Je, hii silaha mpya ya Uturuki inakwenda kubadili sheria za mchezo?

Je, hii silaha mpya ya Uturuki inakwenda kubadili sheria za mchezo?

Leo MoD wa Taiwan kaulizwa swali, je wakivamiwa wanaweza jilinda akasema wameshanunua silaha nyingi sana, na kuna nyingine ziko njiani zinakuja.
Akasema kuwa na silaha tu haiwezi kusaidia kama huna watu wanaoitetea nchi yao, akasema wananchi wake wako tayari kwa lolote kutetea nchi na uhuru wao....
Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha

Ila mchina muoga sana, nimeona jana BBC wakisema China imemaliza mazoezi yake huko mpakani mwa Taiwan.
 
Anti-ship warfare ni ngumu zaidi na ya gharama. Meli ina countermeasures nyingi especially hii Anadolu inayoenda kuwa flagship ya Turkish Navy.

Mpaka uweze kuipiga meli inabidi uisogelee. Anadolu ina air defense system itaona ndege zinazosogea kufyatua air launched anti ship missiles. Meli yenyewe inakuwa na ndege zake palepale za kuilinda, hapa tunazungumzia drone carrier ambayo ni kama aircraft carrier ndogo.

Ingekuwa ni true carrier kama za China au Marekani zinazojitosheleza ingeenda na carrier battle group ikisindikizwa na submarine kwa ajili ya submarines za adui, destroyer kwa kupigia meli za adui, ndege za electronic warfare kuzuia mawasiliano ya adui, ndege ya airborne early warning kujulisha movements za silaha za adui, fighters kuzuia ndege za adui, helicopters kama sehemu ya anti-submarine force na za rescue missions, replenishment ship na mengineyo.

Melivita kubwa hazipigwi kirahisi hivyo na hata zikipigwa bado ni muhimu. Ni sawa useme tusipande magari kwa sababu yanapata ajari.

Hata hivyo leo wamefanya kuizindua, inahitaji process nyingine kuwa commissioned na Navy baada ya kupitia ukaguzi na zoezi la miezi kadhaa kupima mifumo yake. Kama NavyView attachment 2584660 itakuta haikidhi inaikataa mpaka kampuni zinahusika pamoja na wizara ya ulinzi ziikamilishe. Na Anadolu imezinduliwa mapema kwa sababu za kisiasa, uchaguzi mkuu unakaribia na Erdogan anataka aitumie kama achievement ila in reality bado kwangu mimi naona inahitaji si chini ya miaka miwili kuwa relevant.

Kingine kuna ndege zinahitajika kutumika hapo ila hazijakamilika. F-35 ilibidi itumike kwake ila Uturuki iliondolewa kwenye programu. Drone yao TB-3 ya Bayraktar iko tiyari nimeona imepokea order kutoka kwa foreign customers mapema sana, labda kutokana na mafanikio ya TB-2. TB-3 ndio nyingi na lengo kuu la hii drone carrier ila bado meli inahitaji ndege za kuilinda
Sasa hapo Kizilelma ndio kwanza sijui imefanya test ya taxiing mwaka huu au jana mwishoni. Bado sana hiyo naamini miaka kama mitatu ijayo itakuwa bado. Ndege nyingine ya Hurjet ni light attack sidhani kama itakuwa ngumu ukizingatia Uturuki wana advanced trainer jet wanaongeza vitu vingine. Ndege za kutua kwenye carrier zina changamoto kidogo, unakuta runway haifiki urefu wa pitch ya mpira.

Classification ya Anadolu ni mpya kwenye majeshi ila Iran inayo meli kama hiyo moja imejaa kutu ilichukua meli kubwa ya kiraia ikakata sehemu yake ikajenga deck. Ukiiona tu unaona imetengenezwa kivyakevyake. Uturuki ndio wametoa class mpya, meli mpya mahususi tangu inaundwa ingawa walibadiki gear angani.
Classification yake kwa majeshi mengine ingekuwa amphibious ship kama Mistral ya Ufaransa mbili ziliuzwa Misri, hii ni helicopter carrier. Japan na South Korea wanazo carriers ndogo na nzuri sana zile nazo zinaingia classification hii.
Dah!.. Uturuki wanakuja juu sana kwenye hii defense industry miaka ijayo atakuwa military power nini ?
 
Marekani inahamu Sana kuzichapa na china. Naona wanatafuta sababu tu ya kuivaa china. Pengine lengo ni kuishusha kiuchumi. Wataalamu hebu tupieni neno kuhusu hilo nini hasa marekani anakitafuta kwa china?
 
Marekani inahamu Sana kuzichapa na china. Naona wanatafuta sababu tu ya kuivaa china. Pengine lengo ni kuishusha kiuchumi. Wataalamu hebu tupieni neno kuhusu hilo nini hasa marekani anakitafuta kwa china?
Hakuna nchi dunia ya leo wanaeza kumpiga mchina ukiona nchi Hadi biological weapons anaoagopeka ni hatari Sana China anaeza pukutisha L.A yote kwa amplified moja ya korona version...
 
Dah!.. Uturuki wanakuja juu sana kwenye hii defense industry miaka ijayo atakuwa military power nini ?
Wanataka kuwa imara eneo lako halitaki ukae kizembe. Wapo na Iran pembeni huwa hawapendani, wapo na Greece maadui wa kihistoria na wana strait inayopitisha meli kwenda Russia na Pacific na kurudi Ulaya.
 
Hakuna nchi dunia ya leo wanaeza kumpiga mchina ukiona nchi Hadi biological weapons anaoagopeka ni hatari Sana China anaeza pukutisha L.A yote kwa amplified moja ya korona version...
China anaogopeka kwa biological weapon gani mzee. Corona yenyewe ugonjwa wa kitoto huu unakuzwa na media, kwanza umeua Wachina wengi kuliko Wamarekani. Marekani ina stockpile ya bio weapons kwenye labs zao za miongo na miongo iliyopita, Russia ana stockpile ya Cold war enzi za USSR mahabara zimefungwa uko. Virusi kama Botulinum vimegandishwa uko uje uwatishe na ugonjwa unaodhibitiwa kwa tangawizi
 
Leo ndo umeona hivyo baada ya Ukraine kuwapelekesha?
Ametupelekesha akina nani kwani mm ni Mrusi au?
kwani Urusi amesha shindwa vita mpaka useme anapelekeshwa?
Urusi tutajua ameshindwa vita mpaka pale atakapo kimbia kwa aibu kama Marekani alivyo kimbia Vietnam, Afghanistan na Somalia baada ya kipigo cha mbwa koko.

Au tutajua Urusi amepelekeshwa na kushindwa iwapo ataya tema maeneo aliyo yateka kutoka Ukraine kama Israel ilivyo itema rasi ya Sinai mwaka 1972 baada ya kupokea kipigo kutoka Misri au kama alivyo itema ardhi ya Rebanon baada ya kipigo cha aibu kutoka kwa Hizibullah mwaka 2006

Au ukitaka kujua kuwa vita sio lele mama iulize Israel nn kilicho ikuta baada ya kujaribu kuivamia Gaza mwaka 2014 kwa lengo la kuiangamiza Hamas.

Au ukitaka kujua vita sio lele mama iulize Saudia na vibaraka wake kimewakuta nn baada ya kiwaparamia waasi wa kihuthi.

Ukitaka kujua vita sio lele mama iulize Urusi ilitumia miaka mingapi mpaka kuwashinda waasi wa kichechinia na ililipa gharama kiasi gani.
 
Back
Top Bottom