Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Ni kweli matatizo yetu sio katiba mpya. Umekiri kwamba tunahitaji viongozi imara na waadilifu, najaribu kuwaza kwa sauti huenda pia hii katiba inatoa huo mwanya wa kupata viongozi wa siyo imara na waadilifu, hapo unaonaje?

Je wewe kwa upande wako Unadhani nini kinazuia kupata hiyo dola yenye nguvu ya kubadilisha hali ya mambo ikiwemo kupambana na hiyo mifumo mibaya ya dunia ya manunuzi?

Je hauoni kwamba kuwa na dola yenye uwezo wa kupambana na mifumo mibaya ya manunuzi ya dunia ni sawa na kuwa against na wakubwa wa dunia?

Na kwanini wanasiasa wa afrika wanan'gan'gania kushika dola hali yakuwa wanafahamu fika kuwa hawawezi kubadili hali ya mambo?

Mwisho nini kifanyike kuipata dola ya aina hiyo?

Funguka mkuu tujifunze.
Wanahakikisha kuwa huwezi kupata fedha za kigeni (USD/Euro) kwakuwa wao ndio wanapanga ubora na bei ya pamba, korosho, kahawa, chai, dhahabu yako. Hivyo utalazimika kwenda kuwakopa wao kwa riba kubwa. Muda wote utakuwa unahangaika namna ya kuingia kwenye masoko yao kwa bei yao na kulipa madeni yao. Hii ndio sababu Afrika yote iko hoi hata zile nchi zenye Katiba mpya na vyama vipya madarakani.

Hatua ya kwanza mtambue yule anaedhamini kampeni za chama cha mgombea na malengo yake, pili soma sera za mgpmbea na chama chake, tatu angalia integrity ya wale wanaomsaidia kupiga kampeni mgombea. Hapo utagundua kuwa hakuta kuwa na lolote.
 
hana sifa stahiki kwa nafasi hiyo maoni yangu na mtazamo wangu.
si muaminifu,
si mzalendo, uzalendo wake wa mashaka.
si mstahimilivu
si muungwana
ana majivuno na dharau kupindukia,
amepungukiwa hekima na Busara,
si mtarabibu wala mstaarabu,
ni mbishi asie na utii,
hana mipango bali lawama,
haaminiki kitaifa bali ng'ambo kwa watwana,
ana uchu na tamaa mno,
ni mbinafsi hatari,
ni mpenda fujo sana,
ana chuki na wanaotofautiana nae kimtazamo,
ni mjeuri mwenye elimu
ana hasira iliyofichika.

nadhani Mbowe anafaa zaidi.
ni mstahimilivu,
Mzalendo asiye na shaka,
si mbishi,
ni mtulivu, mwenye hekima na Busara
hajivuni na wala haringi,
muongea kwa utaratibu na ustaarbu,
Hatukani wala kukejeli mtu,
Hana chuki wala habagui wenye tofauti na mtazamo wake.
si mbinafsi.
Anaaminika kitaifa na kimataifa
Jamaa ni muungwana sana,


nakuja kumalizia ngoja nipande daladala kwanza...........
🙄🙄🙄🙄

Umebeba kila neno linalo - denominate sifa ukampachika nalo Tundu Lissu..

It's a wisdom to think and analyse things rather than being judgemental..
 
Wanahakikisha kuwa huwezi kupata fedha za kigeni (USD/Euro) kwakuwa wao ndio wanapanga ubora na bei ya pamba, korosho, kahawa, chai, dhahabu yako. Hivyo utalazimika kwenda kuwakopa wao kwa riba kubwa. Muda wote utakuwa unahangaika namna ya kuingia kwenye masoko yao kwa bei yao na kulipa madeni yao.

Its so bad. Anyway ngoja tuendelee kuiota Afrika yenye neema, hata kama itakuwa miaka 500 ijayo.

Maana kutoka kwenye hayo makucha ya hao wapanga bei za mazao na dhahabu zetu kunahitaji sacrifice.

Ila kwa generation hii ya viongozi wa Afrika sidhani kama Afrika itaweza kujinasua kwenye hayo makucha.
 
🙄🙄🙄🙄

Umebeba kila neno linalo - denominate sifa ukampachika nalo Tundu Lissu..

