Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Kama wazazi wapo, hii kesi ni ndogo sana; inamalizwa kifamilia
 
Habari za shughuli ndugu zangu,naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa manzoni mwa mwaka huu,baada ya mazishi kuna kikao cha ndugu kilikaa kujadili mustakabali wa familia kama ilivyo desturi sasa kwenye kikao kile,wengi walikuwa ni ndugu wa mke wangu,wengi wao hata nilikuwa siwafahamu,kikao kikamteua shemeji yangu ambaye ndiye kaka mkubwa wa mke wangu awe msimamizi wa mirathi, mke wangu alikuwa na Mali alizochuma yeye mwenyewe kabla hatujaoana,na mimi nilikuwa na zangu binafsi,na kuna kiwanja alikinunua kwa kaka yake huyohuyo wakati tukiwa tunaishi pamoja,higher kiwanja tukajenga nyumba za kupangisha,na tukapata mpangaji mmoja aliyepanga vyumba vyote 8,wakati huo mimi nilikuwa nipo nje ya mkoa kikazi,kwa hiyo hata wakati ujenzi unaendelea,mimi sikuwepo,mtu aliyekuwa akisimamia ujenzi ni huyo kaka wa mke wangu,kwa kuwa hakuwa na shughuli yoyote kipindi hicho hivyo nikawa namlipa asaidie kusimamia ujenzi na hata shughuli nyinginezo za ujenzi kwenye nyumba nyingine niliyokuwa naijenga mtaa mwingine ambayo ndiyo tunayoishi hata sasa,sasa tabu imekuja baada ya yeye kukabidhiwa jukumu la kusimamia mirathi,kwanza alikosana na yule mpangaji hali iliyomlazimu mpangaji yule kuhama mimi nikiwa sipo,kisha akawapangishia wapangaji wengine bila kunitaarifu,baadaye kodi ikaanza kusumbua,mara anitumie mara asitume,nikaamua kumfuata ili anieleze tatizo ni nini,baada ya kufokeana sana akaniambia yeye ndiye msimamizi wa Mali zote kwa hiyo sipaswi kumpangia,ni takribani miezi mitano sasa hajaleta kodi ya nyumba,wale wapangaji sijui aliwaseti vipi,maana kila nikijaribu kuwafata huwa wananikwepa,nadhani hajafungua mirathi mahakamani kwani kuna vielelezo ambavyo angepaswa kuvipata kutoka kwangu ila hakuwahi kuniomba nimpatie,sasa nafikiri nimpeleke mahakamani,ila huko sina nijualo especialy kwa kesi ya aina hii,naamini hapa kuna wajuzi wa mambo kama haya,hivyo naomba mchango wenu wa mawazo ili niweze kuilinda haki ya familia yangu nikiwa na ujasiri,natanguliza shukrani zangu kwenu.
Nimesoma kwa makini nimebaini kuwa hii ndoa yako ilikuwa na shida in some points ni vile tu vitu vingi umeficha kwa faida yako binafsi.. unayokutana nayo sasa ni matokeo ya hayo matatizo uliyokuwa unapambana nayo kwenye ndoa yenu hapo awali.. tafuta njia muafaka ya kumaliza tatizo hilo la familia, Mungu akusaidie.
 
Habari za shughuli ndugu zangu,naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa manzoni mwa mwaka huu,baada ya mazishi kuna kikao cha ndugu kilikaa kujadili mustakabali wa familia kama ilivyo desturi sasa kwenye kikao kile,wengi walikuwa ni ndugu wa mke wangu,wengi wao hata nilikuwa siwafahamu,kikao kikamteua shemeji yangu ambaye ndiye kaka mkubwa wa mke wangu awe msimamizi wa mirathi, mke wangu alikuwa na Mali alizochuma yeye mwenyewe kabla hatujaoana,na mimi nilikuwa na zangu binafsi,na kuna kiwanja alikinunua kwa kaka yake huyohuyo wakati tukiwa tunaishi pamoja,higher kiwanja tukajenga nyumba za kupangisha,na tukapata mpangaji mmoja aliyepanga vyumba vyote 8,wakati huo mimi nilikuwa nipo nje ya mkoa kikazi,kwa hiyo hata wakati ujenzi unaendelea,mimi sikuwepo,mtu aliyekuwa akisimamia ujenzi ni huyo kaka wa mke wangu,kwa kuwa hakuwa na shughuli yoyote kipindi hicho hivyo nikawa namlipa asaidie kusimamia ujenzi na hata shughuli nyinginezo za ujenzi kwenye nyumba nyingine niliyokuwa naijenga mtaa mwingine ambayo ndiyo tunayoishi hata sasa,sasa tabu imekuja baada ya yeye kukabidhiwa jukumu la kusimamia mirathi,kwanza alikosana na yule mpangaji hali iliyomlazimu mpangaji yule kuhama mimi nikiwa sipo,kisha akawapangishia wapangaji wengine bila kunitaarifu,baadaye kodi ikaanza kusumbua,mara anitumie mara asitume,nikaamua kumfuata ili anieleze tatizo ni nini,baada ya kufokeana sana akaniambia yeye ndiye msimamizi wa Mali zote kwa hiyo sipaswi kumpangia,ni takribani miezi mitano sasa hajaleta kodi ya nyumba,wale wapangaji sijui aliwaseti vipi,maana kila nikijaribu kuwafata huwa wananikwepa,nadhani hajafungua mirathi mahakamani kwani kuna vielelezo ambavyo angepaswa kuvipata kutoka kwangu ila hakuwahi kuniomba nimpatie,sasa nafikiri nimpeleke mahakamani,ila huko sina nijualo especialy kwa kesi ya aina hii,naamini hapa kuna wajuzi wa mambo kama haya,hivyo naomba mchango wenu wa mawazo ili niweze kuilinda haki ya familia yangu nikiwa na ujasiri,natanguliza shukrani zangu kwenu
Njoo in box I can Assist.
 
