Je, kama wanaume watapewa wanawake wapya na mabikra wapya Mbinguni, sisi wanawake wa Duniani tutapelekwa wapi?

Je, kama wanaume watapewa wanawake wapya na mabikra wapya Mbinguni, sisi wanawake wa Duniani tutapelekwa wapi?

Kwanza kabisa Mola wako hamdhulumu mtu yoyote aliyefanya jitihada kwenye kufanya matendo mazuri, ipo hivyo kwa Wanaume na Wanawake wote watalipwa kwa wema wao....SO, WANAWAKE NAO WATAENDA ENJOY PEPONI KWA ENJOYMENTS TOFAUTI TOFAUTI MOLA WAO NDIYO ANAJUA ZAIDI.


Na ukipata nafasi pitia hizi Aya hapa tafadhali 👇🏽
Al-Ahzab 33:35

إِنَّ ٱلْمُسْلِمِينَ وَٱلْمُسْلِمَٰتِ وَٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ وَٱلْقَٰنِتِينَ وَٱلْقَٰنِتَٰتِ وَٱلصَّٰدِقِينَ وَٱلصَّٰدِقَٰتِ وَٱلصَّٰبِرِينَ وَٱلصَّٰبِرَٰتِ وَٱلْخَٰشِعِينَ وَٱلْخَٰشِعَٰتِ وَٱلْمُتَصَدِّقِينَ وَٱلْمُتَصَدِّقَٰتِ وَٱلصَّٰٓئِمِينَ وَٱلصَّٰٓئِمَٰتِ وَٱلْحَٰفِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَٱلْحَٰفِظَٰتِ وَٱلذَّٰكِرِينَ ٱللَّهَ كَثِيرًا وَٱلذَّٰكِرَٰتِ أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا

Hakika Waislamu wanaume na Waislamu wanawake, na Waumini wanaume na Waumini wanawake, na wat'iifu wanaume na wat'iifu wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanao subiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao sadaka wanaume na wanawake, na wanao funga wanaume na wanawake, na wanao jihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanao mdhukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume na wanawake, Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na ujira mkubwa.

An-Nisa' 4:40
إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَظْلِمُ مِثْقَالَ ذَرَّةٍۖ وَإِن تَكُ حَسَنَةً يُضَٰعِفْهَا وَيُؤْتِ مِن لَّدُنْهُ أَجْرًا عَظِيمًا

Hakika Mwenyezi Mungu hadhulumu hata uzito wa chembe moja. Na ikiwa ni jambo jema basi Yeye hulizidisha na hutoa kutoka kwake malipo makubwa.
Wao wata enjoy namna gani shekhe tufafanulie. Maana kwa wanaume mi naona hiyo zawadi ni nzuri sana. Mabikra 72 si jambo dogo.
 
View attachment 2520159
Wakati mwingine nikiona mada na kuitafakari nazoom avatar, nione akili ya mtoa mada inaweza kuwa na uhusiano na yeye mwenyewe?.
Screenshot_2023-02-17-09-55-33-171_org.mozilla.firefox~2.jpg

Mbona tofauti yenu ndogo. Wewe umeweka avatar ya zezeta yeye kaweka ya kwake anayesubiria wanawake 72.
 
As-salamu alaykum ndugu zangu.

Naomba kuuliza, Quran tukufu 2:25, 4:57 imeandika kwamba wanaume watapewa wanawake wapya na mabikra wazuri huko Akhera.

Pia ukisoma Quran tukufu 38:52 inaongelea kwamba kuna mabikra tayari wa kutosha huko Ahera wakiwasubiri wanaume.

Zaidi ukisoma Quran tukufu 44:54 inataja sifa za mabikra hao kuwa ni wenye macho mazuri, macho meusi mapana na warembo kwelikweli.

Swali langu ni iwapo wanaume wetu na waume zetu watapewa wanawake wapya na wanawake hao wako tayari walishaandaliwa, sisi wanawake wa Duniani tutapelekwa wapi iwapo waume zetu wa hapa Duniani tayari watapewa wanawake wengine?

Hakuna mahala popte kwenye Quran tukufu ambako sisi wanawake wa Duniani tumeahidiwa chochote huku waume zetu wakiahidiwa wanawake wapya.

Ahsante.
Wanawake ni wasaidizi tu mtulie, Mungu aliumba mwanaume kwanza kisha mwanamke akaletwa kumtoa upweke mwanaume, kwahiyo hata sisi waisrael wanawake kwenye sensa tulikuwa hatuwahesabu, shida siku hizi wanawake mmeota mapembe
 
Ndio maana watu hawaogopi kujilipua kumbe kuna ahadi ya mabikira 72 😀😀.Utaratibu ukoje ndugu zangu?
 
Kwenye Qur'an mwanaume anawakilisha humanity pale ambapo mwanamke hajatajwa,mwanamke mwema atapata yaleyale ambayo mwanaume mwema atapata, Kama ilivyo kwa mwanaume muovu na mwanamke muovu
Kwahiyo mwanamke naye atapewa wanaume marijali 72 na mito ya pombe kama mwanaume alivyoahidiwa??
 
Ndio maana watu hawaogopi kujilipua kumbe kuna ahadi ya mabikira 72 😀😀.Utaratibu ukoje ndugu zangu?
Hii sio kwa kujilipua ni kufanya mambo mazuri, utapata hao wanawake na raha nyingine, sasa kuna faida gani ya kutii amri za Mungu duniani halafu huko peponi hakuna raha?
 
Kwahiyo mwanamke naye atapewa wanaume marijali 72 na mito ya pombe kama mwanaume alivyoahidiwa??
Mwanamke kaumbwa kumsaidia kumtoa mwanaume upweke hawezi kuwa na bonus sawa na mwanaume
 
Hiyo dini ni ya kumlinda mwanaume ni mfumo dume angalia tu kule uislam ulikoanzia wanawake wanavyotendewa, hawaruhusiwa kusoma, kuwa viongozi, kumiliki mali, hata kuendesha gari. Uislam unamkandamiza mwanamke mpaka mwisho ingawa wanawake nao ni tatizo kubwa wakiachiwa wafanye wanavyotaka mfano angalia nchi za wazungu
Angalia nyie mliompa nafasi mnavyopelekeshwa
 
Mtakua ma beki 3, ndo mjue mfumo gani unatumika peponi, maana huku duniani mnapambana kuwa sawa na wanaume.
 
Mwanamke kaumbwa kumsaidia kumtoa mwanaume upweke hawezi kuwa na bonus sawa na mwanaume
Aisee kwahiyo yeye hana chake huko peponi? Kuna haja gani ya yeye kuendelea kumtumikia mola Ili hali hajampa hazina yeyote baada ya maisha haya?
 
Aisee kwahiyo yeye hana chake huko peponi? Kuna haja gani ya yeye kuendelea kumtumikia mola Ili hali hajampa hazina yeyote baada ya maisha haya?
Chake si mke wetu tunaenda nae 😂😂😂
 
Mathayo 22:29
Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

Mathayo 22:30
Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.
 
Back
Top Bottom