Je, Israel ana combat superiority dhidi ya Iran?

Iran ana jeshi kubwa sana ,yaani idadi ya wanajeshi, lakini kwa suala la air supremacy Israel wako vizuri kwa sababu alichonacho USA ujue hicho ni cha Israel, hizo ndege za F-35A Israel anazo ambazo Iran hana uwezo wa kuzuia ndege hizo, pale Syria zipo S400 za Russia kwanini ndege za Israel zinaingia na kutoka bila kunasa? Pia hakuna namna ya kuishinda taifa lenye nyuklia, wana slogan yao ya Samson Option ambayo wanasema endapo kuna kitisho cha kufuta taifa la kiyahudi pale middle East Israel iko tayari kufyatua makombora ya nyuklia na kumuangamiza adui kabla hajawaangamizwa. Pia kutokana na kila nchi ya kiarabu na Ulaya kubwa na wayahudi, hao nao wako kazini, unashangaa kuona wanajeshi wa kiyahudi waliko maarifa ya ulaya na America, Africa, Austlaria, nchi za kiarabu ikitokea vita huwa wanaenda kwa ajili ya kupigana upande wa Israel, hawa wana utaalam mbalimbali wa kijeshi tofauti na Iran. Tunakumbuka kile kisa cha mwanajeshi wa Iraq alivyotoroka na ndege ya jeshi la Iraq na kuipeleka Israel , hiyo ndege ilikuwa made on Rusia . Kitu kingine ni vyepesi kupata watu wa Iran ambao wanaweza kusaliti nchi yao kutokana na upinzani uliopo hasa wale wenye ninasaba na utawala wa Shaa iliyopinduliwa miaka ya 1970 kuliko kupata wasaliti ndani ya Israel.
 
Halafu Israel alivyo mbabe kairushia Iran vi drone vitatu tu milikpuko imeskika vyombo vyote vya habari vya Iran vikaripoti milipuko hiyo na serikali ya Iran ikafunga viwanja vyote vya ndege vya Iran kisa vidrone vitatu .Halafu Israel kakaa kimya utafikiri hakuna chombo Cha Israel kuandika Wala serikali ya Israel kusema chochote.Kelele na vilio vinasikika Iran tu aliyevirusha Yuko kimya Iran aliyerushiwa kelele kibao .Ndipo ukue kidume Israel kilipiga kweli Sio utani
 
Wewe hujawahi kumsikia Gonen Segev former energy minister wa israel na mashtaka yake ya kutumiwa na wairan kupeleka taarifa za kijasusi kwao ulimwengu wa sasa ni tofauti iran na israel wote pia wanaadvantage ya kutumia takribani watu 4000-10000 ambao ni wayahudi wa asili ya iran kwenye mambo ya ya ujasusi maana hawa wanaenda kote kote iran na israel.
Acha sie huku washabiki maandazi kuna wazaliwa wakiyahudi wairan ambao asili yao ni israel na tehran pale yapo masinagogi.
 
Iran ana missile power kushinda taifa lolote pale middle east.
Pia Iran anatumia airdefense system ya khordak na Bavaar-373 na alishawahi kuzitumia kabla zikatungua drone za USA.
Ingekua anga la Iran ni jepesi basi Israel angeishambulia Iran kupitia Iraq kirahisi sana kama afanyavyo Syria.
Pia Syria kuna s-300 ambazo haziwi activated muda wote,s-400 hazijawa deployed Syria wala Iran.
 
Tuache udini tuongee uhalisia Iran iko vizuri katika medani ya vita.
-Rejelea vita za Iraq-Iran 1980-1988.
Iran ilipigana na Iraq ya Saddam Hussein ikifadhiliwa na USA ila Iran ilihimili vita kwa miaka nane na kumcjosha Iraq na washirika wake,kiasi wakaomba majadiliano mezani.
-Hizbollah ni kundi linalopokea mafunzo toka Iran na silaha toka Iran,2006 hizbollah waliwapiga IDF na kuwaondosha Bint jubeir na kuwarudisha mpaka Shebah farms.
-Houthi ni chama cha siasa kilichoamua kushika silaha kupinga utawala wa Mansour Yemen amae alikua akisapotiwa na USA na Saudi arabia,Iran aliifadhili jeshi na silaha Houthi kuanzia 2011-2022 dhidi ya Saudi arabia na USA waliotaka kurudisha utawala wa Mansour Yemen.
-Houthi hao hao wameifunga red sea baab al mandib hadi sasa sapoti yao ikiwa Iran kisilaha na kijeshi.
Ukitizama utapata jibu kuwa Iran ni taifa lenye uweledi kisilaha na kivita.
Ndio maana watu wanajiuliza kama Hizbollah tu au Hamas inayofadhiliwa na Iran inasumbua Israel,je Israel ikipambana na Iran mfadhili mkuu in full force itakuaje?
 
