Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Je, mtu huyu nimfungulie kesi ya aina gani?

Mkuu Capt Tamar pole sana!.

Ila nina maswali kadhaa napaswa kukuuliza.

1.Je wewe ni mume halali wa marehemu?(mmefunga ndoa?)

2.Mlibahatika kupata watoto wewe na mkeo?

3.Ilikuwaje kaka mtu akawa msimamizi wa mirathi ya dada yake wakati wewe mume wake upo?

Naomba tafadhali unijibu mkuu maana sielewi!
Kuna wakat unakuwa na akili kuna wakat unakuwa ovyo sana
 
Pole sana Mkuu na msiba.na maswahibu unayopitia kwa sasa.

Sijaweza kusoma comment zote ila kama kutakuwa na comment ambayo imesema nitakayokueleza basi naungana nayo.

Haya twende kazi,

Nitaeleza kazi za msimamizi wa mirathi kwa ufupi sana ili upime je anazifanya huyo msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo

Kazi kuu ya msimamizi wa mirathi ni kutambua na kukusanya mali za marehemu na kisha kuzigawa kwa warithi wake, ndani ya miezi 6. Sasa swali ni je huyo msimamizi wa mirathi amezitambua na kuzikusanya mali za marehemu mkeo?, baada ya kuzitambua na kuzikusanya amezigawa kwa warithi wa hizo mali?. Je, amefuata muda uliowekwa na sheria yaani miezi 6?. (Majibu unayo ila nitaeleza chakufanya ikiwa ni tofauti)

Sasa jambo gani ufanye ikiwa hajafuata muongozo wa sheria.

Hapa unatakiwa kwenda kufungua pingamizi dhidi ya msimamizi wa mirathi ukiitaka mahakama itengue/ifute uteuzi wake kwa kuwa hawezi kukusanya na kugawa mali z marehemu na pia amekuwa mharibifu/mpotevu wa mali za marehemu na zaidi ya yote amejinufaisha yeye binafsi.

Sasa kabla ya kufanya yote haya kuna jambo unatakiwa uwe na uhakika nalo kwa 100% ambalo ni Je, huyu shemeji yako aliteuliwa na Mahakama kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo?, au mliishia kwenye kikao cha familia/ndugu?.

Kama alipeleka maombi ya kuteuliwa Mahakamani basi sasa hapo unatakiwa kuomba mahakama itengue/ifute uteuzi wake. Kama hakuwahi kupeleka maombi ya kuteuliwa Mahakamani na mahakama.ikayakubali maombi yake basi huyo sio msimamizi wa mirathi kwakuwa ni Mahakama pekee yenye uwezo wa kuteua msimamizi wa mirathi na mahakama hiyo ni Mahakama ya Mwanzo au ahakama Kuu na sio ahakama nyingine zilizosalia.

Sasa kama hakuwahi kupeleka ombi Mahakamani, wewe sasa unatakiwa kupeleka maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo Mahakamani. Hapa utatakiwa kuwa na muhuktasari wa kikao cha familia kukupendekeza kama msimamizi wa mirathi ikiwa mkeo hakuacha wosia.

Ikiwa ni ngumu kuitisha hicho kikao wewe nenda mahakama ya mwanzo fungua hivyo hivyo ombi la kuteuliwa kisha ieleze ahakama kwanini.hakuna muhuktasari wa kikao na hapo utaeleza kuwa aliyependekezwa hajafungua mirathi na anapoteza mali za marehemu ambapo hata marehemu asingezipoteza hivyo. (Shawishi Mahakama ila chunga usiwe unalalamika).

Kuna swala la wosia, kama mkeo aliacha wosia basi fuateni wosia unasema nini na hapa ni lazima bado kufungua mirathi mahakamani ila uzuri hapa hamtakuwa na sababu ya kikao cha kumteua msimamizi wa mirathi sababu tayari katajwa na wosia.

Mimi ni haya tu kwa sasa naamini utapata mwanga wakutosha kujua ufanye nini, ukiwa na maswali usisitekuuliza. Naweza nikachelewa kujibu ila nitakujibu tu.

Karibu.
Umefafanua vyema sana mkuu, Ningependa kujua je, wosia unaokubalika lazima uwe na vigezo vipi?
 
Mkuu Capt Tamar pole sana!.

Ila nina maswali kadhaa napaswa kukuuliza.

1.Je wewe ni mume halali wa marehemu?(mmefunga ndoa?)

2.Mlibahatika kupata watoto wewe na mkeo?

3.Ilikuwaje kaka mtu akawa msimamizi wa mirathi ya dada yake wakati wewe mume wake upo?

