Capt Tamar
JF-Expert Member
- Dec 15, 2011
- 12,340
- 16,383
- Thread starter
-
- #161
Kile kikao cha kifamilia sijui hata kilifikiaje hitimisho hilo,labda waliangalia ukaribu wake na familia yangu,yule mtu tulikuwa tunamuamini na nilimtumia kwa kazi nyingi tu mkuuHalafu umemuachia shemeji akupangie mali zako na watoto wako, hivi shemeji ameingiaje hapo?
Hapo hakuna kesi ya mirathi, ni baba tu kusimama imara kama Baba wa familia.pol
kwanza pole sana mkuu kwa msiba wa mkeo cha pili tafuta mwanasheria
Hongera kwa kupigania haki yako mkuu,mimi kingine kilichonipa changamoto ni umbali kutoka eneo langu la kazi,maana ni mkoa tofauti,nimekuja hapa wakati huu kwa kuwa angalau kwa sasa naweza kulishughulikia hilo,nina muda kidogo wa mapumziko,shukrani sana mkuuPole sana ndg na kufiwa, Chukua tahadhari sana maana watu wakitaka kudhulumu Mali wako radhi kufanya lolote lile! Mi kuna fala mmoja alijichomeka kwenye Mali za Mzee wetu eti anasema yeye na Mzee walichangia Baba mmoja Mama tofauti wakati hatujawai kumuona hata siku moja toka Mzee wetu Yuko hai, tukakuta kagushi Mirathi yetu na kafanikiwa kuchomoa documents za Nyumba za Mzee,mbona nilimuwashia Moto hadi akawa ananipa mikwara eti ataniachia radhi,mbona alizitema mwenyewe!!
Kweli,kuna mtu hapo kaingiza hii issue yangu na ukosefu wa elimu ya shule!! Kumbe kuna hadi wasomi wabobevu wa masuala mengine hawajui issue tofauti na walichosomea,kuna mzee mmoja ni rafiki yangu na ni msomi wa haja,nilimwomba ushauri juu ya jambo hili akaniambia hajui lolote kuhusu mambo ya mirathi,kawaida sanaSiyo watu wote wanajua Mambo ya Mirathi na taratibu zake, wengine ndiyo hadi waafiwe ndiyo labda wanaweza kuanza kujua Mambo hayo tena kwa kuelekezwa na watu wanaojua utaratibu wa Mirathi!!
Asante,ila umenitisha,nitapambana mkuu,asante sanaPole sana kwa maelezo haya inaonesha una vigezo vyote vya kushinda kesi.
Ushauri wangu kuwa makini sana na huyo shemeji yako, siku zako za kuishi zinahesabika. Pia usianike kila kitu humu anaweza kuwa anakuchora tu. Tafuta mwanasheria mzuri akusaidie kaka.
Nafasi ya mzazi, itumiwe na shemeji aliyemsomesha na kumlea, na muweke makubaliano ya kunufaika kwa watoto na wao kupitia mali za marehemu; hawa ndugu wengine hawana maamuzi kwenye hilo.Mkuu Equation x wazazi wa mke wangu walishafariki mke wangu akiwa mdogo sana,akalelewa na shemeji yake.
Asante sana mkuu,kuna mdau hapa ameniunganisha na mwanasheria mmoja,nimempigia simu tukaongea kidogo,amenieleza hivi hivi kama ulivyoeleza hapa,tena kumbe naye alikuwa anasoma thread hii,au ndiyo wewe mkuu?shukrani sana,umenitia moyo sanaHaina maana ya kwamba kikao Cha familia au ukoo kikishakaa na kumteua msimamizi wa mirathi ndo Basi kashakuwa, mahakama ndo inayomuidhinisha na kwa sababu walifunga ndoa ya kikristo special forum/court hapo ni mahakama ya wilaya ambapo kunaprocedure za kufuata ambazo mme au watoto lazima wahusishwe coz ndo warithi, mashauri ya mirathi hasa kwa wakristo Ni tofauti kidogo na waislam au waamini kimira ambao wao nimakahama ya mwanzo tu na Hakuna complication Sana primary court,... Huku mahakama ya wilaya lazima huyo anaejiita msimamizi wa mirathi afanye PETITION FOR LETTER OF ADMINISTRATION, lazima pawe na CONSENT OF THE HEIRS yaani warithi wawe wamemkubali huyo jamaa kuwa msimamizi, Kuna issue za general citation zitatoka , kuna form ya administration of bond without surety ambapo huyo msimamithi wa mirathi lazima aweke bond ya kiasi Cha pesa au Mali yake Kama dhamana ili asije akafuja au kutumia Mali za marehemu,..na kwa maana hio huyo msimamizi wamirathi Kama Hakuna taratibu hizo nilizozitaja hapo juu kufuatwq Basi huyo jamaa sidhani Kama anatambulika na mahakama kama msimamizi wa mirathi ,kikao tu Cha kumteua msimamizi wa mirathi hakitoshi...na hata Kama ikitokea kaaidhinishwa na mahakama na bado hafanyi wajibu wake bado anweza akawe revoked kwa sheria na anashitakiwa... Na as long as wewe una ndoa na mnawatoto kwenye issue ya mirathi ninyi ndo most favorable Sana kuliko hao ndugu wengine hasa kwenye Mali ambazo mlichuma wote
hapana sio Mimi# Ila IAM a lawyer tooAsante sana mkuu,kuna mdau hapa ameniunganisha na mwanasheria mmoja,nimempigia simu tukaongea kidogo,amenieleza hivi hivi kama ulivyoeleza hapa,tena kumbe naye alikuwa anasoma thread hii,au ndiyo wewe mkuu?shukrani sana,umenitia moyo sana
Ondoa shaka mkuu,huyo jamaa hata help ya kunilogea labda aje kuniomba,nadhani ni njaa tu zinamsukuma kufanya hivyo,ndugu zake wa kuzaliwa wamemwita na kumtaka mara kadhaa aachane na Mali za watu,sasa hivi amewa block wote,hakuna kitu ataachiwa mkuu,nitaleta mrejesho hapa,wadau hapa wamenipa nguvu na are ya kupigania haki yangu kwa mustakabali wa familia yangu,nipo njiani sasa hivi,nimeanza rasmi.Hapa ndio kuna kutoana roho sijui kwanini akili yangu huwa haitakagi kigombea mali. Yaani huwa niko radhi nimuachie tu mtu.
