Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Wanazo zote na za ziada ndio maana uchaguzi wa mwaka tulimshauri Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha uwezo zaidi ya Magufuli!

Ila kwa uchaguzi wa 2025, niliwaomba Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye! hivyo iwapo CCM itamsimamisha mgombea Mwanamke, TL asigombee maana itakuwa ni aibu kushindwa na Mwanamke!.

Unless kama sauti hii ni yake YEYE, Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke then TL agombee, wapambane!.

P
Ndio ujanze Link kwenye nyusi za watu hv
 
Hakuna sifa kuu kwa kiongozi wa nchi kuwa nayo inayozidi UZALENDO kwa nchi yake.

Kwa hiyo napendekeza uanzie kwenye sifa hiyo.

Kiongozi wa nchi ni muhimu awe na dira inayomwongoza ni wapi nchi anayoiongoza iende na kwa mipango gani na wakati maalum. Siyo maswala ya kubahati sha tu

Kiongozi ni lazima awe na imani na wananchi wake, kwamba hawa watu ndio walio na uwezo wa kujiletea maendeleo na kubadilisha hali duni ya maisha yao. Hayo mengi sana tunayopigiwa kelele kuhusu uwekezaji, hiyo ni kuongezea tu juu ya juhudi zetu wenyewe

Kiongozi ni atakayeheshimu na kujali mali za taifa hili. Asiyekuwa na uvumilivu kabisa katika kutapanya mali za nchi yetu bila ya mpango maalum. Madini yote sasa karibu yamesombwa, lakini ukiuliza ni miradi ipi iliyobadilishwa na madini hayo, hupati jibu hata moja.

Zipo sifa nyingi..., kiongozi anayeweza kujieleza na watu wakaelewa anachozungumzia kwa lugha inayoeleweka; n.k.,
UTU
 
Labda Lowassa tu ila Mbowe, Dr Slaa na Tundu Lissu waligombea Urais wakiwa wanachama hai wa Chadema sio chini ya miaka 15.

Hiyo sio kazi ya CHADEMA, mbunge kama akisaliti unalaumuje chama?


CHADEMA Haina mpango wa kupeleka wabunge maana halitambui wabunge waliopo maana wote waliingia kwa wizi. Wao wamewafukuza Kina Mdee uanachama Wala hakuna mahali walijadili wang''olewe bungeni.


Sio kweli CHADEMA imeshaeleza sana kuwa ikiingia itatekeleza sera ya majimbo/ugatuzi, kuleta katiba mpya Ili kuepusha tozo za ajabu kutungwa na Rais, kufanya PPP kwenye miundombinu n.k Wala hakuna ambacho huwa hawasemi.
Hebu upinzani wawe serious kidogo basii! Ni kweli mzee Slaa pamoja na yote anataka kurudi tena chadema?
 
Kuna watu walijaribu kuwabwekea wapanga bei lakini hawakufua dafu, miongoni mwao wamo, Mwl. Nyerere, Magufuli, Nkrumah, Gadafi, Mugabe, nk. Hali ni ngumu kweli kweli. Mzee Nyerere ilimlazimu kuachia ngazi (kung'atuka) bila kupenda, nchi ilifisika kwa vikwazo.
Dah hatari sana, no way out tuendelee kuwalamba miguu tu.
 
Kupitia sera zake mbovu za Ujamaa nyerere aliharibu uchumi wa nchi like forever

Kupitia sera yake ya uoga wa kutopingwa nyerere alikuja na system ya chama kimoja tu na hivyo kuua demokrasia ya Tz,

Sera zake za azimio la Arusha zilifeli ovyo na kuendelea kuharibu nchi,

Sera zake za mahusiano mema na majirani zikapeleka nchi kupoteza vijana wake wengi kwenye vita vya ukombozi bila sababu za msingi + akaingiza nchi kwenye vita na Idd Amin kisa tu kumsaidia Obote,


Above all Nyerere alikuwa mzalendo lakini hakuwa na akiili na maarifa sahihi + vision sahihi ya taifa bora inabidi liwaje na awekeze kwenye nini,

So unaweza ona kuwa mzalendo tu hakukupi nafasi ya kufanya vizuri kama raisi wa nchi, kuna sifa za ziada inabidi uwe nazo
Haya yote uliyoandika hapa ni ujinga, na situmii neno hilo kama tusi, ninalitumia kwa maana yake halisi.

Kama siyo ujinga, basi utakuwa unayaandika haya kwa kurudia rudia yale yaliyosemwa na wapotoshaji na wewe sasa unayaimba hapa kama kasuku tu, asiyejua anafanya nini.

Kwa mfano:

Huna uwezo wowote wa kuelezea "ubovu wa sera za ujamaa" zilizosababisha "uharibifu wa nchi, 'like forever'".

