JB: Mganda huyu ni nani na anafanya nini Tanzania?

JB: Mganda huyu ni nani na anafanya nini Tanzania?

Kuna watu wako slow tu; tunapenda kuangalia vitu kimoja kimoja badala ya kujumlisha picha nzima. Ni sawasawa na puzzle...
 
Hoja hii ina mambo mengi nyuma ya pazia. Lakini cha msingi ujasiriamali/uwekezaji au jina lolote tunaliwapa watu wanaokuja nchini kufanya biashara kunatakiwa kuongozwe pamoja na mamb mengine: sheria za uwekezaji, udhibitri wa uhalifu wa kimataifa na usalama wa taifa na maslahi ya nchi na raia wake! Mambo nyeti yahusuyo usalama wa taifa na nyendo za watu walioko kweye "dossier" huwa hayawekwi wazi kwa kadamnasi lakini kila raia mwema hutakiwa kutonya wahusika hizo nyedo zenye kutiliwa mashaka ..Njia moja ni watoa mada huku jamvini ni kuziainisha bayana kwa ajili ya hatua muafaka!
 
Mbona kuna wahindi wengi wa Kenya wapo Tanzania wanafanya biashara kubwa kuliko za JB hamuhoji uhalali wa biashara zao?

Wale waganda wa Kinondoni pia walikuwa wafanya biashara mazee, tusiwe wavivu wa kufikiri


Waganda waliotuhumiwa kuua askari, mbwa waachiwa
Posted on March 10, 2008 by admin
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imewaachia huru washitakiwa wanne kati ya watano Raia wa Uganda waliokuwa wakituhumiwa kuua askari watatu pamoja na mbwa.


Mahakama iliwaachia huru raia hao wa Uganda mwishoni mwa wiki mbele ya Jaji Thomas Mihayo baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) kuwasilisha nolle akiiomba mahakama kuwaachia huru kutokana na kuwa hana nia ya kuendelea kuwashitaki.
Kwa mujibu wa nolle iliyowasilishwa mahakamani hapo, iliwataja washitakiwa ambao DPP hana nia ya kuendelea kuwashitaki, ambao ni
Bw. Mawanda Maalo, Bw. Hawalulema Venist, Bw. Sylvester Salugo na Bw. Mohamed Simbwa Mohamed.
Uamuzi wa DPP wa kuwafutia washitakiwa wanne pia uliambatana na uamuzi wa kuendelea kumshitaki mshitakiwa mmoja ambaye pia ni raia wa Uganda Bw. Abdul Karim Msanje, ambaye atakabiliwa na mashitaka hayo ya mauaji.
Mshitakiwa huyo anatumikia kifungo cha miaka 15 jela kufuatia makosa ya kupatikana na silaha pamoja na risasi ambapo alikamatwa na bunduki mbili aina ya SMG AK 47 zenye namba 1975-230912 na 56-3903138 pamoja na risasi 87 ambazo zinadaiwa kutumika kwenye mauaji ya hao askari na mbwa.
Watuhumiwa hao walidaiwa kuwaua askari namba D.1672 Koplo Hassan, E.7324 D/C Ramadhani na E.7999 D/C Deogratius mnamo Mei 25, 2003 huko Kawe, Dar es Salaam.
Mbali na kuua maaskari hao pia walidaiwa kuua mbwa wa polisi, Rogger ambao walikuwa wanatumika katika doria ya siku hiyo.
Ilidaiwa kuwa, majambazi hao walianza kuwafyatulia risasi polisi wakati dereva anataka kuondoa gari hivyo kupoteza mwelekeo na kuacha barabara na kupindukia mtaroni, wakati huo huo majambazi wakiendelea kufyatua risasi.
Mapolisi watatu walikufa papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya ambapo Siku chache baadaye waliwakamatwa Waganda hao kwa tuhuma za mauaji hayo.
Polisi pia walimpiga risasi raia mwingine wa Uganda, Bw. Emmanuel Lugema, ambaye alikuwa akituhumiwa kuwa ni miongoni mwa wavamizi waliokuwa wakijaribu kukimbia.
Source: Majira
 
Wale waganda wa Kinondoni pia walikuwa wafanya biashara mazee, tusiwe wavivu wa kufikiri


Waganda waliotuhumiwa kuua askari, mbwa waachiwa
Posted on March 10, 2008 by admin
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imewaachia huru washitakiwa wanne kati ya watano Raia wa Uganda waliokuwa wakituhumiwa kuua askari watatu pamoja na mbwa.