Naomba tafadhali unijibu mkuu maana sielewi!
Nakazia swali maana hata mimi nimeshindwa kuelewa huyo mke umeishi nae muda gani na kama mmebahatika kupata watoto hao watoto wana umri gani?

Hizo mali anazosimamia shemeji yako zina jina la mkeo,lako au majina yenu wote wawili na kama jina la mkeo kwa sababu gani na wewe ulikuwepo?
 
Mkuu UMUGHAKA ni mke wangu wa ndoa kabisa,ndoa ya kanisani,na vyeti via ndoa ninavyo,tumejaaliwa watoto wawili,wote wapo shule na vyeti vyao vya kuzaliwa ninavyo,mke wangu tulimzika nyumbani kwangu,hapa hapa ninapoishi sasa.
Mkuu huyo Mkeo alikuwa kabila gani kwanza
 
hapo sijaelewa msimamizi wa mirathi anachaguliwa vipi wakati mme bado yuko hai,
hiyo ndoa ipo kisheria ama ilikuwa sogea tuishi?
Swala la Nani awe msimamizi wa Mirathi ni swala la makubaliano ndani ya familia hasa hasa wale ambo ni warithi halali wakubaliane na waampe baraka zao Kama msimamizi wa Mirathi ya Marehemu,hata Jirani anaweza kua msimamizi wenu mradi tu mkubaliane kwa pamoja!!!
 
Haina maana ya kwamba kikao Cha familia au ukoo kikishakaa na kumteua msimamizi wa mirathi ndo Basi kashakuwa, mahakama ndo inayomuidhinisha na kwa sababu walifunga ndoa ya kikristo special forum/court hapo ni mahakama ya wilaya ambapo kunaprocedure za kufuata ambazo mme au watoto lazima wahusishwe coz ndo warithi, mashauri ya mirathi hasa kwa wakristo Ni tofauti kidogo na waislam au waamini kimira ambao wao nimakahama ya mwanzo tu na Hakuna complication Sana primary court,... Huku mahakama ya wilaya lazima huyo anaejiita msimamizi wa mirathi afanye PETITION FOR LETTER OF ADMINISTRATION, lazima pawe na CONSENT OF THE HEIRS yaani warithi wawe wamemkubali huyo jamaa kuwa msimamizi, Kuna issue za general citation zitatoka , kuna form ya administration of bond without surety ambapo huyo msimamithi wa mirathi lazima aweke bond ya kiasi Cha pesa au Mali yake Kama dhamana ili asije akafuja au kutumia Mali za marehemu,..na kwa maana hio huyo msimamizi wamirathi Kama Hakuna taratibu hizo nilizozitaja hapo juu kufuatwq Basi huyo jamaa sidhani Kama anatambulika na mahakama kama msimamizi wa mirathi ,kikao tu Cha kumteua msimamizi wa mirathi hakitoshi...na hata Kama ikitokea kaaidhinishwa na mahakama na bado hafanyi wajibu wake bado anweza akawe revoked kwa sheria na anashitakiwa... Na as long as wewe una ndoa na mnawatoto kwenye issue ya mirathi ninyi ndo most favorable Sana kuliko hao ndugu wengine hasa kwenye Mali ambazo mlichuma wote
Asipotumia huu ushauri wako basi atakua hana shida. Angalizo pia hapa tumesikia ya upande mmoja usikute jamaa ni mfujaji wa mali pia ni mlevi ana wake wengine huko sijui michepuko ambayo itaathiri welfare ya watoto na mpaka muda huu watoto nani anaishi nao usikute baada ya wife kufariki jamaa alijitoa kwenye jukukumu la malezi wanaume tunakuwaga wrpesi sana kujiondoa kwenyr malezi hili linaweza kumuathiri. UMEMPA USHAUR BOMBA TENA WAKISHERIA.
 
Pole sana Mkuu na msiba.na maswahibu unayopitia kwa sasa.

Sijaweza kusoma comment zote ila kama kutakuwa na comment ambayo imesema nitakayokueleza basi naungana nayo.

Haya twende kazi,

Nitaeleza kazi za msimamizi wa mirathi kwa ufupi sana ili upime je anazifanya huyo msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo

Kazi kuu ya msimamizi wa mirathi ni kutambua na kukusanya mali za marehemu na kisha kuzigawa kwa warithi wake, ndani ya miezi 6. Sasa swali ni je huyo msimamizi wa mirathi amezitambua na kuzikusanya mali za marehemu mkeo?, baada ya kuzitambua na kuzikusanya amezigawa kwa warithi wa hizo mali?. Je, amefuata muda uliowekwa na sheria yaani miezi 6?. (Majibu unayo ila nitaeleza chakufanya ikiwa ni tofauti)

Sasa jambo gani ufanye ikiwa hajafuata muongozo wa sheria.