Kutokana na uandishi wako inaonyesha wewe ni hawa wa siku hizi msiokuwa na nyuma wala mbele katika kuelewa mswala ya kidunia.
Kama ujamaa wa Nyerere" umeweza kuharibu nchi, like forever", wewew hata katika hili tu huwezi kuona ubovu wa akili yako katika kuyang'ang'ania haya ya miaka chungu nzima iliyopita? Umeuona mfano upi wa nchi ya mfumo wa kibeberu (unakotoa jina lako), hapa Afrika na kwingieko ambako 'ujamaa wa Nyerere' haukuwagusa, na sasa ni mfano mzuri wa kuigwa?

Sitapoteza muda mwingi na kukujibu upuuzi mwingine ulioandika huko chini.

Niakupa ushauri tu, achana na tabia za kukaririshwa mambo. Umejaaliwa akili, zitumie kufikiri na kupata majibu sahihi ya maswala unayotakiwa kuyakariri kama kasuku.
 
Ana akili Sana kama za Nyerere.
Hakuna unishi kuwa akili anzo lakini ni za kuwa Rais wa nchi au TLS? Kuna wakati nashangaa watu wenye akili nyingi wanatetea watu wanaozidi kuzaana kwa Kasi na wanyama wanaozidi kuzaana kwa kasi waishi pamoja kwenye eneo ambalo haliongezeki ukubwa; mwisho wa watu na wanyama hao ungekuwaje? Watu wenye akili nuingi sana wanatetea wamachinga wanaozidi kuongezeka idadi Yao kila siku na kila mwaka waendelee kufanya biashara barabarani, mitaani, mwisho wake utakuaje? Wakati mwingine unaona professor anaongoza wizara vibaya kuliko asiye na PhD. Kuna wakati mwingine unamkuta mbunge wa darasa la sana anajenga nzuri kuliko mbunge mwenye PhD. Nadhani akili peke yake sio kigezo pekee Cha kuwa kiongozi bora.
 
Hana sifa, anafaa kuwa mwanaharakati, angalau awe mbunge kwaajili ya kuichachafya serikali. Hata uwaziri tu hana sifa.
 
Hebu upinzani wawe serious kidogo basii! Ni kweli mzee Slaa pamoja na yote anataka kurudi tena chadema?
Politics is a game of numbers, sio sababu wanamhitaji ila sababu wanajua ni anti CCM basi Wana take advantage kumtumia kuwaongezea political power and influence.
 
Haya yote uliyoandika hapa ni ujinga, na situmii neno hilo kama tusi, ninalitumia kwa maana yake halisi.

Kama siyo ujinga, basi utakuwa unayaandika haya kwa kurudia rudia yale yaliyosemwa na wapotoshaji na wewe sasa unayaimba hapa kama kasuku tu, asiyejua anafanya nini.

Kwa mfano:

Huna uwezo wowote wa kuelezea "ubovu wa sera za ujamaa" zilizosababisha "uharibifu wa nchi, 'like forever'".

Kutokana na uandishi wako inaonyesha wewe ni hawa wa siku hizi msiokuwa na nyuma wala mbele katika kuelewa mswala ya kidunia.
Kama ujamaa wa Nyerere" umeweza kuharibu nchi, like forever", wewew hata katika hili tu huwezi kuona ubovu wa akili yako katika kuyang'ang'ania haya ya miaka chungu nzima iliyopita? Umeuona mfano upi wa nchi ya mfumo wa kibeberu (unakotoa jina lako), hapa Afrika na kwingieko ambako 'ujamaa wa Nyerere' haukuwagusa, na sasa ni mfano mzuri wa kuigwa?

Sitapoteza muda mwingi na kukujibu upuuzi mwingine ulioandika huko chini.

Niakupa ushauri tu, achana na tabia za kukaririshwa mambo. Umejaaliwa akili, zitumie kufikiri na kupata majibu sahihi ya maswala unayotakiwa kuyakariri kama kasuku.
Mwambie huyu kaka ili aelewe. Mfano, Kenya ya Jomo, Malawi ya Kamuzu na DR Congo ya Mobutu hawakuwa na ujamaa hata kidogo, waliamua kuendelea na ujamaa wao, je, hizo nchi Zina afadhali gani Leo kuliko Tanzania? Ujamaa wa Nyerere ndio msingi wa umoja wetu unaouona Leo hii. Bila ujamaa ule wa Nyerere huenda Leo hii wazazi wako wasingekuwa na mahali pa kulima, huenda hata wewe usingekuwa umesoma shule. Ujamaa ule ndio uliowapokonya mabeberu (dini) shule zao na kuwapa watoto wa maskini wasome humo.
 
