Ambivert88
JF-Expert Member
- Aug 16, 2022
- 3,609
- 6,388
Wewe hujui unachokijua na YouTube imekuharibu ubongo wako watu km nyinyi ndio kila kitu mnaiuliza Google eti "Google kwanini mimi mpaka sasa sina demu?"ukufuatilia youtube utagundua wanamazingaombwe wote ni ujanja tu wanatumia hakuna muujiza wowote, wana akili ya haraka sana katika kubadili mambo na vitu vingi vitakavyotumika vinakuwa vimeandaliwa tayari, ingawa ni kipaji lkn lengo lake yeye ni kutengeneza hela kwako baada ya kufanya wewe umwamini. kama kutengeneza hela ingekuwa rahisi hivyo niambie alikuwa na utajiri wa kiasi gani?.
Unaiuliza Google?
Mimi nmeshuhudia mwenyewe sio kwa kuiuliza YouTube wala Google haya km ni hivyo alikua anatoa hadi matunda ndizi ndizi machungwa kwenye Gazette alikua analifungafunga km anaweka kitu kisha mnapuliza kila mmoja anaona ndani hamna kitu analifunga kisha analinyanyua juu km vile Yesu anaitisha mikate akishusha chini kufungua machungwa haya hapa tunayamenya tunayala na hapo utasema ameenda kuyaficha wakati anafanya tunamuona?
Acha uzwazwa ile ni elimu km elimu zingine it's Magic (Uchawi) ila sio Ushirikina (Witch craft)
Ushaelewa hapo sasa?
Mimi nmeshuhudi nyumbani kwetu tena kuna kipindi ilikua hatuna majani ya kuungia chai Jamaa alikua anafanya tu yake mambo yake yaani dakika sifuri anatupea majani ya kuuingia chai na tunaunga tunapika na tunakunywa chai
Alikua Magician wa aina yake yaani sometimes tupipi pipi anafanya tu km anakupanguda pua kamasi hivi akitoa anakugawia mapipi kibao mkononi mwake yalipotoka hujui
That's magic kiswahili mnaaita Uchaaaawi