Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

Je, inawezekana kila kitu ni mpango wa Mungu?

Unaweza kuthibitisha uchawi upo na si hadithi tu?

Babu zetu walipowaona wazungu wana redio, na wanaweza kutabiri kupatwa kwa jua, waliwaita wachawi.

Je, kutumia redio ni uchawi? Kuweza kutabiri kupatwa kwa jua ni uchawi?

Unajuaje kwamba unachofikiri wewe ni uchawi leo si kitu ambacho kinaweza kuelezewa vizuri tu kesho bila uchawi kama leo tunavyoweza kuelezea redio na kupatwa kwa jua, vitu ambavyo babu zetu waliviona uchawi, bila kuhitaji nadharia ya uchawi ?
Asili za babu zetu ni wapi?
 
Ok, mkuu nijuze kadri ya uelewa wako
1.Ni nini asili ya viumbe Duniani,vinaendeshwa na nani na nguvu toka kwa nani?

Sijui,na kutokujua kwangu tu kunaonesha hakuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote. Angekuwepo na kama yeye ndiye asili ya vyote hivi, angeweka wazi kiasi ya kwamba kusingekuwa na mjadala asili ya hivi vyote ni nini.

Pia,dhana nzima ya asili ya hiki ni nini na asili ya kile ni nini inafanya kazi kama tunaongelea vitu vya middle to large scale in the universe. Ukienda huko chini kabisa katika quantum level, cause and effect, the essential idea behind "asili ya hiki ni nini" inavunjika. Concept nzima ya cause and effect inavunjika, the universe becomes probabilistic.

2.Unaelewa nini juu ya mwili, Roho,Nafsi,Uzima na Kifo?

Kati ya hivyo, vinavyothibitishika kwamba vipo ama physically ama as a state ni mwili uzima na kifo, roho, na nafsi ni nini?

3. Kabla ya vitu hivyo unavyoviona kulikua na nn na nini hatima yake?

Vitu gani? Be specific please. Pia, swali lako bado limejikita katika msingi wa "cause and effect". Narudia, cause and effect is not fundamental,it is only evident at the mid tolarge scale levelof the universe, if you go deep enough, at the quantum levelfor example, cause and effect breaks down. The universe becomes probabilistic.
4. Kila kilicho na mwanzo huwa na mwisho je ni nini mwanzo wa wa hii dunia na mwisho wake ni nini?
Muale wa mwanga unaoenda katika spidi ya mwanga una experience muda wote kwa pamoja, muda uliopita, uliopo na ujao wote uko pamoja.

Dhana nzima ya muda ni mazingaombwe unayoyaona kwa sababu wewe huwezi kwenda kwa speed ya muale ya mwanga, ungeweza, kungwkuwa hakuna muda.

Dunia imeanza kamasehemu iliyojimega kutoka jua (read Laplace) na itaishia kuunguzwa na jua litakapopanuka miaka bilioni 5 ijayo, kama si kabla.

Kwa kunjibu hayo maswali naomba sasa uthibitishe kwamba Mungu hayupo.

Ambacho hakipo, nje ya dhana na mantiki, hakithibitishiki kwamba hakipo, kwa sababu hakipo ili kithibitishike kwamba hakipo, na kingekuwepo kithibitishike kwamba hakipo, kisingewezakuthibitishika kwamba hakipo, bali kingethibitishikakwamba kipo.

Uthibitisho, nje ya dhana na mantiki, ni uwanja wa vilivyopo, si uwanja wa visivyopo.

Nishathibitisha kimantiki kwamba Mungu hayupo (proof by contradiction, Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo,dunia aliyoiumba isingekuwa na baya lolote.Dunia ina mabaya mengi, hivyo, Mungu huyo hayupo)

Hujaweza kuupinga uthibitisho huu.

Kama unasema Mungu yupo, ni kazi yako kuthibitisha Mungu yupo.