Politics is a game of numbers, sio sababu wanamhitaji ila sababu wanajua ni anti CCM basi Wana take advantage kumtumia kuwaongezea political power and influence.
Ni mpiga kura mjinga TU anaeweza kuzubaishwa mara zote siku zote kwa mara moja. Siku hizi ninawatizama usoni wagombea na records zao. Kuna wabunge ambao walijenga mahoteli badala ya kujenga Chama mashinani, na wengine wajumba, wengine mashamba makubwa, nk. Sikujua kama siasa ni ajira za watu kama ajira za watu wengine tu. Mwanzo nillikuwa nafahamu kuwa kazi ya siasa ni kazi ya umma kwa manufaa ya umma.
 
Kwanini hizo sifa aulizwe kuwa nazo Tundu Lissu, na wengine wote kasoro Mwalimu Nyerere wasiwe wameulizwa kama wanazo?

Hebu chukulia mfano wa huyu tuliye naye sasa, halafu nipe sifa hata moja tu ya kipekee inayomtambulisha kuwa na sifa za urais?

Kwa maoni yangu, Tundu Lissu anazo sifa kumzidi Mwinyi, Kikwete na ningesema hata Magufuli, isingekuwa uigizaji wa uzalendo aliojaribu kuuonyesha.
Naambiwa kuwa urais sio mtu bali ni taasisi, Sasa sijui ni Mama Samia, taasisi ya urais au CCM anayejenga hizi barabara zote ninazoziona zinajengwa, anaesambaza maji na umeme vijijini na mijini, anaejenga haya madarasa mapya ninayoyaona mashuleni, anaejenga viwanja vya ndege kule Msalato, anaemalizia kujenga Bwawa la umeme, madaraja na reli ya SGR, anaewapa vijana miradi ya kilimo. Ninahitaji mtu mwenye akili timamu anifahamishe polepole bila jazba kuhusu ubaya wa Mama Samia dhidi ya Marais wetu wengine waliopita. Mtu aje afafanue kuwa Samia hafanyi nini au anafanya nini pungufu au zaidi ya wenzake waliomtangulia.

Rais Samia ni muumini wa total football, JPM alikuwa muunini wa kwenda na vipandevipande. JPM alikuwa anasimamisha mambo mengine ili kufanikisha mambo mengine haraaka, lakini Mama Samia anafanikisha mambo yote kwa wakati mmoja polepole. Wakati wa JPM tuliona kuwa kipaumbele chake kilikuwa ni ujenzi, ujenzi, ujenzi, ujenzi, ujenzi na kusimamisha mambo mengine kwanza. Tuliona nchi kama vile imetekwa na jeshi, kila barabara kila mtaa, kila site ya ujenzi, kila lindo kulikuwa na wanajeshi/polisi. Polisi walikuwa anapita njia yoyote na upande wowote wa barabara bila kuzingatia alama za barabarani.

Bahati mbaya ujenzi ujenzi ujenzi huu ulifanywa zaidi katika mikoa 3 tu Tanzania ya Dar es Salaam, Dododoma na Mwanza/Geita/chato.
 
Hata Mimi nakubali sana kuwa Mbowe anafaa sana kwenye uongozi wa juu na ndiyo sababu chama chake kimeweza ku survive hata katika nyakati ngumu wakati wote. Yupo resilient na anajua ku manage anger. Tatizo kubwa la hao ndugu zetu ni nepotism...Kwenye chama chake ameonyesha hili wazi wazi. Na sijui kwanini hao ndugu wa eneo Hilo wanashindwa kuficha hiyo tabia ya nepotism ya hali ya juu
Akina Tinubu
 
Mwambie huyu kaka ili aelewe. Mfano, Kenya ya Jomo, Malawi ya Kamuzu na DR Congo ya Mobutu hawakuwa na ujamaa hata kidogo, waliamua kuendelea na ujamaa wao, je, hizo nchi Zina afadhali gani Leo kuliko Tanzania? Ujamaa wa Nyerere ndio msingi wa umoja wetu unaouona Leo hii. Bila ujamaa ule wa Nyerere huenda Leo hii wazazi wako wasingekuwa na mahali pa kulima, huenda hata wewe usingekuwa umesoma shule. Ujamaa ule ndio uliowapokonya mabeberu (dini) shule zao na kuwapa watoto wa maskini wasome humo.
Ungemweleza yule mkuu, 'kavulata', siyo mimi, kwa maana haya yote ninayafahamu na zaidi.
Wanachokosa kuelewa watu wengi hapa ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani isiyokuwa na ujamaa ndani yake.

Hawa ambao ni kama wamewekewa 'software' ya kukariri maelezo ya kibepari wanafikiri huko nchi zinazojitangaza kuwa za kibepari hakuna ujamaa.
Hawa hawajishughulishi kabisa kujaribu kuelewa lengo lililokuwepo katika ujamaa wa Mwalimu Nyerere lilikuwa ni nini.
 
Back
Top Bottom