Watu wa hivyo hawakawii hata kwenda kukuroga nawe ufe. Kuwa makini mkuu. Watoto wako bado wadogo kama iko ndani ya uwezo wako embu baki tu ukimtazama.
Ila ukiweza basi komaa, japo naanza kunusa hatari.
Sidhani kama unaeleweka mkuu,nimepigwa chini kwenye nini?kunitupilia mbali kivipi?nani wa kunitupilia mbali sasa? Hebu kuwa serious kidogo mkuuUmeshapigwa chini kitendo cha kunyimwa usimamizi was mirathi ilikuwa mbinu ya kukutupolia mbali na kukudhulumu
Usiwe unawajibu watu kama hao..🚮Sidhani kama unaeleweka mkuu,nimepigwa chini kwenye nini?kunitupilia mbali kivipi?nani wa kunitupilia mbali sasa? Hebu kuwa serious kidogo mkuu
...Hakuwa Hata na Haja ya Kuchaguwa Mtu Mwingine awe Msimamizi wa Mali za Mkeo wakati wewe Upo hai!Ww ni mtu mzima,kwa nini ulishindwa kushinikiza ili uwe msimamizi wa.mirathi.Kama kweli una haki katika mali hizo mkatae huyo msimamizi.Wanasheria watakusaidia zaidi
Ndg yangu wala usijali,siyo kosa kabisa Mtu kuchelewa kujua Mambo na taratibu za Mirathi japokua zipo kwenye vitabu vya Sheria zetu na ndiyo maana tuna Wana Sheria Kama vile tulivyo na ma Dr kwa ajili ya watu Wagonjwa! Na Mara nyingi Mambo ya Mirathi yanakuja Kama kuna Mali za Marehemu zenye mgogoro ndiyo huwa linaangaliwa swala zima la Mirathi na taratibu zake!!Kweli,kuna mtu hapo kaingiza hii issue yangu na ukosefu wa elimu ya shule!! Kumbe kuna hadi wasomi wabobevu wa masuala mengine hawajui issue tofauti na walichosomea,kuna mzee mmoja ni rafiki yangu na ni msomi wa haja,nilimwomba ushauri juu ya jambo hili akaniambia hajui lolote kuhusu mambo ya mirathi,kawaida sana
Ndoa ya kanisani,na vyeti vyote viwili ninavyo,sasa nimejua kuwa kumbe ni hitaji la kisheria ukoo au familia kukaa kikao baada ya mazishi na kumpendekeza msimamizi wa mirathi,na anaweza kuwa yeyote mwenye uchungu na Mali za marehemu,tatizo lililojitokeza hapa ni tamaa,asante mkuuhapo sijaelewa msimamizi wa mirathi anachaguliwa vipi wakati mme bado yuko hai,
hiyo ndoa ipo kisheria ama ilikuwa sogea tuishi?
Asante mkuuNdugu umezaa nae watoto wawili ina maana hizo mali ni za hao watoto wenu wawili ila msimamizi mkuu ilitakiwa ubaki wewe hata kwa mali alizo zichuma kabla kwa sababu ana watoto. Ungekua hujazaa nae hata kama pia sheria ina kutambua kua una haki lakini ki ustaarabu ungewaachua ndugu zake, as long unezaa nae hizo mali ulitakiwa uzisimamie kwa manufaa ya hao watoto. Ninacho kiona mimi hapo maregemu anaonekana ndo alikua bread winner of the familiy na bado alikutawala wewe na huo udhaifu umeendelea nao mpaka baada ya mke kufariki. Nini cha kufanya kama ulisign huo waraka wa kumteua huyo msimamizi wa mirathi ambalo wengi wamekuambia ni kosa kubwa ulifanya. Unapaswa kutafuta mwanasheria akusimamie kwamba huna imani na msimamizi wa mirathi ainisha haya matendo aliyo kwisha kuyatenda. nafasi hiyo ipo na una haki kwa kiasi kikubwa sana
Kabisa...Hakuwa Hata na Haja ya Kuchaguwa Mtu Mwingine awe Msimamizi wa Mali za Mkeo wakati wewe Upo hai!
Ulibugi. Tafuta Wakili Mzuri umueleze A to Z.
Wanakuchezea hao...[emoji35]