James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

Mzee aligoma kukiri kosa ili atoe mamilioni na atoke. Mzee hakutaka kununua uhuru/haki yake. Ama kweli Mungu anasema mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Leo mzee yupo huru.
Usimuhusishe Mungu kwenye jambo lolote linalohusu serikali ya TZ na watanzania wake, na hususani wakati bado chama cha kijani na watu wake wanarindima, huna hakika na chochote katika hili kuwa ni haki au uonevu.

Usilitaje bure.....
 
Wana CHADEMA wanachopinga ni Rugemalira kufungwa hku upande wa serikali hakuna mshtakiwa hta mmoja. Tulitegemea tuone kina Muhongo, Werema, Ndulu n.k na wao wanabananishwa sio tu private sector. Walioiba pesa stanbic mbona hawakukamatwa? Vp waliokula mgao??

Same na kesi ya kina Sioi unaona wazi kuna uonevu na wao wataachiwa soon if at all bado wapo ndani.

Bottom line serikali ya JPM ilikua biased kwenye mapambano ya ufisadi. Ilikamata wafanyabiashara tu ikaacha wanasiasa. Hivi Nchambi au Lugola kesi zao za ujangili na Rushwa ziliishia wapi??

Muache uonevu
Hapana mkuu!
..
Chadema ya sasa inamuona Ruge malaika. Lakini kumbuka kina Ruge walikomaliwa sana na kina Lisu kipindi kile cha Jk.

Sijaona chadema hii ya sasa ikitaka hao uliowataja waunganishwe na Ruge ila tunaona wakifurahia sana Ruge kutoka wakidai alionewa!

Tangu Gwajima awe mshenga wa kumleta EL pale chadema ndio ukawa mwisho mwema wa mapamabano dhidi mafisadi uliasisiwa na kina Slaa.

Ndio maana nasema nikiona mtu yeyote kwenye nafasi alafu akapiga mihela yake ntamsifu sana.

Kurajiribu kuwapigania watz ni kujichosha bure. Ndio sababu juzi nilisema Mbowe anahangaikia kitu gani? Anapata tabu kwa ajili ya mijitu isiyojielewa? Au labda ananufaika na harakati zake?
 
Daaaaah! Apumzike mzee wa watu! Aanze kuona unafiki wa wale waliokuwa wanagawana yale mahela yake.
Nafikiri hata akina Mgeja wasioziamini fedha za EPA huenda wakarudishiwa ili waendeleze walioachia.

Msoga kazaneni kuwakomboa watu wenu maana muda si rafiki,hutujui ajaye kesho atakuja na lipi?
Maana hatujui kama Mtemi Hangaya ataendelea kutawala 2025.
 
Watoto wake wajifunze jinsi baba yao alivyojitoa kutetea mali yake kwa kukubali kuteseka miaka 4 akiamini ktk nguvu zake..
Ili kesho wajue thamani ya mali hiyo kuisimamia....
 
Salaam Wakuu,

Leo nimepita maeneo ya Mahakama ya Kisutu, Nikakuta Mkurugenzi wa kampuni ya VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, James Rugemalira anatabasamu akiwa na ndugu zake wakipeana hugs na kuchumiana. Inaashilia kuna dalili nzuri leo Mzee wa Henken akaliona jua. Langu Dua.

_MG_0435.JPG
James Rugemalila(Kulia) na mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh(Kushoto), wakiwa chini ya ulinzi wa Polisi kabla ya kupanda kizimbani Mahakamani Kisutu Jijini Dar.

Tarehe 19 Jun, 2017 TAKUKURU wawafikisha mahakamani Seth Na Rugemalila kwa uhujumi uchumi. walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakishtakiwa kwa makosa sita ya uhujumu uchumi, likiwamo la kuisababisha Serikali hasara ya jumla ya takriban Sh358 bilioni.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi aliyataja mashtaka mengine yanayowakabili wawili hao kuwa ni kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na kuisababishia hasara Serikali.

Zaidi Soma:

1). TAKUKURU yawafikisha mahakamani Harbinder Sethi na James Rugemalira kwa kosa la Uhujumu uchumi

UPDATE:

Rugemalila yupo huru!

