Je, dini ni upendo au ni chuki? Vita na mauaji yaliyokithiri

Je, dini ni upendo au ni chuki? Vita na mauaji yaliyokithiri

Madhara ya watu kuacha dini ni makubwa Sana kwenye Jamii, tutapata kizazi kisichojua jua kutenganisha mabaya na mema. Kupata Jamii isiyo na maadili,Jamii isiyo na maadili utoa viongozi wabovu.
mzwhpo7tiav71.jpg

Ume iona hii chart, je hayo uliyo andika kama madhara ya watu kuacha dini yapo kwa kiwango gani katika hayo mataifa ?

Vipi na sisi taifa lililo na watu wengi wenye dini hayo mambo uliyo orodhesha yapo kwa kiwango gani ?
 
View attachment 2458368
Ume iona hii chart, je hayo uliyo andika kama madhara ya watu kuacha dini yapo kwa kiwango gani katika hayo mataifa ?

Vipi na sisi taifa lililo na watu wengi wenye dini hayo mambo uliyo orodhesha yapo kwa kiwango gani ?
Wao sio sisi, mfumo wao wa malezi na maadili yao tu ni dini tosha.
 
Unaji kanganya kupitia maelezo yako ya awali na sasa.

Kuwa na siku njema.
Hao ni watu wa mataifa mbalimbali kila moja lina dini imedominate, uislamu, Ukristo,uyuda,shinto,bhudha, nk. Kupata mlinganisho ni hadi upate picha kuhusu hali yao kimaadili ipoje.
 
Je Mungu wa hizo dini ndie anaye toa maagizo hayo yatekelezwe na wafuasi wake ?
Hakuna. Usihukumu usije ukahukumiwa
Ambaye anajua hana dhambi awe wa kwanza kumrushia jiwe huyu kijana. Wote tuna dhambi huwezi kumhukumu mwenzako ikiwa wewe una dhambi. Mungu ndiyo anahukumu.
Mungu hana dini.
 
Hao ni watu wa mataifa mbalimbali kila moja lina dini imedominate, uislamu, Ukristo,uyuda,shinto,bhudha, nk. Kupata mlinganisho ni hadi upate picha kuhusu hali yao kimaadili ipoje.
Kwa ni hiyo chart ime elezea nini ?
 
Hayo kuwa Uislamu ulianzishwa na ukatoliki ili kuitawala Arabia.
Mbona lipo wazi,mfano chek tu mafundisho yaliyomo kwenye Quran imekopi kutoka yaliyopo kwenye Biblia yaani vitabu vya Injili,taurat na zaburi.
Maelezo ya kina yapo ukisearch google utapata. Mfano. Did Roman Catholic creat islam?,
Uislamu ni ukatoliki. Nk utapata link mbalimbali. Hata JF upo uzi huo.
 
Majimaji war 1905-07
Algeria war of independence 1954-62
Kagera war 1967-69
Ukraine war 2022-
Chinese civil war 1945-49
WWI 1914-18
WWII 1939-45

Hii ni baada ya wote Yesu na Muhammad (PBUH) kuishi na kufa lakini sababu za vita hapo juu haikuhusisha dini yoyote ile na orodha ni ndefu sana siwezi andika yote hapa.
Andiko lime jikita katika dini na vita zake sio ukoloni na vita za ukombozi, kwa kua hizi vita ulizo orodehesha hapa zina tutoa nje ya andiko.
Hii inatokea pale wanaodai wanafuata dini fulani (hizo tatu ulizotaja) hawafuati kikamilifu.
Kufuata dini kikamilifu ni kufanya nini ? Na kivipi unasema hao hawakufuata dini kikamilifu wakati walihusika katika usambazaji na uteteaji wa dini mpaka kufika maeneo mbalimbali ?
Maana ya dini ni; Dini ni mfumo wa maisha ya wanaadamu, kwa maneno mengine ni muenendo mzima wa maisha ya mwanaadamu ndiyo dini.

