Je, ualimu ni kwa ajili ya watu maskini?

Je, ualimu ni kwa ajili ya watu maskini?

Nyie ambao sio walimu mmefanikiwa kiasi gani katika haya maisha

Kuna wakati ukiwakuta watu wanawaponda walimu Ila tazama hao wapondaji ndo utajua kuwa hii nchi na MTU mweusi ni MTU mjinga Sana.
Pokea changamoto hakuna anaempinga mwalimu, nawajua washikaji wengi waliokacha ualimu wakaenda kujiongeza kwenye mambo Yao mengine, wengine kabla ya kuajiriwa walijiongeza huko sasahivi uwaambii kitu kuhusu kufundisha hawataki kabisa kusikia.
 
Leo nimejisikia vibaya Sana baada ya kumsikia Mzazi mmoja akimgombeza Mtoto wake aliyekua na ndoto ya kusomea ualimu, maongezi yao yalikua hivi.

Mtoto: baba Mimi nataka kusomea ualimu.

Baba: hivi umechanganyikiwa? yaani uende ukawe Mwalimu? Walimu Wana maisha gani? Eeeh! Wana kipi Cha maana? Sitaki kusikia hizo habari zako Bora ukaombe chuo Cha diploma uombe hata clinical officer nitalipa ada.

Yale maneno yamenifanya nitafakari Sana, kundi la walimu linaonekanaje? Mbona wapo wengi wenye uwezo? Hivi Kuna mtu yoyote anatamani angelikua Mwalimu? Je kutopewa heshima kwa walimu inasababishwa na nini? Je ni ugumu wa kazi? Au salary ni ndogo? ..

Mwisho, unaweza kuruhusu mtoto wako asomee ualimu?
Daah
 
Ualimu ni fani moja nzuri na yenye soko kubwa kama utajua namna ya kujiongeza. Kwasababu kila siku watu kuna jambo wanataka kulifahamu so watahitaji mwalimu wakuwafundisha.

Tatizo ni kuwa vijana wengi wanaohitimu ualimu wanabaki kuwa waalimu wa masomo waliyosomea chuo utasikia mimi mwalimu wa jiografia mara kiswahili au sayansi, wameshindwa kutumia ujuzi na maarifa yao ya kufundisha kufundisha wqtu mambo mbali mbali.

Mfano, kama mtu kasoma ualimu alafu akajielimisha juu ya matumizi ya AI labda ChatGTP au hata sanaa fulani kama muziki au jambo lolote akawa na ufahamu wa hilo jambo anauwezo wa kuhamisha ufahamu au ujuzi wake huo kwa watu wakamuelewa na kumlipa.

Kifupi ukisoma ualimu ukahitimu wafundishe watu vile unavyovifahamu au kuwa na kipaji navyo serious kwa kutumia maarifa ya ufundishaji uliyonayo.

Najua ni ngumu na pengine nikaonekana motiveshno spika ila bila kuwqza nje ya box mwqlimu hauwezi kutoboa japo ndio fani yenye wateja wengi kuliko fani zingine zote.

Umeshindwa yote anzisha basi twisheni au homework aider kwa njia ya digitali uwe unafanya mambo kama mtaaluma sio mbabaishaji, watu wana smartphone wanaweza kutumia na watoto wao. Ujue sio kila mzazi anajua kutafuta kipenyo a kipeuo, why asijiunge na program yako kama inamuondolea aibu ndogo ndogo na mwanae anapata elimu.

Watakulipaje, jisajili Lipa kwa simu kuwa na website na App ya android na Ios fanya kazi kama msomi. Vaa vizuri, eneo la ofisi smart, tumia kamera quality, set up nzuri usikike vizuri, engage na mteja wako. Nusu saa Tsh. 200 hapo una wateja 10+

Ila uandae mtaji wa kama milioni tatu, maana hakuna biashara ya maana isiyo na mtaji wa pesa.

Kwa atakayeokota jambo haya, kila la heri ndugu mwalimu
Asante point kubwa hii, yote kwa yote nilichoelewa zaidi hapa ni kuwaza nje ya box na sio kutegemea mshahara.
 
Pokea changamoto hakuna anaempinga mwalimu, nawajua washikaji wengi waliokacha ualimu wakaenda kujiongeza kwenye mambo Yao mengine, wengine kabla ya kuajiriwa walijiongeza huko sasahivi uwaambii kitu kuhusu kufundisha hawataki kabisa kusikia.
Hamna changamoto yoyote unaishi katika illusion Sana.