Hujaweza kuthibitisha hilo.
 
Unaweza kuthibitisha uchawi upo na si hadithi tu?

Babu zetu walipowaona wazungu wana redio, na wanaweza kutabiri kupatwa kwa jua, waliwaita wachawi.

Je, kutumia redio ni uchawi? Kuweza kutabiri kupatwa kwa jua ni uchawi?

Unajuaje kwamba unachofikiri wewe ni uchawi leo si kitu ambacho kinaweza kuelezewa vizuri tu kesho bila uchawi kama leo tunavyoweza kuelezea redio na kupatwa kwa jua, vitu ambavyo babu zetu waliviona uchawi, bila kuhitaji nadharia ya uchawi ?
Thibitisha nawewe kama kweli babu zetu waliwaona wazungu ni wachawi kisa tu wanaweza kutabiri yajayo! Kama si hadithi tu hizo.
 
Thibitisha nawewe kama kweli babu zetu waliwaona wazungu ni wachawi kisa tu wanaweza kutabiri yajayo! Kama si hadithi tu hizo.
Kabla sijakuthibitishia, naomba uniambie uthibitisho wa aina gani utakuridhisha?

Usije kuwa mtu unayetaka ligi ya kuthibitisha tu.

Ukija hivyo, hata mimi naweza kukwambia thibitisha wewe nimtu upo na si bot tu.
 
Asili za babu zetu ni wapi?
Sijui, lakini haiwezekani kuwa kwa Mungu mjuzi wa yote, mweye uwezo wote na upendo wote.

Ingekuwa hivyo, asingeachia wauzwe utumwani miaka mingi wapate shida sana.

Tena kwa wazungu ambao walidai wanamjua sana huyo Mungu.

Unaamini habari hizi?

Mungu yupo, kawaachia mababu zetu wauzwe utumwani miaka yote hiyo?

Au utataka nithibitishe mababu zetu waliuzwa utumwani pia?
 
Je’ ni kweli kila kitu ni mpango wa Mungu? Kwa muujibu wa biblia yapo maandiko mengi ambayo kwakweli yana hitaji tafakari nzito, kuyaelewa. baadhi ya maandiko ya biblia…Ni kama haya.
Mkuu usijisumbue kutafuta "kumwelewa" MUNGU, huwezi hata siku moja kumwelewa MUNGU wala kuyajua mawazo yake na akili zake. Unachotakiwa wewe kukifanya ni KUTII tu basi. Zitii Amri zake na uyashike mafundisho yake, uwe tajiri au uwe maskini jukumu lako kama mwanadamu ni KUTII tu basi.

Hakuna kiumbe anayemwelewa MUNGU, siyo Malaika, wala siyo Mashetani, wala siyo Wanadamu, wala siyo Wanyama, hakuna anayeweza kumwelewa BWANA MUNGU. Isipokuwa tu viumbe wake wote wanauwezo wa kuamua KUMTII na kufanya vile anavyotaka yeye. Tena yeye hamlazimishi kiumbe yeyote yule KUMTII, amewapa viumbe vyote hiari ya kuamua KUTII au KUASI.

Wale wanaochagua kutii amewatengea zawadi(neema) ya kuishi naye MILELE sababu yeye MUNGU ni wa milele; na wale wanaochagua KUASI amewatengea adhabu na kifo cha milele vile vile. Sasa basi kutokana na hoja yako, ni kweli ndiyo MUNGU anajua kila kitu na anapanga matukio, lakini MUNGU hakupangii utende dhambi au utende mema.

