Je, tutarajie Rais Samia Suluhu kumrudisha Paul Makonda tena kwenye mfumo wa siasa?

Weka mapungufu pembeni, Makonda ni kiongozi mzuri Sana.
Hakuna binadamu asiye na mapungufu(kasoro), Kama yupi nionyesheni.

Mh. Makonda ni kiongozi mzuri ambaye kwa wakati huu utawala huu atatusaidia sana.

Mama Samia ikikupendeza fanya jambo kwa huyu Mtu, Kuna sehemu mbili naziona ana-fit Sana.

1) Waziri wa mambo ya ndani
- Simaanishi aliyepo ni kiongozi mbaya la hasha, Ila bado kuna mambo hayaendi sawa. Wezi wanatulaza macho, huwezi amini nyumba yako Ila usiku kucha unawaza kuwa mlinzi. Mh Makonda ni mtu ambae kwenye utendaji Hana simile. Wizara itabadilika hii, Mama fanya jambo hii wizara inataka Mtu mtata,mbishi na jasiri.
Najua Kuna nafasi za ubunge wa kuteuliwa bado zipo wazi, fanya jambo mama.

2) Mkuu wa mkoa wa Dar
- Watu wanasema TZ ipo dar, kuna ukweli hapo.
Aliyepo ni mzuri Ila yupo slow Sana,Kuna mambo mengi yamekwama kunahitajika Mtu wa ku-push mambo yaende. Huu mkoa unahitaji Mtu mtata sana aina ya makonda.

Mama fanya jambo, aina ya watu kaama Mh.Makonda sio wa kuwaacha kwenye utawala wako.

Jembe hili, Field Marshall
Chini ni picha ya Field Marshall Paul Makonda
 
Yaani Makonda kabisa???
Mnapo andika hivi vitu mna kuwa mmetumwa au mna kuwa mmevuta bangi?
Mnamjua Makonda na makando kando yake au mnamjua kwa sura yake?
Hebu tafuteni mada za kuweka hapa na muachane na wafu wazikwe waliko fia.
 
Yaani Makonda kabisa???
Mnapo andika hivi vitu mna kuwa mmetumwa au mna kuwa mmevuta bangi?
Mnamjua Makonda na makando kando yake au mnamjua kwa sura yake?
Hebu tafuteni mada za kuweka hapa na muachane na wafu wazikwe waliko fia.
Nimesema hapo kuwa HAKUNA asiye na mapungufu. Makonda bado ni kiongozi mzuri, uzuri wa kiongozi sio kuongea taratibu Bali ni kutekeleza na kuleta Maendeleo kwa watu
 
Sio Mimi nakuita hivyo bali watu wengi wanamuita hivyo
 
Kama umetumwa ishia hapo hapo, hivi Tanzania tumelogwa na nani jamani, mtu kavamia kituo cha redio tena cha washikaji zake, sembuse mimi na wewe pelekeni ujinga wenu na njaa zenu SUKUMA GANG.
Hayo yameshapita, tulikubaliana tunaanza upya
 
Naona kawapa hela mje kumtetea humu ndani alipewa madaraka kidogo tuu akaua watu akipewa wengine itakuwaje akae kwa kutulia
 
Una haki ya kuwa na msimamo huo....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…