Je, kuna baadhi ya Familia zimebarikiwa?

Je, kuna baadhi ya Familia zimebarikiwa?

mnaweza kuwa wote vipanga lakini bado msiwe na mafanikio sana
Hii ni kama unaongelea ukipanga wa darasani
Ilo kabila ambalo wamebarikiwa sana kuwa vipanga na akili nyingi lakini yetu mkoa wao uko kwenye list ya mikoa masikini nchi hii.
Kinachotakiwa hapo ni ukipanga uwe wa juu sana au moderate lakini wana mafanikio makubwa kimaisha nitatolea mfano familia ya MO na Bakhresa.
Hawa kielimu wako moderate sio vilaza sana wala sio vipanga sana lakini wana mafanikio makubwa mno kiuchumi
Kweli mkuu umenena.
 
Pole kwa ajali .

Ila mkuu bloodline haina uhusiano na destiny yako.

Mafanikio na maisha generally hutegemea maono (vision) ukiwa na uwezo wa kuitazama kesho yako unaweza kufanikiwa .

So usiamini mambo ya bloodline
kama hakuna issue ya blood line mbona wewe una maono lakini ni masikini wa kutupwa
Acha kuwa motivational speaker unawahubiria watu kitu wewe kimekushinda
 
Habari Wakuu.

Hivi inakuje kuna baadhi ya familia unakuta watoto wote wana akili, wamesoma mpaka level za juu kabisa. Au unakuta familia nyingine karibu wote wana uchumi mzuri, wana biashara kubwa na mafanikio kede kede.

Kwa upande mwingine unakuta familia nyingine watu karibuni wote hawaja fanikiwa kielimu wala kiuchumi. Wana umasikini uliotopea.

Je, hizo familia zinazo kuwa na watu wengi walio fanikiwa ni kuwa wamebarikiwa au ni genetics au nini ndugu wajumbe.

Karibuni kwa michango yenu.

Hujajua baraka za kweli ni zipi io ndio sababu??
 
Kuna familia fulani ya wahindi....walinijuza kwamba wao toka Enzi ukoo wao wanapata riziki kwenye kazi za vyuma....Sasa akanijuza sisi tunafeli kwa sababu hatujui kusudi au kazi zinazotuhusu....akatoa mfano kwa familia nyingine ya wahindi wao ni vyakula tu.....na wengine wao ni wajenzi tu.....wasafirishaji.....mafundi nguo etc....wanaweza kufanya vingi kwa pamoja lakini kuna cha KWAO toka ENZI..
NA HICHO NDICHO KINACHOWAPA 👍
 
Habari Wakuu.

Hivi inakuje kuna baadhi ya familia unakuta watoto wote wana akili, wamesoma mpaka level za juu kabisa. Au unakuta familia nyingine karibu wote wana uchumi mzuri, wana biashara kubwa na mafanikio kede kede.

Kwa upande mwingine unakuta familia nyingine watu karibuni wote hawaja fanikiwa kielimu wala kiuchumi. Wana umasikini uliotopea.

Je, hizo familia zinazo kuwa na watu wengi walio fanikiwa ni kuwa wamebarikiwa au ni genetics au nini ndugu wajumbe.

Karibuni kwa michango yenu.
Swali fikirishi je unajua akili inavyo fanya kazi tuanzie hapo kwanza
 
Niwaambie kitu ndugu zangu
Wakati mwingine inategemeana na initiator au aliyeaanza alifanya nini.Sasa unakuta wanaofuatia wanafuata nyayo za kuwa masikini sana au kuwa na mafanikio sana.
Nitatolea mfano familia ya kina Mwapachu
Baba yao alikuwa anaitwa Hamza Kibwana Bakari Mwapachu tokea Tanga
Alioa mwaka 1938 alimuoa Juliana ambaye ndio mama wa Harith Bakari Mwapachu na wengine
Walikutana Makerere na bwana mdogo wake Nyerere wakaanzisha tawi la kutetea wanafunzi wa Tanganyika wakati huo TAWA baadae wakabadili chama wakakiita TAA.
Wakiwa Tabora Hamza alikuwa mwenyekiti wa TAA Nyerere akiwa katibu wake hiyo ilikuwa mwaka 1947
Hamza alikuwa tabibu wakati Nyerere alikuwa Mwalimu st Mary
Hamza akaja kuwa waziri wa kwanza wa mambo ya ndani baada ya Uhuru bahati mbaya hakuishi sana alifariki mwaka 1962 mwaka mmoja tu baada ya Uhuru.

Katika utawala wa Nyerere kwa kutambua mtoto wa nyoka ni nyoka alimteua Bakari Mwapachu mtoto wa Hamza kuwa mkurugenzi mkuu wa ATC.

