Japan yaitangaza Tanzania kuwa Kitovu cha Uwekezaji, viwanda. Honda kujengwa nchini

Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo

Nilizani kuwa kwako nje ya nchi ungekuwa una mambo chanya kwa vijana wenzako ambao atujaenda Ulaya,jadili Mnakasha
Narudi katika uzi nitakuwa wa mwisho kupongeza sababu Matukio na Matokeo ni vitu tofauti
"Vox popoli vox dei"
 
Safi kabisa. Wanaobeza ziara za Mhe. Rais nje ya nchi wanune wasinune wamesikia.

komboka kichwani wewe! we unadhani ni akili sana kucheza position zote peke yako? forward ucheze wewe, winga zote mbili wewe, beki mwenyewe! we unaona akili sana hiyo? alienda kwenye kazi za waziri wa fedha WEF, alienda kwenye kazi za waziri wa nje AU, alienda kwenye kazi za mambo ya ndani SADC. Serekali siyo duka la Mkinga mmoja hilo wewe....
 


ichi kinogesho kina haja kweli?

Eti "Ni matokeo ya Ziara ya Rais Kikwete Japan". Sio uongo wa kisiasa huu? Nyie watu wa Ikulu msipende kudanganya-danganya watu kirahisi rahisi hivyo. Yaani Kikwete kaenda juzi tu hapa la leo-leo feasibility ya Honda ishakamilika, feasibility ya reli ya kati ishafanyika na maamuzi wajapani wanayafanya leo?

Kwani Mungesema ni Matokeo ya Economic Diplomacy imeanza tangu kipind cha Mkapa Mngeonekana wajinga? Jifunzeni kutuheshimu Watanzania tuna akili ya kuelewa mambo jamani. Punguzeni zarau. Eti
Ni matokeo ya Ziara ya Rais Kikwete Japan. My Foot!
 
inashangaza sana kuona kila jambo linalotokea watu wanalichukulia negetively, hivi swala hapa ni kikwete au maslahi kwa nchi, ni ulitaka rahisi asitafute wawekezaji, au bado mna mawazo ya nyerere kwamba tuache raslimali kwa kua haziozi, soo what? jaribuni kuwa positive angalau kidogo achani kuwaza giza kila wakati jaribuni kuiona nuru! kwa mtindo huu hamtakaa mzione fursa hata kama zitakua sebuleni kwenu! jipange acha kupiga mayowe..period!
 
Guys, personally siipendi CCM, lakini kama tutatuliza akili zetu na kuwa positive na kutumia fursa hizi vizuri bila ubinafsi na rushwa, Tanzania ya miaka mitano mpaka kumi ijayo itakuwa yenye maendeleo na uchumi imara. Kuna watu hawaelewi ni kwa nini 5 Asian tigers kama Korea Kusini, Malaysia na nyinginezo zimeweza kutoka kimaendeleo?? Waliweza kutumia fursa za technolojia na misaada ya kimifumo na uwekezaji katika elimu vilivyo. Kwa kifupi walijitambua wana nini na wanataka nini.

Kwa sasa kuna mwamko mkubwa sana wa kujitambua kwa wa Tanzania, tupo pazuri tunahitaji kubadili attitude za watanzania, wapende kufanya kazi, rushwa idhibitiwe, uzalendo pia uongezeke na hili si jukumu la serikali pekee ni sisi wote.

Mwisho nimalizie, HAKUNA JINSI NI LAZIMA TANZANIA IWE SUPER POWER AFRIKA MASHARIKI NA KATI BY 2025, dalili zote zinaonyesha hivyo. TUACHE KUJIDHARAU JAMANI CHONDE CHONDE.........
 
Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo

"MSUKULE ni mtu aliechukuliwa kwa nguvu za giza ili atumike kwenye shughuli zisizohitaji akili kama kulima shamba kwa faida ya mwenye Msukule. Chadema inawatumia vijana wasiojitambua kama misukule kwenda kufanya maandamano yasiyo halali na vurugu huku wao viongozi wamekaa majumbani kwao wakiwaangalia kwenye TV wanavyokula mkong'oto.

Kama kweli CHADEMA wanatetea haki kusingekuwa na ubaguzi wa matibabu ndani ya chama, wengine wanafanya checkup ujerumani wakati wengine wanalazwa third class muhimbili
.....JITAMBUE!"

Ukiwa msukule unawaona wenzio ndio misukule, huwezi kujitambua. Pole kaka.
 
wajapan ni wawekezaji wa kweli,huwa hawana longolongo,kwa upande wangu nina imani sana na wawekezaji wa kijapan
 
sasa nchi inauzwa kwa 10% mikataba mibovu, tunawatoa wanachi kwenye maeneo yao tunawapa wawekezaji, nchi yetu tunakuwa wakimbizi.
 
Hii thread imebeba ujumbe muhimu na mzito kwetu lakini kwa sababu haina chadema wala sheikh ponda ndani inaonekana ya hovyo

Umeona eee! Hii ni habari njema sana kwa uchumi na taifa ambayo tulitakiwa tujadili jinsi ya kushirikiana na hao wajapan bila kupunjwa! Hata vyombo vya habari vilitakiwa vifanye zaidi kwa kuchambua na kusaidia kuongeza uelewa wa jamii jinsi ambavyo tunaweza kuchangamkia fursa hizi. Wataishia copy/paste ya taarifa ya ikulu, na kutuambia tu kwamba Rais amesema tuchangamkie fursa! Swala muhimu la Tuzichangamkieje, hakuna atakaesema chochote!
 
hapo kwenye kujenga viwanda ndiyo penye magumashi , kurasini yote wamepewa wachina na waarabu badala ya ile propaganda ya upanuzi wa bandari ! Sasa bila shaka hawa watapewa kariakoo , maana hawataki kuwapeleka nje ya mji , ni kama vile nchi hii mwisho wake DSM .
 
Tatizo hizo neema haziji bila ya ufisadi ndani yake!
 
nchi yetu ni shamba la bibi

Stuka acha kulalamika! Muda wa kulalamika lalamika na kushutumu wakoloni umepitwa! Changamka kuza uchumi wako mwenyewe. Kwenye ujamaa tulitoka tangu mwaka 1985, Tz ni nchi ya kibepari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…