Je, ni wakati wa vijana kufikiria kutafuta kazi nje ya nchi?

Jaribu DRC, RWANDA au SA. Tatizo ni kwamba sirikari wanajua lakini hawatangazi kazi hizo.

Mwambie anaetaka hiyo michongo sio mimi. Sio kazi ya serikali kukutafutia kila kitu mambo mengine ni kujiongeza wenyewe tu, nawajua watu zaidi ya 10 from TZ na KE waliofundisha lugha vyuo mbalimbali duniani, serikali has nothing to do with it, ni juhudi zako tu.
 
Aliyekwambia karne hii ya automation kuna ajira popote pale ni nani ? Utakwenda huko na kufanya kazi ambazo ni unwanted kwa wazawa na mwisho wa siku usishangae ukachukiwa kwamba unachukua kazi zao...

Ila umeongelea Tech na dunia ya sasa ambayo ni kijiji unaweza ukafanya lolote popote ulipo (ila its not that easy; having good idea alone ni one thing idea yako kwenda mainstream you need a lot to click at the same time)

Sio wakati wa vijana kufikiria kwenda kutafuta kazi pengine bali ni wakati wa hawa watumishi wetu (watawala) kufikiria ni jinsi gani wanaweza kutumia hii nguvu kazi wanayoiambia iendelee kuwa wachuuzi au kuwafundisha kuendelea kuwa tegemezi kama wao wanavyofanya (omba omba)
 
Hakuna nchi nyepesi kufanikiwa kama Tanzania. Nakiri kusema hivyo, sio kwamba nautajiri sana ila laiti ningelitambua Hilo wakati nikiwa na age ya 20 pale leo ningekuwa mbali sana. Hii nchi nyepesi nyie... Nimeenda huko vijijini watu wamefungua maduka ya dawa, wanatibu hawana ht elimu ya kuuza dawa, hv ni nchi Gani utakutana na huo mteremko. Watu wanawakopesha wakulima 40,000 mwisho wa msimu anavuna gunia la mpunga. Watu wanakopesha wafanyakazi kwa riba ya 100%. Msimu wa kiangazi ukienda huko umasaini ng'ombe mkubwa unampata kwa laki mbili ukijakumtunza vizuri miezi mitano mbele unaenda kumuuza laki nane. Ardhi ya kutosha wapo cheap labour wa kutosha kwa ajili ya kilimo. Yapo mengi mno ni sisi tu akili imelala
 
K

Kuna chimbo la kazi abroad nimelistukia majuzi linaaitwa Indeed nimeapply kazi nyingi za sales na marketing kazi za kampuni za Arizona hapa Nina interview kama 4 za online ,
Acha uongo , hakuna kampuni ya kukuajiri wewe kizembe hivyo kutokea Tanzania ,Marekani kuna kitu kinaitwa LMIA (Labour market impact assessment ) ,Hilo ni rungu lililoshikiliwa na serikali ya Marekani kupitia department of Labour , Hakuna mwajiri yoyote anayeweza kuajiri foreigner bila kupata hicho kibali LMIA na kinalipiwa hicho kaa ukijua ,yaani mwajiri analipa si chini ya 2000+ USD kukipata ili kukuajiri wewe foreigner ,na sio guarantee na hiyo fee ni nonrefundable ,LMIA anatuma maombi department of Labour na wakikataa hiyo pesa yake hairudi na hawezi kukuajiri , wewe na kazi yako hiyo ya sales ni mwajiri gani wa kugharamika kutoa pesa ili aajiri foreigner ambaye first of all ni liability kwa sababu ni mgeni wa mazingira inabidi apate training upya na wakati kuna wazawa hapo hapo for immediate hire ,Hakuna mwajiri wa kufanya biashara kichaa .

Hata hao wahindi unaowaona wanaingia Marekani wengi wao ni watu ambao wamefanya na makampuni ya software India ,kuna makampuni ya Marekani kama Facebook ,Twitter , Microsoft NK wametoa contacts Kwa makampuni madogo ya software na Engineering India so wanaofanya kazi katika hivyo vikampuni vidogo kama subcontractor rahisi kuingia Marekani kwa sababu tayari wako familiar na mfumo mzima wa kazi na issues kibao ,na LMIA inakuwa rahisi na sababu nyingine kubwa ni kwamba sekta yenyewe ya IT ina uhitaji mkubwa wa watu hivyo inakuwa haina ugumu sana ,ingawa kwa sasa hayo makampuni mengi Silicon valley yamepunguza wafanyakazi ,hasa hao wageni na wengi wanalazimika kurudi kwao maana visa zao ni za kazi na kazi ukiisha mkataba Una grace period ya miezi mitatu kutafuta nyingine na ikikosa ni lazima uondoke .
Kampuni nyingi sana Marekani zimepunguza wafanyakazi na bado zinaendelea kufanya hivyo kutokana na jinsi uchumi wa dunia ilivyo ovyo kwa sasa ,maana wanasema kuna uwezekano wa Recession kutokea soon .so kampuni zina punguza gharama kwa kupunguza wafanyakazi .
 