Hapa unatakiwa kwenda kufungua pingamizi dhidi ya msimamizi wa mirathi ukiitaka mahakama itengue/ifute uteuzi wake kwa kuwa hawezi kukusanya na kugawa mali z marehemu na pia amekuwa mharibifu/mpotevu wa mali za marehemu na zaidi ya yote amejinufaisha yeye binafsi.

Sasa kabla ya kufanya yote haya kuna jambo unatakiwa uwe na uhakika nalo kwa 100% ambalo ni Je, huyu shemeji yako aliteuliwa na Mahakama kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo?, au mliishia kwenye kikao cha familia/ndugu?.

Kama alipeleka maombi ya kuteuliwa Mahakamani basi sasa hapo unatakiwa kuomba mahakama itengue/ifute uteuzi wake. Kama hakuwahi kupeleka maombi ya kuteuliwa Mahakamani na mahakama.ikayakubali maombi yake basi huyo sio msimamizi wa mirathi kwakuwa ni Mahakama pekee yenye uwezo wa kuteua msimamizi wa mirathi na mahakama hiyo ni Mahakama ya Mwanzo au ahakama Kuu na sio ahakama nyingine zilizosalia.

Sasa kama hakuwahi kupeleka ombi Mahakamani, wewe sasa unatakiwa kupeleka maombi ya kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mkeo Mahakamani. Hapa utatakiwa kuwa na muhuktasari wa kikao cha familia kukupendekeza kama msimamizi wa mirathi ikiwa mkeo hakuacha wosia.

Ikiwa ni ngumu kuitisha hicho kikao wewe nenda mahakama ya mwanzo fungua hivyo hivyo ombi la kuteuliwa kisha ieleze ahakama kwanini.hakuna muhuktasari wa kikao na hapo utaeleza kuwa aliyependekezwa hajafungua mirathi na anapoteza mali za marehemu ambapo hata marehemu asingezipoteza hivyo. (Shawishi Mahakama ila chunga usiwe unalalamika).

Kuna swala la wosia, kama mkeo aliacha wosia basi fuateni wosia unasema nini na hapa ni lazima bado kufungua mirathi mahakamani ila uzuri hapa hamtakuwa na sababu ya kikao cha kumteua msimamizi wa mirathi sababu tayari katajwa na wosia.

Mimi ni haya tu kwa sasa naamini utapata mwanga wakutosha kujua ufanye nini, ukiwa na maswali usisitekuuliza. Naweza nikachelewa kujibu ila nitakujibu tu.

Karibu.
Sawa kabisa mkuu,naomba kwanza unieleweshe jambo moja zaidi,mtu aliyeteuliwa na familia kusimamia mirathi anapaswa kwenda kuthibitishwa na mahakama,nimeambiwa kwa ndoa ya kikristo ni mahakama ya wilaya tu,lakini pia mtu huyo atapaswa kwenda na vielelezo kadhaa,vikiwemo muhtasari wa kikao cha familia,hati ya kifo,barua ya kiongozi wa serikali wa eneo alilokuwa akiishi marehemu na kiapo,sasa hati ya kifo ninayo mimi,na hakuwahi kunitaka nimpatie kwa sababu yoyote,mwenyekiti wa mtaa tunaoishi pia ameniambia kuwa hakuna mtu aliyemwendea kutaka barua yoyote kuhusiana na mirathi ya mke wangu,huyu mwenyekiti ni mtu wa karibu na familia yangu sana,ila nyumba na viwanja vyenye utata vipo kwenye mitaa tofauti tofauti,sasa je kuna uwezekano wa huyo ndugu kupata hati nyingine ya kifo tofauti na ile niliyonayo?na je nikitaka kuonana na kiongozi wa mtaa nitapaswa kwenda kwa huyu wa hapa tunapoishi au kule ambapo ndipo penye hizo Mali? Hata hivyo ni takribani miezi kumi na moja imeshapita toka mke wangu alipofariki,na kwa maelezo yako ya kisheria ni wazi kuwa alipaswa awe ameshafunga jalada la mirathi,kitu ambacho hajafanya hadi muda huu,na sidhani kama alikwenda mahakamani.
 
Umefafanua vyema sana mkuu, Ningependa kujua je, wosia unaokubalika lazima uwe na vigezo vipi?
Kwenye wosia huwa kuna mitazamo tofauti tofauti sana ya upi ni wosia halali ila kwa ujumla wake ni kuwa, wosia uwe umeandikwa na marehemu, uwe una mashahidi kulingana na sheria inavyoelekeza, uwe uliandikwa wakati Marehemu akiwa kwenye hali nzuri kiakili, uwe umetunzwa sehemu isiyoweka mashaka juu ya uhalali wake.