Dini hizi ktk ile hali ya uhalisi wake kama alivyokuja nayo Mussa (AS), Yesu(AS) na Muhammad (PBUH) hazina shida kabisa na zilikua ktk misingi na lengo lake.
Dini sio tu mfumo wa maisha, dini ina husisha swala la kuabudu kitu kiitwacho na wana dini Mungu au Muungu. Mfumo wa maisha haukamiliki kuitwa dini kama hausishi swala la kuabudu.

Ndio maana sio kila mfumo wa maisha ni dini.
Dini ktk uhalisi wake hakuna kushika mapanga, haya mapanga ya akina Anti Baraka, Al Qaeda, Alshabaab, Lord Resistance Army na wenzao wako kinyume kabisa na mafundisho ya dini zote tatu.

Mathalani, Uislam unahalalisha vita endapo moja ya sababu ya kuingia vitani ni pale ambapo jamii itapokonywa ardhi yake, na hata katika vita hivyo kuna sheria za kufuatwa ikiemo kutokata miti bila sababu, kutoua watoto, wanawake, wazee wala walemavu na hata wakishinda vita basi ni dhambi kulazimisha maadui wao kusilimu wala kubomoa makanisa na masinagogi wala kuua wachungaji, marabi na watumishi wa dini.
Anhaa kumbe halalishwa kwa vitu maalumu tu ? Kwa nini usihalalishwe upendo kwa vitu vyote na sio dini kuchukua uamuzi huo ?

Vile Vita vya kijihad vilivyo sambaza uislam west Africa vili kuwa nini kwako ?

Kwa hiyo wayafanyayo hayo makundi kwa kutumia maamrisho ya Quran hawapo sahihi ?
Dini hizo zote zinahimiza upendo na ushirikiano baina ya watu wa imani tofauti.

Mathalan ukristo unahimiza watu kuwapenda majirani zao kama wanavyozipenda nafsi zao.

Uislam pia unahimiza kuwatendea wema majirani, na tafsiri ya ujirani ni nyumba arobaini toka nyumbani kwako hao wote wanahesabika kuwa ni majirani.

Uislam unaruhusu Muislam kumuoa Mkristo.

Uislam unaruhusu Muislam kula nyama ya mnyama aliyechinjwa na Myahudi ama Mkristo (sharti mchinjaji awe amemtaja mungu mmoja wakati wa kuchinja)

Kwahiyo Mafundisho ya dini hizi tatu hayafundishi chuki, ubaguzi wala uharibifu wowote bali kinyume chake.
Kuwa ita watu makafir sio chuki na ubaguzi?, Kuwa ita watu wapumbavu wasio amini wao sio ubaguzi na chuki ? Kuwaita watu wapotevu wale wasio kubalina na mafundisho ya dini zao sio chuki na ubaguzi ?

Wana wapendaje watu wasio na dini wakati wame wapachika jina la wana wa shetani, waovu, wachawi kila jambo lisilo faa wana pachikwa.

Wewe ndugu muislam ana ruhusiwa kula nyama iliyo jinjwa na mtu asiye muislam ? Waislam wa wapi hao ? Imekwisha sahau vurugu zilizo tokea katika ya waislam na wakristo hapa nchini kuhusu hilo swala ?

Una semaje mafundisho ya hizo dini haya ruhusu chuki wakatik kwa matendo na maneno chuki zina zihirishwa na hizo dini.
Mafundisho ya dini hizi zote yanafundisha Mungu wa upendo.
Mungu wa upendo aliye amrisha Vita na chuki kwa wasio wafuasi wake si ndivyo ?
Hapana, kimsing jamii unayoiona hii leo ni matokeo ya wao kwenda makanisani na Misikitini, unadhani zimeharibika? Basi jaribu kuondoa hizi dini uone uharibifu ulio wa kweli.
Huo uharibifu ulio kuwepo kabla ya hizi dini ni upi ? Naomba uni orodheshee
Zipo sababu za msingi ktk kuanziwha vita takatifu kwenye dini hizi.

Nitasemea uislam, kwenye Uislamu moja ya sababu ya jamii ya kiislam kuingia vitani ni kama kutatokea jamii nyingine itakayo lenga kuwapora ardhi yao.

Niamini mimi hata atikee mtu atake kukupora nyumba yako ni lazima huyo mtu utamuona ni shetani.