Ukisoma kitabu cha MWANZO utaona kuna mahali BWANA MUNGU anamwambia Kaini hivi;

"kwanini una ghadhabu? Na kwanini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde". MWANZO 4:6-7

Hivyo basi kutokana na maneno hayo hapo juu ya MUNGU kila unalolitenda ni hiari yako mwenyewe, MUNGU hakupangii utende mema au mabaya, uamuzi ni wako. Isipokuwa yeye kama MUNGU anaweza akaamua uwe Mfalme, au akakupa Utajiri, au uwe na watoto wangapi, n.k. lakini ni kwa kusudi maalumu. Yeye huwa na makusudi yake, na makusudi yake ni kwa faida ya wengi, siyo kwa faida ya mtu mmoja. Hata hivyo makusudi yake hayakufanyi wewe utende dhambi au mema na ndiyo maana mwisho wa siku ameweka hukumu.

Mkuu blackstarline fahamu kwamba huwezi KUMWELEWA BWANA MUNGU; akili zake wala mawazo yake hayachunguziki. Wewe jitahidi kumtii, kuzishika Amri zake, maagizo yake na imani ya YESU KRISTO na siku moja utamwona uso kwa uso.
 
Sijui, lakini haiwezekani kuwa kwa Mungu mjuzi wa yote, mweye uwezo wote na upendo wote.

Ingekuwa hivyo, asingeachia wauzwe utumwani miaka mingi wapate shida sana.

Tena kwa wazungu ambao walidai wanamjua sana huyo Mungu.

Unaamini habari hizi?

Mungu yupo, kawaachia mababu zetu wauzwe utumwani miaka yote hiyo?

Au utataka nithibitishe mababu zetu waliuzwa utumwani pia?
Nakama hujui tu asili yako na babu zako! Huoni kama unajitaabisha kuhu mambo ya Mungu na pia hujui unalo lisimamia?
 
Nakama hujui tu asili yako na babu zako! Huoni kama unajitaabisha kuhu mambo ya Mungu na pia hujui unalo lisimamia?
Hapana.

Ngoja nikupe darasa.

Katika mantiki (logic) kuna kosa moja la kimantiki linaitwa "non sequitur". Mtu akifanya kosa la "non sequitur"katika kufikiri kimantiki maana yake anafanya kosa la kuunganisha mambo mawili ambayo hayana uhusiano.

Mathalani.

Nikiuliza, ubini wako nani wewe? Ukasema "Ramadhani". Nikasema, aaaah, kumbe wewe ni Muislamu. Hapo nimefanya kosa la "logical non sequitur".

Nimeunganisha vitu viwili ambavyo havina uhusiano wa moja kwa moja kama vitu ambavyo vina uhusiano wa moja kwa moja.

Nimechukulia kwamba, mtu mwenye ubini wa Ramadhani ni lazima atakuwa Muislamu.

Kumbe kuna Mchungaji Jaji Augustino Ramadhani!

Ndilokosa ulilofanya wewe hapa.

Mfano mwingine wa kihesabu.

Umeniuliza, square root ya 2 ni ngapi? Nikasema sijui. Ukasema basi kama hujui, square root ya 2 ni 10.

Nikakwambia jibu lako si la kweli, ni la uongo. Square root ya 2 haiwezi kuwa 10.

Unaniambia, sasa wewe hujui square root ya 2 ni nini, nikikwambia ni 10 utanibishiaje wakati hujui square root ya 2 ni nini?

Hujui kwamba, naweza kuwa sijui square root ya 2 ni nini, lakini nikajua kwamba square root ya 2 ni ndogo kuliko 2, na ukinipa jibu lolote la square root ya 2 ambalo nikubwa kuliko 2, nitajua ni jibu la uongo, lina contradiction. Lina contradict principle ya muhimu kwamba square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2.

Ukisemakwamba kama sijui asili yangu na babu zangu siwezi kuelewa kwamba Mungu yupo na ndiye asili, ni sawa na kuniambia kwamba, kamasijui square root ya 2 ni nini, siwezikuelewa kwamba square root ya 2 ni 10.

Naweza kujua square root ya 2 si 10 bila kujua square root ya 2 ni nini, kwa kujua tu kwamba square root ya 2 inatakiwa iwe ndogo kuliko 2, isi contradict principle kwamba square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2.