Kama kuna mtu hapa anabisha aingie leo Indeed au LinkedIn aaply kazi Marekani halafu atatupa mrejesho hapa , hutapata hata hiyo interview na pia sababu ni moja kubwa pia ,utahitaji World education system assessment result , mfumo wa elimu bongo na USA ni tofauti ,kama ni nafasi ya Proffessional job au trade / kazi za ufundi ni lazima hilo rungu likuhusu ,ni lazima ufanyiwe hiyo assenent ,kama elimu yako ulisomea Marekani hapo sawa ,ila kuna nchi ni exception ,mfano China na India hicho kizuizi hamna ,sasa ni mikataba waliyofanya hizo nchi mpaka mifumo yao ya elimu ukafanyiwa assement na wakapewa go ahead na kuwa categorised kama sawa na huko hizo nchi nyingine ,sasa ni mtu kamalizia India anaweza enda kufanya kazi USA ,UK nk bila kikwazo kama sisi ,
Serikali haikwepi wajibu wake kwenye hili suala
 
Na huu ndio ukweli, huyo uliyemtag kwa comment ya kwanza kama hajakuelewa achana nae.

Hakuna muajiri wa nchi za west atakuoffer interview kwa kazi ya maana kwa elimu yako ya bongo ya kuunga unga na experience uchwara. Ili upewe “Job sponsorship” lazima uwe extra sana kielimu, au kwa experience ya kazi.

Otherwise ni kutafuta visa kwa mfumo wa kawaida tu wa kujilipia kila kitu, ukifanikiwa kupata ufike kule ndio utafute kazi Professional/non professional.

Hapo pa skills assessment hapo hahah! Ukiambiwa usubmit ushahidi wa course ulizosoma ndio utajua elimu yetu ina tatizo mahala!
 
We jamaa IVI ata Indeed upo kweli watu kibao wanapata kazi kupitia umo ata Leo saa 11 jioni EAT nilikuwa nifanyiwe interview kupitia zoom sema nicaicancel ,we Tomaso nini😀😀Indeed kazi kibao za nje aswa US labda ungesema issue ya kuingia US ndo ngumu ila sio kufanyiwa interview mi ninazo interview kalibia 3 zote kutoka makampuni ya Arizona,
 
Unasahau sirikari ina makubaliano mfano na SA kusupply walimu wa kiswahili.
 
Habari ndugu,

Mimi ni kijana wa miaka 23.

Nimepambana hapa Bongo, ila nataka nitafute zaidi nje ya mipaka ya nchi, hususani Ulaya na Amerika.
Naombeni ushauri kama kuna mtu anajua geographia ya nchi yoyote anaweza kunieleza, kisha mimi nitatafakari wapi pa kuanzia.

Note: Sipo hapa kuomba connection, nipo hapa kuomba mawazo tu ya ujuzi wa waliobahatika kwenda au hata kwa kusikia (ziwe habari za kweli).
 
mm kaka nataka bandua ya mualiko nichek pm
 
Naomba kwanza kabla ya kutulaum sisi vijana unijumlishie Jumla ya gharama ya passport na visa na nauli ya safari kutoka Tanzania hadi Kuwait kwa mfano.

Baada ya hapo uje kutulaum sisi vijana
Passport 150000/= unaweka bando shilingi ngapi na kubet kwa mwezi kuingia inst na betting sites?
Nauli to Kuwait ni kama 1 m hivi
 
Very sad and exhausting brother. Viongozk wetu kwa makusudi na maslahi yao binafsi wanafanya mambo yanakuwa magumu, pasi na tija.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Mwl nyerere na CCM ndo walianzisha upinzani dhidi ya diaspora
 
Nimekusoma mkuu ni kweli hata mimi niliapply kazi sana za electrician indeed na sijawahi kupata kumbe iko ndio kigezo arafu kingine hawa jamaa awaamini elimu za bongo
 
Ina maana ulikuwa hujawahi kufikiria hili before? Tafuta kazi popote kijana ili mradi iwe kazi halali
 
Ina maana ulikuwa hujawahi kufikiria hili before? Tafuta kazi popote kijana ili mradi iwe kazi halali
 
Ina maana ulikuwa hujawahi kufikiria hili before? Tafuta kazi popote kijana ili mradi iwe kazi halali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…