Vinakuwa vita vitakatifu kwa sababu; wakazi wa ile ardhi ni watu wa Mungu, wanaomuabudu na kufuata sheria zake kikamilifu… yeyote anayepanga kuharibu utaratibu huu mzuri wa Mungu huyo ni mharibifu na anapaswa kuonywa kuachana na chokochoko zake, ikiwa maonyo hayatafanya kazi basi ni lazima apigwe kikamilifu kwa msaada wake Mungu ili kuokoa sheria, utaratibu na watu wa Mungu.
Sababu za msingi ni zipi kuanzisha mauaji ya watu wakati hizo dini zime jiita dini za upendo na haki ?
kwa hiyo maamrisho ya mauaji yame haralishwa katika uislam je upendo na amani hapo upo wapi ? Kwani matumizi ya njia za amani haiwezekani ? Na kwa nini dini ihusike kupigania ardhi kwa vita ?
Nita muona shetani kwa misingi ipi ?

Kwani huyo Mungu wa hiyo dini hawezi kuirudisha hiyo ardhi kwenu kwa njia ya amani bila kuwa amrisha wafuasi wake kupigana vita vya umwagaji damu ?
Wasambazaji halisi wa hizi dini Mussa (AS), Yesu (AS) na Muhammad (PBUH) walikuwa ni watu wema na mfano bora sana kwa watu wao na ndiyo maana walipata wafuasi wengi sana.

Pta picha Yesu(AS) amefariki miaka 2000 iliyopita lakini mpaka sasa kuna zaidi ya watu bilioni 2 wanamuamini na kufuata mafundisho yake

Pata picha Muhammad (PBUH) kafa zaidi ya miaka 1400 iliyopita lakni mpaka sasa kuna zaidi ya watu Bilioni 1.5 wanamuamini na kufuata mafundisho yake.

Ingekuwa watu walisambaziwa kwa hofu niamini wangekwisha achana na mafundisho yao.

Kwa maana aliyewatia hofu keshakufa yanini wabaki na mafundisho yao?
Hata China Mao aliye kufa zaidi ya miaka 30 iliyo pita aliye ua watu kwa sera zake mbovu mpaka leo kuna watu wana muamini na wengine wana mchukulia mtakatifu kufa miaka mingi iliyo pita haifanyi makosa yasi sahihishwe.

Kuwa na wafuasi wengi sio kigezo kuwa hicho kitu ni bora kila pande na hakina madoa.

Kwa hiyo hivyo vita vitakatifu vilikua upendo na sio hofu kuridhia mafundisho kwa shingo uapande, una ifahamu Age of reason in Europe kili tokea kitu gani ?

Bado mafundisho yaliyo rithishwa vizazi na vizazi yana watia hofu wafuasi wake kuhusu adhabu watakazo pata siku wa mwisho endapo wakijitenga na hizo dini na huyo Mungu wa hizo dini.
Hapana, idadi kubwa ya waumini hawajui sehemu kubwa ya historia ya Dini zao.

Na hili ni tatizo kubwa.
Wanapaswa kujifunza zaidi ili wawe huru kimaamuzi na kiimani na sio kuishi kama wafungwa au watumwa.
Ni hatarishi kivipi? Sijaelewa
Kwa wale ambao hawakuwa wafuasi wake toka kale mfano upagani
Mwafrika si mtumwa tena, Mwafrika ni mtu mwerevu mwenye maarifa ha mazingira yake.

Mwafrika ana uwezo na utambuzi wa kugundua kuwa Mungu yupo na ili tuishi ktk jamii yenye maadili na maendeleo ni lazima tufuate sheria zake.

Ziko dini nyingi ila ni jukumu la Mwafrika kutafiti na kujua ni ipi dini ya kweli ili aifuate.
Kwa hiyo mwafrika ni shabiki tu katika uwanja wa hizi dini ?
Kwahiyo sababu ya uharibifu hapa duniani si Dini, sababu ni mwanaadamu mwenyewe.

Maana uharibifu tuliuanza hata kabla ya dini hazijaja na tunauendeleza angali dini zipo na tena tunazitumia kama kichaka cha kufichia dhamira zetu ovu.