Jamani hivi inakiwaje MTU anaonewa na binadamu mwenzako kiasi hiki na wewe unakiwa tu kama mjinga fulani upo tu.

Hapo hamna haja ya mahakama wala Mwanasheria,orodhesha mali za mkeo ambazo ulimkuta nazo zifanyie valuation thamani. baada ya hapo itisha kikao wawake wazi uwaeleze kuwa Mali za marehemu mkeo ambazo ulimkuta nazo ni za watoto.

Na kwa sababu wewe Baba na Mume bado upo ndio msimamizi wa mali hizo full stop.Atakayepinga akafungue mashitaka mahakamani.Mali ambazo mlichuma wote hizo ni zako-acha kuwa bwege.
**pole sana kwa kufiwa na mwenza.
 
Pole sana.
Hana Haki wala Hakuna cha kubugi wala kuchelewa. Afterall baada ya msiba hukuwa sawa kwa kufiwa.
Tafuta mwanasheria. Mirathi ipi wanayotaka kuigawanya wakati mmewe upo.
Zile mali alizochuma dada yao peke yake hizo ndio wao wakae vikao vyao , wewe wape ushirikiano tu.
Ameqeka kufuri kwenye nyumba yako kavunje uendelee .
Mchukulie RB kwake akamatwe kwa kuingia na kupoteza vitu ndani y hiyo nyumba
Hata mali alizochuma Dada yao haziwahusu maana marehemu ameacha watoto,zingewahusu kama marehemu hana watoto.
 
Habari za shughuli ndugu zangu,naombeni mnishauri kwa jambo hili ambalo naona nalazimika kulifanya, nilipata msiba kwa kufiwa na mke wangu wa ndoa manzoni mwa mwaka huu,baada ya mazishi kuna kikao cha ndugu kilikaa kujadili mustakabali wa familia kama ilivyo desturi sasa kwenye kikao kile,wengi walikuwa ni ndugu wa mke wangu,wengi wao hata nilikuwa siwafahamu,kikao kikamteua shemeji yangu ambaye ndiye kaka mkubwa wa mke wangu awe msimamizi wa mirathi, mke wangu alikuwa na Mali alizochuma yeye mwenyewe kabla hatujaoana,na mimi nilikuwa na zangu binafsi,na kuna kiwanja alikinunua kwa kaka yake huyohuyo wakati tukiwa tunaishi pamoja,higher kiwanja tukajenga nyumba za kupangisha,na tukapata mpangaji mmoja aliyepanga vyumba vyote 8,wakati huo mimi nilikuwa nipo nje ya mkoa kikazi,kwa hiyo hata wakati ujenzi unaendelea,mimi sikuwepo,mtu aliyekuwa akisimamia ujenzi ni huyo kaka wa mke wangu,kwa kuwa hakuwa na shughuli yoyote kipindi hicho hivyo nikawa namlipa asaidie kusimamia ujenzi na hata shughuli nyinginezo za ujenzi kwenye nyumba nyingine niliyokuwa naijenga mtaa mwingine ambayo ndiyo tunayoishi hata sasa,sasa tabu imekuja baada ya yeye kukabidhiwa jukumu la kusimamia mirathi,kwanza alikosana na yule mpangaji hali iliyomlazimu mpangaji yule kuhama mimi nikiwa sipo,kisha akawapangishia wapangaji wengine bila kunitaarifu,baadaye kodi ikaanza kusumbua,mara anitumie mara asitume,nikaamua kumfuata ili anieleze tatizo ni nini,baada ya kufokeana sana akaniambia yeye ndiye msimamizi wa Mali zote kwa hiyo sipaswi kumpangia,ni takribani miezi mitano sasa hajaleta kodi ya nyumba,wale wapangaji sijui aliwaseti vipi,maana kila nikijaribu kuwafata huwa wananikwepa,nadhani hajafungua mirathi mahakamani kwani kuna vielelezo ambavyo angepaswa kuvipata kutoka kwangu ila hakuwahi kuniomba nimpatie,sasa nafikiri nimpeleke mahakamani,ila huko sina nijualo especialy kwa kesi ya aina hii,naamini hapa kuna wajuzi wa mambo kama haya,hivyo naomba mchango wenu wa mawazo ili niweze kuilinda haki ya familia yangu nikiwa na ujasiri,natanguliza shukrani zangu kwenu.
Ngoja nikomenti kabla sijasoma uzi
Mfungulie kesi ya uchochezi au uhujumu uchumi!
 
