Je, Mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?

Je, Mungu kaumba baadhi ya wanadamu kwa upendeleo wa akili na maarifa?

Na Haya ni moja ya matokeo ya mfumo wetu wa elimu au mtaala.......

Mifumo yetu ya elimu imedizainiwa uwe msaidizi wa mzungu au uwe mtengenezaji wa alichokigundua mzungu.......

Na kibaya zaidi inakufanya Ina kufanya ujione mzungu na kujikataa.........

Naamini mtoa mada ameleta hii mada kwa mihemko na sio ki uchunguzi kama msomi

Lakini ndio hivyo kama hata cha kumfundisha mtoto tunapangiwa na wazungu unategemea huyo mtoto atakuwa na akili gani.....!!?

NB;

Kuna shida kwenye mitaala ya elimu na mataifa mengine yameligundua hayo mapema sana na kufanya mabadiliko na kupiga hatua kubwa......
Unamaanisha tuzirud elimu zetu za asili na tuache elimu ya kimagharibi et??
I try to imagine hyo elimu itakuwaje[emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
Hii elimu tuliyonayo ni ya kishenzi sana.Ni elimu ya kutambia tu mtaani na si elimu ya kuleta mabadiliko.Na hata serikali inavyolipa watu wake,hailipi utendaji bali inalipa cheti,kwa hiyo hata vyuoni zinafanyika faulo za hatari ili mtu apate cheti na kinakuwa kama kibali cha kulipwa zaidi.
Niliona tofauti kidogo kwa wazungu,wao wanalipa uwezo wa kazi.Hata kama mtu ni darasa la saba kama anauwezo wa kuzalisha,wanalipa pesa nzuri sana.Nimeshuhudia mtu mmoja aliajiriwa kama meneja Australia mgodini akiwa darasa la saba tu tena la Tanzania. Alibahatika kufanya mgodini na akonesha uwezo mkubwa sana kiasi kwamba wazungu ilibidi wamkubali.
Kama serikali zetu zingekuwa zinamiliki timu,ungeshangaa wachezaji wangekuwa wanalipwa mishahara kwa vigezo vya elimu hata kama hawashindi ama hawafungi magoli.Hii ndiyo inaua sana uwezo wetu na kuturudisha nyuma.
Wako watu wanaonesha vipaji vikubwa kama kutengeneza silaha,dawa n.k wanakamatwa au kufungiwa kabisa.Huu ni ushenzi mkubwa.
Kuna kaukweli humu
 
Kuna mambo mengi sana yamejificha nyuma ya pazia mpaka tupo hivi tulivyo...

Chochote utakachogundua au kuvumbua kama mwaAfrica, nchi zilizoendelea zishajiwekea utaratibu (System) kwamba ili viwe vya kimataifa vipitie katika mfumo ambao wameuunda wao... Kama kimetoka Africa hakiwezi pitishwa hata siku moja...

Mfano vumbua kitu kizuri kama mwaAfirica nchi zilizoendelea hawatokipitisha... Ila badilisha uraia mathalani kua mmarekani na kitu hicho hicho, kitapitishwa kua cha kimataifa...

Akili tunazo, uthubutu tunao na uwezo tunao, ila system ndiyo tatizo...


Cc: mahondaw
 
Unamaanisha tuzirud elimu zetu za asili na tuache elimu ya kimagharibi et??
I try to imagine hyo elimu itakuwaje[emoji13] [emoji13] [emoji13]

Wachina na wahindi wanachukua maarifa na kuyanufaisha mataifa yao

Sisi tunachukua umagharibi kama ulivyo na kuukana utaifa wetu

Wachina kwa kuchukua tu maarifa wameweza kubadilisha mfumo mzima wa elimu kuwa kwenye lugha Yao kwa maslahi yao.....

Ndio maana ni rahisi kumkuta mchina mwenye maarifa mengi lakini hajui kingereza.....

Watanzania bila ya kujinasibisha na mzungu bado haoni kama usomi wake umekamilika.....
 
Bro unanitia uchungu nasoma hadi mwili unatetemeka aisee.
Mtu mwenye uwezo wa kuwaza haya lazima umesoma.