Dini ni kama kisu, Jikoni kinakata nyanya vitani kinatoa uhainwa mtu.

Je, tunathubutu kusema kisu ni kiovu?

Hapana, mtumiaji wa kisu ndiye ana hiyari akitumie kwa uovu au kwa wema.
Sijasema kuwa chanzo cha machafuko hapa duniani ni dini pekee la hasha usini nukuu vibaya .

Nimezungumzia dini kama chombo kinachoitwa chombo cha amani na upendo huku kikiwa kimejaa Vita za kutosha zilizo gharimu mauaji makubwa ya watu , chuki , masengenyo, utumwa, ubaguzi n.k

Chanzo cha machafuko dunia pia ukabila una husika, ukanda, siasa, tamaduni, falsafa n.k
 
Mbona lipo wazi,mfano chek tu mafundisho yaliyomo kwenye Quran imekopi kutoka yaliyopo kwenye Biblia yaani vitabu vya Injili,taurat na zaburi.
Maelezo ya kina yapo ukisearch google utapata. Mfano. Did Roman Catholic creat islam?,
Uislamu ni ukatoliki. Nk utapata link mbalimbali. Hata JF upo uzi huo.
Kwahiyo mfanano wa mafundisho ndiyo sababu ya kuwa Ukatoliki umeanzisha Uislamu?

Nashauri kama jambo huna ushahidi nalo, hujalisoma, huna uhakika nalo usiliseme mkuu.
 
Hakuna. Usihukumu usije ukahukumiwa
Ambaye anajua hana dhambi awe wa kwanza kumrushia jiwe huyu kijana. Wote tuna dhambi huwezi kumhukumu mwenzako ikiwa wewe una dhambi. Mungu ndiyo anahukumu.
Mungu hana dini.
Kwa hiyo huyo Mungu ana amrisha wafuasi wake kwenda kuuwa watu wasio upande wake hivyo ndivyo anavyo hukumu sio ?
 
Kwahiyo mfanano wa mafundisho ndiyo sababu ya kuwa Ukatoliki umeanzisha Uislamu?

Nashauri kama jambo huna ushahidi nalo, hujalisoma, huna uhakika nalo usiliseme mkuu.
Zipo ajenda nyingi nje ya mfanano
 
Kwa hiyo huyo Mungu ana amrisha wafuasi wake kwenda kuuwa watu wasio upande wake hivyo ndivyo anavyo hukumu sio ?
Maana yake.
Kipindi Yesu akihubiri, wakatokea watu wanataka kubeba mawe wamponde mwanamke kahaba. Yesu akawajibu
"Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumrushia huyu mwanamke jiwe" hakuna aliyethubu kwa maana hiyo Mungu ndiye anahukumu.
Mfano hai Sodoma na Gomora
 
Maana yake.
Kipindi Yesu akihubiri, wakatokea watu wanataka kubeba mawe wamponde mwanamke kahaba. Yesu akawajibu
"Ambaye hana dhambi awe wa kwanza kumrushia huyu mwanamke jiwe" hakuna aliyethubu kwa maana hiyo Mungu ndiye anahukumu.
Mfano hai Sodoma na Gomora
Mbona hautaji na vita na mauaji yaliyo kuwa yana tekelezwa kwa maamrisho ya huyo Mungu ?

Na kwa nini huyo Mungu ahukumu kwa mauaji ya kutisha wakati yeye na wafuasi wa dini zake wameji tanabaisha kuwa ni wa upendo vifo vya kutisha ni upendo ?
 
Mbona hautaji na vita na mauaji yaliyo kuwa yana tekelezwa kwa maamrisho ya huyo Mungu ?

Na kwa nini huyo Mungu ahukumu kwa mauaji ya kutisha wakati yeye na dini zake wameji tanabaisha kuwa ni wa upendo vifo vya kutisha ni upendo ?
Mungu hana dini wala Yesu hana dini
Dini ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu.
 
Mungu hana dini wala Yesu hana dini
Dini ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu.
Kwa ni huyo Mungu na huyo Yesu umemjua kupitia mafundisho ya nini ? Au ume mjua kupitia vitabu vya kihistoria ?
 