Naweza kuwa sijui asili yanguwala ya mababu, lakini pia nikajua asili yetu si Mungu na Mungu hayupo, kwa sababu dhana nzima ya kuwepo Mungu ina contradiction kama vile dhana ya square root ya 2 ni 10 ilivyo na contradiction.

Ndiyo maana huwezi ku prove factually kwamba Mungu yupo.

Kwa sababu hayupo.

Unaweza ku prove Mungu yupo, factually?
 
Sijui,na kutokujua kwangu tu kunaonesha hakuna Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote. Angekuwepo na kama yeye ndiye asili ya vyote hivi, angeweka wazi kiasi ya kwamba kusingekuwa na mjadala asili ya hivi vyote ni nini.

Pia,dhana nzima ya asili ya hiki ni nini na asili ya kile ni nini inafanya kazi kama tunaongelea vitu vya middle to large scale in the universe. Ukienda huko chini kabisa katika quantum level, cause and effect, the essential idea behind "asili ya hiki ni nini" inavunjika. Concept nzima ya cause and effect inavunjika, the universe becomes probabilistic.



Kati ya hivyo, vinavyothibitishika kwamba vipo ama physically ama as a state ni mwili uzima na kifo, roho, na nafsi ni nini?



Vitu gani? Be specific please. Pia, swali lako bado limejikita katika msingi wa "cause and effect". Narudia, cause and effect is not fundamental,it is only evident at the mid tolarge scale levelof the universe, if you go deep enough, at the quantum levelfor example, cause and effect breaks down. The universe becomes probabilistic.

Muale wa mwanga unaoenda katika spidi ya mwanga una experience muda wote kwa pamoja, muda uliopita, uliopo na ujao wote uko pamoja.

Dhana nzima ya muda ni mazingaombwe unayoyaona kwa sababu wewe huwezi kwenda kwa speed ya muale ya mwanga, ungeweza, kungwkuwa hakuna muda.

Dunia imeanza kamasehemu iliyojimega kutoka jua (read Laplace) na itaishia kuunguzwa na jua litakapopanuka miaka bilioni 5 ijayo, kama si kabla.



Ambacho hakipo, nje ya dhana na mantiki, hakithibitishiki kwamba hakipo, kwa sababu hakipo ili kithibitishike kwamba hakipo, na kingekuwepo kithibitishike kwamba hakipo, kisingewezakuthibitishika kwamba hakipo, bali kingethibitishikakwamba kipo.

Uthibitisho, nje ya dhana na mantiki, ni uwanja wa vilivyopo, si uwanja wa visivyopo.

Nishathibitisha kimantiki kwamba Mungu hayupo (proof by contradiction, Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo,dunia aliyoiumba isingekuwa na baya lolote.Dunia ina mabaya mengi, hivyo, Mungu huyo hayupo)

Hujaweza kuupinga uthibitisho huu.

Kama unasema Mungu yupo, ni kazi yako kuthibitisha Mungu yupo.

Hujaweza kuthibitisha hilo.
Nime like comment zako si kwamba ni nzuri ila juhudi yako unayoifanya kumjua Mungu..Jifunze na usifanye Moyo wako kuwa Mugumu Mungu ni mwema naamini ipo siku atajifunua kwako nawe utamjua na kamwe hutomwacha. Endelea kudadisi na kutafuta juu ya uwepo wake.
Mimi nimeshashuhudia matendo makuu yake na amani niliyonayo moyoni kamwe haielezeki...hata sasa nina ujasiri wa kusema Mungu yupo tena ni mwema sana na fadhili zake hazichunguziki walio wake tunamjua naye tulio wake anatujua pia!
 
Mkuu usijisumbue kutafuta "kumwelewa" MUNGU, huwezi hata siku moja kumwelewa MUNGU wala kuyajua mawazo yake na akili zake. Unachotakiwa wewe kukifanya ni KUTII tu basi. Zitii Amri zake na uyashike mafundisho yake, uwe tajiri au uwe maskini jukumu lako kama mwanadamu ni KUTII tu basi.

