Jana nimeenda club kwa mara ya kwanza, nimetoka nduki baada ya kuuziwa maji 4000/=

Hahaha
 
Wa hali ya chini anaenda club kufanya nn? Si aende dukani kwa mangi?
 
Usiige maisha wala kutaka kujilinganisha na mtu mwingine.....Maisha ni Siri kubwa kuhusu swala la kupata hela Kila mtu ana mbinu zake za kupata hela ni ngumu Sana kuuziwa silaha zote za mtu(Mbinu za kupata hela)

Pambana , pambana,pambana
Kuna mchina aligoma kuniuzia saa ya nakshi kwenye ndege. Nikadhani amenidhalilisha....nilipofika Mtaa wa Congo, Dar es Salaam nikamuelewa yule Dada wa Kichina kwenye ndege!!!!
 
Naomba udadavue vizuri yaani ulikuwa huna hela au ....?
Dolali nilikuwa nayo Tena wakati huo naitwa "Kelele"....sema nilikuwa nimeangukia kwenye trick za marketing officers wa saa za nakshi, yule Dada wa kichina ndiye aliniokoa. Yaani nilitaka kununua muhogo uliochemshiwa Manzese kwa Bi-Nyau na kufungwa kwenye karatasi zenye Nembo ya KFC kwa bei ya nyumba ya Ufukweni Zanzibar.

Wakati mwingine, binafsi na hisi ni ulimbukeni wangu kununua kitu kwa bei ya juu wakati najua kitu hicho hicho naweza kukipata sehemu nyingine kwa bei ya chini.
 
Seen.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…