Mungu hana dini wala Yesu hana dini
Dini ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu.
Turudi kwenye majibu ya maswali yangu kuhusu maamrisho ya huyo Mungu kwa wafuasi wake kutekeleza.
 
Andiko lime jikita katika dini na vita zake sio ukoloni na vita za ukombozi, kwa kua hizi vita ulizo orodehesha hapa zina tutoa nje ya andiko.
Sikutoi nje ya mada najaribu kukuonesha kuwa si dini pekee iliyoleta vita, hata kabla ya dini zote vita na uharibifu vilikuwepo.

Na ukitaka kulifahamu vizuri Thomas Hobbes alieleza nadharia yake kuhusu ‘state of nature’ yaani kabla ya dola hali ilikuaje, anasema ilikuwa ni mbaya sana vita kati ya mtu na kila mtu, ustaarabu wala utaratibu haukuwepo kabisa.

Hizo vita za dini ulizotaja ni kasehemu kadogo sana ka picha kubwa ambayo hujataka kuionesha.


Kufuata dini kikamilifu ni kufanya nini ? Na kivipi unasema hao hawakufuata dini kikamilifu wakati walihusika katika usambazaji na uteteaji wa dini mpaka kufika maeneo mbalimbali ?
Mkuu kuna dhana ndogo sana naona zinakuchanganya, na hiyo ni sababu tayari una majibu yako kichwani (prejudice) kama unataka tuelewane nashauri ufungue akili yako, usitake kila jibu liendane na kile ambacho tayari unacho kichwani.

Umezisoma dini hizo tatu? Yaani mafundisho yake kutoka ktk vitabu vyake?

Na kusema kusoma sisemi kuwa umeona watu wanaodai kuwa wafuasi wa dini hizo wanavyoishi?

Kuna tofauti kati ya Mafundisho ya dini yanavyosema na Wafuasi wa dini tunavyoishi, ukielewa tofauti hii hili seali usingeuliza.

Kama ume ‘observe’ wafuasi wa dini wanavyoishi na hujajisumbua kufungua kurasa za Torati, Injili au Quran basi huwezi jibu hili swali, nashauri uzisome dini, usisome wafuasi wa dini mkuu.
Dini sio tu mfumo wa maisha, dini ina husisha swala la kuabudu kitu kiitwacho na wana dini Mungu au Muungu. Mfumo wa maisha haukamiliki kuitwa dini kama hausishi swala la kuabudu.
Sisi waislam tunafafanua maana ya dini kuwa ni mfumo wa maisha ya mwanaadamu.

Hilo suala la haukamiliki mpaka uhusishe Mungu hilo lako mkuu.

Ndio maana sio kila mfumo wa maisha ni dini.
Hii maana ni yako mkuu, au una ‘scholary reference’?
Anhaa kumbe halalishwa kwa vitu maalumu tu ? Kwa nini usihalalishwe upendo kwa vitu vyote na sio dini kuchukua uamuzi huo ?
Mkuu nauliza tena umesoma dini?

Maana unaandika ni kama vile umetazama wafuasi wa dini kisha ukaleta uzi hapa.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Mafundisho ya Dini ambayo huwa yanaegea kwenye vitabu vya dini husika, ukitaka kukosoa DINI ni lazima ukosoe maandiko mkuu, ukitaka kukosoa watu hapo unakosoa wafuasi wa dini, kuna tofauti.

Leo hii Wafuasi wa dini wengi hawaishi kama dini zinavyotaka.

Ungesoma Mafunzo ya dini ungekuwa na jibu kuwa Upendo kwa kila mtu umehimizwa sana.

Na kama ungeelewa asili ya wanaadamu tulivyo usingeuliza kuhusu ‘prgamatic conditions’ iliyo ktk uislam inayohalalisha vita.

Hivi vitu ni rahisi mbona mkuu.
Vile Vita vya kijihad vilivyo sambaza uislam west Africa vili kuwa nini kwako ?
Mkuu umesoma Mafundisho ya Dini?

Ni wapi kwenye Quran na Hadith sahihi (Hizi ndizo nguzo na Mafundisho ya Uislam) wamesema Waislam wafanye kama wanavyofanya magaidi wa Afrika Magharibi?