Jibu la hayo yooote ni kwamba sisi sote Mungu alituumba sawa ila bahati mbaya sisi weusi tuna ROHO MBAYA SANA.

ubinafsi, chuki, lawama, maseng'enyo laana nk.

Nahisi kutoa machozi [emoji36] let me quit bro.
Daah.... N kweli ....yaan n Africa ambako tunauana cc kwa cc...ukiandalia Global peace index(GPI)utaona idadi kubwa ya nvhi zisizo na aman n za Africa,kitu cha ajab n kwamba tunauana cc kwa cc na kwa maliasili zetymu wenyewe...hii roho mbaya cjui tumetoa wapi
 
Mbona north Korea wako strict kulko hapa ila wanateknolojia kubwa,nuclear ,rockets,na sayansi mbalimbali mkuu....sisi labda kuna kasoro nyngne
Huwezi kufananisha akili kubwa za North Korea na hawa mazuzu yenu.

Things are strict there, yeah, i know..... Lakini atleast vitu wanavyovifanya vina some sort of sense..... Sio hawa zero brain wenu wanaokimbizana na wavaa milegezo!

Unakimbizana na milegezo wakati mezani kwako kumejaa maji machafu ya visima.
 
Turudi nyuma wenzetu hata kabla ya Yesu hajazaliwa walishakuwa na shule na vyuo. Miaka 2000+ baadae ndo wakaja kutuzindua kwakututawala kwanza na kuweka shule chache. Waafrika tumeweza kusoma na kuandika hata miaka mia haijapita bado, tumeanza kujiongoza hata miaka mia haijapita, hata sera, sheria na mfumo unaotumiwa kuongoza bado ni wa wakoloni wetu, na ni bado sana kujilinganisha na wazungu wametuacha mbali sana kwa maelfu ya miaka. Viongozi wetu bado hawajui kabisa namna ya kuongoza wamejikita zaidi ktk kutawala kwa mabavu maanake wamekopi sera ya utawala wa mkoloni bado. Leo ukimwuliza rais wako kwanini hatuendelei? Atakujibu hajui kwanini.
Duuuh..kaz ipo kweli
 
Mungu alimuitaga mzungu na mwafrica ili awape akili.akawaambia wawai saa kumi na mbili asubuhi.mzungu kaja mda wa saa kumi na mbili asubuhi,mwafrica kaja saa nne asubuhi.nafkiri jibu umelipata
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Yaonyesha umeandika kwa hisia kali sana ndugu.

Ni kweli kuna tofauti kubwa kati ya Wazungu/Wanateknolojia na Weusi/Wana silia, ila pia ukumbuke kujiuliza hivi ni vyote wafanyavyo Wazungu/Wanateknolojia Dunia inavihitaji? tofautisha mahitaji ya Wazungu/teknoloji na mahitaji ya Dunia/ardhi/uhai.

Sehemu kubwa ya gunduzi zao ndio zime/zinazalisha sumu yote inayoiangamiza Dunia leo, bila hizo teknolojia tusingekuwa na haya mabadiliko tabia nchi, miti inakatwa ili ikazalishe fanicha viwandani, bahari inachafuliwa na viumbe wanaangamia huko.n.k.

Bila hizo gunduzi tunazoita maendeleo, nadhani binadamu angeishi maishi ya asili tu ambayo ndio haswa ilikuwa kusudi la Muumba wa Ulimwengu na mahitaji ya dunia hai.

Kama unakubaliana nami kuwa Dunia kwa sasa ipo taabani, mito inakauka, joto linaongezeka, magonjwa yasiyotiba kuongezeka n.k basi ukubaliane nami pia kuwa Dunia ingekuwa salama sana bila uwepo wa Mzungu/Mwanateknolojia.

Unapofurahia uwepo wa Gari, Ndege, Meli, fridge, AC n.k pia ujue haya maangamizo ya uhai wa dunia yanatoka huko.

