Je, kweli ni ngumu kuishi na mwanaume aliyewahi kuoa?

Je, kweli ni ngumu kuishi na mwanaume aliyewahi kuoa?

Anhaa kum
😀😀 Kumbe na wewe umewahi kuoa ?
Dah ni kweli naona ni kazi kweli maana hata Mimi hata nikipata demu yeyote lazima nianze kumfananisha na mke wangu wa zamani hasa usafi ,kauli nzuri ni hapo najikuta naachana na wengi sababu nilishamzoea yule kitabia na kisosholojia inakuwa ngumu kukubali tabia mpya za mdada mwingine .
Ila najipa Imani nitafanikiwa kufit kwenye life la mtoto wa mtu ,few days
Mnajua kututesa haki 🤣🤣
 
Kwa msaada wa akili mnemba
Miss Aaliyyah
Ni kweli kwamba kuna changamoto ambazo zinaweza kutokea wakati mwanamke anaishi na mwanaume aliyewahi kuoa, hasa ikiwa kuna masuala yasiyokuwa yametatuliwa kutoka ndoa ya awali. Mojawapo ya changamoto hizo ni kama zifuatavyo

1. Masuala ya kihisia: Mwanaume anaweza kuwa bado anashughulikia majeraha ya kihisia kutoka kwa ndoa ya awali, na hii inaweza kuathiri uhusiano wa sasa.

2. Mahusiano na familia ya awali: Ikiwa kuna watoto au mahusiano ya karibu na mke wa zamani, yanaweza kuleta migogoro au changamoto katika uhusiano mpya.

3. Matarajio ya tofauti: Mwanaume aliyewahi kuoa anaweza kuwa na matarajio au mazoea yanayotokana na uhusiano wa awali, ambayo yanaweza kugongana na matarajio ya mwanamke mpya.

4. Kumlinganisha na mke wa zamani: Hili linaweza kuwa tatizo ikiwa mwanaume ana tabia ya kulinganisha mwenza wa sasa na aliyekuwa naye awali.
Sawa Asante sana
Umefafanua vizuri sana Asante
 
Uzoefu, unaonesha hili jambo, Kwa kiasi kikubwa linataka kufanana na ishu ya Kuoa Mwanamke aliyewahi kupitia mahusiano mengi kabla hajaolewa nawe.

Kuna ile tendency ya kufanya ulinganisho.

Kwamba alipotoka alikuwa anapewa huduma fulani fulani, ambazo wewe humpatii.

Kuna moment alikuwa anafurahia huko alipokwepo, lakini kwako asipate.

Kwahiyo inapotokea unam-treat tofauti anaweza kuanza kukulalamikia bayana ama kupitia marafiki zako.

Hata hivyo ni rahisi sana kuweza kuishi na kumkamata Mwanaume wa hivi.

Kwanza ishi naye Kwa kumheshimu, jitahidi usimvunjie heshima yake kama Mumeo na Baba wa watoto wako.

Pili mpe mapenzi yatakayomfanya Baba wa watu asione Wala kukumbuka kwingine.

Tatu, kuwa na kauli nzuri Kwa Mumeo, hata kama amekukosea, mueleze taratibu. Kwa kuwa yeye ni mtu mzima, najua ataelewa.

Kila la heri Mjukuu, kumbuka Kadri mvinyo unavyozidi Kulala ndivyo unavyozidi kuwa mtamu
Babu hii changamoto ya wengi unaweza Kuta unampenda sana mumeo kumbe yeye anampenda mke wa zamani

Ishu ya malezi nayo kama ni changamoto
Mm sio Babu nilivo dhaifu nitakufa mapema mm nitafutie new model mjukuu wako niienjoy 😀
 
Back
Top Bottom