Je, ualimu ni kwa ajili ya watu maskini?

Nakuhakikishia mkuu,labda comb aliyosomea isiwe na fani za maana za kusomea,angalia watu wanapiga pcm,PCB,cbg wenye one wanakimbilia wapi na hata comb za arts weng wanataman hata kusomea sheria,uwalimu ni option ya mwisho kwamba atafanyaje anatokea familia duni na anaangalia kupata mkopo kirahisi
 

Fanya utafiti mdogo,alama za kwenda uhandisi na udaktari halafu ulinganishe na za kwenda kusomea uwalimu ngazi ya degree,tulinganishe wapi wanavigezo vikubwa
 
Kusema ukweli Ualimu kutoboa mfano nyumba Kali 2,gari angalau Harrier na mlo draft =Never. Ukiachana na pesa kiduchu lkn majungu na kuoneana wivu pindi mmja anapopambania maisha yakee.

Fikilia mtu unatoka shule saa11 eti mnapambana watoto wafaulu,Mwisho wa mwezi laki 4. Familia inaitaka pesa ndugu wanaitaka pesa,nguoo kukeep status Ongeza na michepuko.

Pia ukijishugulisha na Biashara ikashine,ukikaa vibayaa unahamishwa wapo unapelekwa chakaa ambako hutofanya chochote ubaki kufunfishaa tu hapoo umasknii milelee.

Hivyobasi Ili Tasnia ya Ualimu iheshimike lazima Kuna mambo yawekwe sawa:

1.Ongezeko la mshahara 2.Kazi Mwisho saa 8 mchana weekend Free watu wapate mdaa wakujitafutia kipatoo.3.walimu certificate wote waondolewe kwenye system,Hawa ndo walevii mpaka chokaa mtu mpaka anajikojolea au mademuu haswaa familia hawajali.4.pia wale maafisa wajitambue sio kusikiliza majungu na wivu hovyoo na kuhamisha hamisha kiipuzi.All in all Ualimu nikazi Yaa Amani sana kama mtu unajielewa na upo Eneo zuri.
 
Hivo vitu sioni faida yake Cha msingi umeelewa nilichomaanisha na ndio mana unanijibu basii hiyo tu yatosha.
Hao wamilisi wa lugha ndo wanapambana na vimishahara vya kifeisali
 
Toka tupate uhuru hakuna kiongozi yeyote wa CCM ambaye kampa mwanae au mjukuu kazi ya ualimu.
 
Kwanza hayo mambo ya wanaosomea ualimu hawakufaulu vizuri sio kweli, nenda pale UD mlimani main campus na division two yako ya mwisho kaombe ualimu halafu uone Kama utapata, Kuna Watu Wana one zao nzuri na wanasomea Ualimu.

Issue ya mshahara pia inategemeana na mwalimu wa shule gani/sekta ipi, Kuna shule X mitaa ya Tabata walimu wanalipwa milioni kadhaa na Wana push mikoko ya maana kweli kweli.
Shule Kama Feza, Baobab, Kaizirege n.k mishahara ya hao waalimu sidhani Kama kipato chako kinaingia hapo.
Kuna waalimu wamejiongeza wanafanya issue zao na wanafundisha na wana maisha Safi tu.
Mwalimu pia ni mtumishi ambae kupitia kituo chake Cha kazi anaweza kutengeneza 'mifumo' ambayo itamsaidia asiguse mshahara wake.

Unasema hujaona mwalimu mwenye hela hapa mjini hujui kuwa MC Gara B ni mwalimu, A teacher by Profession...πŸ˜…
Ndugu being a teacher is not a bad thing, Sana ni blessing ambayo ikitokea 'ukijiongeza vyema' unaweza kutoboa tu, bila kuiba wala kuvunja Sheria.
 
Mkuu hizo tusiime cjuw fountain gate sio shule za serikali,na huyo gara b Hela yake ni nje na uwalimu,halafu hao walimu wako unaosema Wana Hela kawafananishe na wahandisi wa kwenye makampuni makubwa au hata madaktari wa hospital kubwa ndio utaelewa kuwa hiyo ni kazi ya mshahara mdogo,,nakukumbusha tu mwalimu mwenye hela hapa bongo tunaemfaham kwa vijana ni teacher KONDE πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ (joking),labda nikuulize mshahara wa mwalimu mwenye degree ambae anaanza kazi ni shingapi ili tukufananishie na wenzake kama wanasheria,wahandisi,madaktari,wafamasia n.k
 
Halafu mkuu usidhan mm nawadharau walimu hapana,nawaheshimu sana tu maana ni kazi halali inayowapa kipato,hii maada kama wadau hijatuelewa ni kwamba tunailaumu serikali kutowapa maslahi mazuri angalau kama watumishi wa kada nyingine wanavyofanyiwa au hata wapewe zaidi maana wao hawana malupulupu Wala hawawez fanya namna ya kupata kitu ndani ya kazi yao,hizo sekta nyingine watu wanalipwa hela nyngne nje mishahara,vikao vingi,mara shift za usiku,Bado rushwa pia,lakin mwalimu hawez kula rushwa yoyote na Bado serikali inawaweka mazingira magum ndiomaana inaonekana ni kazi ya watoto wa familia maskini
 
Mwalimu halmashauri anaeanza ni 822,000/= ni sawa na mwanasheria wa halmashauri hawapishani Sana, SEMA kwenye ualimu ni dry hakuna posho n.k
 
Ukweli ni kwamba ualimu sio tu kazi ya kimaskini bali pia ni kazi ya kitumwa hasa hapa Tanzania.

Binafsi nilikata moto baada ya kwenda field mwaka wa kwanza, nimekuta maisha ya huko sio poa kabisa.



Honestly, Tunasomea ualimu kwa sababu ya umaskini tu na hamna mzazi anayetaka mwanaye asomee ualimu.
 
Tatizo ni kwamba kwenye Ualimu hakuna rushwa, posho wala hongo za hapa na pale

Mwalimu ukiona anahela ni labda awe amejiongeza kwenye biashara nje ya kazi yake ya ualimu

Mwalimu hawezi kupata mafanikio makubwa kwa kutumia kazi yake hiyo hiyo ya ualimu pasi na kufanya kingine nje ya kazi tofauti na watu wa kada zingine
 
Coarse
 
HaKuna sehemu nimesema hizo ni shule za serikali I know for a fact what am talking about....
Hizo kampuni kubwa na mahospital makubwa sijui unazungumzia ya private au binafsi?
Hata Gara B sijasema kwamba hela kaipata kwenye ualimu nilikuwa nakukumbusha mwalimu akijiongeza anaweza kupata maokoto fresh tu
And according to him education career ndiyo ilikuwa ground ya yeye kusimamia na kutokea...

Halafu basic salary ya mwalimu wa degree inaendana na kada kibao tu, wanakuja kutofautiana kwenye issue za allowances na vipesa vya hapa na pale na wengine wezi tu kibao.
 
Hili nalo mkalitazame
 
Ualimu bongo ni utahira walimu wengi ni zero kichwani mtu ana alama za chini anaenda somea kushika chaki mwisho wasiku anazalisha division 4 na 0 za kutosha. Ualimu ni laana
 
Mwalimu halmashauri anaeanza ni 822,000/= ni sawa na mwanasheria wa halmashauri hawapishani Sana, SEMA kwenye ualimu ni dry hakuna posho n.k
Duh hizo fani zingine ni balaa. Sasa mfano mwanasheria wa halmashauri anapata wapi posho? Kwani ana safari au anafanyaje ili kupata hiyo ela nzuri? Na mishahara yao kwa sasa ni kiasi gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…