Je, Rais Magufuli alikuwa na Pacemaker au Defibrillator? Ilidukuliwa?
Mkuu acha kutupanga...maneno ya kwenye vijiwe vya kahawa acheni na hili la kusema ameuliwa nilihisi tu watu wangezusha....
GUYS,,SIYE TUNATAARUFA ZA NDANI..KIFAA ALICHIKUWA NACHO KILIWEKWA MWAKA JANA BAADA YA KILE CHA KWANZA KUEXPIRE..HIKI CHAPILI KINGEEXPIRE MWAKA 2030,,LAKINI KILISIMAMA GHAFLA NAKUAGIZA KINGINE ILIKIWA NI PROCESS.NDO MAANA MH RAIS KABLA YA KUFARIKI ALIWAITA WATU TOFAUTI NA KUWAAGA.NAWALE WAKARIBU AKAWAAMBIA HATA VITU VYA SIRI KAMA MABEYO ALIYOSEMA. LAKINI PIA TUNASIKIA KUNAMIKATABA MIKUBWA YA KUCHIMBA MADINI NA GAS..WAINGEREZA NA WACHINA WALITOA TERMS ZAO MKUU AKAKATAA KAMA FINAKA DECISION MAKER..NA BAADA YA HAPO AKAPOKEA UBALOZI WA UINGEREZA BUKOBA NA UGENI WA CHINA HUKO BUKOBA.BAADA YA HAPO AKAANZA KUONA MABADILIKO.ISSUE YA CORONA YEYE AMEISHAIUGUA ILE YA MWANZO NA ALIOONA NDO MAANA ALIKUWA ANAWAHIMIZA KUJIFUKIZA NK KWANI ANAUZOEFU WA KWAKE NA FAMILIA YAKE KUUGUA NA KUPONA.KUONYESHA KUWA KUNA ASSASNATION..MNAKUMBUKA KUNAWACHUNGAJI WALUTABIRI KIFO CHAKE MWEZI MMOJA KABLA LAKINI PIA TH 17 FEB KUNAMTU ALIANDIKA KWA KIINGEREZA KWENYE FACEBOOK KUWA MAGUFURI ANGEFARI TH 17 MARCH..NA KWELI IKATOKEA,,HII INAMAANA HAWA WATU WALIJUA KILICHOKUWA KINAENDELEA.
 
1. Hujuma katika kifaa cha Pacemaker

Katika Lugha nyepesi kabisa, kazi ya kifaa cha Pacemaker ni kuratibu mapigo ya moyo. Ni katika mazingira magumu sana kifaa hiki kuleta shida. Aidha, Kutokana na evolution ya technology, mfumo wa kifaa hiki unaweza kuharibiwa kwa kutumia data base na access code zilizotumika ku program kifaa.

Unahitaji kupata access ya zile code kisha uwe na muhusika umbali mdogo ili kuharibu mfumo wa kifaa kwa kukihamuru kusababisha shock na kufanya mapigo ya moyo kutorandana tena. Kama kutakuwa hakuna wataalamu wa kuliona hilo kwa haraka na kuwahi kukibadili kifaa, hatari itakuwa ni kubwa kwa maana muda mwingi utapotezwa kwenye first aid za ku support maisha yake badala ya kuondoa kifaa kilichoharibiwa mfumo. JPM alivyokuwa anahudhuria mikutano yake na kujichanganya na watu, ni dhahiri kwamba ilikuwa ni rahisi kwa mtu mwenye nia ovu kutekeleza dhima hiyo kwa msaada wa Mabeberu na vibaraka wa ndani.
Wachache watakuelewa. Ila umeandika ukweli mtupu
 
Mwenye nia ovu nani? kwa lengo gani ili iweje? Mpendwa alikuwa sio mtu wa musafiri na hapa nchini alikuwa na ulinzi madhubuti acheni propaganda mtu kufa ni kawaida.
 
Ndo maana mimi nawashangaa wanaosema Jiwe kauliwa wakati mtu alikua anaonesha mgonjwa tangu mwaka jana hata miguu yake akikaaa kwenye kiti ilikua kama vifupa vitupu....


Ila Mungu amuweke panapostahili,ameumaliza mwendo
Aliyeua kwa Upanga na yeye atakufa kwa Upanga pia, hivi ni nani alihoji kifo cha Mzee Mkapa? Yule mzee hakuonesha dalili ya kuumwa na hata wanajeshi kipindi wanaubeba ule mwili wake wanaonekana kabisa kutumia nguvu nyingi (Yumkini wale wanajeshi waliomba likizo baada ya zoezi lile). Na tukumbuke ni Mkapa pekee ndiye alikuwa na uwezo wa kumwambia Ukweli Marehemu Magufuli, the rest wastaafu kama Mwinyi alikuwa mzee wa kusifia na Kikwete mara chache sana alitumia utaalamu wa lugha kusema utaawala wa Magufuli. Ila Mkapa kifo chake ni cha Utata sana, mstaafu tunasikia tu amefariki.