Watoto wa Hamza wengine wote walikuja kuwa na mafanikio makubwa sana kwenye nyanja za kielimu na vyeo watoto wa Hamza wengine ni

Harith Bakari Mwapachu
Bakari Mwapachu
Rahma Mwapachu mjane wa mwanasheria wa kwanza Jaji Mark Bomani huyu Rahama alishakuwa head of marketing communication
Heri Ali Mwapachu
Juliana Mwapachu
Wendo Mtega Mwapachu
Tunu Mwapachu
Jabe Jabiri Mwapachu

Majina niliyoandika hapo Juu nimechanganya watoto wa Hamza na wajukuu zake
wengi hapo juu wamesomea masomo fani mbali mbali na sheria wingereza na wengine bado wako huko

Familia yote hii ni kubwa iliyojaliwa kuwa na Tunu katika nyanja mbali mbali ukitizama kiundani muasisi wa yote haya ni baba yao.

Sikatai ziko familia ambazo muanzilishi alikuwa vizuri lakini waliofuata bado wakawa ni hopeless siwezi kuzitaja hapa maana ni watu maarufu.

Hapa nchini lipo kabila silitaji maana ni watani zangu pamoja na kwamba MUNGU amewapa uwezo na IQ kubwa hadi darasani lakini ajabu mkoa wao uko kwenye list ya mikoa masikini nchini wao pamoja na elimu yao ni badala ya kutumia akili sasa ni matambo matambo tu.Na kudharau kazi zile ngumu wanawake wao ndio majembe lakini wanaume kuvaa tai biashara ya kuuza mkaa au kuchemsha supu ya utumbo wanaona ni kashfa lakini kumbe inaingiza kipato kikubwa kwa siku akili yao yote ni kuajiriwa tu.

Hapo sasa ndipo linapokuja kuwa na mkono wa MUNGU katika familia husika

Ipo mifano ya familia nyingi tu mfano familia za kina Mbowe,Mo Dewji,Bakhresa,Marealle,Bomani,Rupia,bila kusahau mimi familia ninayotoka wakati mwingine nashangaa hatutumii nguvu nyingi ila mambo yanakwenda ila kikubwa kwa familia yangu tunajali elimu kuliko kitu chochote mtoto akikosa ada wa familia flani au baba flani tunaweka harambee kumchangia darasa la chini kabisa ni form four std 7 tulishaifuta toka enzi ya ukoloni hata baba zetu hakuna aliyeishia std 7 n.k

Achaneni na motivational speakers wanasema sijui weka malengo fanya hiki sijui malezi mazuri.Unaweza ukafanya yote haya na bado tu mambo yasiende kabisa au yakaenda kwa kusua sua.Ni hadi MUNGU aweke mkono wake.Yuko motivational speakers alitunga kitabu chake kiitwacho jinsi ya kupata mafanikio na kuwa tajiri.Wakati wa uzinduzi wa kitabu chake akaniomba nimchangie uzinduzi nikamuambia kisome hicho kitabu chake utapa pesa uzindue kitabu chako.

Kitu kikubwa MUNGU humnyanyua mtu yeyote anayetaka hata kama alikuwa chini MUNGU hana upendeleo

Motivational speaker ambaye anaweza kunishawishi nikamsikiliza ni Erick Shigongo.This person came from humble beginning hakuwa na taaluma ya uandishi wa habari alisoma kitu kingine kabisa.Alishawahi andika wasifu wake na kuandika aliyoyapita hadi kufika alipo.
huyu ana walk the talk yaani anahubiri alichopitia na anachokifanya sio hawa wengine wako theoretical sio pragmatic
 
Kuna familia fulani ya wahindi....walinijuza kwamba wao toka Enzi ukoo wao wanapata riziki kwenye kazi za vyuma....Sasa akanijuza sisi tunafeli kwa sababu hatujui kusudi au kazi zinazotuhusu....akatoa mfano kwa familia nyingine ya wahindi wao ni vyakula tu.....na wengine wao ni wajenzi tu.....wasafirishaji.....mafundi nguo etc....wanaweza kufanya vingi kwa pamoja lakini kuna cha KWAO toka ENZI..
NA HICHO NDICHO KINACHOWAPA
Ni kweli Wahindi wana stick kwenye kitu kimoja na wanaweka bidii wana fanikiwa.
 
