Je, kweli ni ngumu kuishi na mwanaume aliyewahi kuoa?

Je, kweli ni ngumu kuishi na mwanaume aliyewahi kuoa?

Kwa msaada wa akili mnemba
Miss Aaliyyah
Ni kweli kwamba kuna changamoto ambazo zinaweza kutokea wakati mwanamke anaishi na mwanaume aliyewahi kuoa, hasa ikiwa kuna masuala yasiyokuwa yametatuliwa kutoka ndoa ya awali. Mojawapo ya changamoto hizo ni kama zifuatavyo

1. Masuala ya kihisia: Mwanaume anaweza kuwa bado anashughulikia majeraha ya kihisia kutoka kwa ndoa ya awali, na hii inaweza kuathiri uhusiano wa sasa.

2. Mahusiano na familia ya awali: Ikiwa kuna watoto au mahusiano ya karibu na mke wa zamani, yanaweza kuleta migogoro au changamoto katika uhusiano mpya.

3. Matarajio ya tofauti: Mwanaume aliyewahi kuoa anaweza kuwa na matarajio au mazoea yanayotokana na uhusiano wa awali, ambayo yanaweza kugongana na matarajio ya mwanamke mpya.

4. Kumlinganisha na mke wa zamani: Hili linaweza kuwa tatizo ikiwa mwanaume ana tabia ya kulinganisha mwenza wa sasa na aliyekuwa naye awali.
 
Anhaa kum
😀😀 Kumbe na wewe umewahi kuoa ?
Dah ni kweli naona ni kazi kweli maana hata Mimi hata nikipata demu yeyote lazima nianze kumfananisha na mke wangu wa zamani hasa usafi ,kauli nzuri ni hapo najikuta naachana na wengi sababu nilishamzoea yule kitabia na kisosholojia inakuwa ngumu kukubali tabia mpya za mdada mwingine .
Ila najipa Imani nitafanikiwa kufit kwenye life la mtoto wa mtu ,few days
Mimi toka nimechomoka kwa yule nahisi kama nimetoka gereza la ADX Florence la huko colorado , yani mtato wa mtu anikiambia habari za kumuoa ninashtuka sana kwa kwel😂😂
 
Mwanaume alietoka kuoa anakuwa amebeba experience (bad or good), so vitu vingi vitakuwa si vipya kwake, now wameanzaje mahusiano yao hapo ndipo msingi wa yote. Walianza kwa upendo, mwanaume / mwanamke alipenda kweli, au it was random attachment?
Kama hakukuwa na upendo but sense of majukumu ndio viliwakutanisha ndivyo watakavyo chukuliana wakiishi pamoja

Wakichukiliana kwa mapenz, wataenda hivyo hivyo ila kama walichukuliana kwa majukumu ndivyo vitavyo wakuta
Hapo nimekuelewa Sasa
Ikitokea kuwa na mwanaume wa namna hii vipi unaweza kumuweka kwenye mstari maybe mwanamke kama ana weakness au huyu mwanaume analinganisha mwanzo na Sasa hiv
 
Ukiwa mwanamke bwana ni Raha tu .
Sasa dada kaleta swali badala utoe mawazo yako ila umejipa kazi kwenda kufanya utafiti alafu ulete mrejesho ila ningekuwa ni Mimi nimeuliza vipi jamani wanume wenzangu ni kweli nikiwa bahili nitakuwa tajiri ungenipa jibu la mkato ,Mara utajua wewe .

Aisee wanawake waheshimiwe tu .
Member wengi humu nimewawekea Standard zao kwahiyo acha kujipa Umuhimu wa kunielekeza jinsi ya kumjibu mtu. Ninavyo mjibu Lucas Mwashambwa ni tofauti nitakavyo mjibu Mshana. Au nitakavyomjibu Faiza Foxy ni tofauti nitakavyo mjibu Cute Wife.
 
Mwanamke ndo atakuwa na jukumu la kuamua kupigania ndoa au kushindwa akatembea
Mimi binafsi kwa muda ndio nimekua nikipigania ndoa mpaka sasa nimenyoosha mikono.
Huko nyuma katika moja ya vikao vya usuluhishi nilishawahi tamkiwa na wife mbele ya baba angu mzazi kuwa "aniache aone kama sijapata mtu ndaninya siku mbili tu atakaenipa maisha mazuri zaid ya haya" 😅
Kwasasa nimeamua kunyoosha mikono
 
Uzoefu, unaonesha hili jambo, Kwa kiasi kikubwa linataka kufanana na ishu ya Kuoa Mwanamke aliyewahi kupitia mahusiano mengi kabla hajaolewa nawe.

Kuna ile tendency ya kufanya ulinganisho.

Kwamba alipotoka alikuwa anapewa huduma fulani fulani, ambazo wewe humpatii.

Kuna moment alikuwa anafurahia huko alipokwepo, lakini kwako asipate.

Kwahiyo inapotokea unam-treat tofauti anaweza kuanza kukulalamikia bayana ama kupitia marafiki zako.

Hata hivyo ni rahisi sana kuweza kuishi na kumkamata Mwanaume wa hivi.

Kwanza ishi naye Kwa kumheshimu, jitahidi usimvunjie heshima yake kama Mumeo na Baba wa watoto wako.

Pili mpe mapenzi yatakayomfanya Baba wa watu asione Wala kukumbuka kwingine.

Tatu, kuwa na kauli nzuri Kwa Mumeo, hata kama amekukosea, mueleze taratibu. Kwa kuwa yeye ni mtu mzima, najua ataelewa.

Kila la heri Mjukuu, kumbuka Kadri mvinyo unavyozidi Kulala ndivyo unavyozidi kuwa mtamu
 
Hapo nimekuelewa Sasa
Ikitokea kuwa na mwanaume wa namna hii vipi unaweza kumuweka kwenye mstari maybe mwanamke kama ana weakness au huyu mwanaume analinganisha mwanzo na Sasa hiv
Now sasa ita depend na maturity ya mwanaume. Kama bado ana linganisha means haja move on, and hiko si kitu kizuri.

Mwanaume ambae ametoka huko anatakiwa awe mature enough kujua kila mwanamke ana different behaviour na namna ya kuwaelekeza nayo ni different
 
Back
Top Bottom