Lete aya au hadith.

Kama huna maana yake hujasoma dini, ila umetazama wale wanaojiita wafuasi wa dini, kitu ambacho hakitoshi kuwa kipimo cha dini.

Kuna Dini na wafuasi wa Dini, tupo pamoja mkuu?
Kwa hiyo wayafanyayo hayo makundi kwa kutumia maamrisho ya Quran hawapo sahihi ?
Ni wapi kwenye Quran imeamrisha hilo?

Nimekueleza sharti moja la vita ktk Uislamu na sharti za yepi haramu kuyafanya, je, hao unaosema wanafuata amri za Quran wametimiza sharti hizo?

Ukitaka kukosoa dini kosoa maandiko nasi tutafurahi kuja kujadiliana nawe, watu wamepewa ‘free will’ kufanya wanachotaka, hata wakisema ni wafuasi wa dini fulani ni jukumu lako kujiridhisha kama ni kweli wanafuata Mafundisho ya dini wanayoidai.

Na si iwe umekaa YouTube umeona mtu kavaa ninja anadai muislam nawe unahitimisha kuwa ni Muislam, ama unamuona mtu kavaa vazi la msalaba basi unahitimisha ati anamfuata Yesu (AS).

Do your homework mkuu:
Kuwa ita watu makafir sio chuki na ubaguzi?,
Kwani nini maana ya kafiri? Usijekuwa unachukia ilhali ni kweli wewe ni kafiri.

Ni sawa mtu ni mjinga, ukimuita mjinga anachukia japokuwa ni kweli yeye ni mjinga.
Mjinga ni mtu asiyejua jambo.

Kuwa ita watu wapumbavu wasio amini wao sio ubaguzi na chuki ?
Mfano bibilia inasema Zaburi 14:1 “Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema”.
Kwahiyo hapa Mpunbavu ni yule anaeamini hakuna Mungu, na kama wewe unaamini hakuna Mungu kwa maana hii ya kifungu hiki wewe sio Mpumbavu?

Kwa kiswahili Mpumbavu ni mtu asieyeelewa kile alichofundishwa, je, kama utafundishwa jambo na ukashindwa kuelewa wewe si Mpumbavu?

Mamluki ni askari wa kukodiwa, Je, wewe ukawa ni askari na ukakodiwa wewe si Mamluki?

Nadhani ktk hili ni watu kukataa nafasi walio nazo tuu.

Wakati mwingine ukiitwa Kafir uliza maana ya kafir, kisha jitathimini kama unaendana na maana hiyo, kama ndiyo basi wewe ni kafir.

Tumeelewana mkuu?
Kuwaita watu wapotevu wale wasio kubalina na mafundisho ya dini zao sio chuki na ubaguzi ?
Vilevile, kwani mpotevu maana yake nini?

Hapo hakuna chuki wala ubaguzi ni kwamba mtu kaambiwa ukweli na amekasirika.
Wana wapendaje watu wasio na dini wakati wame wapachika jina la wana wa shetani, waovu, wachawi kila jambo lisilo faa wana pachikwa.
Sasa rejea kwenye vifungu vya dini vinasemaje, kama vinahamasisha upendo hata kwa asiyeaminj basi suala la kuwaita wana wa shetani ni uzushi wa wafuasi wa dini na hilo halihusiani na Dini.

Soma dini, achana na wafuasi wa dini.
Wewe ndugu muislam ana ruhusiwa kula nyama iliyo jinjwa na mtu asiye muislam ?
Siyo asiye muislam, ni aliye Ahluh kitaab yaani aidha Mkristo au Myahudi.
Waislam wa wapi hao ?
Sio waislam wa wapi, hiyo ruhusa imetoka ktk Quran suuratil Maaidah:5
Imekwisha sahau vurugu zilizo tokea katika ya waislam na wakristo hapa nchini kuhusu hilo swala ?
Tazama dini inasemaje? Soma Quran soma Biblia soma Taurati

Kama ulikusudia kuwakosoa Wafuasi wa dini basi ungewalenga hao, nimeingia kwenye uzi huu nikijua zinakosolewa dini.
Una semaje mafundisho ya hizo dini haya ruhusu chuki wakatik kwa matendo na maneno chuki zina zihirishwa na hizo dini.
Ni wapi kwenye Biblia au Quran inahamasishwa chuki?
Mungu wa upendo aliye amrisha Vita na chuki kwa wasio wafuasi wake si ndivyo ?
Ni wapi chuki imeamrishwa? Nukuu kifungu.

