Je, kuna baadhi ya Familia zimebarikiwa?

Je, kuna baadhi ya Familia zimebarikiwa?

Niwaambie kitu ndugu zangu
Wakati mwingine inategemeana na initiator au aliyeaanza alifanya nini.Sasa unakuta wanaofuatia wanafuata nyayo za kuwa masikini sana au kuwa na mafanikio sana.
Nitatolea mfano familia ya kina Mwapachu
Baba yao alikuwa anaitwa Hamza Kibwana Bakari Mwapachu tokea Tanga
Alioa mwaka 1938 alimuoa Juliana ambaye ndio mama wa Harith Bakari Mwapachu na wengine
Walikutana Makerere na bwana mdogo wake Nyerere wakaanzisha tawi la kutetea wanafunzi wa Tanganyika wakati huo TAWA baadae wakabadili chama wakakiita TAA.
Wakiwa Tabora Hamza alikuwa mwenyekiti wa TAA Nyerere akiwa katibu wake hiyo ilikuwa mwaka 1947
Hamza alikuwa tabibu wakati Nyerere alikuwa Mwalimu st Mary
Hamza akaja kuwa waziri wa kwanza wa mambo ya ndani baada ya Uhuru bahati mbaya hakuishi sana alifariki mwaka 1962 mwaka mmoja tu baada ya Uhuru.

Katika utawala wa Nyerere kwa kutambua mtoto wa nyoka ni nyoka alimteua Bakari Mwapachu mtoto wa Hamza kuwa mkurugenzi mkuu wa ATC.

Watoto wa Hamza wengine wote walikuja kuwa na mafanikio makubwa sana kwenye nyanja za kielimu na vyeo watoto wa Hamza wengine ni

Harith Bakari Mwapachu
Bakari Mwapachu
Rahma Mwapachu mjane wa mwanasheria wa kwanza Jaji Mark Bomani huyu Rahama alishakuwa head of marketing communication
Heri Ali Mwapachu
Juliana Mwapachu
Wendo Mtega Mwapachu
Tunu Mwapachu
Jabe Jabiri Mwapachu

Majina niliyoandika hapo Juu nimechanganya watoto wa Hamza na wajukuu zake
wengi hapo juu wamesomea masomo fani mbali mbali na sheria wingereza na wengine bado wako huko

Familia yote hii ni kubwa iliyojaliwa kuwa na Tunu katika nyanja mbali mbali ukitizama kiundani muasisi wa yote haya ni baba yao.

Sikatai ziko familia ambazo muanzilishi alikuwa vizuri lakini waliofuata bado wakawa ni hopeless siwezi kuzitaja hapa maana ni watu maarufu

Hapo sasa ndipo linapokuja kuwa na mkono wa MUNGU katika familia husika

Ipo mifano ya familia nyingi tu mfano familia za kina Mbowe,Mo Dewji,Bakhresa,Marealle,Bomani,Rupia,bila kusahau mimi familia ninayotoka wakati mwingine nashangaa hatutumii nguvu nyingi ila mambo yanakwenda ila kikubwa kwa familia yangu tunajali elimu kuliko kitu chochote mtoto akikosa ada wa familia flani au baba flani tunaweka harambee kumchangia darasa la chini kabisa ni form four std 7 tulishaifuta toka enzi ya ukoloni hata baba zetu hakuna aliyeishia std 7 n.k

Achaneni na motivational speaker wanasema sijui weka malengo fanya hiki sijui malezi mazuri.Unaweza ukafanya yote haya na bado tu mambo yasiende kabisa au yakaenda kwa kusua sua.

Kitu kikubwa MUNGU humnyanyua mtu yeyote anayetaka hata kama alikuwa chini hana upendeleo
Umenikumbusha kuhusu motivation speakers, watu wanapenda kusikia mafanikio ya motivation speakers wakati hawana sifa kumbe km huna sifa hata moja ya ujasiriamali huwezi kufanya biashara yoyote
 
Hebu soma nilichoandika kirefu kidogo kuhusu familia ya Mwapachu utapata kitu hapo
Sawa sawa mkuu ngojea niipitie tena.