Sasa hapo sio kazi yangu tena kujiuliza ni kwa nini Mungu alimleta Mzungu/Mwanateknolojia, ila kuna kila dalili kuwa Mzungu/Mwanateknolojia alikuja baadae, na dunia ilikua salama kwa muda wote kabla ya uwepo wa Wanateknolojia hao.

Kuhusu tiba, ugunduzi wa madawa n.k, nadhani kuna mengi sana hatuyajui kuhusu Dunia tangu zama na zama, hivyo bado ni ngumu kujiridhisha kama tuliishi tu bila namna yoyote ya kujitibia kabla ujio wa Wanateknojia, basi ndio kusema bila teknolojia hii race ingeangamia? nitakuwa wa mwisho kuamini hivyo, sehemu kubwa ya magonjwa yanayohitaji hizo tiba za hali ya juu nayo huzalishwa na uwepo wa hizo hizo teknolojia, mfano saratani mbalimbali n.k. Mimi naamini tiba zote huweza kupatikana kwenye mimea tukitumia zetu vizuri.

Tukiongelea ujenzi n.k, kuna ujenzi wa enzi hizo ulifanyika bila teknolojia iliyopo leo, mfano ni zile Piramidi za Misri, kwa hiyo sioni kama Binaadamu tulihitaji sana teknolojia ya sasa ndio tufanye shughuli zetu.

Hizo almasi na dhahabu unazozitaja hazina uhusiano wowote na uwepo/uhai wa dunia, ni Wazungu/Wanateknolojia hao hao ndio wanaozihitaji na kutufanya tuchimbue ardhi yetu kama wehu, hata tukiziacha huko ardhini hakuna tunachopoteza.

Kuhitimisha maelezo yangu ni kuwa, Mzungu/teknolojia ni artificial na Mweusi ni asilia, hivyo kaa chini ujiulize Dunia inahitaji asili au artificial?
Hapa mkuu Nina walakini na mawazo yako...

Ukiangalia suala LA uchafuz wa mazingira hata cc licha ya kuwa hatuna viwanda tunachangia kwa kiasi kikubwa..mfano vtu kama kilimo kinachangia sana uharibifu wa mazngira na mwisho tumebaki na majangwa tu.

Kihusu matibabu sikatai yanatoka kwenye mimea ila shida inakuja kwenye kujua n mmea UPI na kiwango kipi kinamfaa magonjwa hapo panahitaji ugunduz ambao cc weusi hatijafikia...hebu angalia magonjwa kama malaria,kichaa cha mbwa,surua n.k je kwa kutumia mitishamba ambayo huna uhakika NAyo kuna kupona kweli mkuu??

Unavosema uhitaj wa mineral extraction hatuna hapo huoni ndio kuonyesha how mbumbumbu we are?? We stay on natural wealth without utilizing them!! Is that not foolishness of highest rank ndugu yangu??

Try to imagine ur current life how it would have been if u font have cell phone,no transport yaan ukitaka kuna dar kutoka kigoma inakubid utembee HV is that normal life??

Bado hujanishawishi ndugu....
 
Mkuu umeibua hoja nzuri sana. Nataka nikufahamishe tu kuwa kama tukitazama kwa hoja yako hiyo ya Upendeleo basi Mungu alitupendelea maarifa sisi waafrika ila tu hatuna juhudi hasa kizazo hiki cha sasahivi.
Mwandishi Walter Roodney aliwahi kuandika kitabu cha HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA. Katika kitabu hiko ameelezea namna gani Afrika ilikua na maendeleo zaidi ya wazungu.
Ukisema kwamba waafrika hatuna maarifa ya kugundua kitu unakua unakosea sana. Kwanza tambua kwamba uhusiano wa Mzungu na mwafrika ulianza mnamo karne ya 15. Hapo tunazungumzia miaka ya 1400.
Wazungu walipokuja Afrika kwa mara ya kwanza, walikuta tayari tumeendelea kuzidi wao wenyewe kiasi kwamba wakaiga sehemu kubwa ya teknolojia yetu na kwenda kuziendeleza kwao. Najua utabisha katika hili, lakini nitakudhibitishia kwa nadharia za kihistoria na kisayansi kupitia nyanja zifuatazo.

