Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

We Unahisi kwenye Hadithi Ya abimeleki Ilistahili kuwepo Hapo??

Mwanzo 21:22-34??

Mwanzo kabisa Nilizungumza Kitu kinaitwa Documentary Hypothesis au JEPD theory kama Umesoma Theology utanielewa Nachokisema..
Kama utaweza nenda Kapitie maana yake na usome pia kuhusu Mahusiano yake na Mpangilio wa Matukio kwenye Biblia Agano la kale Especially Torati..

Ngoja nichokoze kidogo Kitu kabla sijakujibu

Unafahamu kuhusu Beersheba na kuhusu kupewa Jina la beersheba unahisi Nani ana Authentification ya Hilo jina?

Ni Ibrahimu:-

Kama mwanzo 21:31

"Kwa hiyo akapaita mahali pale Beer-sheba, kwa sababu waliapa huko wote wawili."

Au ni Isaka:-


Mwanzo 26:33

"Naye akakiita jina lake BeerShiba; kwa hiyo jina la mji huo likawa Beer-sheba, hata leo."


umewahi kusikia Story ya Abimeleki na Ibrahimu na Sara (Soma Kwenye mwanzo 20:1-18)?
Vipi inatofauti Gani na Story ya Farao na Ibrahimu na Sara ( Soma mwanzo 12:12-20)?


Sasa Tuache hao Inatofauti Gani kati ya Story hizo na Story ya Rebeca Na isaka ?(soma mwanzo 26:6-10)

Kuna Kitu Umegundua Kwenye Hizo hadithi?
sasa Nakushauri Soma Documentary hypothesis au JEPD theory tena siku hizi hakuna haja Uende kozi ya Theology uyajue haya..

Sasa Turudi kwenye Concern yako...


Eneo Ambalo Linatajwa Ni Eneo ambalo Ibrahamu alikuwa akiwa na Umri wa Miaka 100 na Ndyo muendelezo wa Hiyo mwanzo 22 ukitoa story ya Abimelek ambayo ukiisoma Utaona Ibrahim anatoka kanaani Kwenda moria..

Wakati huko nyuma tunaambiwa alikuwa anakaa nchi ya wafilisti Beersheba..

So story ya 21 na Story ya 22 Haziungani..
Ila zinaungana na Story ya Mwanzo 21:21..

Kwa hiyo story ya mwanzo 21:21 muendelezo wake ni mwanzo 22:1..

Ukijifunze Textual analysis Utagundua story ya Abimelek ni added Story muulize Mchungaji yoyote au Mtu yoyote aliyesoma Theology na aliwahi kusoma Course ya textual Critic au Textual analysis

Kwanza mimi sijasoma theology. Nasoma biblia kujifunza tu.

Documentary Hypothesis
nimeiosoma ila ni mawazo ya wanadamu tu hasa wanatheology wanaotumia hekima za kibidamu yenye kikomo, ndio maana kuna mambo mengi watu wameyatambua mpaka kwenye ujio wa Yesu alipokuja. D hypothesis kama ni kwel basi biblia yote haina maana ni story za kusadikika.

Ukiangalia matukio ya Mwanzo 12;12-20, 20:1-8, 26:6-10 ni tofauti kabisa japo yanafanani. Ila ni Mungu ndio aliyefanya kwasabab hawezi kuchanganya uzao wake na wanadamu ndio maana kila wakati alikua anazui hichi kitu. Soma Mwanzo 6.

Twende kwenye maswali yako.

Beersheba inaanza kuonekana kwenye Mwanzo 21:14 kuwa palikua na jangwa la Beersheba Ibrahimu na Ismael walipita tu kwenye jangwa hili. Mwanzo 21: 21 inaonesha Ibrahimu na Ismael alilipita jangwa la Beersheba akenda mpaka jangwa la parani ambapo Ismael aliishi parani.

Kwaio hapa tuna miji mitatu Hebron, Beersheba na parani utasoma hizi sehem tatu vizur.

Mwanzo 21;22 Abimeleki baada ya kuona Ibrahimu amemsogelea kwa kuogopa yaliomtokea miaka ya nyuma kwenye Mwanzo 20. Ndio maan alikuja kutafta mapatano na Ibrahimu. Ibrahimu alikua anashuka kusini kwasabb ya njaa kali na kusini palikua kuna hauweni ya malisho kwa ajiri ya mifugo yake. Mwanzo 26:1.