Bado wosia huo utaje warithi na mali za marehemu, umtaje msimamizi, usibague mtoto yoyote wa marehemu ikitokea ukasema mtoto fulani asipewe urithi basi uweke na sababu ambazo za msingi ni kama mtoto hakumtunza mzazi wake huyo au kama alitaka kumuua/kumdhuru.

Sasa hayo yanaweza yakawepo au yasiwepo kwa ukamilifu wake na bado wosia ukawa halali, itategemea na mazingira.

Unaweza ukakuta maelekezo tu kwenye note book au diary ya marehemu yakageuka wosia. Uhalali wa wosia huwani vurugu mechi sana. Mfano mzuri wosia wa marehemu Regnald Mengi

Nadhani umepata picha Mkuu.
 
Nakazia swali maana hata mimi nimeshindwa kuelewa huyo mke umeishi nae muda gani na kama mmebahatika kupata watoto hao watoto wana umri gani?

Hizo mali anazosimamia shemeji yako zina jina la mkeo,lako au majina yenu wote wawili na kama jina la mkeo kwa sababu gani na wewe ulikuwepo?
Nimepata naye watoto wawili,mmoja ana miaka 9 na mwingine 5,nimeishi na mke wangu kwa miaka 9,ni hivyo mkuu
 
Asipotumia huu ushauri wako basi atakua hana shida. Angalizo pia hapa tumesikia ya upande mmoja usikute jamaa ni mfujaji wa mali pia ni mlevi ana wake wengine huko sijui michepuko ambayo itaathiri welfare ya watoto na mpaka muda huu watoto nani anaishi nao usikute baada ya wife kufariki jamaa alijitoa kwenye jukukumu la malezi wanaume tunakuwaga wrpesi sana kujiondoa kwenyr malezi hili linaweza kumuathiri. UMEMPA USHAUR BOMBA TENA WAKISHERIA.
Watoto ninaishi nao mimi,na kuhusu ufujaji na hayo mengine sina kabisa mkuu,ndiyo maana nimeweza kuwekeza vitega uchumi na kuilea familia yangu vyema kabisa mkuu,ushauri nimeuzingatia na nitaufanyia kazi haraka, asante
 
Kwenye wosia huwa kuna mitazamo tofauti tofauti sana ya upi ni wosia halali ila kwa ujumla wake ni kuwa, wosia uwe umeandikwa na marehemu, uwe una mashahidi kulingana na sheria inavyoelekeza, uwe uliandikwa wakati Marehemu akiwa kwenye hali nzuri kiakili, uwe umetunzwa sehemu isiyoweka mashaka juu ya uhalali wake.

Bado wosia huo utaje warithi na mali za marehemu, umtaje msimamizi, usibague mtoto yoyote wa marehemu ikitokea ukasema mtoto fulani asipewe urithi basi uweke na sababu ambazo za msingi ni kama mtoto hakumtunza mzazi wake huyo au kama alitaka kumuua/kumdhuru.

Sasa hayo yanaweza yakawepo au yasiwepo kwa ukamilifu wake na bado wosia ukawa halali, itategemea na mazingira.

Unaweza ukakuta maelekezo tu kwenye note book au diary ya marehemu yakageuka wosia. Uhalali wa wosia huwani vurugu mechi sana. Mfano mzuri wosia wa marehemu Regnald Mengi

Nadhani umepata picha Mkuu.
Asante sana brother umenipa elimu ya bure. God bless You
 
Sawa kabisa mkuu,naomba kwanza unieleweshe jambo moja zaidi,mtu aliyeteuliwa na familia kusimamia mirathi anapaswa kwenda kuthibitishwa na mahakama,nimeambiwa kwa ndoa ya kikristo ni mahakama ya wilaya tu,lakini pia mtu huyo atapaswa kwenda na vielelezo kadhaa,vikiwemo muhtasari wa kikao cha familia,hati ya kifo,barua ya kiongozi wa serikali wa eneo alilokuwa akiishi marehemu na kiapo,sasa hati ya kifo ninayo mimi,na hakuwahi kunitaka nimpatie kwa sababu yoyote,mwenyekiti wa mtaa tunaoishi pia ameniambia kuwa hakuna mtu aliyemwendea kutaka barua yoyote kuhusiana na mirathi ya mke wangu,huyu mwenyekiti ni mtu wa karibu na familia yangu sana,ila nyumba na viwanja vyenye utata vipo kwenye mitaa tofauti tofauti,sasa je kuna uwezekano wa huyo ndugu kupata hati nyingine ya kifo tofauti na ile niliyonayo?na je nikitaka kuonana na kiongozi wa mtaa nitapaswa kwenda kwa huyu wa hapa tunapoishi au kule ambapo ndipo penye hizo Mali? Hata hivyo ni takribani miezi kumi na moja imeshapita toka mke wangu alipofariki,na kwa maelezo yako ya kisheria ni wazi kuwa alipaswa awe ameshafunga jalada la mirathi,kitu ambacho hajafanya hadi muda huu,na sidhani kama alikwenda mahakamani.
Hapa nitakujibu kwa vipengele Mkuu.