Hakuna kiumbe anayemwelewa MUNGU, siyo Malaika, wala siyo Mashetani, wala siyo Wanadamu, wala siyo Wanyama, hakuna anayeweza kumwelewa BWANA MUNGU. Isipokuwa tu viumbe wake wote wanauwezo wa kuamua KUMTII na kufanya vile anavyotaka yeye. Tena yeye hamlazimishi kiumbe yeyote yule KUMTII, amewapa viumbe vyote hiari ya kuamua KUTII au KUASI.

Wale wanaochagua kutii amewatengea zawadi(neema) ya kuishi naye MILELE sababu yeye MUNGU ni wa milele; na wale wanaochagua KUASI amewatengea adhabu na kifo cha milele vile vile. Sasa basi kutokana na hoja yako, ni kweli ndiyo MUNGU anajua kila kitu na anapanga matukio, lakini MUNGU hakupangii utende dhambi au utende mema.

Ukisoma kitabu cha MWANZO utaona kuna mahali BWANA MUNGU anamwambia Kaini hivi;

"kwanini una ghadhabu? Na kwanini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde". MWANZO 4:6-7

Hivyo basi kutokana na maneno hayo hapo juu ya MUNGU kila unalolitenda ni hiari yako mwenyewe, MUNGU hakupangii utende mema au mabaya, uamuzi ni wako. Isipokuwa yeye kama MUNGU anaweza akaamua uwe Mfalme, au akakupa Utajiri, au uwe na watoto wangapi, n.k. lakini ni kwa kusudi maalumu. Yeye huwa na makusudi yake, na makusudi yake ni kwa faida ya wengi, siyo kwa faida ya mtu mmoja. Hata hivyo makusudi yake hayakufanyi wewe utende dhambi au mema na ndiyo maana mwisho wa siku ameweka hukumu.

Mkuu blackstarline fahamu kwamba huwezi KUMWELEWA BWANA MUNGU; akili zake wala mawazo yake hayachunguziki. Wewe jitahidi kumtii, kuzishika Amri zake, maagizo yake na imani ya YESU KRISTO na siku moja utamwona uso kwa uso.
Huwezi kumwelewa Mungu.

Kwa sababu hayupo.
 
Nime like comment zako si kwamba ni nzuri ila juhudi yako unayoifanya kumjua Mungu..Jifunze na usifanye Moyo wako kuwa Mugumu Mungu ni mwema naamini ipo siku atajifunua kwako nawe utamjua na kamwe hutomwacha. Endelea kudadisi na kutafuta juu ya uwepo wake.
Mimi nimeshashuhudia matendo makuu yake na amani niliyonayo moyoni kamwe haielezeki...hata sasa nina ujasiri wa kusema Mungu yupo tena ni mwema sana na fadhili zake hazichunguziki walio wake tunamjua naye tulio wake anatujua pia!
Thibitisha Mungu yupo.

Hujathibitisha.
 
Tatizo ya Atheist ni moja kwamba wana argue kwamba kama Mungu angekuwepo 'Kungekuwa hakuna vita, Waafrika hawangeenda Utumwani, Tungekula Matunda kila siku, Tungesoma Bila Matatizo... '

Atheists wanaamini kama kweli Mungu 'angetupenda sisi' bhas tusingeziona shida kamwe

Ila kama vile nimesema ilo ndo tatizo, Mungu hayupo ivo...
 
Huwezi kumwelewa Mungu.

Kwa sababu hayupo.
Hiyo ni hiari yako kuamini kama yupo au kutoamini, hakuna anayekulazimisha wala yeye MUNGU hakulazimishi uamini. Lakini amini usiamini, ipo siku inakuja, aliyoiandaa yeye mwenyewe MUUMBA wa mbingu, dunia na vyote vilivyomo; siku hiyo utajua kuwa hakika yeye ni BWANA MUNGU na hakuna mwingine na mbele yake utapiga magoti!