Mkuu hivi wale Wayahudi wa uongo waliosemwa kwenye Ufunuo 3:9 ndiyo wakina nani? Sio hawa mnaowasujudu sasahivi wakina Netanyahu?
 
Duniani ni USA pekee na NATO ndio zina expeditionary capabilities, zinazofata ni France na kwa mbali ni Britain.

Sababu iliyoifanya Russia isiwe na Makoloni Africa ndio sababu inafanya Jeshi lao lisiwe na uwezo wa kwenda kokote dunia ambapo wametenganishwa na maji (Hawana Jeshi kubwa na Imara ya Majini, and for good reason they don't have to)

Israel na Iran haziwezi kupigana directly, zaidi ya kupigana vita vya kuharibu miundombinu muhimu makombora ya masafa marefu, sababu hakuna nchi inayoweza kuchukua udhibiti wa eneo la Mwenzake bila kuvuka nchi jirani.

Ili Askari wa Iran waingie Israel na kuteka miji inabidi Kuwe na vita ambayo either, Syria, Lebano au Jordan wawe upande wa Iran na kuruhusu majeshi yao yawepo kwenye hizo nchi, in that scenario, Itakuwa halali kwa Israel na Washirika wake kuteka na kuongeza ardhi yao kwenye maeneo ya Syria, Lebanon au Jordan, na kama Iran atashambulia vikosi ya Marekani vilivyoizunguka basi watakuwa legitimate target wa USA na watajustify Uzamivi wa Marekani Iran, ndio maana Iran hataki Marekani aingilie au awe karibu yake.

Iran na Israel hawatapigana as long as Hakuna Iraq na Syria hazijaamua zenyewe kuivamia Israel, Iraq alishakula kipondo cha haja so for as long as wako kwenye good sense watabaki kama buffer zone.
 
Vita ya Iraq-Iran ilikuwa hivi na pande kinzani.

Israel alimsaidia Iran

During the conflict, Iraq received an abundance of financial, political, and logistical aid from the United States, the United Kingdom, the Soviet Union, France, Italy, Yugoslavia, and the overwhelming majority of Arab countries.

While Iran was comparatively isolated to a large degree, it received a significant amount of aid from Syria, Libya, China, North Korea, Israel, Pakistan, and South Yemen.
 
Na wewe unaamini Israel na Pakistan wamsaidie Iran?
Unaamini Syria na South Yemen ambazo zilikua na political instability ziisaidie Iran??
North korea ilikua bado inachechemea tokea vita za mgawanyo wa Korea na haikua ni mahusiano madhubuti ya kidiplomasia na Iran ukizingatia mwaka mmoja nyuma 1979 Iran ilifanya mapinduzi kuipindua serikali yake.
Sio kila article mnazisoma na kuzileta hapa mkuu.
 
Kitu kimoja nimejifunza humu ndani watu wengi hamna knowledge ya masuala ya Dunia.

Yemen unayoijua Leo ni muungano wa miaka ya 1990s wa Yemen mbili North na South Yemen upande wake unataka kujitenga na North Yemen ambayo wanakaa Wahouthi.

Kuhusu Israel kuisaidia Iran, Kama hujui kabla ya Mapinduzi ya Kiislam, Iran na Israel walikuwa na mpango wa kujenga Bomba la Mafuta kwenda Europe hadi Leo mpango upo.

Na Kama hujui zaidi ya 50% Ndege za kijeshi za Iran ni F14 za Marekani na Spare parts zake walikuwa wanapewa na Israel.

Nchi ya kwanza Middle East kuitambua Israel ni Iran.

Make your history right, ndio ujadili kila mada
 
Niishie kusema unaokoteza habari pasi na kuzihakiki.
Halafu unasoma ki google google.
Huko google kuna mpaka article zinasema USA aliisaidia Iran kisirisiri.

