Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Je, ni mfuko gani wa UTT AMIS uko vizuri zaidi?

Kwa maelezo ya wahusika hapa, huu mfuko wa UTT sio uwekezaji wa kuvuna haraka haraka na kwa wingi, bali uwekezaji salama usio na stress, hivyo faida huwa kidogo kidogo na pole pole.
Kwa mfano, hiyo 10ml ikiweza kuiwekeza kwenye Liquid fund, utakuwa na uhakika wa kuvuna wastani wa shilingi laki moja kila mwezi, huku pesa yako ikiwa iko salama.

Binafsi nimeanza kuuelewa fresh huu mfuko, muda sio mrefu nitajiunga, unanifaa.
Thamani ya hisa inaongezeka pia
 
Kwa maelezo ya wahusika hapa, huu mfuko wa UTT sio uwekezaji wa kuvuna haraka haraka na kwa wingi, bali uwekezaji salama usio na stress, hivyo faida huwa kidogo kidogo na pole pole.
Kwa mfano, hiyo 10ml ikiweza kuiwekeza kwenye Liquid fund, utakuwa na uhakika wa kuvuna wastani wa shilingi laki moja kila mwezi, huku pesa yako ikiwa iko salama.

Binafsi nimeanza kuuelewa fresh huu mfuko, muda sio mrefu nitajiunga, unanifaa.
Nikiweka kwenye umoja ama bond nitavuna laki laki hiyo hiyo? Na maana kwamba kati ya mifuko yao upi unaasilimia kubwa zaidi?
 
Umoja fund
Screenshot_2022_0523_174054.png
 
Nawashuku sana wakuu mbarikiwe sana nyote mliojitoa kuchangia kwenye huu uzi ni madini madini tupu, mfuko huu ni mzuri kwa vijana Kwa mfano ukifanya uwekezaji sasa miaka 10 ijayo na kuendelea unajikuta umri umeenda na unaukwasi wako km walivyosema wahenga fainali uzeeni. Muda ni sasa tuwekeze huko uzuri mfuko wenyewe huko chini ya serikali ni sehemu sahihi.
 
Yan nmesoma mwanzo mwisho txt kalbia 250+...
Sas n muda wangu [emoji1320]

Mwanzo niliona kwa Mh Kigwangala alizungumzka hii issue ya UTT kupitia Twitter na nikaifatilia na baadae mpaka nikaenda CRDB...ingawa bado sikuelewa km nilivyo elewa leo hii

Yan uzi umechambliwa vzr sanaa ukiwa Na experience ndan yakeee

Yan kila kitu kimechambuliwa kutoka kweny nn maana aya UTT.

Jinc ya kununua vipande na mpapa sas namna ya
Faida na ongezeko la faida kwa sku aiseee [emoji120][emoji120]


Na kaka ulie kama kiongoz ubalikiwe sanaaaa
 
Je unaweza kuweka kila mwezi au ukiweka mara moja basi
Unaweka hela muda wowote siku yoyote kiasi chochote kuanzia sh. 10,000. Tumia simu airtel money, tigo pesa, mpesa au nenda tawi lolote la crdb. Crdb ni mawakala wa utt. Sio lazima uende ofisi za utt. Maliza kila kitu kidigitali. Tumechelewa mno. Wahindi wabazijua saba hizi mavitu ya mutual fund, forex etc.
 
Mkuu, Mimi naomba nisaidie kujua namna ya kujiunga hasa nikiwa mbali na ofisi zao.
Nenda tawi lolote crdb karibu yako. Jaza form. Pia tumia simu LIPA BILL. chagua UTT. endelea na steps zinazifuata. Tunechelewa mno....wahindi wanazijua hizi issue za Forex, mutual fund long time!! Umejua sasa wajulishe na ndugu, jamaa na marafiki!!!
 
Wakuu pmwasyoke na Vladimir Lenin hili swali halijapata majibu.

Binafsi niliwahi kumsikia mkuu wa mkoa wa Dodoma akizungumzia hii issue na Mungu jalia nimepata vi million 100 sina uzoefu wa biashara kwa hiyo nilitaka nilitaka niviweke huko kama nikipata hata 12M kwa mwaka nitakuwa nahesabu 1M kwa mwezi ambayo ni matumizi tosha kwangu na familia yangu.

Naomba msaada wa reliability ya uwekezaji huu. Asante

Aquila non capit muscas
Weka Bond Fund. UTAKULA HELA ACHA KABISA. SAFETY/SECURITY 100%
 
Mimi nimewekeza Umoja, nikifikisha kiasi fulani cha pesa nitawekeza kwenye Bond.Nakumbuka kuna mdau alisema unaweza kubadilisha mfuko.
Kubadilisha inaruhusiwa lakini huwezi toka umoja kwenda bond fund. Kwa nini? Kwa sababu UTT hela zilizochangwa kwenye mifuko hiyo wanaiwekeza katika sehemu tofauti.
Unaweza kuhama toka liquid kwenda bond. Au bond kwenda liquid.
Watoto(umri ukizingatiwa) kwenda umoja.
 
Naona kama kikundi cha watu flani wanachati
Mmoja anauliza,mmoja anajibu..anyway
I hope this isn’t a scam !

Guy’s be careful with your money!
Only Place i can trust is a bank only.
Hakuna faida rahisi rahisi duniani hapa
UTT AMIS ni taasisi ya Serikali ya Jamuhuri ya Tanzania chini ya wizara ya Fedha. Ofisi zao zipo. Mawakala wao wapo(CRDB). Pia wakati wa maonesho ya sabasaba ukipata muda tembelea banda lacwizara ya fedha humo ndani utakutana na taasisi zote za hiyo wizara ikiwemo UTT. Ni kweli ni vizuri kuwa muangalifu.
 
Kubadilisha inaruhusiwa lakini huwezi toka umoja kwenda bond fund. Kwa nini? Kwa sababu UTT hela zilizochangwa kwenye mifuko hiyo wanaiwekeza katika sehemu tofauti.
Unaweza kuhama toka liquid kwenda bond. Au bond kwenda liquid.
Watoto(umri ukizingatiwa) kwenda umoja.
Kiuhalisia unaweza kuswitch kutoka mfuko wowote kwenda mwingine. Kinachofanyika ni utt kununua vipande vyako vote vya mfuko unaouacha, ila fedha hizo badala ya kukupatia wanakununulia mfuko unaotaka kuhamia. Haya yanafanywa automatic na utt mara baada ya mteja kutaka switching.
 
Back
Top Bottom