Mark my words mkuu Kiranga , time will tell.
 
Hiyo ni hiari yako kuamini kama yupo au kutoamini, hakuna anayekulazimisha wala yeye MUNGU hakulazimishi uamini. Lakini amini usiamini, ipo siku inakuja, aliyoiandaa yeye mwenyewe MUUMBA wa mbingu, dunia na vyote vilivyomo; siku hiyo utajua kuwa hakika yeye ni BWANA MUNGU na hakuna mwingine na mbele yake utapiga magoti!

Mark my words mkuu Kiranga , time will tell.
Sitaki kuamini. Nataka kujua.

Sijadili imani. Najadili facts.

Inaelekea hujanielewa kabisaaaaaaaaa.

Mungu angekuwepo, usingekuwa na haja ya kusema "time will tell".

Angejulikana yupo kwa wote muda wote.
 
Uthibitisho hauwezi kuwa mtazamo uliosahihi?

Nikilitazama jua, linawaka, nikasema kwa mtazamo wangu jua linawaka hapa,na kweli jua linawaka, huomtazamo wangu hauendani na ukweli na hivyokuwa mtazamo sahihi ambao pia upo katikauthibitisho kwamba jua linawaka hapo nilipo?
Hapo kuna vitu viwili,kwanza ni mtazamo wako kuwa jua linawaka na pili ni huo ukweli kuwa jua linawaka.

Sasa wewe umeona kabisa kuwa jua linawaka(uthibitisho) halafu tena unasema kwa mtazamo wako jua linawaka!!!

Bado tunarudi pale pale tu mtazamo na uthibitisho.
 
Wale wanaochagua kutii amewatengea zawadi(neema) ya kuishi naye MILELE sababu yeye MUNGU ni wa milele; na wale wanaochagua KUASI amewatengea adhabu na kifo cha milele vile vile. Sasa basi kutokana na hoja yako, ni kweli ndiyo MUNGU anajua kila kitu na anapanga matukio, lakini MUNGU hakupangii utende dhambi au utende mema.
Sawa mkuu nimekwelewa vizuri sana, swali kabla sijatenda dhambi Mungu anajua nitatenda dhambi?
 
Hapo kuna vitu viwili,kwanza ni mtazamo wako kuwa jua linawaka na pili ni huo ukweli kuwa jua linawaka.

Sasa wewe umeona kabisa kuwa jua linawaka(uthibitisho) halafu tena unasema kwa mtazamo wako jua linawaka!!!

Bado tunarudi pale pale tu mtazamo na uthibitisho.
Mtazamo hauwezi kuwa katika kweli ukaendana na uthibitisho?
 
Imani haijadiliwi, ukishaingia katika mjadala, huku unafikiri unajadili imani, wewe ndiye uliyepotea njia.

Kuna watu kibao hawajadili imani zao hapa, kwa sababu wanajua suala zima la kujadili imani ni mufilisi wa mawazo.

Mimi najadili facts, sijadili imani.

Imani unaruhusiwa kuamini chochote unachotaka.

Lakini, katika facts, Mungu hayupo.

Ndiyo maana huwezi kuthibitisha kwamba yupo factually
Wewe unaongea pumba tupu,nakwambia hivi ukizungumzia suala la Mungu ujue unazungumzia jambo la imani.

Suala la kwamba kuna Mungu ni imani, wewe unataka kuliondoa hili jambo kwenye nafasi yake na kwenda kuliweka kwenye nafasi ambayo si yake ili upate kusema kuwa tumeshindwa kuthibitisha.

Halafu ukisema watu hawajadili imani basi pia hatutoweza kujua ni ipi imani potofu na ipi sahihi.
 
Back
Top Bottom