Iran unayoizungumzia wewe ni ile ya 1978 kushuka chini ambayo ilikua na urafiki na kina USA na Israel na wamagharibi.
Iran unayoitaja ya 1980 iliopigana na Iraq ni Iran ya serikali ya mapinduzi ya kiislam iliyopindua utawala uliokua rafiki kwa USA na Israel.
Iran hiyo ndio ya kina Khomeini huyu wasasa.
Na ndio Iran hiyo iliyotangaza kuifuta Israel mara tu ilipoanzisha dola ya kiislam 1979 baada ya mapinduzi,unadhani Israel ataisaidia nchi kama hiyo!?
Sijui kama hili wewe ulilifuatilia!
Ndio maana USA aliisapoti Iraq kwa sababu alitaka kufanya regime change utawala anaoutaka urudi sio huo wa kina Khomeini uliopinga US influence pale middle east.
Yemeni ni taifa ambalo toka miaka ya nyuma lina political instability ikiwemo Syria political instability zilianza toka 1958.

Acha kuokoteza story google ukajifanya unajua.
Google everyone types on his own perspectives.
 
Unaandika ushuzi tu na hizo propaganda zenu za Samson option...

Israel haina uwezo wowote kukabiliana na Iran, air superiority ni kwa Hamas, Syria na Iraq, lakini kwa taifa kama Iran hawawezi.


Kwanza hawana ndege ya kwenda hadi Iran kushambulia na kurudi sasa hio air superiority wanaitolea api mbele ya Iran?
Iran walishaterenmsha stealth drone ya US.

Hizo F 35 kwenye vita si kitu, hakuna ndege ambayo ni stealth ikaweza ku confuse radar asilimia 100.

Hata radar ya 1945 ww2 inaweza kuiona F 35 vizuri tu endapo ikiwa configured kuiona F 35.


S-125 ilishawahi kupiga stealth ya US miaka ya 90's. Hizo ni lugha za kibiashara tu.

Kuhusu nuclear bombs inapaswa ujiulize kwanini Iran anajua Israel ana nuclear na bado akatuma drones na missiles kiasi kile na Israel haikujibu?

Israel ikitumia nuclear nayo itapigwa na nuclear, huo ujinga hawawezi fanya, nuclear sio big deal kwa sasa hadi Pakistan zipo.

Inasikitisha sana..
 
Sasa utakuwa na taarifa Ipi kuzidi google πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚.

Vijana mbona mna akili ndogo, hata vitu rational tu.

Chanzo cha maarifa ni kusoma si kitabu kimoja pekee, Ila kusoma taarifa tofauti.

Sasa wewe ni Nani aliyekwambia Syria ina machafuko Kama sio taarifa tofauti.
 
kawaulize hao wairan kuhusu kombora linaitwa rampage, kawaulize juzi hilo kombora limewafanya nini? limerushwa kutoka huko huko ndani ya nchi yao ndo maajabu sasa
 
iran kapigwa juzi na kombora la rampage kutokea hapo hapo nchini kwake umesikia ameongea tena?
 
Hizo mbwembwe zipo Afrika kwa wapumbavu.Comrade Hitler aliwanyoosha kisawa Sawa,mpaka leo wakisikia Wanazi wanakumbuka yaliyo wakuta kwenye zile kambi.
wachina wenyewe kipindi cha world war 2 waliuliwa na wajapan kama kuku.
ila sasa hivi ebu nenda kawaguse wachina tukuone. so acha kuongea zilipendwa
 
kawaulize hao wairan kuhusu kombora linaitwa rampage, kawaulize juzi hilo kombora limewafanya nini? limerushwa kutoka huko huko ndani ya nchi yao ndo maajabu sasa
Dunia iko wazi sana siku hizi sio kama zamani, jidanganyeni wenyewe.
 
Google kuna vyanzo tofauti kama wikipedia,Quora humo watu huandika yale wanayoona sahihi kulingana na uelewa wao,ila mengine sio sahihi.
Mie hufuata nakala za vyombo vikuu vya habari mathalan France24,CGTN,Aljazeera English.
Hivi vyombo vya kimataifa vya habari huwa na nakala tofauti tofauti na zilizothibitishwa.
 
wachina wenyewe kipindi cha world war 2 waliuliwa na wajapan kama kuku.
ila sasa hivi ebu nenda kawaguse wachina tukuone. so acha kuongea zilipendwa
Kwa akili zako unaamini Israel ikikutana na Germany sasa hivi Israel anampiga Germany!?
Jidanganye,Germany akiamua kuitandika Israel sasa hivi anaitandika Israel inafutika inasambaratika.
Germany is still Germany kijana.
China ni taifa lilikopiga hatua katika kila nyanja huwezi liweka sawa na Israel ni matusi,China ni mshindani wa USA katika nyanja zote huwezi muweka sahani moja na Israel.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…