Hongereni pia kwa kuthamini elimu hata kufanya harambee kuwasomesha wengine. Haya tumeyaona zaidi kwenye jamii za nchini Kenya, huku kwetu michango ya harusi ndio kipaumbele.
 
Sifahamu tufahamishane ndugu.
Akili ni uwezo wa kutafsiri ulicho kihifadhi kwa kukiona ama kujifunza, uwezo wako wa kutafsiri jambo haraka kwa mulekeo chanya hapo utaambiwa una akili sana, binadamu ana akili sana ila binadamu huyo huyo ni mvivu wa kufikiri na ukitaka kujua binadamu ana akili sana pindi akipata tatizo huamsha ubongo wake na kutatua tatizo Akisha tatua tatizo matako hulia mbwata , kumbe akili zilezile angelikuwa anazitumia kila siku ange fika mbali sana
 
Sawa sawa mkuu ngojea niipitie tena.
Hebu pitia pitia mkuu tujadili hii mada maana kama ni maadili watoto wetu tunawapa mno na kuwalea vizuri yet bado hatukwamuki motivational speakers wanatukoroga sana.
Tukifahamiana vizuri tutafanyiana inbox tuwe tunajadili vizuri hata kufahamiana unaonekana ni mkereketwa mwenzangu
 
Uko sahihi mleta mada kuna famili hata vifo sio vingi watoto baba bibi ba mababu wote wako hai, katika umri mkubwa, na hizo familiya hakuna magonjwa majongwa yaani mpaka unajiuliza, ilikuwaje familiya fulani watu almost wote walikufa ktk umri mdogo na familiya nyingine wako hai mpaka wajukuu nae wanaanza kuzeeka dah
 
Akili ni uwezo wa kutafsiri ulicho kihifadhi kwa kukiona ama kujifunza, uwezo wako wa kutafsiri jambo haraka kwa mulekeo chanya hapo utaambiwa una akili sana, binadamu ana akili sana ila binadamu huyo huyo ni mvivu wa kufikiri na ukitaka kujua binadamu ana akili sana pindi akipata tatizo huamsha ubongo wake na kutatua tatizo Akisha tatua tatizo matako hulia mbwata , kumbe akili zilezile angelikuwa anazitumia kila siku ange fika mbali sana
Hii ni kweli mkuu nashukuru sana nimejifunza.
 
Hakuna kitu kinaitwa bahati. Wanasaikolojia walishafanya tafiti kuhusu bahati wakagundua kuwa watu waliokuwa wanadhaniwa wana bahati walikuwa makini katika maamuzi na vitu wanavyofanya, na wale waliodhaniwa wana mikosi ilikuwa ni kinyume.
Watanzania wengi tunapenda kufanya mambo kiholela halafu baadae tunasingizia tuna mikosi au tumerogwa.

Mfano, Imagine jamii inaishi bila choo, wanalala bila net. Wanaumwa mara kwa mara shuguli za uzalishaji mali zina dorola, kwa sababu muda mrefu wanatumia kujiuguza, wanakuwa maskini, watoto wanakufa, halafu tunasema wana mkosi.
Wanasaikolojia uchwara ndio wanasema hakuna kitu kama bahati,
Kuzaliwa katika familia ambayo wazazi wako ni Rais, tajiri, watu maarufu au mazingira yenye maendeleo ni bahati ya kwanza kwa sababu sio watu wote wanazaliwa katika familia za aina hiyo n na mazingira ya aina hiyo.

Kuna watu wanafanya maamuzi mabaya ambayo huenda yangewapoteza kabisa muelekeko kimaisha ila kwa sababu ya bahati labda hayo maamuzi hayadhuru sana tofauti na wengine wasio na bahati hiyo.
 