Mahakama iliwaachia huru raia hao wa Uganda mwishoni mwa wiki mbele ya Jaji Thomas Mihayo baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP) kuwasilisha nolle akiiomba mahakama kuwaachia huru kutokana na kuwa hana nia ya kuendelea kuwashitaki.
Kwa mujibu wa nolle iliyowasilishwa mahakamani hapo, iliwataja washitakiwa ambao DPP hana nia ya kuendelea kuwashitaki, ambao ni
Bw. Mawanda Maalo, Bw. Hawalulema Venist, Bw. Sylvester Salugo na Bw. Mohamed Simbwa Mohamed.
Uamuzi wa DPP wa kuwafutia washitakiwa wanne pia uliambatana na uamuzi wa kuendelea kumshitaki mshitakiwa mmoja ambaye pia ni raia wa Uganda Bw. Abdul Karim Msanje, ambaye atakabiliwa na mashitaka hayo ya mauaji.
Mshitakiwa huyo anatumikia kifungo cha miaka 15 jela kufuatia makosa ya kupatikana na silaha pamoja na risasi ambapo alikamatwa na bunduki mbili aina ya SMG AK 47 zenye namba 1975-230912 na 56-3903138 pamoja na risasi 87 ambazo zinadaiwa kutumika kwenye mauaji ya hao askari na mbwa.
Watuhumiwa hao walidaiwa kuwaua askari namba D.1672 Koplo Hassan, E.7324 D/C Ramadhani na E.7999 D/C Deogratius mnamo Mei 25, 2003 huko Kawe, Dar es Salaam.
Mbali na kuua maaskari hao pia walidaiwa kuua mbwa wa polisi, Rogger ambao walikuwa wanatumika katika doria ya siku hiyo.
Ilidaiwa kuwa, majambazi hao walianza kuwafyatulia risasi polisi wakati dereva anataka kuondoa gari hivyo kupoteza mwelekeo na kuacha barabara na kupindukia mtaroni, wakati huo huo majambazi wakiendelea kufyatua risasi.
Mapolisi watatu walikufa papo hapo na wengine kujeruhiwa vibaya ambapo Siku chache baadaye waliwakamatwa Waganda hao kwa tuhuma za mauaji hayo.
Polisi pia walimpiga risasi raia mwingine wa Uganda, Bw. Emmanuel Lugema, ambaye alikuwa akituhumiwa kuwa ni miongoni mwa wavamizi waliokuwa wakijaribu kukimbia.
Source: Majira

Kweli kabisa mkuu, na huyu jamaa alikuwa na duka kubwa la mafriji na vifaa vya umeme used pale Kinondoni, watu tulikuwa tunamjua kuwa ni mfanyabiashara mzuri kumbe alikuwa na shughuli nyingine!!
 
Kumbe marafiki wa JB wanajulikana,lol! Actions speak louder than words....
 
Ujinga kama huu wako ndio janga halisi la kitaifa-watu kupenda uzushi au ku-conclude mambo bila hoja au ushahidi wowote!JB(ingawa simjui) ni janga la taifa kivipi?Halipi kodi?Yeye ndie anayefanya sisi tusifanye kazi na kuishia kuimba nyimbo za ufisadi na freemason?Kuna mtanzania amezuiliwa kufanya biashara Uganda?Tatizo letu ni elimu ya kukariri na kujibu mitihani ya darasani tu.Huu ndio utandawazi uliokariri darasani,watu wanazunguka dunia nzima kutafuta business opportunities.Acha JB afanye kazi huku sisi tukiendeleza porojo zetu za kuogopa kujiunga na EAC kwa sababu ya uvivu wetu.Unamwita JB malaya na kusahau kuwa kama ni umalaya si anaufanya na Watanzania wenzetu,kwa nini tusiwalaume hao watanzania wenzetu,let's deal with our own failures first.

Well said mkuu. Tumekuwa watu wa kufuatilia issue za watu (si vibaya kama kuna mashaka) na kila tunapoona wamefanikiwa harakaharaka tunawaza ni mafisadi. Ni afadhali mtu anayekuja na jina la JB humu jamvini aje na ushahidi unaoonesha uwalakini kwenye mali anazomiliki. Lakini kama ni kuumizwa na utajiri wake tu itakuwa haina maana yoyote.