1. Mahakama yakufunglia.shauri la mirathi ni aidha Mahakama ya mwanzo au Mahakama Kuu, na hapa nakushauri ukafungue Mahakama ya Mwanzo, utaratibu sio mgumu.

2. Swala la vielelezo hapa inabidi kwabza uwe na uhakika 100% kama je, alifungua shauri la mirathi Mahakamani na kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi?.

3. Ili kufungua shauri la mirathi vielelzo vinavyotakiwa ni Cheti cha kifo, muhkasari wa kikao kumteua msimamizi, wosia kama upo, na nyaraka nyingine kadiri Mahakama itavyohitaji ikiwa ni pamoja na cheti cha ndoa, barua ya serikali ya mtaa

4. Kuhusu wapi utafungua shauri la mirathi ikiwa mali zipo sehemu tofauti tofauti, ni Mahakama iliyopo eneo alipofia marehemu.

Kama kuna ambacho sijagusa utanijulisha.
 
Hapa nitakujibu kwa vipengele Mkuu.

1. Mahakama yakufunglia.shauri la mirathi ni aidha Mahakama ya mwanzo au Mahakama Kuu, na hapa nakushauri ukafungue Mahakama ya Mwanzo, utaratibu sio mgumu.

2. Swala la vielelezo hapa inabidi kwabza uwe na uhakika 100% kama je, alifungua shauri la mirathi Mahakamani na kuteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi?.

3. Ili kufungua shauri la mirathi vielelzo vinavyotakiwa ni Cheti cha kifo, muhkasari wa kikao kumteua msimamizi, wosia kama upo, na nyaraka nyingine kadiri Mahakama itavyohitaji ikiwa ni pamoja na cheti cha ndoa, barua ya serikali ya mtaa

4. Kuhusu wapi utafungua shauri la mirathi ikiwa mali zipo sehemu tofauti tofauti, ni Mahakama iliyopo eneo alipofia marehemu.

Kama kuna ambacho sijagusa utanijulisha.
Asante,ila hujagusia kuhusu uwezekano wa yeye kupata hati nyingine ya kifo tofauti na hii niliyonayo,au kama anaweza kuthibitishwa na mahakama pasipo kupeleka hati hiyo,na pia nimeambiwa kuwa kwa ndoa za kiislamu na kimila mirathi inafunguliwa mahakama ya mwanzo,na kwa ndoa ya kikristo na ambapo thamani ya mirathi haizidi tsh 100,000,000 basi ni mahakama ya wilaya,au mahakama kuu ikiwa thamani ya Mali itazidi kiwango hicho,niweke sawa kwa hili pia mkuu,nashukuru mno brother.
 
Hujanielewa mkuu,nimesema siku hiyo ya mazishi ambayo ndiyo kikao kilikaa sikuwa sawa kiakili,hivyo sikuzingatia kuhusu habari ya mirathi
Pole sana. Na hii ndio shida mara nyingi hivi vikao vinafanyika siku ya mazishi jioni so unakuta bado umevurugwa na hapa wajanja ndio wanajipenyeza na kama wao ndio walikuwa wengi na wana tamaa ya mali lazima wakuzidi akili wakijua kufuatacho ITV.
 
Nafikiri huyo shemeji yako, hana nguvu yoyote kisheria kuzimiliki hizo mali maana mwenye mali alikuwa na familia, sasa atakaesimama kwenye mali hizo ni mumewe,ilikuaje mpaka shemeji aje kusimamia mirathi upande wa dada yake.?
 
Kuna harufu ya Jinai hapa Kama kweli atakua na form no IV ya usimamizi wa Mirathi! Forgery inanukia, endelea kuchimba huko Mahakamani ujuwe ukweli wote! Anafunguwaje Mirathi ya Marehemu bila ya Vielelezo muhimu vya Marehemu Kama vile hati ya kifo!!??
 
Back
Top Bottom