Hilo moja, Mzee Mangula kidogo tu afe kwa Sumu na inasemekana walikuwa kwenye kikao huko cha CCM, tukumbuke Mangula ni makamu mwenyekiti wa CCM na inawezekana hata kwenye kikao anakaaga karibu na Mwenyekiti. Kwa nini polisi waseme tunataka tuanze uchunguzi wa nani alimuwekea Sumu Mangula halafu ghafla, tunaona hakuna cha Uchunguzi wala nini mpaka mzee wa watu akarudi zake kijijini. Katika hali ya kawaida kaa kwenye nafasi ya Mzee Mangula, una boss ambaye ni mwenyekiti wako na anauwezo wa kuchunguza juu ya tukio la kuwekewa Sumu halafu ghafla unaona yupo kimya.

Lingine, Marehemu Magufuli alionekana mgonjwa tangu mwaka jana ila ndio hivyo madaraka matamu mno. Magufuli ukimuangakia usoni unaona kabisa hana sura angavu na unaona kabisa kuna mambo anajutia, akikaa kwenye kiti unaweza kusema amekaa mlemavu wa miguu.

Na la mwisho achana kauli ya CDF Mabeyo, marehemu alipotembelea Kurasini mwezi Februari kuna kitu alifungwa kama kitambaa cheusi hivi kwenye mkono wake wa kushoto. Na inawezekana alijua pia hana siku nyingi za Kuishi ndio maana hata Uteuzi wa Bashiru kuwa KMK ulifanyika kwa ghafla sana na siku ya Uapisho wa Katibu Mkuu kiongozi, Hayati Magufuli hakuongea kama ilivyo kawaida yake na tukaambiwa ana Ratiba zingine. Ni ratiba gani alikuwa nazo, wanajua watu wa Ikulu lakin mawazo yangu inaonekana alishauriwa na Madaktari wake asisimame kwa muda mrefu au kuzungumza.

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Hilo la PSU na Mimi naunga hoja mkono.
Inakuaje watu wa nje wanapata taarifa za ndani kabisa za Ofisi Kama ile. Eg kigogo na lissu.
Kama taarifa nyeti Kama hizo zinatoka vip usalama wa Nchi yetu?
Kuna watendaji wasio wazalendo na waaminifu kule. Intensive investigation should be done.
Mwisho. Naamini katika Mungu iwe mpendwa wetu wakati wake ulikua sahihi au lah inategemeana na Makusudi ya Mungu.
 
Corona IPO! Wanakufa watu wasiyo na kiberiti cha kupmulia, sembuse mwenye hicho!
CORONA NI HATARI! OLE WAO WENYE MIZAHA!
Bibilia iko wazi kabisa! Katika harakati za kupambana na yule muovu msiache kutumia kila siraha ya maangamiz
Someni Efeso 6:11-18
 
Korona uchanganye na pacemaker uchanganye na ngoma hutoboi
 
Pesa zimetumika sana kuzungushwa JPm jamani.
Tuachieni pesa zetu,Kodi zetu zipumue kidogo.
Uchunguzi wa nini?
 
Nina mashaka na ziara ya Morogoro ziara za viwandani kuna jambo la kufikirisha...
 
GUYS,,SIYE TUNATAARUFA ZA NDANI..KIFAA ALICHIKUWA NACHO KILIWEKWA MWAKA JANA BAADA YA KILE CHA KWANZA KUEXPIRE..HIKI CHAPILI KINGEEXPIRE MWAKA 2030,,LAKINI KILISIMAMA GHAFLA NAKUAGIZA KINGINE ILIKIWA NI PROCESS.NDO MAANA MH RAIS KABLA YA KUFARIKI ALIWAITA WATU TOFAUTI NA KUWAAGA.NAWALE WAKARIBU AKAWAAMBIA HATA VITU VYA SIRI KAMA MABEYO ALIYOSEMA. LAKINI PIA TUNASIKIA KUNAMIKATABA MIKUBWA YA KUCHIMBA MADINI NA GAS..WAINGEREZA NA WACHINA WALITOA TERMS ZAO MKUU AKAKATAA KAMA FINAKA DECISION MAKER..NA BAADA YA HAPO AKAPOKEA UBALOZI WA UINGEREZA BUKOBA NA UGENI WA CHINA HUKO BUKOBA.BAADA YA HAPO AKAANZA KUONA MABADILIKO.ISSUE YA CORONA YEYE AMEISHAIUGUA ILE YA MWANZO NA ALIOONA NDO MAANA ALIKUWA ANAWAHIMIZA KUJIFUKIZA NK KWANI ANAUZOEFU WA KWAKE NA FAMILIA YAKE KUUGUA NA KUPONA.KUONYESHA KUWA KUNA ASSASNATION..MNAKUMBUKA KUNAWACHUNGAJI WALUTABIRI KIFO CHAKE MWEZI MMOJA KABLA LAKINI PIA TH 17 FEB KUNAMTU ALIANDIKA KWA KIINGEREZA KWENYE FACEBOOK KUWA MAGUFURI ANGEFARI TH 17 MARCH..NA KWELI IKATOKEA,,HII INAMAANA HAWA WATU WALIJUA KILICHOKUWA KINAENDELEA.
Humu kuna nyuzi 3 zikitabiri magufuli atatawala kipindi kimoja.

Kuna wa kuzungumzia utabiri wa Sheikh Yahya wa 2006.

Kuna wa 2018.

Kuna wa 2020
 
...Ndio Leo nafahamu kwamba Rais wetu aliwekewa Kifaa cha Pacemaker kinachoratibu mapigo ya Moyo!
 
Back
Top Bottom