako alihamia kutokea Nachingwea. Na aliteuliwa kuwa mbunge akiwa katibu wa CCM wa wilaya ua Masasi mbona hilo liko wazi mkuu!!
Kaka uko sahihi kabisa!

Mimi nilikua natetea kwamba Kikwete kafanya kazi Nachingwea kama Katibu wa CCM Wilaya,Masasi alihamishiwa na sidhani hata mwezi alimaliza akateuliwa kua Naibu Waziri!

1. Nimewahi fanya kazi Lindi na Mtwara,pale Nachingwea ofisi za CCM Wilaya jina la Kikwete lipo kwenye orodha ya Makatibu.

2. Lakini Masasi jina la Kikwete halipo kwenye orodha ya Makatibu wa CCM Wilaya ya Masasi,maana yake Kikwete pale Masasi hakukaa kabisa zaidi yakupita tu!

3. Sawa na Maharage Chande,aliteuliwa kuwa MD wa TTCL,kabla hajaanza kazi akapangiwa kazi nyingine ya MD wa Posta,kwa hiyo Maharage Chande hawezi sema alikua MD wa TTCL wakati hata kazi hakufanya pale!

4. La mwisho kabisa,vijana wa 2000, wana shida sana,hawapingani kwa hoja,wao wanakimbilia matusi na kutweza utu wa mtu,sasa kuna wakati na sisi wazee tunashindwa vumilia,tunatoa kanzu na bargashia tunawashughulia kiswahili swahili! Jamii Forum imekua na vijana wa hovyo sana!

5. Zamani watu tulikua tunajadili kwa hoja zenye ujazo,mtu anakupinga kwa ushaidi,na sio matusi!
 
Kumbuka alisoma Kibaha sekondari Shule ya vipaji maalum
Duh! Unaweza soma special school, lakini ukawa huna akili!

Wenzake aliosoma nao University of Dar Es Salaam, Uchumi most of them ni Phd holder's, kina Prof Benno Ndulu ndiyo darasa moja na Jakaya
 
Mwinyi.Na kwamba hakuwa na connection yeyote,kwa kuwa alikuwa katibu wa CCM tu pale Masasi. Cheo cha chini kabisa. Nyuz nyingi humu zinakuwa chai tu.
Masuala ya kisiasa Hata AI inazimia ikiulizwa mambo hayo. Nadhani umenielewa.
 
Huenda kifo alichomaanisha makamba si kifo cha mwili bali utawala. Makamba Jr, Mwinyi Jr,Ridhiwani wote hawa ni watawala wajao.
Wema hawafi!

Hao uliowataja pamoja na baba zao wana wema gani kwa nchi hii?
 
Kwa hiyo alikushauri pia kuuza raslimai zetu na kuingia mikataba ya hovyo ,kiasi kile mkuu!
Basi kama ndie alikulea hukulitemdea haki kabisa Taifa hili Mkuu!
Najaribu kuona "alama alizoziacha nyuma" kikwete inanipa shida sana kuzijua!
 
Duh! Unaweza soma special school, lakini ukawa huna akili!

Wenzake aliosoma nao University of Dar Es Salaam, Uchumi most of them ni Phd holder's, kina Prof Benno Ndulu ndiyo darasa moja na Jakaya

Si kila mtu anahitaji PhD. Majority ya wanaofanya kazi katika vyuo kama Lecturers ndiyo wanahitaji hayo ma PhD zaidi. Wengine akishapata digrii yake moja inamtosha tu.
 
Duh! Unaweza soma special school, lakini ukawa huna akili!

Wenzake aliosoma nao University of Dar Es Salaam, Uchumi most of them ni Phd holder's, kina Prof Benno Ndulu ndiyo darasa moja na Jakaya
Mmh ulitafuta sababu ukajiridhisha? Kina Zuckerberg na vipawa vyao ni dropout
 
Kaka uko sahihi kabisa!

Mimi nilikua natetea kwamba Kikwete kafanya kazi Nachingwea kama Katibu wa CCM Wilaya,Masasi alihamishiwa na sidhani hata mwezi alimaliza akateuliwa kua Naibu Waziri!

1. Nimewahi fanya kazi Lindi na Mtwara,pale Nachingwea ofisi za CCM Wilaya jina la Kikwete lipo kwenye orodha ya Makatibu.

2. Lakini Masasi jina la Kikwete halipo kwenye orodha ya Makatibu wa CCM Wilaya ya Masasi,maana yake Kikwete pale Masasi hakukaa kabisa zaidi yakupita tu!

3. Sawa na Maharage Chande,aliteuliwa kuwa MD wa TTCL,kabla hajaanza kazi akapangiwa kazi nyingine ya MD wa Posta,kwa hiyo Maharage Chande hawezi sema alikua MD wa TTCL wakati hata kazi hakufanya pale!

4. La mwisho kabisa,vijana wa 2000, wana shida sana,hawapingani kwa hoja,wao wanakimbilia matusi na kutweza utu wa mtu,sasa kuna wakati na sisi wazee tunashindwa vumilia,tunatoa kanzu na bargashia tunawashughulia kiswahili swahili! Jamii Forum imekua na vijana wa hovyo sana!

5. Zamani watu tulikua tunajadili kwa hoja zenye ujazo,mtu anakupinga kwa ushaidi,na sio matusi!
Kweli umeandika ukweli 100 %
Ushauri wangu ni kwamba uwe unawakwepa wale ambao matusi kwao ndio ukamilifu wa hoja zao !!
 
Back
Top Bottom