ELIMU
(Hesabu na maandishi)
Hesabu nyingi unazoziona hivi leo zilianzia MISRI (Egypt). Njia hii tunayotumia leo kuhesabu ilianza zaidi ya miaka 35000 iliyopita kutoka Africa. Wamisri walianza kuandika vitabu kuhusu hesabu za kugawanya kuzidisha, hesabu za sehemu na Geometry.
Mfumo wa kuandika herufi tunazozitumia leo, ulianza Misri pia mnamo miaka ya 3100 KB (Kabla ya kristo).
Kalenda inayoipa dunia siku 365 na robo , ilitengenezwa na wamisri. Kugwanywa kwa masaa 24 kwa siku kulianza misri zamani sana na enzi hizo walitumia misimu hasa ya maji kutambua masaa.

DAWA

Katika hoja yako umesema kwamba wazungu wamegundua dawa. Sio kweli!! kuna tofauti kati ya kugundua na kuendeleza. (invent and develop)
Dawa zinazotumiwa leo ziligunduliwa Africa zamani sana huko Misri, Nigeria na Afrika kusini enzi hizo kabla nchi hizo hazijapewa hayo majina. Walitumia mizizi na mimea kutibu magonjwa mbalimbali. kwamfano Salicylic acid kwaajili ya kupunguza maumivu ambayo leo hii wazungu wameindeleza tunaitambua kama Aspirin. Kaolin Acid kwaajili ya ugonjwa wa kuhara ambayo leo hii dawa inaitwa Kaopectate. Utafiti umeendelea kueleza kua, waafrika walikua na uwezo wa kufanya upasuaji (under antiseptic conditions) wakati huo ujuzi huo ndo ulikua unaanza kuibuka barani ulaya.

ENGINEERING
Moja ya kidhibiti hai cha utafiti kwamba Africa ilikua na maengineer na maachitecture wake hata kabla ya wazungu ni Pyramid of Giza (Cairo) ambayo ipo kwenye maajabu saba ya dunia. Utafiti unaonyesha Pyramid hyo ilijegwa mnamo Miaka ya 2580 KB (Kabla ya kristo) kipindi ambacho hta mzungu hakuwa na jengo lolote la ajabu kama hilo. Kinachofanya pyramid hii iwe ya ajabu ni ufundi uliotumika.
Waliosimamisha pyramid ile walibeba tani milioni sita na nusu za mawe ambapo kila jiwe lilikuwa na tani zisizopungua 9. Kwa kipindi hiko ambapo hakukua na mawinch wala minyororo wala cement waliwezaje kupandisha haya mawe? Ni wazi kabisa mwafrika alikua na teknolojia ya kipekee kabla ya mzungu.

Nina mifano mingi natamani kukushirikisha ila kwa leo naishia hapo. Waafrika tuna akili na kama ni upendeleo basi Mungu alitupendelea sisi. Ila tu waafrika sisi ni wavivu kujituma na kufikiri. Mzungu hana akili kama tunavyodhani, ila tu kapewa juhudi na kiu ya kujifunza. Sisi tumelala sana na kwa mantiki hiyo Mzungu anaokana ana akili kuliko sisi.
ASANTENI!!
 
Hapa mkuu Nina walakini na mawazo yako...

Ukiangalia suala LA uchafuz wa mazingira hata cc licha ya kuwa hatuna viwanda tunachangia kwa kiasi kikubwa..mfano vtu kama kilimo kinachangia sana uharibifu wa mazingira na mwisho tumebaki na majangwa tu.

Kihusu matibabu sikatai yanatoka kwenye mimea ila shida inakuja kwenye kujua n mmea UPI na kiwango kipi kinamfaa magonjwa hapo panahitaji ugunduz ambao cc weusi hatijafikia...hebu angalia magonjwa kama malaria,kichaa cha mbwa,surua n.k je kwa kutumia mitishamba ambayo huna uhakika nayo kuna kupona kweli mkuu??

Unavosema uhitaj wa mineral extraction hatuna hapo huoni ndio kuonyesha how mbumbumbu we are?? We stay on natural wealth without utilizing them!! Is that not foolishness of highest rank ndugu yangu??