Kuhusu vita kwenye Uislam zipo sababu ‘legitimate’ za kuanzisha vita, na zipo sheria za nini cha kufanya na nini si cha kufanya.

Kama unaijua asili ya wanaadamu katu huwezi kuondoa uwezekano wa vita, kufanya hivyo ni kuota.

Nitolee mfano mmoja wa jamii iliyostawi pasina vita au hata ‘elements’ zake.
Huo uharibifu ulio kuwepo kabla ya hizi dini ni upi ? Naomba uni orodheshee
Uko ‘serious’ hujui?
Mauaji, Ubakaji, Wizi, Rushwa, Uzinzi, Vita, Uchawi, Ulevi, Ufiraji, Kamari, Utumwa n.k
Sababu za msingi ni zipi kuanzisha mauaji ya watu wakati hizo dini zime jiita dini za upendo na haki ?
Mkuu Nakushauri hebu soma Human Nature kitabu kaandika Robert Greene,

Hobbes's Doctrine of the State of Nature kaandika Charles Edward Merriam kwa kuanzia.​


Tatizo ni kuwa hauna taarifa za kutosha za mambo unayozungumzia.

Wengi kama wewe huwa mnadhani suala la Dini ni suala jepesi lakini mnasahau kabisa asili ya Binaadamu na umuhimu wa hizi dini.
kwa hiyo maamrisho ya mauaji yame haralishwa katika uislam je upendo na amani hapo upo wapi ?
Mkuu unajua chochote kuhusu asili ya Binaadamu? Au walau Saikolojia zetu?

Nashauri soma hivyo vijitabu hapo juu walau wakati mwingine usiulize seali rahisi kama hili.

Kwenye Uislam mauaji ni halali kwa sharti maalum.

Moja mtu huyo aliua mtu au watu wengine pasina hatia.
Pili, mtu huyo alibaka na kusambaza fitna ktk ardhi.

Nikuulize swali; Leo akatokea mtu akambaka na kumlawiti mama yako, dada yako, mkeo na binti yako kisha akawa anajisifia kuhusu hilo

Ni adhabu gani utampa?

Kama utamsamehe ni kiasi gani cha watu utakuwa unawahamasisha kufanya kama alivyofanya wakijua watasamehewa na hakuna kitu watafanywa?

Panya fikra, tazama kwa mapana zaidi mkuu.
Kwani matumizi ya njia za amani haiwezekani ?
Unajua chochote kuhusu Peace building au peace keeping mkuu?

Umefutilia walau michakato ya kupatikana amani sehemu zenye mitafaruku?

Kama ndiyo hutauliza swali hilo.

Narudia mkuu soma asili ya Binaadamu, uhalisia wake sio kuota.


Na kwa nini dini ihusike kupigania ardhi kwa vita ?
Mkuu nisamehe najibu maswali yako kwa kuuliza swali.
Unajua lengo kuu la kuwepo dola?
Nikusaidie tu, ni ‘its survival’ na ukileta suala la ‘survival’ basi vita ‘isn’t an option’

Dini hutumika ktk kuunganisha watu wanaoitwa pamoja kupigania ardhi yao.
Rejea ‘Spanish colonization of South America’

Mkuu ukitaka kuunganisha watu katika lengo moja unatumia nini?mwalimu miaka ya ‘60 alitumia utaifa wetu kutuunganisha dhidi ya Uganda.

Wayahudi wanatumia Uyahudi wao kuunganisha watu na Wakristo kutetea ardhi wanayodai kuwa ni yao.

