Je, CCM na TISS wanakuzwa nguvu zao kuliko uhalisia (Overrated)?

Vile vile CCM imejishikanisha na Dola, hakuna namna utatenganisha ÇCM na Dola. Leo makanari wa Jeshi wanapewa ukuu wa mikoa, wialaya, ubalozi, nafasi kwenye mashirika n.k. hivyo hakuna namna hawa watu wakawa kinyume nao.
Hili lipo wazi kabisa, uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 umethibitisha hili.
 
Wewe unatumia mihemko kwenye mjadala. Ni tatizo la Watanzania wengi.
 
Ccm wasikudanganye Hawana hiyo master plan ya kuandaa viongozi, viongozi wengi wameazima kutoka chadema, kina kitila katambi na wenginena

BADO mtu wa cdm akiunga mkono juhudi wanashangilia mpaka wanafanya sherehe kuanzia kamati kuu na nec yao.

Waliyo wapuuzi wametumia trillions kuwawshawishi wapinzani Waunge mkono juhudi
 
Nadhani waliondolewa kwenye utendaji wakabaki kuwa washauri tu...Hii ilifanyika sambamba na mageuzi yale yaliyosimamiwa na WB/IMF enzi za awamu ya tatu...

Nikiangalia kwa jicho la tatu, hapa wale wenzetu waliona chombo hiki kingeendelea kuwa kilivyokuwa kingekwamisha mambo mengi sana yasitokee jinsi wanavyotaka wao na remote control zao kupitia wanasiasa ambao huwaghilibu kwa vi incentives fulani fulani na kutokana na background zetu za kukirimiwa tukalainika basi ikawa asabuhi ikawa jioni; ufisadi ukatamalaki, makundi yakajengeka huku wao wakishindwa kuingilia kati kwakua kuna level yao ambayo hawawezi vuka.

Pamoja na constraints zoooote hizo, bado wamefanya kazi kwa weledi na uaminifu ndiyo sababu hadi leo bado nchi haija vurugika. Nchi yetu relatively ina taasisi moja wapo hiyo ambayo ni imara...CCM pia imesaidia kuendeleza hii consistency japo kuna wachache ambao wanataka kupoka madaraka na kuyamiliki (tupende au tukate CCM bado ni taasisi imara ambayo imeshindikana mtu kuimiliki). Hapa tukae mguu sawa sote wenye nia njema na nchi yetu kukataa hilo, ili katika hii transition ya kufiwa pasipo kutegemea tuweze kujenga taasisi zetu huru na imara...Nikifikiria hayo sioni jinsi ambavyo wazee wetu waaminifu watashindwa kuunda a neutral body itakayowekewa makatazo ili itupeleke salama katika kuandika Katiba mpya na kutengeneza serikali pamoja na kuondoa hizo dosari zinazoiuzia idara yetu kuingilia utendaji pale inapobodi hasa kukitokea hatari ya mtu kupitia vyeo vya siasa kuamua matamanio yake yawe ndiyo ya watu wote kwakua tu ana institution power...
 
Kinachowabeba ccm na tiss yao ya kipuuzi ni ujinga wa wananchi
 

CCM Kama chama Legacy yake kubwa inang’arishwa sana na Mwl JK Nyerere hapo ndipo kinapopata heshima kubwa na kuwa ni chama pendwa kwa wazee ,watu wazima na hata baadhi ya vijana (sio wote)

Kwa walio wengi wanakiona CCM ndio chanzo cha amani tulio nayo sasa (siwalaumu). Yawezekana kuna ukweli ndani yake lakini haiondoi ukweli kua mitazamo hiyo imejengwa kutokana na kua na chama kimoja madarakani tangu uhuru na kufumbata madaraka ya uongozi na kuminya kukua na kustawi kwa vyama pinzani (siwalaumu chama chochote kingefanya hivo)

Nje ya tanzania ni kweli CCM inaoneka ni chama imara na kinabeba sifa zote nzuri za uongozi tulizo nazo leo pamoja na amani amabayo tumekua tukisifiwa!!…
Sifa hizo ni pamoja na
-Kuwa chachu ya uhuru wa nchi nyingine za Africa ikiwemo Msumbini,SA,nk
-CCM inatajwa kua ndo kikwazo cha Rwanda kushindwa kuingilia mambo ya ndani hasa ukizingatia ndicho chama chenye nguvu na kilichoshika serikali !! Ikumbukwe kwamba Rwanda imeweza kua inaingilia mambo ya ndani ya nchi majirani DRC,Burundi na hata Uganda nchi ambayo wamekua marafiki kwene mikatakti yao!!..Hapa chanzo cha mzozo ni ushiriki wa Tanzania katika kutokomeza m23 mwaka 2013,pia mzozo wa PK na kikwete Uliopelekea operation ya kuwafukuza wahamiji haramu Kigoma miaka ya nyuma (katafute jikumbushie)

-Lakini pia CCM inatazamwa kama chama chenye ushawishi kwa nchi za SADC na nchi majirani

TISS kama Taasisi imekua imara tangu kipindi cha Mwalimu ambapo miaka ya 60 Tanzania ilikua n nchi yenye nguvu na ushawishi mkubwa kusini mwa jangwa la sahara!!

Lakini pia imekuja kung’ara kipindi cha Mkapa
ambapo nchi ilikua inapitia baadhi ya sintofahamu ikiwepo vurugu 2001,Vugu vugu za kidini na vitu vya ivo!!

