Tutajie hao wanawake waliodhulumiwa Mali walizochuma na waume zao hapa kama wapo, yaani naamisha kudhulumiwa na mtaraka wake na sio ndugu wa mume wake.Je, wanawake waliotapeliwa mali walizochuma na wake zao, mbona hawafi?
Hiyo sentence ya "Mali tulizochuma wote" ipo kwa ajili ya kurahisisha utapeli wa mwanamke kwa kivuli Cha ndoa.Hakuna Mali inayochumwa na mwanamke. Hela ya mwanamke siku zote ni yake pekee yake hata akikupa utairejesha tu. Tofauti na hapo wewe utakuwa unaishi sayari nyingine.
Hii sentence ya "Mali zilizochumwa" ndo imetufikisha hapa tulipo. Na ukiuliza mlichuma nae vipi ataambiwa Mimi nilikuwa namfulia nguo na kumpikia na kumpa maji ya kuoga akitoka kazini nilimkuta Hana kitu nk sababu ambazo hazina mashiko. Kwahiyo nikipeleka nguo Kwa dobi chakula nikala Kwa mama ntilie siwezi kuwa na Mali?
Ama nao watahitaji mgao kipindi wakinihudumia na kuoa Mali ?
Hizi 50-50 zitatutesa sna na migogoro imeanzia hapo na Bado.
Ulizia Sasa wamechuma vipi wote utaskia eti nilikuwa namfulia, nampikia pamoja na kumnyooshea nguo... Yaani hivyo tu halafu leo hii mgawane assets zako zote pasi kwa pasu... That's daylight robbery
Leo hii Kuna wanawake wameolewa wanafanya kazi na vipato vyao ndani havionekani na Wala hata hizo kazi za ndani hawafanyi, zinafanywa na madhouse girls ambao na wao mishaara wanalipwa na mwanaume....
Ila Sasa siku ikitokea ndoa imevunjika utamskia mwanamke huyo kwa kujiamini kabisa na yeye anasema hizo Mali za mumewe wamechuma wote na amemvumilia mengi sana na Tena wakati unakuta anabubujikwa na machozi ya uongo uongo....
Aisee hiki kizazi Cha wanaume kinadhulumiwa sana Mali na wake zao wakiitumia mahakama kama rubber stamp ya kufanyia dhuluma hii.
Honestly I thank God for redpill