Try to imagine ur current life how it would have been if u font have cell phone,no transport yaan ukitaka kuna dar kutoka kigoma inakubid utembee HV is that normal life??

Bado hujanishawishi ndugu....
Nadhani una miss pointi ndugu.

Nimeeleza vizuri hapo juu kwa kuhoji "je tunahitaji kila kinachotokana na teknolojia?"

Sidhani kama athari za kilimo zina ukubwa sawa na uharibifu unaosaabishwa na viwanda na uvunaji holela wa miti, ni asilimia ngapi ya mashamba yapo kando ya mito, na je kama hali ya kunyesha mvua ingebaki ileile tangu awali ni wanagapi wangeenda kulima kando ya mito? je ni kweli jamii zetu hazikuwa na mila/makatazo ya uharibifu wa mazingira?
nakumbuka hotuba moja ya Mwalimu alisema kwao Wazee wao waliaminishwa kuwa kukata miti ni kukaribisha mikosi/mashetani...sasa je huoni jamii zetu zilikuwa na njia za kutunza mazingira ila ni taarifa sahihi tu hazipatikani kuhakiki ni kwa jinsi gani kila jamii ilikuwa na mbinu zake...sasa kwa nini nisiamini kuwa pia enzi hizo jamii ziliweka marufuku kulima kando ya mto?

Kuhusu tiba sidhani kama kuna haja ya kuzusha mabishano, hebu jiulize ni jamii ngapi unazifahamu ambazo mpaka sasa wanaamini kwenye tiba ya baadhi ya mimea? na mimea sio lazima ilenge mimea ya porini...hata mboga na matunda tunayotumia kila siku...hivi kama kuna virutubisho unahitaji kutoka kwenye Parachichi unahitaji kipimo gani mahsusi ili ufikie uhitaji? wewe kula parachichi tu basi halitokudhuru, hiyo malaria unayoitaja nayo kumbuka imekuzwa sana na uwepo mabadiliko ya tabia nchi, yaliyosababishwa na teknolojia..sehemu kama Lushoto haikuwa na Malaria awali, sasa wao wangehitaji dawa ya nini?

Hizo simu za mikononi, Ndege za kukupeleka Kigoma unaposema, kwa nini unanilazimisha nidhani kwamba nisingeishi salama bila uwepo wake? kwani ni lazima niende Kigoma? ndio maana nimehoji tulihitaji kula kilicholetwa na teknolojia?
 
Turudi nyuma wenzetu hata kabla ya Yesu hajazaliwa walishakuwa na shule na vyuo. Miaka 2000+ baadae ndo wakaja kutuzindua kwakututawala kwanza na kuweka shule chache. Waafrika tumeweza kusoma na kuandika hata miaka mia haijapita bado, tumeanza kujiongoza hata miaka mia haijapita, hata sera, sheria na mfumo unaotumiwa kuongoza bado ni wa wakoloni wetu, na ni bado sana kujilinganisha na wazungu wametuacha mbali sana kwa maelfu ya miaka. Viongozi wetu bado hawajui kabisa namna ya kuongoza wamejikita zaidi ktk kutawala kwa mabavu maanake wamekopi sera ya utawala wa mkoloni bado. Leo ukimwuliza rais wako kwanini hatuendelei? Atakujibu hajui kwanini.
HAPA NAONA BORA TUKACHUNGUZE HISTORIA KABLA YA GERMAN EAST AFRICA, YAANI KABLA YA "TANGA-NYIKA" ILIYO UNDWA NA MJERUMANI.
TANGA = BAHARI .. SAIL
NYIKA = MBUGA .. WILDERNESS

TULIKUA NA WATU WENYE ELIMU ZA HALI YA JUU.
WATU WENYE UJASIRI WAKUMONDOA MJERUMANI VITA VYA MAJI MAJI..
KABLA YA HAPO TULIKUA AKINA NANI SISI?!?! [emoji362] [emoji353] HISTORY WHERE FROM TO DATE. TUTAPATA MAJIBU YA KWANINI TUMEBAKI KUZUBA
 
Back
Top Bottom