Jana nimeenda club kwa mara ya kwanza, nimetoka nduki baada ya kuuziwa maji 4000/=

Mi nikiendaga bar nikijiona hela ya mawazo afu nataka v i p nachukua zangu bapa za elfu 10 tatu natia mfukon nikifika pale naagiza maji ya buku tano afu naweka bapa mezan ukiuliza hizo bapa hapo ndan chupa ni elfu 70 vitatu sawa na laki mbili na ushee bas wana wananiona done kumbe nimetokanazo kitaa kwa buku 30 kauli mbiu yangu ni .2024 maisha ni kujiongeza'
 
Hila wadau tuambiane ukweli mnapata pesa wapi za kuspend kiroho mbaya hivyo? Hamna majukumu? Au mna pesa nyingi Sana mnatafuta sehemu ya kuzitumia?
I see, ukitafakari hii kauli, unaona kabisa jamaa kawaza vema sana. Deep down hizo pesa watu wanatumia hovyo zina siri kubwa sana.

Mkuu, kubali maisha yana level, uzuri uliona uko sehemu isiyoyako, ukaondoka.
 
Nenda Rock beach kule kwa mia mbili miambili ukajipongeze mirinda nyeusi
 
Huyu aende liquor store tu apewe kiti nje ya barabara akae anywe Maji bila mziki, sehemu za starehe mtaumizana tu ataondoka hajala maana mbavu tatu za mbuzi choma ni 50000
sema waja mna laana,kwa hiyo mtoto wa mwenzenu achezee muziki nje ya geti kisa ana hela ya mawazo[emoji23][emoji1787]
 
heineken buku nane, sisogei kamwe
 
Hiyo bar wanayo ruhusu kuingia na kinywaji chako ni wapi uko?
 
[emoji16][emoji16] Huko sirudi Tena wameshanikosa kudadeki, nitarudi nikiwa na uwezo wa kuchafua meza kama nyie sijui itakua lini lakini nitarudi ku-clear jina langu.
Sehemu kama hizo kama wewe ji kabwela inatakiwa unaenda ukiwa full yaani umekuka na kushiba then unaenda kuburudika ata ukinunua maji ya 4000 sio mbaya unakunywa mpaka ahsubuhi.

Kuna siku nilikua malaika beach nikaambiwa wine yq 12000 wao wanauza 45k nikasema hii nikawa nafanya kazi ya kuwachenga wahudumu huku naendelea kula burudani saafi.
 
Huyu aende liquor store tu apewe kiti nje ya barabara akae anywe Maji bila mziki, sehemu za starehe mtaumizana tu ataondoka hajala maana mbavu tatu za mbuzi choma ni 50000
Watu wanapenda tu kuskia mziki mzuri, kuona mazingira mazuri mataa yana waka waka bend inampigia mziki na wafanyakazi wamevaa vizuri wanatabasamu tayar kwa kumhudumia.


Unazani commission ya 200 ya maji italipia vitu vyote hivi haiwezekani. Ndo maana wamiliki wengi wa hizi sehemu wameeamua kutafuta faida kwa kuongeza charges kwaa bidhaa. Utaingia bure ila maji ya 700 tunakuibia 4000 [emoji16][emoji16] iyo 3300 unalipia hizo services nyingine
 
Hiyo bar wanayo ruhusu kuingia na kinywaji chako ni wapi uko?
kwahy we ukienda pale utakua unajionesha umebeba pombe??? kutoka nje kwanza nafs yako haitakusuta?? Nimesema bapa unaweka mfukon haijalish koti kubwa au sulual pana mbona watu tunaenda bar kubwa na beg mgongon na hatuulizwi au sura yako watu wakikutazama wanahis muharifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…