-Pia awamu ya tano Taasisi hii nyeti iliboreshwa kwa mishahara minono na kupewa kipau mbele sana!!
-Taasisi hii pia imefanya kazi kubwa kutoa taarifa za muhimu juu ya kundi la kigaidi lililotaka kuo mizizi KIBITI, na kufanikisha kulisambaratisha kama si kulipoteza kabisa ndani ya nchi

- TISS imeonekana na kazi kubwa sana hasa ukizingatia Raisi aliyekua madarakani ali waamini sana na kuwa tumia kupita kiasi ukilinganisha na mtangulizi wake!!

Inadhaniwa katika kipindi hiki TISS ilikua inapitia Transformation ya hali ya juu!! Hasa kutokana na utofauti ambao raisi na serikali ilikua ikiufanya!!
-Uongozi uliokuepo ulitofautiana na serikali zingine hivo kuwakana au kuwageuka wanasiaasa na wafanyabiashara waliokua na mizizi katika serikali kwa zaidi ya miaka kumi hivo kuongeza maadui wa serikali ya kipindi hicho!! hivyo TISS ilipewa mzigo mkubwa kwani maaduni wa utawala waliongezeka

-Pia inasadikika TISS iliactivate /kuanzisha kitengo cha intelligencia ya uchumi , ambapo walikua wakifanya intervertion juu ya Mipango ya kiuchumi ya nchi za kigeni juu ya nchi ya tz!! Hilo lilileta taswira tofauti hasa kipindi cha korona,Ukuta wa merelani,Bandari ya bagamoyo, pia walisaidia kuanza ujenzi wa bwawa la Mwl nyerere katka mto rufiji ambalo hata Mwl nyerere alikaliwa kooni na nchi za magharibi hivo kushindwa kulianza ( Ikumbukwe kwamba kazi ya intelligencia ni kukusanya taarifa na kuisaidia kufanya maamuzi sahihi) hivo hayo mambo yaliyotajwa ndio mchango wake

-Pia Taasisi hii nyeti ndiyo ilimuwezesha raisi wa kipindi hicho kuwez kujua kila kinachoendelea nje na ndani ya nchi!! Ikiwemo kila taasisi zote za tanzania!! Mtu atajiuliza Raisi alikua anajuaje makosa/Madudu kwene wizara fulani hasa ukizingatia alikua abafanya ziara za kushtukiza !!Hapa ndipo kinapokuja hiki kitengo kuwa effective kwene kupeleka taarifa zote

-Pia kitengo hiki ndicho kilikua muhimili na usalama wa kiongozi wa nchi hadi sasa!!

Kufeli!!…
-Ccm na tiss kufeli…..Ndiyo

-CCM haikua imejiandaa wala kujipanga kwa mabadiliko ya haraka kiasi hiki!!.Kama ilivo kawaida hatukuwai kupata dharula kama nchi iliyopata ya raisi kufia madarakani (failure ya kwanza hawakuliona likija)
Ila walielewa kua VP ndiye raisi mtarajiwa pindi ambapo raisi atafariki akiwa madarakani lakini hawakuona uwezekano au walipuuza sana hilo kutokea (Hili linajidhihirisha walivopigwa butwaa pindi msiba ulivotokea iliwachukua muda kujipanga na hawakupangika hadi leo wanafuana)

-Hivo kitendo cha Raisi kutoka ilihali yupo madarakani na hajamaliza muhula ilivuruga mipango yoooote iliyopangwa (Na tuwe wawazi huu haukua sehemu ya mpango wao nadhani)

TISS nao hawakuliona hili ( So pamoja na effective yao lakini hili liliwaponyoka na hapo tunasema Failure of intellince of Tiss)
 
Sasa nachojiuliza kama CCM ni mabingwa wa siasa inakuaje hawakujiandaa na mbadala wa JPM (maana ugonjwa wake ulifahamika) kiasi walalamike as if SSH ni zao la CUF au TLP?
Hawa ccm kwa porojo na propaganda hawajambo.

Masterplan ya miaka 75 mbele lakini miaka hii miwili tu full kulalamika🤣🤣
 

Mkuu ukifuatilia hamna raisi anaetaka Katiba mpya !!Hayupo
Kila raisi akifika anafurahia madaraka mapana ambayo katiba imemuachia….
Kama kweli JMK alitaka katiba basi jiulize miaka 10 aliyokaa alishindwaje??
Utagundua nayy hakua serious alitaka atumie uhuru aliokua nao alafu akiwa anatoka ndo aanzishe ili imbane rais mwingine si yy!! kitu ambacho raisi anaekuja nae hawez kubali kuendeleza!! HIVO hivo kwa JPM nae angefanya hivo mwaka wa mwisho anaanzisha mchakato!!..
Rais pekee atakae badilisha katiba ni yule ataye anza nayo anapoingia madarakani
 
Kwani Rais ndio anaamua katiba mpya? Na ndio maana nimesema TISS na CCM wapo overrated maana ilipaswa wasimamie walichoweka kwenye ilani Yao ya 2015.

TISS inge organise lobby groups kuanzia bungeni mpaka majukwaa ya dini na burudani kuleta vuguvugu la katiba mpya maana mwisho wa siku katiba ni kwa faida ya wote sio Rais pekee.

Hata CCM kama chama lazima watambue katiba ni muhimu kwao pia, mfano wao wanasema wanaishauri Serikali lakini katiba inasema Rais hawajibiki kuchukua ushauri!!! So unakuta hata wao wanakosa meno kwenye katiba ya sasa maana Rais anakua juu ya chama by far so hakuwezi kuwa na uwajibikaji wa serikali.

So katiba isiwe kwa hisani ya Rais ila kwa integrated approach ya makundi yote Ili mchakato uanze kwa matakwa ya wananchi na sio maamuzi ya Rais. Tumeona hata huko nyuma kuna sera zililetwa baada ya kelele za Raia na lobbyists.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…