Je, Ualimu ni daraja la mwisho kwa utumishi?

Je, Ualimu ni daraja la mwisho kwa utumishi?

NI kwa nchi zetu hizi za kimaskini zilizojaa rushwa na watu wenye akili km mleta mada. Nenda kwa wenzetu walioendelea hasa wazungu halafu urudi hapa jukwaani uandike tena kuhusu kada hii barikiwa ya ualimu. Walimu wanatimiza makusudi ya Mungu kuwapatia elimu wanadamu. Maandiko yasema "mtafute sana elimu angalia usimwache akaenda zake" Mi nawaheshimu sana walimu halafu nawapenda sana watoto wadogo ikiwa pamoja na kuwafundisha, na nyie mliolaaniwa kila mara walimu wanadharaulika, mmelaaniwa.
Mimi ni ticha. Ktk jamii inayoamua mambo bila ya tafiti za kuaminika (hasa afrika) ni vigumu sana kuona athari (hasi au chanya) juu ya mwalimu. Hapa Tanzania kila mwaka huwa inatangazwa ufaulu umeongezeka(wa mitihani tu) lakini upande mwingine ambao mwalimu hapimwi kwa matokeo ya mtihani wa mtoto (ambao ni hatari sana ukipuuzwa) hakuna anayejali.
Kwa mfano; unaniletea mtoto ninakaa nae miaka 2+7+4+2 then kila nikimtazama naona kitaaluma haendi popote (KWA SAUTI KUBWA, HAENDI POPOTE) ila namuona ni mwana jamii mzuri sana (dereva, mfanya biashara, mama au baba bora, mchungaji au imamu mzuri nk nk nk)hivi huwa mnajiuliza kitu gani mimi kama mwalimu nawekeza aweze kuwa hivyo? Utanipima kwa lipi ktk haya? Serikali inanipimaje hapa? (Extra curriculum?)
Jamii zote zinazofanya tafiti na kuamua kwa tafiti ndizo huona mwalimu ni FUTURE hivyo huakikisha saikolojia yake ipo chanya kwa muda mwingi kwani wanatambua generation ipo mikononi mwake. Sisi huku future ipo kwa wanasiasa ( yamejengwa mavyumba sijui mangapi vile na kujisifu kidato cha kwanza wote kwa mara ya kwanza wameanza pamoja!) Ila nani anauliza HAO KIDATO CHA KWANZA WOTE WAMEANZA KUSOMA PAMOJA? Lakini mimi ticha nipo nao tu na roho inauma juu ya jamii yangu hii ( wameejirundika wanakaa chini nk) lkn kuna kitu wapata (toka kwenye roho ya mwalimu) ila mwanasiasa anayejilipa vizuri yeye anawatangazia amewaletea shule (shule au kituo cha kukusanya watoto!)
Ugumu wa maisha ya mwalimu ni wakutengenezwa pia ili asiwe huru sana(free thinker) maana hawezi kudhibitika na tabaka tawala. Kujua hili ndio maana hata wakuu wa shule wao wanapewa daraja jingine (mwajili/madaraka allowance) sababu tu kumfanya mwalimu awe muoga toka chini kabisa mwisho naye huleta jamii ya waoga tu.
WASALAAM.
 
Kuna kitu kinaitwa re categorization, huwa mara nyingi naona watu wanatoka ualimu kwenda uhasibu, uchumi, uanasheria, nk ila ni nadra sana kusikia mtu anaomba recategorization atoke uhasibu, uchumi nk kwenda ualimu. Sababu ni nini hasa?
Una ugomvi na Mpwayugu!?
JamiiForums471477416.jpg
 
Kwa hiyo na hawa daraja la tatu A walipata Division 1 au 2.

Hata hao waliofika shahada ya kwanza wakiwa chuoni kwao ni bora liende tu, maana hata ukipata gentlemen degree wanaajiriwa.

Hii ni semi professional until ianzishiwe body yake na kumaliza astashahada, stashahada, shahada, uzamilo na uzamivu
Hao hao unaowadharau kwa kuandika ufedhuli kuwahusu ndo walikufundisha kuandika hizo stupidity ideas.
 