Mashtaka yake yameondolewa chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwanendo wa Makosa ya Jinai

Ningekuwa "wakili msomi", walahi ningejitolea bure kabisa kumsaidia kesi ya kudai fidia huyu baba wa watu!
 
Lugemarila afungue mashtaka dhidi ya serikali kwa kumuweka ndani kwa miaka mitano iwapo hawakuwa na kesi dhidi yake. Kwa thamani ya utajiri wake, fidia ya kuzuiwa kufanya shughuli zake kwa miaka mitano ni karibu trilioni tano.
 
Inasikitisha serikali hii mtu anashikiliwa miaka 4 bila ya ushahidi. Serikali iliyopita ilikuwa ya hovyo aisee, hongera mzee wetu umeonesha ujasiri
 
Salaam Wakuu,

Leo nimepita maeneo ya Mahakama ya Kisutu, Nikakuta Mkurugenzi wa kampuni ya VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, James Rugemalira anatabasamu akiwa na ndugu zake wakipeana hugs na kuchumiana. Inaashilia kuna dalili nzuri leo Mzee wa Henken akaliona jua. Langu Dua.

_MG_0435.JPG
James Rugemalila(Kulia) na mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh(Kushoto), wakiwa chini ya ulinzi wa Polisi kabla ya kupanda kizimbani Mahakamani Kisutu Jijini Dar.

Tarehe 19 Jun, 2017 TAKUKURU wawafikisha mahakamani Seth Na Rugemalila kwa uhujumi uchumi. walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakishtakiwa kwa makosa sita ya uhujumu uchumi, likiwamo la kuisababisha Serikali hasara ya jumla ya takriban Sh358 bilioni.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi aliyataja mashtaka mengine yanayowakabili wawili hao kuwa ni kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na kuisababishia hasara Serikali.

Zaidi Soma:

1). TAKUKURU yawafikisha mahakamani Harbinder Sethi na James Rugemalira kwa kosa la Uhujumu uchumi

UPDATE:

Rugemalila yupo huru!

Mashtaka yake yameondolewa chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwanendo wa Makosa ya Jinai

Amekuwa kama Taliban, dah. Sasa wampe kadi zake za benki tuanze jeuri mtaani.
 
Hii nchi ni ngumu sana yaani mtu unapewa kesi haina dhamana halafu unaachiwa kirahisi tu, kwaiyo ofisi ya DPP ilifungua mashtaka kwa uonevu bila kuwa na upelelezi huyu ni mtu anayejulikaba vipi kwa wale ambao hawajulikani si wanaozea jela bila sababu, kwanza ni matumizi mabaya ya pesa na rasilimali za umma pili kifungu Cha kumnyima mtu dhamana kinaenda kinyume na haki za kikatiba na kibidamu kwa sababu mtu Hana hatia mpaka mahakama imkute na hatia
 
Yaani jizi lililo kwiba ma bilioni ya shilling za watanzania lina achiwa huruuu!!!! daa kweli mwenda zake tunamkumba!
 
Mfanyabiashara James Rugemalira ameachiwa huru leo.



NOTE
MAHAKAMA NDIO ILITAKIWA ITOE UAMUZI MAPEMA KWAMBA HUYU MZEE HANA HATIA. NA SIO KUTOKA KWA KAULI YA RAIS. KWA KAULI YA MAREHEMU MAGUFULI ALIFUNGWA NA KWA KAULI YA RAIS SAMIA KAWA HURU. TANZANIA HAIWEZI KUISHI KWA KAULI ZA MTU ALIYEKO MADARAKANI. TUNAHITAJI KUBORESH MFUMO WETU WA KUTOA HAKI.
This is the point man.
 
Kuna wengine wanasema YES atoke kaonewa..
Kuna wengine wanasema NO ni lijizi hili..

Wengine wanasema majizi wanarudi mtaani.
Wengine wanasema mwendazake aliwaonea.

Hii ndio raha ya uhuru wa mawazo...tuendelee kuishi kwenye ardhi ya Mwenyezi Mungu na tumshukuru saaaaaana..
 
Back
Top Bottom