Wewe utatumia ninj, au ushapata picha kuongoza taifa au jamii hali huwaje?
Nita muona shetani kwa misingi ipi ?
Mtu akuporae nyumba yako, akambaka na kumlawiti mama yako, mkeo, dada yako, bintiyo utamuona ni mkombozi? Au ?
Kwani huyo Mungu wa hiyo dini hawezi kuirudisha hiyo ardhi kwenu kwa njia ya amani bila kuwa amrisha wafuasi wake kupigana vita vya umwagaji damu ?
Vizuri, sisi tunaishi duniani, Mungu katupa akili, muongozo na uwezo wa kuyakabili mazingira yetu. Ni juu yetu kufuata muongozo kufanya hivyo na kufanikiwa.

Maisha hapa duniani si chochote ila mtihani kwetu sisi, mungu katupa vyote hivyo ili wenyewe tujioime na tuone tunastahiki ufalme wa mbingu au la.
Hata China Mao aliye kufa zaidi ya miaka 30 iliyo pita aliye ua watu kwa sera zake mbovu mpaka leo kuna watu wana muamini na wengine wana mchukulia mtakatifu kufa miaka mingi iliyo pita haifanyi makosa yasi sahihishwe.
Na wapo wengi hawakuua mtu mmoja lakini hii leo hakuna wanaomkumbuka, Yesu (as), Muhammad (PBUH) na Mussa (as) wamefanya mengi makubwa ambayo wewe binafsi na akili ulizonazo huwezi fanya hata kufikia theluthi.

Kuwa na wafuasi wengi sio kigezo kuwa hicho kitu ni bora kila pande na hakina madoa.
Hiko ni kigezo kizuri sana, leo hii hakuna mtumwa wala hakuna anaeshikiwa panga kwenda msikitini au kanisani au kumwamini Mungu lakini tazama ni wangapi wanamuamini.

Kwa hiyo hivyo vita vitakatifu vilikua upendo na sio hofu kuridhia mafundisho kwa shingo uapande, una ifahamu Age of reason in Europe kili tokea kitu gani ?
Naam watu waliridhia wakaenda vitani kupigana kulinda ardhi zao, mama zao, binti zao na wake zao.

Siifahamu Age of Reasoning hebu nielimishe mkuu.
Bado mafundisho yaliyo rithishwa vizazi na vizazi yana watia hofu wafuasi wake kuhusu adhabu watakazo pata siku wa mwisho endapo wakijitenga na hizo dini na huyo Mungu wa hizo dini.
Naam ni sahihi kabisa, mkuu ulitaka iweje?
Wanapaswa kujifunza zaidi ili wawe huru kimaamuzi na kiimani na sio kuishi kama wafungwa au watumwa.
Naam nakubaliana nawe, sifurahii watu walio waumini wa dini fulani kufuata imani hiyo kibubusa. Ninaamini kila mmoja anapaswa kuifuatilia imani yake kiundani kisha kufikia hatma yake mwenyewe.
Kwa wale ambao hawakuwa wafuasi wake toka kale mfano upagani
Nukuu kifungu cha chuki toka kwenye misahafu.

Achana na watu, tujikite kwenye misingi ya imani hizo.
Kwa hiyo mwafrika ni shabiki tu katika uwanja wa hizi dini ?
Hayo umesema wewe, hakuna mahali nimesema hivyo mkuu.
Sijasema kuwa chanzo cha machafuko hapa duniani ni dini pekee la hasha usini nukuu vibaya .
Vizuri, nami nikakuonesha jambo ambalo hukutaka kulionesha kuwa hayo machafuko ya dini ni kijisehemu kidogo tu cha sehemu kubwa ya vita na machafuko yaso na kichwa wala miguu.


Nimezungumzia dini kama chombo kinachoitwa chombo cha amani na upendo huku kikiwa kimejaa Vita za kutosha zilizo gharimu mauaji makubwa ya watu , chuki , masengenyo, utumwa, ubaguzi n.k
Ni kweli, ila elewa asili ya wanaadamu, Dini ni chombo tu kama utaifa kinachotumiwa na baadhi ya watu kufanya yale yasofaa.
Chanzo cha machafuko dunia pia ukabila una husika, ukanda, siasa, tamaduni, falsafa n.k
Tena hivi ndivyo vimeichafua dunia kwa sehemu kubwa kuliko hata dini.
 
Back
Top Bottom