Niwaambie kitu ndugu zangu
Wakati mwingine inategemeana na initiator au aliyeaanza alifanya nini.Sasa unakuta wanaofuatia wanafuata nyayo za kuwa masikini sana au kuwa na mafanikio sana.
Nitatolea mfano familia ya kina Mwapachu
Baba yao alikuwa anaitwa Hamza Kibwana Bakari Mwapachu
Alioa mwaka 1938
Walikutana Makerere na bwana mdogo wake Nyerere wakaanzisha tawi la kutetea wanafunzi wa Tanganyika wakati huo TAWA baadae wakabadili chama wakakiita TAA.
Wakiwa Tabora Hamza alikuwa mwenyekiti wa TAA Nyerere akiwa katibu wake hiyo ilikuwa mwaka 1947
Hamza alikuwa tabibu wakati Nyerere alikuwa Mwalimu st Mary
Hamza akaja kuwa waziri wa kwanza wa mambo ya ndani baada ya Uhuru bahati mbaya hakuishi sana alifariki mwaka 1962 mwaka mmoja tu baada ya Uhuru.

Katika utawala wa Nyerere kwa kutambua mtoto wa nyoka ni nyoka alimteua Bakari Mwapachu mtoto wa Hamza kuwa mkurugenzi mkuu wa ATC.

Watoto wa Hamza wengine wote walikuja kuwa na mafanikio makubwa sana kwenye nyanja za kielimu na vyeo watoto wa Hamza wengine ni
Harith Bakari Mwapachu
Bakari Mwapachu
Rahma Mwapachu mjane wa mwanasheria wa kwanza Jaji Mark Bomani
Heri Ali Mwapachu
Juliana Mwapachu
Wendo Mtega Mwapachu
Tunu Mwapachu
Jabe Jabiri Mwapachu

Familia yote hii ni kubwa iliyojaliwa kuwa na Tunu katika nyanja mbali mbali ukitizama kiundani muasisi wa yote haya ni baba yao.

Sikatai ziko familia ambazo muanzilishi alikuwa vizuri lakini waliofuata bado wakawa ni hopeless ziwezi kuzitaja hapa maana ni watu maarufu

Hapo sasa ndipo linapokuja kuwa na mkono wa MUNGU katika familia husika

Ipo mifano ya familia nyingi tu mfano familia za kina Mbowe,Mo Dewji,Bakhresa,Marealle,Bomani,Rupia n.k

Achaneni na motivational speaker wanasema sijui weka malengo fanya hiki sijui malezi mazuri.Unaweza ukafanya yote haya na bado tu mambo yasiende kabisa au yakaenda kwa kusua sua.

Kitu kikubwa MUNGU humnyanyua mtu yeyote anayetaka hata kama alikuwa chini hana upendeleo
Umeandika vema sana ndugu na umetazama jambo hili kwa upana sana. Historia nzuri pia umetupa ya akina Mwapachu.
 
Akili ya maisha, urithi wa akili&mali ndio sili pekee ya utajiri vizazi na vizazi.

Mwanaume unakwenda kutongoza mwanamke wa hovyo hovyo, tabia za hovyo, background ya familia yao&ukoo wao uko hovyo then utegemee wewe utadumu na huyo mwanamke katika maisha bora&bahati?

Au mwanamke anazaa na kijana mpuuzi asiye na akili timamu wala mindest ya utafutaji&malezi bora kwa watoto, unadhani hapo mkitengeneza familia mtapata watoto timamu? au familia yenu itakuwa na nidhamu ya mali na matumizi sahihi ya pesa?

Utajiri&akili vinakwenda sambamba na waanzilishi wa familia na background kidogo ya hawa waanzilishi wa familia ni namna gani maisha yao, watoto wao na wajukuu wao wataishi vipi na ukoo utakuwa vipi.

Usitegemee kuzaa na fala alafu watoto wasiwe mafala, hapo unakuwa mwendelezo wa ukoo wa mafala wenye maisha ya kifala.

Akili ni mwendelezo wa mafunzo+urithi wa mambo mtoto aliyofunzwa na wazazi wake+ aina ya elimu anayoipata mtoto ili aiendeleze kwa vizazi vingine.

Angalia familia zote mnazoita zina bahati,baraka,utajiri, idadi ya wasomi, utagundua tu ktk hizo familia suala la malezi ni kubwa, adabu, heshima, utii na muendelezo wa mafunzo ya wazazi wao ni mkubwa japokuwa hawakosekanagi watoto mafala ambao husumbua familia&ukoo, hawa watoto wa aina hii wapo kila familia hata kwa makapuku na wale wajawa mikosi huwa hawakosi mitoto mifala ya aina yake.

Usitegemee uzae na mwanamke/mwanaume wa malezi ya kijanjajanja/uswahiliswahili alafu utegemee vizazi vyenu kutengamaa kiakili&kiuchumi hiyo haipo labda mkaishi mbali na uyo mtu wako awe anajielewa, namaanisha awe tayari kujitoa ktk limitation za maisha ya ukoo wake.

Hakuna muujiza katika haya mambo.
Jibu limejitosheleza.
 
Back
Top Bottom