Kazi yoyote unayoijua huwa haina uwezo wa kukupa mafanikio makubwa Ila unaweza kutumia kazi yako Kama stepping stone ukawekeza in various things.


Mafanikio huwa yanamfata MTU mwenye malengo makubwa na mazuri na MTU smart na sio MTU mwenye decent income.


Kuna watz wangapi kupitia decent income zao wamewekeza kufika hata angalau mil 500 so think twice and deeply.
 
Kuna MTU alikuwa mbunge wa ccm wa Bukoba siwezi mtaja jina lakin baada ya kutoka bungeni alirudi kuwa broke.

Kuna watu kibao walikuwa TRA Ila leo wapo broke.

Kuna wengine walikuwa jeshini na vyeo vikubwa Ila now wapo broke.

The list is endless

Wote hawa Sababu ya wao kuwa broke walikosa Financial education kutoka Kwa walimu ili wasimame imara.

Unapokuwa mwalimu ,jiboreshe kuwa na maarifa ya muhimu ambayo unaweza mpatia MTU akapata mwanga, kuwa mentor mzuri


Kinachowafelisha walimu ni kutobadilika kutokana na mahitaji ya jamii na kubaki kuamini kuwa niwalimu wa Masomo ya necta tu.


The chances are ,nikubadilika na kuwa knowledgeable enough.
 
• Mkuu, yani kuna watu waajabu sana, Mtu unamchukia/au unauchukia ualimu, ¿¿¿

• Basi sasa achukue huyo mtoto wa miaka saba kisha ampeleke akasomee urubani, [emoji3]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji119][emoji119][emoji119] ni umaskini wa kufikiri.

Wangejua miongoni mwa kazi ambazo hata Mungu anaweza toa thawabu juu ya kile wanachokifanya duniani mwalimu hakosekani kwenye hiyo list.

Hv unajua kumfanya mtu ajue kuandika na kusoma Tena Kwa lugha ambayo hakuzaliwa nayo sio kitu Cha kudharau sema basi tu.

Kumfanya mmasai, mgogo, mmakonde, Muha n.k anaongea English imenyooka kama mzungu nyieeeee nyieee acheni dharau na kazi za watu[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Ndio naweza mruhusu asomee ualimu ila wa watoto wadogo ,awafundishe kusoma na kuandika, kama ata kuwa na huo wito.
Ww unajua utoafuati wa ualimu ni kitu Gani ? Yaani huyo anayefundisha nursery, primary , secondary, chuo.

Hadi useme asomee wa watoto wadogo, mwalimu ni mwalimu no matter utamkuta level Gani au unafikr huo wa watoto unasomwa week 1 sio?
 
Hiki ni kibarua chetu sie masikini tu tusio na 'konekisheni'🤣🤣🤣
Huo ndio uhalisia ndugu? Na Imani Mzazi aliepo TRA au aliepo kwenye position nzuri hawezi kuruhusu mtoto wake awe Mwalimu, hiki ni kichaka kwa sisi waomba Mungu tu tusio na connection na watu, Mimi hobby yangu na ndoto zangu huwa ni biashara lakini unajikuta upo sehemu ambayo moyo haupo kabisa, eg umepangwa kigoma huko yaani ndoto zako zoote zinakufa huko utafanyaje?
 
Ualimu ni shida uko akuna posho, akuna pesa ya kinywaji, akuna pesa ya pango, pesa ya likizo mbaka uende ukadeki pagala la mkurugenzi na akuchapie mkeo ndo upate, promotion mbaka ukaroge, seminar mbaka umuonge mkuu wa shule na afisa elimu, kusimamia mitihani 10% Kwa mkuu, kuenda mark mbaka yesu aludi, mikwara kibao shule aina computer lakini mkurugenzi anataka mtoe A za SoMo la computer, ata mjumbe wa nyumba kumi bosi wako anaweza akaja shule akakufokea Kwa Nini ofisi chafu aujadeki na ikiwezekana kama una kimwili kidogo anakulamba na viboko vitatu vya nguvu, pesa ya mwenge utaki unataka utatoa, makato ya Cwt unayataka uyataki itakatwa TU lete fyoko ushughulikiwe
For sure kada ya kipumbafu Sanaa hii although ndo inanipa kula Ila NI ya kipuuzi HAKUNA mwalimu anaejivunia kua mwalimu
 
Back
Top Bottom