Jamaa yangu Kwa wazazi wake ni pachafu Sana. Mama yake anaishi Kama mnyama

Jamaa yangu Kwa wazazi wake ni pachafu Sana. Mama yake anaishi Kama mnyama

Huyo rafiki yako anakuamini sana na anajua wewe ni rafiki yake wa kweli kabisa,
ndio maana hakua na wasiwasi akakupeleka kwao,

Cha ajabu badala ya kumshauri kama rafiki yako na mtu aliyekuamini,wewe umekimbilia kuja JF kumuanika hali ya kwao na kuja kutuuliza sisi hapa!

Kwanini usingemuuliza huyo rafiki yako huko huko?

Baada ya wewe kuona maisha ya huyo Mama mzee yalivyo,wewe ulitoa msaada gani au ushauri gani? au ndio umekimbilia tu huku JF?
Ungemsaidia huyo Mama ingependeza zaidi au ungemshauri Rafiki yako live ingekua sawa kabisa.
Hawa watu wa namna hii sio wa kuambatana nao popote, achana na kuwakaribisha nyumbani.

Ni kasumba mbaya sana.
 
Kuishi mjini kidogo tu ushaanza kutuona tunaotumia jiko la kuni au maji ya visima vya chemchemi ni wachafu na tunaishi mazingira machafu?

Kuna baadhi ya jamii mzazi hawezi kukubali kwenda kuishi kwa mtoto wake labda watoto muhamie hapo kwake.

Kwahiyo cha muhimu jua kutofautisha maisha na mazingira ya mjini na vijijini, miundombinu ya huko mjini haifanani na huku vijijini.

Na pia ungehoji kwa utulivu kwanini mazingira umeyakuta hivyo labda ungepata maelezo juu ya maamuzi yao, hiyo familia ya rafiki yako.
 
Kuna watu ni kama wamelaaniwa ikiwemo huyu rafiki yangu

Tafsiri ya maendeleo Kwa MTU mweusi itakuwa Ina maana tofauti.

Juzi nilimsindikiza jamaa yangu Kwa wazazi wake aisee ni pachafu Sana. mama yake anaishi Kama mnyama.

Nyumba hovyo, choo cha makuti hamna maji, mama yake around 70 yrs anabeba ndoo ya maji kichwani.

Is all about shit.

Hivi inakuaje mtu unaishi mjini vizuri then wazazi wanaishi sehemu chafu Kama hizo wanapikia makuni, wanakunywa maji ya visima vichafu, hawana miundombinu mizuri.
Wewe si rafiki kwake.
 
Mimi nilidhani utamwambia na ikiwezekana umpige tafu kiaina ili walau choo kijengwe mwisho wa siku umekuja kumtangaza mwana sio powa ndugu kama kweli unampenda mshikaji ungemwambia ukweli sio kuja kumfanyia unafiki huku
 
Kuna watu ni kama wamelaaniwa ikiwemo huyu rafiki yangu

Tafsiri ya maendeleo Kwa MTU mweusi itakuwa Ina maana tofauti.

Juzi nilimsindikiza jamaa yangu Kwa wazazi wake aisee ni pachafu Sana. mama yake anaishi Kama mnyama.

Nyumba hovyo, choo cha makuti hamna maji, mama yake around 70 yrs anabeba ndoo ya maji kichwani.

Is all about shit.

Hivi inakuaje mtu unaishi mjini vizuri then wazazi wanaishi sehemu chafu Kama hizo wanapikia makuni, wanakunywa maji ya visima vichafu, hawana miundombinu mizuri.
Sawa umetuambia sisi lakini na yeye umemchana kama hivi unavyotuambia? Kama haujafanya hivyo bhasi huu ni unafki na umbea
 
Back
Top Bottom