Chapa makofi huyo shemeji mtu wape wapangaji notisi vunja kufuli weka wapangaji wapya.
Kanuni yangu Mali yangu ni ya watoto wangu na mke wangu,Mali ya mke wangu ni ya kwangu na watoto wangu.acha kuwa lazy lazy wewe changamka,ukitaka ubaya chezea mali yangu au familia yangu
 
yanii simple mbona kwanza huyo bado hajawa msimamizi wa mirathi kisheria itakuwa bado hajaapa mahakamani hivyo nenda serikali ya mtaa kalalamike huko anaitwa then mkane na tumia hizo sababu kuwa huna imani nae kuwa hukubaliani na kile kikao cha familia then kiitishwe kikao kingine pindua meza akisogelea nyumba zako muitie mwizi.
Watu wengi wamechangia kwa hisia siyo kisheria. Shemeji anaweza kuwa kuwa msimamizi.
Wewe upo sahihi. Msimamizi wa mirathi lazima akaape mahakamani na lazima muhutasari wa kikao cha wana familia ndugu wa mfiwa uwasilishwe mahakamani.
Kama hajaenda mahakamani basi huyo ni batili kisheria kufanya kazi za usimamizi kabla hajarasimishwa.
 
Kosa la kwanza wanakaaje kikao wagawane majukumu ya kuangalia mali wakat wewe ndio muhusika mkuu?
Inawezekana wanahis wewe umedandia mali za dada yao
 
Msimamizi wa mirathi lazima ateuliwe na wanafamilia/ukoo ambao wewe ndiye mhusika mkuu, huyo shemeji yako aliteuliwa na nani?. Yawezekana kwenye hizo mali kuna mchango wake huyo shemeji yako na walikuwa hawakushirikishi ila wewe unajua ni mali ya mke wako.
 
Kwanza ulionaga wapi MKE anafariki kinakaa kikao Cha mirathi?

Nnachojua mke akishafariki automatically Mali zote zinabaki chini ya mume, na ndo anacontroll kila kitu. Na hakuna mahojiano.
Mkuu naona wachangiaji wengi wanaikwepa sana hio point,,, Kikao cha mirathi.!?? Halafu Ukweni.!?? Ili iweje.!?? Ndugu wa Mume nao walikuwa wapi.!??? Tatizo liko hapa na wala sio hio mirathi au aliyechaguliwa.

Sawa mfiwa ulikuwa na wakati Mgumu,,,, Je,Ndugu wa Mume walikuwa wapi.!? Walishiriki kikao?? Nini sababu ya kikao kufanyika Ukweni.!??

Mleta uzi Pole sana kwa Kufiwa na Mkeo.. Kilichofanya ufike hapo ndio kitafanya ushindwe hata huko Mahakamani... Rekebisha Mentality yako.. Unaonekana Mtoto wa mama sana,,, Kuwa Mwanaume kwanza ndio ulishughulikie hilo...

Be a man,,, Stay taliban...
 
Mkuu naona wachangiaji wengi wanaikwepa sana hio point,,, Kikao cha mirathi.!?? Halafu Ukweni.!?? Ili iweje.!?? Ndugu wa Mume nao walikuwa wapi.!??? Tatizo liko hapa na wala sio hio mirathi au aliyechaguliwa.

Sawa mfiwa ulikuwa na wakati Mgumu,,,, Je,Ndugu wa Mume walikuwa wapi.!? Walishiriki kikao?? Nini sababu ya kikao kufanyika Ukweni.!??

Mleta uzi Pole sana kwa Kufiwa na Mkeo.. Kilichofanya ufike hapo ndio kitafanya ushindwe hata huko Mahakamani... Rekebisha Mentality yako.. Unaonekana Mtoto wa mama sana,,, Kuwa Mwanaume kwanza ndio ulishughulikie hilo...

Be a man,,, Stay taliban...

ROBERT HERIEL msaidie huyu mawazo kisheria
Jamaa katuangusha Sana
 
Msimamizi wa mirathi lazima ateuliwe na wanafamilia/ukoo ambao wewe ndiye mhusika mkuu, huyo shemeji yako aliteuliwa na nani?. Yawezekana kwenye hizo mali kuna mchango wake huyo shemeji yako na walikuwa hawakushirikishi ila wewe unajua ni mali ya mke wako.
Probably mtoa mada alkua analelewa au alishalishwa limbwata (mume wa mchongo)
 
Back
Top Bottom