Ni kweli kabisa. Kuna watu hawajui hao motivation speaker ila wame toboa sana.
Hilo la motivation speakers nimelikuta kwangu naandika kitabu cha ujasiriamali kunawatu wataka nieleze Hadithi ya mafanikio yangu,(success story), nikabaki kushangaa mfano Hadithi ya mafanikio niliyoyapata wakati wa awamu ya 3 usingeliweza kuitumia ili ufanikiwe awamu ya 5, ama ninakuwa na Hadithi ya mafanikio ya bidhaa iliyo pigwa maruku kwasasa ama kwa kitu kilichopita na wakati, hili lina tukumbusha kuhusu uvivu wa kufikiri
 
Hebu pitia pitia mkuu tujadili hii mada maana kama ni maadili watoto wetu tunawapa mno na kuwalea vizuri yet bado hatukwamuki motivational speakers wanatukoroga sana.
Tukifahamiana vizuri tutafanyiana inbox tuwe tunajadili vizuri hata kufahamiana unaonekana ni mkereketwa mwenzangu
Ni kweli nimepitia vizuri nimelewa, hongereni kwa kuweza kufanya harambee na kusaidia wengine wapate elimu, ni familia au koo chache zinaweza kufanya haya.

Kama ulivyosema ni kweli watu wana jitahidi kwenye malezi ila unakuta bado hawa fanikiwi. Ndio maana nimona tujadiliane juu ya hili ni namna ya kujifunza juu ya jamii zetu.

Hakika wewe ni mkereketwa mwenzangu nitakutafuta inbox.

Mfano wa familia uliyotaja ya Marealle juzi niloona wakimuaga mzee Gasper George Marealle kanisani tena Askofu mkuu alifika, ukisikia historia yake na watoto wake wote wame fanikiwa vyema mpaka una furahia.
 
Shule shule peleka mtoto shule iwe ya kata au vipi mkomalie asome na muaminishe kuwa huu ndio urithi wako onyesha umuhimu wa shule mtoto ajue kuwa elimu ni jambo kubwa si jambo la kuchezea akijua mmoja wengine watajua na watafuta na mafanikio yatafuta ila kama watoto unawaminisha shule si chochote basi umaskini kwenye familia hauwezi ondoka koo nyingi na familia nyingi zenye umaskini wa kupindukia ni familia na koo ambazo zilidharau elimu so komaa na elimu kwani watoto wakielimika watajua jinsi ya kusolve matatizo yao wangine watajiliwa watapata vipato watabadilisha maisha ya nyumbani nk

Ukiwa na elimu utajua upambanie wapi mfano leo hii vijana wenye sifa wanapambana na nafasi ya kazi ya upolisi, haya kijan akienda uko akipata ajira si njaa inapungua huo ni mfano mmoja

Mafanikio ya kweli na ya siyo na longo longo ni kwenye elimu

Angalia jamii unayoishi familia ambayo ina vijana hata watatu walio ajiliwa serikali au secta binafsi jinsi inavyo heshimika hata kama uko walipo hawana vyeo familia inapata status ya kipekee so ujachelewa komaa na kusomesha kama ujabalikiwa watoto saidia wale wenye kuonyesha wanaipenda elimu kwenye ukoo wako jitoe wasiaidie ili mfute laana ya ufukara wa ukoo saidia awe mtoto wa dada nani au nani mpe support watambiana mjomba furani ukimpigia sm masuala ya shule akatai kukupa pesa

Pekeleni wakajifunze ujuzi VETA nk
 
Kwa mtoto kuwa na Akili za shule most of the time Genetics matter, kama wewe ni kutoka familia ya vipanga hata uamue kupuuzia shule , kwenye nekta utapata four tu hata D mbili. Hata kama shule ulienda kwa kutegea. Ukitoka familia ya vilaza digrii huwa msamiati mnaousikia kwa wengine au redioni, shetani anawaandama, inakuwa tu shule hampendi bila sababu mnachukia kukaa darasani naturally, mnachukia kujisomea, mkijisomea ikija pepa mlikosoma ticha hatoi maswali na hata akitoa maswali hamkumbuki majibu sahihi, kusoma shule mnaona ni kituo cha polisi, mnasema bora shule iishe mkaendeshe daladala au boda!