Mwanzo 22:19 baada ya jaribu la kumtoa isaka kafara. Ibrahimu alirudi mpaka Beersheba, inaonesha makazi ya Ibrahimu na Isaka ilikua ni Beersheba kama Mwanzo 21:34. Inayosema Ibrahim alikaa na wafilisti miaka mingi kabla ya jaribu la kumtoa kafara Isaka.

Hata ukisoma Mwanzo 28:10 na Mwanzo 46:5 yote yanaonesha Beersheba waliishi Ibrahimu na Isaka. Maana ibrahim, isaka na yakobo wote waliishi hapo kama Mungu anavyojitambulisha.

Hapa nakujibu swali la umri wa isaka wakati wa kutolewa kafara hakuwa mchanga. Kama unabisa lete ushaidi wa maandiko. Kama utatumia Qur'an pia itakua vizur
 
Na vipi Kuhusu Andiko hili Mkuu Daudi?

Mwanzo 16:3

"Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe.

And Sarai Abram's wife took Hagar her maid the Egyptian, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan,
and gave her to her husband Abram to be his wife."


Nikuulize kitu Daudi?
Unajua Hajri alitokea wapi alikuwa Princess wa Misri na alipewa ibrahimu kipindi kile farao alipoogopa mkono wa Mungu..

Baada ya kukaa miaka kumi kwa sheria ya Waebrania Ilimpasa Ibrahimu kumuachia huru ila mkewe sara alionelea kuwa Asimuache ila amuozeshe kwa Mumewe....

Kuna watoto wengi tu ambao wametoka kwa wamama ambao ni Vijakazi..

Mtoto wa Yakobo Dani Ni wa Bilha ambaye ni Kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Naftari Ni wa Bilha ambaye ni kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Gadi ni mtoto w zilpa ambaye ni kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Asheri ni mtoto wa Zilpa ambaye ni kijakazi..

Katika Vijakazi wote wakeze Yakobo hakuna hata mmoka yakobo aliyekuwa amemuoa..

Soma mwanzo 29 mpka mwanzo 30
Safi sana Kuna wengi elimu hii hawana
 
Agano lilifungwa Kipindi Ambacho Isaka hajazaliwa sasa sjui unazungumzia Agano lipi..
Na agano lilikuwa ni Kutahiriwa na Ishmael alitahiriwa ndani ya Agano
Wakati Mungu anmtembelea Ibrahim kwenye mialo ya Mamre alikua tayari ana Ismael lakini alimwambiaje Sara? Utakua mama wa mataifa. Hakuambiwa Hajiri Mmisri wala uzao wake. Pia angalia singularity ya neno mzao na sio wazao. Unatrace uzao kwenye ndoa na ndio maana hata Leo mtoto wa ndoa anatambulika mpaka na mamlaka.
Alitahiriwa maana maagizo yalikua ni watu wote wa nyumbani kwake. Pia kama amemrithi baba yake kwa nini mama amtafutie mke? Kwa Nini mama ndo angolee mahari ya mwanae na baba alikua hai? Mbona Isaka Mzee alimtafutia mke? Unajua Kwa Nini hakumchukulia mke huko Kanaani alikoishi Hali ya ugeni?
 
Hapana Mkuu Waebrania sio Tafsiri hiyo..
Unamfahamu Eber?

Nuhu Alipovuka kwenye Safina..
Alikuwa na watoto watoto (Mwanzo 9:18)..
Shemu, na Hamu, na Yafethi;

Shem ndo alizaa Waebrania wote..

Mwanzo 10:21

"Naye Shemu ambaye ni baba wa wana wote wa Eberi, na ndugu mkubwa wa Yafethi, akazaliwa wana."