Kuna kitu kinaitwa re categorization, huwa mara nyingi naona watu wanatoka ualimu kwenda uhasibu, uchumi, uanasheria, nk ila ni nadra sana kusikia mtu anaomba recategorization atoke uhasibu, uchumi nk kwenda ualimu. Sababu ni nini hasa?
Wanakimbia njaa hao 🤣🤣
 
Hao hao unaowadharau kwa kuandika ufedhuli kuwahusu ndo walikufundisha kuandika hizo stupidity ideas.
Wanasheria Wana kitanzi Cha Tanganyika school of Law.
Wahasibu Wana mziki wa NBAA
Taaluma nyingine Wana pambana mno mfano Wahandisi, Watabibu, Watu wa Manunuzi

Ila Mwalimu ni bora liende tu.
Hakuna ushindani
Hakuna kujiongeza maarifa

Anaye toboa anawaza kubadilisha fani tu.

Wanajeshi, polisi, Magereza, uhamiaji, TISS, GSO hizi ni taaluma nyingine kabisa ambazo siwezi kuzijua.
 
Walimu hawawezi kuthaminiwa kwasababu ni sekta isiyoiingizia chochote serikali zaidi ya setikali kutoa pesa kuiendesha hii sekta. Tofauti na taasisi nyingine ambazo watumishi wake wanaiingizia pesa serikali mfano bandari, reli, TRA n.k

Haya yote yameletwa na sera ya elimu bure...ila elimu ingekuwa ya kugharamikia, walimu wangekuwa na mishahara mizuri sana
 
Walimu hawawezi kuthaminiwa kwasababu ni sekta isiyoiingizia chochote serikali zaidi ya setikali kutoa pesa kuiendesha hii sekta. Tofauti na taasisi nyingine ambazo watumishi wake wanaiingizia pesa serikali mfano bandari, reli, TRA n.k

Haya yote yameletwa na sera ya elimu bure...ila elimu ingekuwa ya kugharamikia, walimu wangekuwa na mishahara mizuri sana
Sera ikiwa sio Bure asilimia 60 ya Watanganyika wataishia elimu ya ngumbaru.
 
Walimu hawawezi kuthaminiwa kwasababu ni sekta isiyoiingizia chochote serikali zaidi ya setikali kutoa pesa kuiendesha hii sekta. Tofauti na taasisi nyingine ambazo watumishi wake wanaiingizia pesa serikali mfano bandari, reli, TRA n.k

Haya yote yameletwa na sera ya elimu bure...ila elimu ingekuwa ya kugharamikia, walimu wangekuwa na mishahara mizuri sana
Mkono Mmoja hujui unachokiongea, laiti ungejua Hawa wapo Asilimia Ngapi ya Watumishi wa Umma wote katika serkali halafu wanalipa sh. ngapi kwa serkali kila mwezi usingesema hivi.
Jamaa wapo wengi na wanalipa kwa mwezi serkal zaid ya Bilion kadhaa ukiwekewa hesabu hapa utajikuta kila mwalimu ukimuona unamuamkia. Mimi yup ninaye mfahamu niliangalia Mshahara wake pesa anayokatwa kwa mwezi PAYE aisee nilisema wazi kuwa hawa jamaa tuwaheshimu.
Wanalipa pesa ndefu kulingana na daraja aliloko.
 
FANI YA UALIMU NI ZERO KABISA.

Serekali iingilie kati hii yafani maana ina watu wa hovyo sanaa.

wana maisha magumu na hawana mawazo ya kutoka huko
 
Sera ikiwa sio Bure asilimia 60 ya Watanganyika wataishia elimu ya ngumbaru.
Bora mzee baba....zamani elimu ilikuwa ni ya viwango...kwanza unalipa ada..so mzazi mwenyewe anaionra uchungu pesa yake so mtoto ni lazima ukakomae skuli...mitihani mpk ya darasa la nne ilikuwa inaheshimika, ukifeli la nne unarudishwa...mtihani wa darasa la saba ulikuwa unaheshimika sio sasa hv hata wasahishaji mitihani hawasumbuki, wanapasisha wote...!! Matokeo yake huku juu tunakuja kupata graduates wengi vilaza
 
Back
Top Bottom