For me, mtoto huchukua akili na maelekezo ya mama wakati wa kusoma shule, mama akikomaa mtoto anaweza kufika hadi chuo kikuu. Hapa of course kuna other factors kama shule unayosoma, the food you eat, the place you live etc.

Mtoto akimaliza shule kuja maisha ya mtaani ya kufanya kazi hapo huchukua maisha ya baba yake kama kioo katika maisha yake kwa kujua au kutokujua, kuna maamuzi atachagua aidha mtoto atamkubali na kumfuata dingi kuuza madafu au kuigiza filamu au atampinga mshua na kukataa kuuza madafu na kuamua kuwa muosha magari.

In most cases if a father is an office guy or civil servant, most of the kids wataangukia kazi za ofisi, baba akiwa mkulima, wanawe wengi watakuwa wakulima pia , baba akiwa polisi hatokosa polisi mmoja kwenye timu yake ya watoto japo huwa kuna exceptional kids ambao watafanya maisha tofauti na ya baba zao. Baba aliepanda ndege ni rahisi kwa wanawe kuja kuzipanda sana hizo ndege tena zaidi ya mshua wao
 
Shule shule peleka mtoto shule iwe ya kata au vipi mkomalie asome na muaminishe kuwa huu ndio urithi wako onyesha umuhimu wa shule mtoto ajue kuwa elimu ni jambo kubwa si jambo la kuchezea akijua mmoja wengine watajua na watafuta na mafanikio yatafuta ila kama watoto unawaminisha shule si chochote basi umaskini kwenye familia hauwezi ondoka koo nyingi na familia nyingi zenye umaskini wa kupindukia ni familia na koo ambazo zilidharau elimu so komaa na elimu kwani watoto wakielimika watajua jinsi ya kusolve matatizo yao wangine watajiliwa watapata vipato watabadilisha maisha ya nyumbani nk

Ukiwa na elimu utajua upambanie wapi mfano leo hii vijana wenye sifa wanapambana na nafasi ya kazi ya upolisi, haya kijan akienda uko akipata ajira si njaa inapungua huo ni mfano mmoja

Mafanikio ya kweli na ya siyo na longo longo ni kwenye elimu
Sawa sawa. Mshike sana elimu usimwache aende zake.
 
Kwa mtoto kuwa na Akili za shule most of the time Genetics matter, kama wewe ni kutoka familia ya vipanga hata uamue kupuuzia shule , kwenye nekta utapata four tu hata D mbili. Hata kama shule ulienda kwa kutegea. Ukitoka familia ya vilaza digrii huwa msamiati mnaousikia kwa wengine au redioni, inakuwa tu shule hampendi mnachukia kukaa darasani naturally, kusoma shule mnaona ni kituo cha polisi, mnasema shule iishe mkaendeshe daladala au boda!

For me, mtoto huchukua akili na maelekezo ya mama wakati wa kusoma shule, mama akikomaa mtoto anaweza kufika hadi chuo kikuu. Hapa of course kuna other factors kama shule unayosoma, the food you eat, the place you live etc.

Mtoto akimaliza shule kuja maisha ya mtaani ya kufanya kazi hapo huchukua maisha ya baba yake kama kioo katika maisha yake kwa kujua au kutokujua, kuna maamuzi atachagua aidha mtoto atamkubali na kumfuata dingi kuuza madafu au kuigiza filamu atampinga na kuwa muosha magari. In most cases if a father is an office guy, most of the kids wataangukia kazi za ofisi, baba akiwa mkulima, wanawe wengi watakuwa wakulima pia japo huwa kuna exceptional kids
Well said, you have nailed it Sir.
 
Back
Top Bottom