Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Naona kama kikundi cha watu flani wanachati
Mmoja anauliza,mmoja anajibu..anyway
I hope this isn’t a scam !

Guy’s be careful with your money!
Only Place i can trust is a bank only.
Hakuna faida rahisi rahisi duniani hapa
Jamii forum ni mahali unapoweza kupata taarifa, maoni, ushauri nk. Hili jukwaa ndio mahali unaweza kupata taarifa za kibiashara, uchumi nk. Ni kweli ni watu wachache wenye interest tunachat na imetusaidia kupata taarifa. Binafsi nimepata information nyingi za UTT kupitia jamii forum. Mimi binafsi sioni Kama kunashida watu wachache wakichati.
 
Naona kama kikundi cha watu flani wanachati
Mmoja anauliza,mmoja anajibu..anyway
I hope this isn’t a scam !

Guy’s be careful with your money!
Only Place i can trust is a bank only.
Hakuna faida rahisi rahisi duniani hapa
Kiongozi upo Dunia hii kweli?
 
Hawa ndio wale ambao jirani yake anaepambana akitoboa maisha basi huamini kuwa ni utajiri wa nguvu za giza, hawaamini ktk kujituma coz ameshindwa hata kuingia kwenye mitandao na platform nyinginezo kufuatilia hki kitu ambacho anakiita scam.
Ndio hivyo, tuna uvivu Fulani watanzania na hili ndio maana wanapigwa sana.Maana UTT wana matangazo mpaka kwenye radio haswa kwenye ligi kuu ya NBC
 
Hivi ukinunua vipande kwa simu inachukua muda gani kusoma kwenye akaunti . ? Na pia ipi bora kununua kwa Mitandao ya simu au bank ?
 
Hivi ukinunua vipande kwa simu inachukua muda gani kusoma kwenye akaunti . ? Na pia ipi bora kununua kwa Mitandao ya simu au bank ?
Baada ya masaa 24 y cku za kazi. Kote kote bora n salama
 
Hivi bila kujaza fomu unaweza kununua vipande na kusoma kwenye account
 
Huu uzi nimeupitia page ya kwanza hadi ya mwisho.
Niseme kwamba JF kwa TZ ndo sehemu sahihi ya kupata taarifa sahihi kwa Kiswahili. Nilianza kusoma km mgeni enzi ikiwa jambo forum hasa jukwaa la vichekesho, badae nikahamia jukwaa la siasa na habari mchanganyiko.
Umri ulivyozidi na kughafilishwa na siasa nikahamia jukwaa na IT badae jukwaa la magari.

Kila Jukwaa nimejifunza na kunipatia vitu sahihihi.

Sasa hivi nimehamia jukwaa hili rasmi. Nawashukru sana wadau.

Baada ya kusoma page zote nimeshawishika na mimi kuingia UTT, nina matumizi mabaya sana ya hela na sijui kuweka akiba.

Umri unakimbia na majukumu yanazidi je inawezaekana nikiwa naweza kila mwezi 1M na sina mpango wa kutoa? Baada ya miaka 2 nitakua na shilingi ngapi hasa kwa account ya Liquid?

Asanteni sana
 
Back
Top Bottom