It's a wisdom to think and analyse things rather than being judgemental..
kwani bandiko linamzungimzia nani 😳 ebo!
 
Mara nyingi kama sio mara zote hakuna Rais asiyependa kupigiwa makofi na kusifiwa ndani na nje ya nchi yake. kwa maana nyingine hakuna Rais asiyependa kufanya vizuri. Shida zinazowapata viongozi wengi zinatokana na wale watu/taasisi/nchi/kabila/dini waliomzunguuka/wanaomsaidia , wale waliomsaidia kuipata nafasi na aina ya watu wanaomsifia na sababu zao za kumsifia.
Hakuna binaadam mwenye akili timamu asiyependa kuonekana na sifa anazoona yeye mwenyewe anazo na watu wengine wazitambue hivyo; kwa hiyo kumsifia kwa sifa hizo alizo nazo.

Mtu anapokuwa kiongozi, akatafuta kusifiwa kwingi zaidi ya sifa alizo nazo hiyo ni dosari.

Hao watu wanaomzunguka na kumpa sifa hizo, hata asizokuwa nazo, na wengi (wote) wa watu hao wakiwa ni wateule wake, maana yake ni kwamba kiongozi huyo ni mpenda sifa tu, ndiyo maana watu hao kawaweka kwenye nafasi hizo alizowaweka kwa misingi ya kumsifia yeye.

Huyu ni kiongozi mbovu.
 
Hakuna binaadam mwenye akili timamu asiyependa kuonekana na sifa anazoona yeye mwenyewe anazo na watu wengine wazitambue hivyo; kwa hiyo kumsifia kwa sifa hizo alizo nazo.

Mtu anapokuwa kiongozi, akatafuta kusifiwa kwingi zaidi ya sifa alizo nazo hiyo ni dosari.

Hao watu wanaomzunguka na kumpa sifa hizo, hata asizokuwa nazo, na wengi (wote) wa watu hao wakiwa ni wateule wake, maana yake ni kwamba kiongozi huyo ni mpenda sifa tu, ndiyo maana watu hao kawaweka kwenye nafasi hizo alizowaweka kwa misingi ya kumsifia yeye.

Huyu ni kiongozi mbovu.
Kiongozi anaweza kuwazuia watu wasimsifu? Muhimu kwake kiongozi anaesifiwa ni kutafakari kwa kina ili kujua ni kwanini nani anamsifu sana kiasi hicho, baaasi. Yaani yule anaetoa sifa hizo ni lazima apekuliwe zaidi kuliko wengine ili kujua kama ni sifa tu au kuna kitu anataka/anaomba/anaiba/anataka kuiba. Vinginevyo kumsifu mtu sio kosa kama amekukuna kwelikweli.
 
Mkuu kuongoza nchi kunahitaji vitu vingi zaidi ya uzalendo,
Nyerere alikuwa mzalendo ila aliharibu hii nchi,
Inahitaji kumchek mtu mwenye kuliunganisha taifa, kuunganisha taifa, kuwa na busara, na kuwa na sera nzuri hususanu wakati huu ambapo tunahitaji zidi kujikomboa kiuchumi tunahitaji kiongozi mwenye sera nzuri za uchumi,
Bahati mbaya kwa Lissu sijawahi sikia akiongelea uchumi, yeye yupo more political based
"Nyerere alikuwa mzalendo ila aliharibu hii nchi"?

Hiki ni kitu gani unachokiongelea hapa hasa. Unaelewa ulichokiandika?
Ukubali kuwa alikuwa 'mzalendo', halafu kwa sababu unaziozifahamu wewe, aamue kuiharibu nchi! Hii inaleta mantiki yoyote?

Haya ndiyo matokeo ya kukariri tu mambo unayosikia yakisemwa na wewe kuyabeba bila ya kuyachambua akilini mwako vizuri.

Sasa kwa kuwa enzi hizi ni za uwekezaji, kama unavyoandika, ungesifu sana kama Nyerere angekuwa kafanya uwekezaji kama unavyohimizwa leo?

Haya, leo tunafanya uwekezaji, kama mtindo wa sasa unavyohimiza, umeiona nafuu yoyote ya ziada?
Mkapa na Kikwete wamefanya sana habari ya uwekezaji; lakini nchi bado ndiyo inakwama zaidi kwenye tope.