Hii spirit ya kushindwa kuthubutu ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Leo hii Kenya Commercial Bank (KCB) ina matawi lukuki hapa kwetu lakini benki zetu kama za NMB, CRDB na NBC zimebaki zikiimba wimbo wa 'simbanking' na Mobile Branches humuhumu ndani. Hivi tumeshindwa kweli kupenetrate kwenye masoko ya EAC hadi kuanza kuoneana vijicho?

Hawa matajiri wetu (ambao wengi wao utajiri ni matokeo ya kufisadi fedha za umma badala ya kutumia njia halali kutajirika) wameshindwa kweli kutumia mapesa yao hayo walau kuwekeza kwenye ukanda huu wa EAC?

Ni bahati mbaya kwamba, Wabongo tumekuwa kama malimbukeni mtu anachuma mamilioni ya fedha badala ya kuwekeza wengi wanakuwa wa kuzunguka kwenye makasino, uzinzi wa kupindukia na anasa za kutisha. Kwa kuwa fedha zinatokana na uharamia + Ufisadi, uchungu unakuwa hakuna. Tunapaswa kubadilika mind set zetu.
 
Kwa kiasi kikubwa inaonekana watu wanamjua kile kilichowekwa mbele yao. Kitu pekee ambacho naona kimekosekana sana ni kushindwa kuhusisha influx pia ya baadhi ya waganda ambao wameamua kubadilisha majina... ili kufanya biashara fulani fulani.

Waliomkaribisha pia wamejioyesha hadharani.
 
Kumbe marafiki wa JB wanajulikana,lol! Actions speak louder than words....

Kulingana na MKJJ sasa tujaribu kuunganisha ujio wake kwanza then tuangalie waganda wenzie waliokaribu yake ambao wanafanya biashara lakini walishabadili majina yao halisi, kwa kumbukumbu zisizo rasmi nafikiri huyu jamaa aliingia kati ya 2003-2004 rais akiwa ..Mr Clean? Sijui Somali Pirates walikomaa lini, Sijui Meremeta ilikomaa lini, Sikumbuki biashara za silaha za Bout zilikomaa lini, anyway nabahatisha tu
 
Wewe si ndio mwenye ile sifa humu JF "Ufataani".

Ulisema sana humu kuhusu Richmond na Dowans ilipogeuzwa na kuwa Symbion ukakaa kimya na kuufyata, kwanini?
:yawn::yawn::yawn:Ngoja nikatafute ugali kwa mama kanjinji wa mtaa wa gerezani.
 
Hotel za East Africa Arusha ni za PPF. Hawa wasomali wanaendesha tu - management lakini majengo ni ya PPF.

Hata paradise ya mkapa tower hawamiliki jengo that is why i told you wanamiliki hotel
 
Mkuu Mwanakijiji samahani naona bado macho yangu yana matongotongo na roho yangu inakataa kuamini hata hiki kidogo ninachokisoma lakini tuendelee na mjadala. Macho yanajawa na matongotongo kwa machozi kwa vile najitahidi kusoma kila mstari na pengine kurudia mara mbili na kujiuliza!'Tanzania yangu aliyetuloga yu wapi mbona hivi jamani???'
 
Lonestriker Mbona umetoka sana povu kwenye hii thread ndugu? What are you not telling us about this JB?

kutokwa povu ndio nini?Sorry dude,not all of us entertain misemo isiyo na maana,I mean sio wote tulikulia vichochoroni.Simjui JB na wala sikuwahi kumsikia kabla lakini bahati nzuri nimefika mpakani mwa Tanzania na Uganda na kujionea tofauti ya wafanyakazi na sisi watu wa porojo.kwa mtu yeyote aliyefika mpaka wa Mutukula atakuambia tofauti ya kimaendeleo iliyopo katika upande wa kwetu na ule wa wenzetu wa Uganda.Binafsi roho iliniuma sana pale Mtanzania mwenzangu aliponiomba hela ya Uganda badala ya kitanzania tena katika ardhi ya Tanzania anapofanyia biashara yake ya mgahawa,do you know why?Ni kwamba vitu vingi wananunua sehemu ya Uganda kwa sababu Sehemu ya Tanzania hamna kitu,ni vibanda viwili vitatu tu.Huu ndio ujinga wetu unao nitoa povu.Na hali kama hii inajirudia katika mipaka yetu mingine.Tumelala then wakija wageni wachapakazi tunaanza kuropoka bila sababu za msingi.
 
