Je, hayati John P. Magufuli alidanganywa na vyanzo vyake vya habari? Maana sasa ni kama kufedheheshana

Je, hayati John P. Magufuli alidanganywa na vyanzo vyake vya habari? Maana sasa ni kama kufedheheshana

Kipindi unachosemea ww Watanzania hawafiki milioni 15 wanaenda shule ni chini ya 4% sasa hv mpo milioni 60 wanaoenda au waliofikisha umri wa kwenda shule 98% wanaenda shule uoni kuna tofauti kubwa ?
Shida unaangalia Enrollment sio quality ya elimu. Yaani ina faida gani 98% wawe enrolled alafu takwimu zinaonyesha zaidi ya elfu 50 wana drop kila mwaka sababu ya ujauzito. Let alone umesikia wanaomaliza la saba hawajui kusoma wala kuandika, well hakuna madawati, Ufaulu la saba kati ya private na public n.k hivi hayo mambo hamyaoni au nyie mmekazana na enrollment tu.
 
Kumbukumbu zinabainisha ata JK alipomaliza muda wake maoni na michango katika mitandao yalikuwa yakionesha kama vile hakufanya chochote..ngoja tuone Mama kama atawakomesha mafisadi..
Ngoja tuone kama ajira zitaongezeka na gharama za kujiajiri kama zitashuka..
 
Mimi binafsi hainingii akilini aliyekuwa msaidizi wako mkuu kama makamu wa rais afanye mabaliko makubwa kama haya kwa muda mfupi.

Kwamba malalamiko ya ukudanyaji kodi hayati JPM hakuyasikia? Malalamiko juu ya wawekezaji kusumbuliwa? Masuala ya ajira na mshahaka unaotakiw? Je, hawaaminiki tena?
daaah mbahangaika sana jamani. Hii ndyo hasara za kuwa dikteta, watu wanakuogopa ukiwepo ukiondoka utajua hujui
 
Kipindi unachosemea ww Watanzania hawafiki milioni 15 wanaenda shule ni chini ya 4% sasa hv mpo milioni 60 wanaoenda au waliofikisha umri wa kwenda shule 98% wanaenda shule uoni kuna tofauti kubwa ?

Wangapi wanafikia kiwango cha elimu ya chini kwa sasa kati ya hao 98%??.
Hatutaki elimu bali elimu bora, kizazi hichi ndio kizazi ambacho mtoto anafika darasa la saba hajui kusoma wala kuandika. Wewe huoni ni ajabu?
 
Suala la elimu bure kwa nchi hii wala sio jambo la ajabu kabisa sisi tumesoma elimu huku tukinywa uji,daftari likiisha unaonda kwa mwalimu wa soma anasaini unaenda zako stoo unapewa daftari,tulikuwa hatukai chini kama sasa hivi dawati moja wanafunzi wawili na madawati yanabaki ya kumwaga tu
Nadhani kipindi hicho we bado ulikuwa kwenye bomba
Darasani mlikuwa wangapi
 
JPM atabaki kuwa kiongozi bora wa kizazi hiki cha sasa ukitoa Nyerere

Najiuliza hv kazi ya makamu wa Raisi ni nini kwa hali inavyooneka tunawalipa watu mishahara na kuwatunza wasiotekeleza majukumu yao aiwezekani makamu wa Rais ambae umezunguka nchi nzima kwenye kampeni tena ukala kiapo cha kumshauri Raisi kwa hekima leo tunashangaa na ww unashangaa mambo yaliofanyika na kuyabadili kana kwamba hukushiriki ktk kuanzishwa kwake.
Mimi mwenyewe sielewi hii inakuwaje ?yani kama hakushiriki kwenye maamuzi
 
Anachofanya mama mtu yeyote lazima ukifanye ilikuondoa wale wazee wa kauli, nimetumwa na raisi nifanye hiki....
 
Baba alikuwa mkoloni mweusi. Alipenda kudamganywa wajanja wakawa wanamwingiza chaka huku wakimpongeza. Si unajua alikuwa mshamba sana mpenda sifa.
Ninyi sahauni kujenga saccos yenu, 2025 sio mbali mtakaa vilevile kama mlivyokaa 2020.
 
Hapa kuna mambo mawili wengi mmechanganya, kuna majadiliano na maafikiano. Inawezekana kabisa katika baadhi ya mambo Rais akamuita Makamu wake wakakaa kujadiliana. Haimaanishi kwamba Rais analazimika kukaa na Makamu wake kujadiliana kila jambo.

Lakini suala jingine ni kwamba, katika majadiliano hayo kama ikampendeza Rais kumuita Makamu wake wakajadili basi Rais hafungwi na ushauri wowote unaotolewa na Makamu wake.

Kwenye majadiliano na wakuu wetu wa kazi Mara nyingi kuna mengi yanaweza kujitokeza na katika hayo huwa unatokea kabisa boss wako akaamua kutokubaliana na ushauri wako simply ana maono yake especially kulingana na cheo alichonacho na legacy anayotaka kuiacha.

Kilichomkuta Rais Samia Suluhu Hassan sio kwamba tu alikuwa ushauri wake haupokelewi lakini waweza kuona wazi kwamba hakuwa kabisa na mtazamo wa approach za mtangulizi wake.

Mama approach yake ni diplomatic na anapenda majadiliano ukiangalia meko hakuwa mtu wa majadiliano akikupigia simu ni kuulizia jambo fulani au kukupatia maelekezo fullstop.

Jiwe hakutaka ushauri hata wa watangulizi wake waliompa uwaziri kwa miaka yote, alikuwa hapokei simu kabisa aliona Tanzania ni kama yake sasa. Only mtu aliyekuwa anamuweza ni uncle Ben.

Jamaa alikaa almost mwezi mzima hajaform baraza la mawaziri kajifungia tu pekee hataki hata Makamu wake ashiriki, mpaka mzee Mkapa alipoenda kumwambia usipotangaza baraza mapema kuna bunge fupi la November to December linakuja mawaziri wako watashindwa kutetea serikali watapigwa Pini, ndio akastuka na kutangaza.

Unaweza kuona huyu mtu alikuwa anajiona yeye ndio anafaa kushinda mtu yeyote. Kidogo hapa mwishoni naona na afya ilianza kuwa mbaya alikuwa anawaachia wafanye wenyewe wateule wake na ndipo walipompiga hela ya kutosha.

Nachoweza kusema ni kwamba, mama hakuwa kwenye nafasi ya kulazimisha jiwe apokee ushauri wake. So kwa sasa mwacheni afanye yake nae alikuwa na maono yake na kila mtu ana maono yake lakini bahati mbaya hatuwezi kuwa wote viongozi.

Kwa sasa legacy ni ya mama anasema KAZI IENDELEE let's hope nae atatupeleka kwenye stage nyingine nzuri zaidi.
 
Back
Top Bottom