"Unto Shem also, the father of all the children of Eber, the brother of Japheth the elder, even to him were children born."


sasa kupitia Eber Ndo tunapata wana wa Eber au Ebrania na hapo hasa ndo kizazi cha waebrania kilipoanza

Tena kwenye Quran waebrania waliotajwa ni ,
Tera(Azar) babaye Ibrahim , Sarah, Isaka, Ishmael, Yakub
 
Kitu muhimu ni tuutafute ukweli, Mungu hakuleta dini wale Yesu hakuleta dini!. Hoja hapa ni nani mkweli na nani muongo?. Mtoto aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni nani?.
P
Kila mtu alete mistari
Kwenye Biblia mambo yote yako bayana
Full story a to z

Kwenye Quran kuna utata kidogo

Ila yote kwa yote aliyetolewa sadaka ni Isaka kwa kuwa, Ishmael muda huo alishaondoka na Mama yake kwenda Mecca hadi kupata kiu na chemchem ya maji ya Zamzam kupatikana
 
Na vipi Kuhusu Andiko hili Mkuu Daudi?

Mwanzo 16:3

"Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe.

And Sarai Abram's wife took Hagar her maid the Egyptian, after Abram had dwelt ten years in the land of Canaan,
and gave her to her husband Abram to be his wife."


Nikuulize kitu Daudi?
Unajua Hajri alitokea wapi alikuwa Princess wa Misri na alipewa ibrahimu kipindi kile farao alipoogopa mkono wa Mungu..

Baada ya kukaa miaka kumi kwa sheria ya Waebrania Ilimpasa Ibrahimu kumuachia huru ila mkewe sara alionelea kuwa Asimuache ila amuozeshe kwa Mumewe....

Kuna watoto wengi tu ambao wametoka kwa wamama ambao ni Vijakazi..

Mtoto wa Yakobo Dani Ni wa Bilha ambaye ni Kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Naftari Ni wa Bilha ambaye ni kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Gadi ni mtoto w zilpa ambaye ni kijakazi..
Mtoto wa Yakobo Asheri ni mtoto wa Zilpa ambaye ni kijakazi..

Katika Vijakazi wote wakeze Yakobo hakuna hata mmoka yakobo aliyekuwa amemuoa..

Soma mwanzo 29 mpka mwanzo 30

Sarah kumpa Ibrahim Hajiri amfanye mkewe haibadili status ya Hajiri kuwa ni mke wa Ibrahim

Ndoa ni suala la kisheria na kimila. Sarah hana mamlaka wala uwezo wa kumuozesha Mwanamke yeyote kwa Ibrahim ilhali yeye ni Mke.

Huko mbeleni tunaona Ibrahim akimwambia Sarah kuwa huyo Hajiri ni kijakazi wake(wa Sarah) hivyo yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuamua uwepo au kutokuwepo kwa huyo kijakazi.

Pili, ishu ya wake za Yakobo ni walewale wawili. Recho na Leah. Hao vijakazi hawahesabiki kama wake Yakobo.

Watoto wa kina Bilha na zilpa walihesabika kwa sababu walikubali mfumo wa familia ha Yakobo. Hawakuwa wasumbufu kwa Mabosi zao.
 
Tikiachana na maandiko tukarudi katika hali ya kawaida, inaonekana mtoto aliyetaka kuchinjwa ni Ishmael. Kwa maana ya kwamba ndiye aliyekuwa mtoto wa pekee, kuchinjwa kwa Isaka kusingemuuma sana Ibrahim maana angejua hata akichinja huyu bado anabakiwa na mtoto wake mwingine wa kwanza ambaye ni Ishmael. Huu ni wangu mtazamo wa hisia zangu binafsi bila kuhusisha vitabu vya maandiko ya dini, labda sasa waje wataalamu wa maandiko watuthibitishie ukweli ni upi.
Mtoto wa pekee alikuwa Isaka

Ishmael alishaondoka kwenda Mecca na mama yake Hajar hadi akapata shida jangwani Mungu akampa chakula na chemchem ya Zamzam ndo hadi leo wakienda Hijja ipo
 
Mtoto aliyezaliwa na kuwa Mwana wa Pekee wa Ibrahim ni Ismail, wakati Isaka anazaliwa, Ismail alikuwa ameisha zaliwa, hivyo Isaka hakuwa mwana wa pekee wa Ibrahim!.
Encyclopedia Britanica Inasema "after Ishmael and Hagar were banished, they settled in Mecca, near which they had found relief and water at the Well of Zamzam. Later, in nearby Minā, Abraham attempted to sacrifice Ishmael (rather than Isaac, as stated in the Old Testament), an event commemorated on Eid al-Adha and in the rituals of the hajj (pilgrimage)"
P
Kamba hii
Ibrahim hakwenda nao (Hajir&Isma) Mecca

