Januari Makamba atapita njia ya Hayati Lowassa katika safari yake ya kisiasa

Januari Makamba atapita njia ya Hayati Lowassa katika safari yake ya kisiasa

Sio siri kuwa shauku ya mh Januari Makamba kuutaka urais ni kubwa sana pengine zaidi ya ile shauku ya mh Lowasa. Lakini kwa bahati mbaya mapito yake hayatatofautina na yale ya Mh Lowasa.

Atajitahidi sana, atakusanya watu, atakuwa kwenye makundi pendwa na hata nyakati nyingine atafika katika 5 bora, lakini kamwe hatachaguliwa kuwa mgombea Urais kupitia CCM.

Hata akifanya kama Lowassa, kuhamia upinzani nako atachaguliwa kuwa mgombea wa Urais lakini safari itaishia kama ile ya Mh Lowasa.
Usimfananishe lowasa na vitu vya hovyo mkuu!!

Mi sipendi aina ya vijana kama yeye wanaofikiri urais ni haki Yao ya msingi kama maji ya kunywa Tena wanautaka Kwa mbeleko za baba zao kisiasa!!

Angalau Dr. Hussein Mwinyi namkubali sana hakuonyesha kama anautaka kabisa lakini akawa coz system ilimuandaa!!

Huyo hawezi kua Raise was nchi nature ishamkataa kabisa!!

Wakiondoka hai anaowategemea na ndoto za urais unaishia hapo hapo!!
 
Wewe ni pimbi kabisa. Mtu katoka nishati ambayo Samia alimpa fedha zote za kukarabati mitambo, akaishia kutuachia mgawo wa umeme mkali kuliko hata ule wa 1993 wakati wa Mwinyi. Huyu ndiye waziri kilaza kuliko wote, yupo hapo kwa sababu ya JK na baba yake tu. Ila uwezo ni ZERO
Alipewa kuchagua wizara anayoipenda, jibu moja kwa moja likawa NISHATI. Samia akamzawadia na kumpa bajeti nzima ya NISHATI na ushehe. Sijui pesa kazipeleka wapi?

Wizara ya mambo ya nje haina pesa kama NISHATI. Mambo ya nje ni BENCHI. Huko kilio chake ni kizito.
Nafikiri ana hasira sana, kwani si Wizara aliyeipenda. Kimsingi Januari M nafasi ya Urais haiwezi. Ningemuomba alikubali hilo.
 
Moto Ni Mkali Na CCM Imepasuka Humo Humo Mbaya Zaidi Umemtaja Mmoja Ila Idadi Ni Kubwa Sana Wanaoutaka Urais Ukisema Tutasema Tanzania Itatikisika Mchana
 
Wagalatia/Walawi Mlisema Zamu Yao Sasa Ama Mmebadili Mnabaki Kobaz
 
Usimfananishe lowasa na vitu vya hovyo mkuu!!

Mi sipendi aina ya vijana kama yeye wanaofikiri urais ni haki Yao ya msingi kama maji ya kunywa Tena wanautaka Kwa mbeleko za baba zao kisiasa!!

Angalau Dr. Hussein Mwinyi namkubali sana hakuonyesha kama anautaka kabisa lakini akawa coz system ilimuandaa!!

Huyo hawezi kua Raise was nchi nature ishamkataa kabisa!!

Wakiondoka hai anaowategemea na ndoto za urais unaishia hapo hapo!!
Wanapofanana ni mwisho wa safari yao, na sio kwa akili au uwezo wa kutatua matatizo ya wananchi. Ile dhamira na shauku ya kuutaka Urais, hapo wanashabihiana.

Kwa mfano, Lowasa katuachia shule za KATA/ KUTWA ambazo ndio mombozi kwa walala hoi katikia kipengele cha Elimu. Kwa hili jina lake litaendelea kuishi kwa maisha yote ya kuwepo kwa mama Tanzania. Viatu kama hivi au mawazo kama haya ndio tatizo ambalo Januari M bado hajaonyesha popote pale.
 
Moto Ni Mkali Na CCM Imepasuka Humo Humo Mbaya Zaidi Umemtaja Mmoja Ila Idadi Ni Kubwa Sana Wanaoutaka Urais Ukisema Tutasema Tanzania Itatikisika Mchana
Idadi ni kubwa mno, lakini tofauti ni mbinu zinazotumika. Kuna ambao wanautaka lakini hawajaunda makundi na wala hawana mbinu chafu kufikia malengo yao. Hawa hatuna matatizo nao, na wajitokeze wengi tu.

Mbaya na kinachoniuma ni wale ambao wapotayari hata kutotoa huduma kwa wananchi wakidhani ndio njia pekee ya kumuangusha yule aliyewateua na anayetarajia kuwa mgombea. Mbinu hii inaniumiza mimi mwananchi wa kawaida na ndio maana napaza sauti.
Ni mara nyingi Rais amerudia kusema kuwa nimewachagua mkawahudumie watanzania, na si kujinadi katika uchaguzi ujao 2025.
 
Hawezi kuwa kama Lowasa, hana uwezo wa kuwa kama Lowasa na hawezi kuwa Lowasa kamwe....
 
Sema kifo cha Magufuli kimefanya ndoto za Urais kwa Makamba ziwe ngumu sana.
Hesabu Zimevurugika za wengi sana waliokuwa wanakinyemelea kiti ukizingatia 2025 tunaenda na Mama hadi 2030 wanachoka kabisa wanajikaza tu.!
 
Back
Top Bottom