Sasa usinielewe kuwa sitaki uwekezaji, lakini unapokuwa kiongozi mzalendo, inakubidi uelewe ni yapi ya kufanya ili uwekezaji huyo unufaishe jamii unayoiongoza.
 
Kiongozi anaweza kuwazuia watu wasimsifu? Muhimu kwake kiongozi anaesifiwa ni kutafakari kwa kina ili kujua ni kwanini nani anamsifu sana kiasi hicho, baaasi. Yaani yule anaetoa sifa hizo ni lazima apekuliwe zaidi kuliko wengine ili kujua kama ni sifa tu au kuna kitu anataka/anaomba/anaiba/anataka kuiba. Vinginevyo kumsifu mtu sio kosa kama amekukuna kwelikweli.
"Kiongozi anaweza kuwazuia watu wasimsifu"? Sana.

Kama ni sifa za kijinga, hao wanaomsifu wenyewe watajua hataki upumbavu huo.

Awamu ya Magufuli na hii ya Samia, kusifu kijinga ni heshima kubwa sana. Wengi inawabeba na kuwapeleka mbali.

Kuna watu wanaona sifa kabisa kujitambulisha kwa wengine kuwa "chawa". Hii nayo imekuwa ni sehemu ya utmaduni wetu mpya!
 
Its so bad. Anyway ngoja tuendelee kuiota Afrika yenye neema, hata kama itakuwa miaka 500 ijayo.

Maana kutoka kwenye hayo makucha ya hao wapanga bei za mazao na dhahabu zetu kunahitaji sacrifice.

Ila kwa generation hii ya viongozi wa Afrika sidhani kama Afrika itaweza kujinasua kwenye hayo makucha.
Kuna watu walijaribu kuwabwekea wapanga bei lakini hawakufua dafu, miongoni mwao wamo, Mwl. Nyerere, Magufuli, Nkrumah, Gadafi, Mugabe, nk. Hali ni ngumu kweli kweli. Mzee Nyerere ilimlazimu kuachia ngazi (kung'atuka) bila kupenda, nchi ilifisika kwa vikwazo.
 
"Nyerere alikuwa mzalendo ila aliharibu hii nchi"?

Hiki ni kitu gani unachokiongelea hapa hasa. Unaelewa ulichokiandika?
Ukubali kuwa alikuwa 'mzalendo', halafu kwa sababu unaziozifahamu wewe, aamue kuiharibu nchi! Hii inaleta mantiki yoyote?

Haya ndiyo matokeo ya kukariri tu mambo unayosikia yakisemwa na wewe kuyabeba bila ya kuyachambua akilini mwako vizuri.

Sasa kwa kuwa enzi hizi ni za uwekezaji, kama unavyoandika, ungesifu sana kama Nyerere angekuwa kafanya uwekezaji kama unavyohimizwa leo?

Haya, leo tunafanya uwekezaji, kama mtindo wa sasa unavyohimiza, umeiona nafuu yoyote ya ziada?
Mkapa na Kikwete wamefanya sana habari ya uwekezaji; lakini nchi bado ndiyo inakwama zaidi kwenye tope.

Sasa usinielewe kuwa sitaki uwekezaji, lakini unapokuwa kiongozi mzalendo, inakubidi uelewe ni yapi ya kufanya ili uwekezaji huyo unufaishe jamii unayoiongoza.
Kupitia sera zake mbovu za Ujamaa nyerere aliharibu uchumi wa nchi like forever

Kupitia sera yake ya uoga wa kutopingwa nyerere alikuja na system ya chama kimoja tu na hivyo kuua demokrasia ya Tz,

Sera zake za azimio la Arusha zilifeli ovyo na kuendelea kuharibu nchi,

Sera zake za mahusiano mema na majirani zikapeleka nchi kupoteza vijana wake wengi kwenye vita vya ukombozi bila sababu za msingi + akaingiza nchi kwenye vita na Idd Amin kisa tu kumsaidia Obote,


Above all Nyerere alikuwa mzalendo lakini hakuwa na akiili na maarifa sahihi + vision sahihi ya taifa bora inabidi liwaje na awekeze kwenye nini,

So unaweza ona kuwa mzalendo tu hakukupi nafasi ya kufanya vizuri kama raisi wa nchi, kuna sifa za ziada inabidi uwe nazo
 
Back
Top Bottom