Udom ujenzi unaisha 2015. KIU NI KAMA BAFU TU.

Ndio yale yale niliyoaandika mwanzo,ugonjwa wetu wa kuendekeza mipango isiyoisha.KIU wana matawi karibu ukanda wote wa Afrika Mashariki,sisi kumalizia tu chuo kimoja inatuchukua miaka kumi!KIU ni chuo binafsi lakini angalia kasi yake ya kukua inazidi kasi ya vyuo vyetu vikongwe ambavyo bado vina intake ya mara moja kwa mwaka!Tuendeleze misemo yetu,ndio urithi wetu(KIU kama bafu!).
 
Well said mkuu. Tumekuwa watu wa kufuatilia issue za watu (si vibaya kama kuna mashaka) na kila tunapoona wamefanikiwa harakaharaka tunawaza ni mafisadi. Ni afadhali mtu anayekuja na jina la JB humu jamvini aje na ushahidi unaoonesha uwalakini kwenye mali anazomiliki. Lakini kama ni kuumizwa na utajiri wake tu itakuwa haina maana yoyote.

Hii spirit ya kushindwa kuthubutu ndiyo imetufikisha hapa tulipo. Leo hii Kenya Commercial Bank (KCB) ina matawi lukuki hapa kwetu lakini benki zetu kama za NMB, CRDB na NBC zimebaki zikiimba wimbo wa 'simbanking' na Mobile Branches humuhumu ndani. Hivi tumeshindwa kweli kupenetrate kwenye masoko ya EAC hadi kuanza kuoneana vijicho?

Hawa matajiri wetu (ambao wengi wao utajiri ni matokeo ya kufisadi fedha za umma badala ya kutumia njia halali kutajirika) wameshindwa kweli kutumia mapesa yao hayo walau kuwekeza kwenye ukanda huu wa EAC?

Ni bahati mbaya kwamba, Wabongo tumekuwa kama malimbukeni mtu anachuma mamilioni ya fedha badala ya kuwekeza wengi wanakuwa wa kuzunguka kwenye makasino, uzinzi wa kupindukia na anasa za kutisha. Kwa kuwa fedha zinatokana na uharamia + Ufisadi, uchungu unakuwa hakuna. Tunapaswa kubadilika mind set zetu.

Mafisadi wa Tanzania huweka pesa kwenye akaunti za nje badala ya kuwekeza na kutoa ajira kwa watu waliowaibia,hovyo kabisa.
 
kutokwa povu ndio nini?Sorry dude,not all of us entertain misemo isiyo na maana,I mean sio wote tulikulia vichochoroni.Simjui JB na wala sikuwahi kumsikia kabla lakini bahati nzuri nimefika mpakani mwa Tanzania na Uganda na kujionea tofauti ya wafanyakazi na sisi watu wa porojo.kwa mtu yeyote aliyefika mpaka wa Mutukula atakuambia tofauti ya kimaendeleo iliyopo katika upande wa kwetu na ule wa wenzetu wa Uganda.Binafsi roho iliniuma sana pale Mtanzania mwenzangu aliponiomba hela ya Uganda badala ya kitanzania tena katika ardhi ya Tanzania anapofanyia biashara yake ya mgahawa,do you know why?Ni kwamba vitu vingi wananunua sehemu ya Uganda kwa sababu Sehemu ya Tanzania hamna kitu,ni vibanda viwili vitatu tu.Huu ndio ujinga wetu unao nitoa povu.Na hali kama hii inajirudia katika mipaka yetu mingine.Tumelala then wakija wageni wachapakazi tunaanza kuropoka bila sababu za msingi.

maelezo yako ni mazuri lakini hapa si sehemu sahihi,rudia kusoma swali hapo juu..
 
maelezo yako ni mazuri lakini hapa si sehemu sahihi,rudia kusoma swali hapo juu..
What is your point?Yaani maelezo yawe mazuri lakini hayatakiwi...logic iko wapi?Umenikumbusha wale wabunge wetu ambao kila mwaka wanatoa kasoro mia na kuishia kuunga hoja.Mpaka sasa hakuna mtu aliyekuja na fact yoyote au hoja yoyote inayoonesha kuwa JB ni janga la taifa.So far watu wanaleta porojo zisizo na connection yoyote na ' JB kuwa janga la taifa'.
 
Back
Top Bottom