Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Rais wa nchi yetu awe na sifa zipi?

Je, ni nani anazo sifa nyingi za kuwa Rais ajae? Je, Tundu Lissu anazo sifa hizo pia?
Hatutaki Rais mwenye sifa bali moyo wa kupenda watu na nchi yake.Nyerere aliwapenda watu na nchi yake na laiti angekuwa Rais ktk nchi ya kidemokrasia kama Sasa,wananchi tungefaidi uchumi wetu
 
Lissu ana vigezo vyote kuwa Rais ila ni wakati sasa chama kimfanyie branding na kimtafutie PR officer.

Kama walivyosema wachangiaji hapo juu lissu na JPM wana tofauti ndogo sana in terms of haiba.

Mnyika alikua hivyo zamani ila naona alipikwa na Mbowe Sasa yupo composed and matured kuliko zamani.

Lissu pia akiwa managed vizuri akajua mipaka ya kauli zake, kupima madhara ya Kila jambo kisiasa na kuwa "statesman" anayeweza ku bond vizuri na watu wa vyama vyote basi hakuna mtu atamzuia kuingiza ikulu.
Una maanisha kuwa Rais lazima apime consequences ya kila neno na tendo lake?
 
Wanazo zote na za ziada ndio maana uchaguzi wa mwaka tulimshauri Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Ila kwa uchaguzi wa 2025, niliwaomba Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! hivyo iwapo CCM itamsimamisha mgombea Mwanamke, TL asigombee maana itakuwa ni aibu kushindwa na Mwanamke!.

Unless kama sauti hii ni yake YEYE, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke then TL agombee, wapambane!.

P
spinning!
 
Wanazo zote na za ziada ndio maana uchaguzi wa mwaka tulimshauri Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Ila kwa uchaguzi wa 2025, niliwaomba Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! hivyo iwapo CCM itamsimamisha mgombea Mwanamke, TL asigombee maana itakuwa ni aibu kushindwa na Mwanamke!.

Unless kama sauti hii ni yake YEYE, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke then TL agombee, wapambane!.

P
"By Lucas Mwanshambwa".
 
Kwa maoni yangu, Tundu Lissu anazo sifa kumzidi Mwinyi, Kikwete na ningesema hata Magufuli, isingekuwa uigizaji wa uzalendo aliojaribu kuuonyesha.
Labda sifa ya kuwa mgombea wa kwanza kuwa mkimbizi, siyo urais.
 
Unaweza ukatupa mfano wa ukabila CHADEMA? Kila chama kina base yake na strongholds na CHADEMA base yake kubwa ilikua kaskazini.

But chama kimekuwa Sasa kilifika stage kikaongoza majiji yote makubwa Arusha, Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya imebakia Dodoma tu alafu bado unakazana kusema ni cha wachagga?

Toka huko kwenye ukabila, in fact siku hizi CHADEMA inakubalika zaidi nyanda za juu kusini kuliko hata huko Uchaggani.
Chadema ni chama kikubwa na makini hata Nyerere aliyasema hayo. Lakini chadema inaendelea kupoteza umaarufu wake sasa kutokana na:
1. Tangu enzi hizo Mwenyekiti wa chama lazima awe wa kabila hilohilo kutoka hukohuko.
2. Wagombea wake wa Urais kutoka CCM na kisha kurudi CCM tena (imani inapotea)
3. Wabunge wa chadema kuhamia CCM na vyama vingine bila chama kuwaomba msamaha hadharani wapiga kura wao walipiga kura, kuhesabu kura na kulinda kura za wagombea wa CDM. Watu wanapoteza imani na wagombea wa chadema, hawana imani nao tena.
4. Kuyakubali matokeo ya uchaguzi waliyoyasusia kimyakimya bila kuwafahamisha wapiga kura wao. Mfano, wanataka akina Halima wafukuzwe ubunge ili wapeleke watu wao wengine kwenye bunge ambalo walisusia matokeo yake ya uchaguzi.
5. Kulalamika majukwaani kuliko kutoa sera zao. Trump kila akipa nafasi huwa anawaambia Wamarekani wenzake kama akirudi tena madaraki 2024 atafanya nini tofauti na Biden kwenye kila jambo.
 
Una maanisha kuwa Rais lazima apime consequences ya kila neno na tendo lake?
Yeah mfano Kulikua hakuna haja ya kuongelea au kukosoa kauli za "hakuna kama Mama". Au hakuna haja ya kwenda Chato na ukaanza mkosoa JPM hata JPM alivyoenda Ikungi na Manyoni alimpamba sana Lissu na kumuita "handsome boy... Akasema ana akili sana na atampa kazi serikalini kwake" that's PR

Sasa Lissu yeye Hana unafiki (Ni kitu kizuri) ila Kwa siasa zetu ni ngumu sana kuungwa mkono na makundi yote. Najua kura zikiwa huru na haki Lissu anamshinda Samia obviously ila tunaongelea Ili awe Rais BORA ni vizuri akapata PR nzuri kuelekea 2025.
 
Wagombea wake wa Urais kutoka CCM na kisha kurudi CCM tena (imani inapotea)
Labda Lowassa tu ila Mbowe, Dr Slaa na Tundu Lissu waligombea Urais wakiwa wanachama hai wa Chadema sio chini ya miaka 15.
Wabunge wa chadema kuhamia CCM na vyama vingine bila chama kuwaomba msamaha hadharani wapiga kura wao walipiga kura, kuhesabu kura na kulinda kura za wagombea wa CDM. Watu wanapoteza imani na wagombea wa chadema, hawana imani nao tena
Hiyo sio kazi ya CHADEMA, mbunge kama akisaliti unalaumuje chama?