Alibaki na mkewe na Isaka
 
Hilo jina Isaka hapo limepachikwa Kwa kulazimishwa
Isaka hajawahi kuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim Kwa sababu yeye ni mtoto wa pili

Ila Ishmael ndio aliwahi kuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim

Wakati Isaka hajazaliwa Ishmael ndio alikuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim

Nyinyi wagalatia mmedanganywa sana na Wazungu
Nini kilimfanya Hajiri&Ismail kuondoka kwenda Mecca hadi kupata kiu na Mungu kuwapa chemchem ya maji ya Zamzam?
 
Mada inasema nani alitolewa sadaka.
Mimi nimesema kwa mujibu wa Biblia ni Isaka.
Kwa mujibu wa qurani ni Ishmaeli.
Sijui wewe unaongea nini tena. (Gen) 22:1
Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.
Mwanzo (Gen) 22:2
Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.

Wewe soma qurani yako inatosha.
Quran haijataja hata jina

Biblia ndo full story kama video vile
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
Habari zote za Ishimaili na Isaka zimeelezwa kikamilifu katika Biblia, na ndio rejea kuu na pekee. Hizo habari haziko popote kwenye Quran.
Na bila ubishi wowote iliyetakiwa kutolewa sadaka ni Isaka.

Waislamu wanaaminishwa uzushi wa Ishimaili kutakiwa kutolewa sadaka pasipo rejea ya Quran.

Tuache kuisingizia Quran mambo ya uzushi na uongo.
 
Umri sio kigezo kwa hoja zifuatazo;
1. Simulizi ya Biblia inataja tukio la kutokea kafara limetokea baada ya Hajiri na íshmael kufukuzwa.

2. Tangu Isaka azaliwe Ibrahim aliishi miaka sabini mingine.

Ibrahim anamtafutia mke Isaka
Lakini hakumtafutia íshmael.
Íshmael alitafutiwa Mke na mama yake, Hajiri. Tena alimuoz
Mkuu,..umri ni kigezo na ni njia rahisi zaidi ya kujua ukweli ni upi,...

Kwa mfano,..kama ikiwa tunaona kwenye Biblia kwamba wakati amri ya kuchinjwa inatoka.......mtoto aliyekusudiwa kuchinjwa tayari kwenye wakati husika alikua anaweza kuongea na kutembea umbali mrefu......

Inabidi tujiulize, Je, kati ya Ismail na Isihaka nani alikua kwenye umri wa kuweza kuongea na kutembea umbali wa zaidi ya km 300,. kwenye wakati huo?


Tukisema tupuuzie suala la umri,.. nadhani itakua tumeamua kwa maksudi kabisa kuukimbia ukweli.
 
Mkuu,..umri ni kigezo na ni njia rahisi zaidi ya kujua ukweli ni upi,...

Kwa mfano,..kama ikiwa tunaona kwenye Biblia kwamba wakati amri ya kuchinjwa inatoka.......mtoto aliyekusudiwa kuchinjwa tayari kwenye wakati husika alikua anaweza kuongea na kutembea umbali mrefu......

Inabidi tujiulize, Je, kati ya Ismail na Isihaka nani alikua kwenye umri wa kuweza kuongea na kutembea umbali wa zaidi ya km 300,. kwenye wakati huo?


Tukisema tupuuzie suala la umri,.. nadhani itakua tumeamua kwa maksudi kabisa kuukimbia ukweli.

Ndio maana nikakuambia Baada ya kuzaliwa Isaka Ibrahim ameishi miaka 70 mbele.
Akatafuta hadi mke
 
Kujadili hii mada inabidi tutambue mambo makuu mawili.
1. Rejea ya habari hizi zipo kwa kina na kikamilifu ndani ya Biblia pekee yako. Hazipo kwenye Quran
2. Biblia inamtaja Isaka kama ndiye mtoto wa ahadi, mtoto wa pekee wa ndoa ya Ibrahimu na Sarah na Isaka ndiye aliyepelekwa kutolewa sadaka.
 
Back
Top Bottom