Kuyakubali matokeo ya uchaguzi waliyoyasusia kimyakimya bila kuwafahamisha wapiga kura wao. Mfano, wanataka akina Halima wafukuzwe ubunge ili wapeleke watu wao wengine kwenye bunge ambalo walisusia matokeo yake ya uchaguzi.
CHADEMA Haina mpango wa kupeleka wabunge maana halitambui wabunge waliopo maana wote waliingia kwa wizi. Wao wamewafukuza Kina Mdee uanachama Wala hakuna mahali walijadili wang''olewe bungeni.

Kulalamika majukwaani kuliko kutoa sera zao. Trump kila akipa nafasi huwa anawaambia Wamarekani wenzake kama akirudi tena madaraki 2024 atafanya nini tofauti na Biden kwenye kila jambo.
Sio kweli CHADEMA imeshaeleza sana kuwa ikiingia itatekeleza sera ya majimbo/ugatuzi, kuleta katiba mpya Ili kuepusha tozo za ajabu kutungwa na Rais, kufanya PPP kwenye miundombinu n.k Wala hakuna ambacho huwa hawasemi.
 
Hujatoa jibu la msingi, kupayuka maan yake nn? Yawezekana mtu anaongea mamb ya kwel kbs na yeny mantiki but approaching ikatafsiriwa tofaut. Pia LISSU sio mropokaji tatizo lenu mnataka mtu akosoe huku anapata mafuta na kuwalambisha asali huku anawakosoa!! LISSU hawez mung'unya maneno penye ukwel anapiga mulemule bila kuremba maneno, kitu ambacho wanaccm hawapendi kbs!!
Wanataka awe anaongea kama Philip Mpango.
 
Benjamini Mkapa alikataa kuitwa MTUKUFU RAIS na akapendekeza aitwe MHESHIMIWA RAIS au NDUGU MKAPA.
Mara nyingi kama sio mara zote hakuna Rais asiyependa kupigiwa makofi na kusifiwa ndani na nje ya nchi yake. kwa maana nyingine hakuna Rais asiyependa kufanya vizuri. Shida zinazowapata viongozi wengi zinatokana na wale watu/taasisi/nchi/kabila/dini waliomzunguuka/wanaomsaidia , wale waliomsaidia kuipata nafasi na aina ya watu wanaomsifia na sababu zao za kumsifia.
 
Hakuna sifa kuu kwa kiongozi wa nchi kuwa nayo inayozidi UZALENDO kwa nchi yake.

Kwa hiyo napendekeza uanzie kwenye sifa hiyo.

Kiongozi wa nchi ni muhimu awe na dira inayomwongoza ni wapi nchi anayoiongoza iende na kwa mipango gani na wakati maalum. Siyo maswala ya kubahati sha tu

Kiongozi ni lazima awe na imani na wananchi wake, kwamba hawa watu ndio walio na uwezo wa kujiletea maendeleo na kubadilisha hali duni ya maisha yao. Hayo mengi sana tunayopigiwa kelele kuhusu uwekezaji, hiyo ni kuongezea tu juu ya juhudi zetu wenyewe

Kiongozi ni atakayeheshimu na kujali mali za taifa hili. Asiyekuwa na uvumilivu kabisa katika kutapanya mali za nchi yetu bila ya mpango maalum. Madini yote sasa karibu yamesombwa, lakini ukiuliza ni miradi ipi iliyobadilishwa na madini hayo, hupati jibu hata moja.

Zipo sifa nyingi..., kiongozi anayeweza kujieleza na watu wakaelewa anachozungumzia kwa lugha inayoeleweka; n.k.,
Mkuu kuongoza nchi kunahitaji vitu vingi zaidi ya uzalendo,
Nyerere alikuwa mzalendo ila aliharibu hii nchi,
Inahitaji kumchek mtu mwenye kuliunganisha taifa, kuunganisha taifa, kuwa na busara, na kuwa na sera nzuri hususanu wakati huu ambapo tunahitaji zidi kujikomboa kiuchumi tunahitaji kiongozi mwenye sera nzuri za uchumi,
Bahati mbaya kwa Lissu sijawahi sikia akiongelea uchumi, yeye yupo more political based
 
Mara nyingi natamani potential candidate akipata nafasi hata ya dk 2 za kuzungumza na wananchi awaambie nini angefanya/atafanya kama angekuwa/atakuwa Rais wa nchi hii. Shida yetu kubwa kuliko zote sio uhaba wa demokrasia bali uchumi mdogo, huduma mbovu na ukosefu wa huduma kabisa. Kule nchi za Uarabuni na Uchina hakuna demokrasia pana lakini hali za maisha na uchumi ni kimbilio kwa watu wa nchi nyingine kutafuta huduma, ajira, mikopo, elimu, afya na starehe. Sitamani kumsikia mgombea anayehubiri demokrasia saaaana kama ya Magharibi na kuacha kutuambia atafanya nini juu ya wezi wa mali ya umma, maji, uchukuzi, elimu, ajira, umeme, gharama za maisha, chakula, hali ya hewa, masoko, mitaji, technolojia, nk. Nataka mtu aeleze polepole kwa kituo nimwelewe bila kunifokea au kulaumu na kubeza wengine.
Kumbuka kuwa Tanzania tulitawaliwa na Waarabu na walituletea shanga na mavazi,kwa hiyo kufafananisha maendeleo ya Tanzania na Waarabu ni ukosefu wa fikra na uzalendo kwa Watanzania wengi.
 
hana sifa, aache kwanza agenda zake za siri, vile vile hatuwezi kua na Rais ambaye ni mgonjwa...sisi wenyewe wagonjwa tutaongozwaje na mgonjwa mwenzetu
 
Back
Top Bottom